Umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18

Umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
104,319
Reaction score
183,600
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
Hilo wazo binafsi nalikataa Tena Kwa sababu, watanzania na Utanzania wetu hata wenye umri wa Hadi 20 .kwamazingira yetu Bado kujitambua na kufanya maamuzi juu ya hatma yao na Taifa lao achilia hata walio bahatika kufika darasa (SII wote ila 80%+)Mimi nafikiri katiba mpya ingetaka angalao mpiga kura Kwa mazingira ya Tanzania awe mwenye angalao kuanzia elimu ya kidato Cha sita na kupata ufaulu au elimu inayolingana nayo Kwa kuanzia.Ili tupate viongozi waliochaguliwa watakayo weza kujua Tanzania inahitaji Nini Kwa maendeleo ya Taifa na watu wake.
 
Mi naonelea uanzie miaka 30 ndo itasaidia zaidii manake vijana wengi waloamua kuendelea na masomo ya ngazi ya elimu ya juu wapo masomoni hawawazi machungu ya waloko mtaaniii
 
Umri wa kugombea urais uwe miaka 25.
Miaka hamsini ambao walitarajiwa kuongozwa na busara na weledi Kwa uzoefu Bado ni changamoto Kwa mazingira ya Tanzania je itakuwaje Kwa mtoto asiyeweza hata kujisimamia(zaidi mtoto wa kitanzania na Utanzania wake)
 
Wapige tu kura kwa umri huohuo.

Mbona CCM wanachipukizi mashuleni.

Na chadema wanachemchem mashuleni.
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
Hivi hawa jamaa huwa wanapita humu jamii forums kweli!!!? Maana kwa aina ya thread utitiri zinazoanzishwa kila siku humu JF, lazima wangebadili mtazamo na kupendekeza umri wa kupiga kura uwe kuanzia miaka 25.
 
Mtoto aliyefikisha umri wa kuanza drs la kwanza aruhusiwe kupiga kura, bila hivyo wapinzani watakuwa wanaambulia patupu kila uchaguzi.
 
Upumbavu huu Nani kalipia huo utafiti?...halafu nchi zinazo jielewa wanaanza miaka 21
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
Hakielimu saa naona wameishiwa vya kujadili hivi mtoto wa miaka 14 anaweza kufanya tathimini na kuamua kwa utashi wake kuwa amchague kiongozi gani kwa sababu gani? majadiliano mengine unaweza jiuliza kama huwa yanafanyika kwa maslahi ya nani?
 
Umri wa kupiga kura kwa tume hii ya sasa ya uchaguzi haina maana.
Wana wakala wa kusambaza kura kwenye mabegi,n.k
So watawasumbua bure watoto.
Wafanye tafiti jinsi tozo zinavyoathiri makuzi ya watoto.
Hata mimi nimewaza hivyo.
Watoto wa miaka 14 ni wale ambao shule ndio kwanza wanaanza kusoma kidato cha kwanza kuna umuhimu gani wasumbuliwe kuwaingiza kwenye purukushani za uchaguzi hali ya kuwa hata hawajui kuchanganua mambo ya kimaisha vizuri,sana sana watakuwa wananunuliwa kirahisi kwa kushinikizwa na walimu wao mashuleni.
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
Akifanya mapenzi kisheria kabakwa kwa sababu hana uwezo wa kuamua, sasa kwenye kura uwezo wa kuamua anaupata wapi? Huo nao ni ubakaji wa kura.
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo

Source ITV habari
Kwani nini hayo mapendekezo hamjayapele kwa Tume ya Warioba iliyokuwa inakusanya maoni ya Katiba Mpya ili yaingizwe kwenye mapendekezo ya Katiba Mpya?
 
Vitu vingine vya kijinga vinapo jadiliwa na watu wazima nashindwa kuelewa uwezo wao wa akili una endana na umri wao ?
 
Asasi ya HakiElimu imependekeza umri wa kupiga kura uanzie miaka 14 badala ya 18 ya sasa

Mapendekezo hayo yamefuatia utafiti maalum uliofanywa na taasisi hiyo
Yaani tuna tatizo la watu kutuchagulia viongozi yeboyebo halafu hawa wanataka tuwaruhusu watoto wapige kua? Mie napendekeza kupiga kura iwe kuanzania mika 25 hadi 65. Nje ya hapo subirini mpewe viongozi
 
Back
Top Bottom