MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 21,764
- 71,793
Wasalaam,
Jana tarehe 8 kikao cha Baraza la Ulinzi na Usalama la Umoja wa mataifa kimeshindwa kupitisha Azimio la kuvamia nchi ya Syria kijeshi lililoletwa na nchi ya Ufaransa.
Aidha ilitegemewa kikao hicho kiruhusu uvamizi wa kijeshi nchini Syria ambapo ndege za mataifa ya nje zingeruhusiwa kuingia nchini Syria na kufunga anga lake ili ndege za kivita za serikali ya Bashar Al Asad zisiruke na kuendelea kuua raia wake.
Nchi ya Urusi kupitia balozi wake wa kudumu wa Umoja wa mataifa ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza hilo la Ulinzi na Usalama wamepinga Azimio la Mfaransa na Hispania kuhusu kuacha kulipua maeneo ya jiji la Aleppo ili warudi kwenye mazungumzo ya mezani.
Pingamizi hili imeambatana na kura ya Hapana (VETO) kutoka Urusi, hivyo kutupilia mbali kabisa Azimio hilo la Baraza la Ulinzi na Usalama.
Na kibaya zaidi ni kwamba Mrusi naye alileta Azimio lake kuhusu nchi ya Syria lakini nalo likapingwa kwa kutumia kura ya VETO kutoka nchi za Magharibi. Serikali ya Uchina imeamua kutofungamana na upande wowote na kuamua kutopiga kura kabisa.
Ikumbukwe mwaka 2011 Azimio namba 1973 la Umoja wa Mataifa ndilo lilirohusu mataifa ya Magharibi yakiongozwa na NATO kwenda kufunga anga la nchi ya Libya na mwisho wake wote tunajua ni nini kilitokea. Mataifa ya Magharibi yalivuka mipaka na kuanza kulipua hadi chini kitu ambacho ni kinyume kabisa na Azimio.
Kinachoniogopesha ni kauli zisizo za Kidiplomasia ambazo zimetolewa na Mabalozi husika katika kikao hicho. Mfano tu, Balozi wa Uingereza bwana Matthew Rycroft amesema "Normally I begin my statement with, ‘Thank you Mr President’, cannot do this today. his council cannot stand by while such misery is meted out on the people of Aleppo. And yet, thanks to you, Mr President, that is exactly what we are doing. Thanks to your actions today, Syrians will continue to lose their lives in Aleppo and beyond to Russian and Syrian bombing. Please stop now."
Balozi wa Marekani naye kasema "One of us, perversely the president of council, is determined for the killing to continue, and is helping carry it out"
Kilichonishangaza zaidi ni pale ambapo wajumbe wa mataifa ya Marekani, Ufaransa, Uingereza na mengine kuamua kutoka wakati balozi wa nchi ya Syria alipoanza kuzungumza kuhusu huu mgogoro.
Kama hawataki kuwasikiliza wahusika, je watamsikiliza nani kwa sasa?
Ikumbukwe kwamba Baraza la Ulinzi na Usalama la Umoja wa Mataifa ndilo pekee lenye uwezo wa kuidhinisha uvamizi wa nchi yoyote ile kama linahisi kuna uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
Uvamizi kama ule wa George Bush wa mwaka 2003 hauruhusiwi na ndiyo umechangia kuleta mambo kama ISIS, AL-NUSRA na Wimbi la Wakimbizi barani Ulaya.
Najiuliza tu,
Jana tarehe 8 kikao cha Baraza la Ulinzi na Usalama la Umoja wa mataifa kimeshindwa kupitisha Azimio la kuvamia nchi ya Syria kijeshi lililoletwa na nchi ya Ufaransa.
Aidha ilitegemewa kikao hicho kiruhusu uvamizi wa kijeshi nchini Syria ambapo ndege za mataifa ya nje zingeruhusiwa kuingia nchini Syria na kufunga anga lake ili ndege za kivita za serikali ya Bashar Al Asad zisiruke na kuendelea kuua raia wake.
Nchi ya Urusi kupitia balozi wake wa kudumu wa Umoja wa mataifa ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza hilo la Ulinzi na Usalama wamepinga Azimio la Mfaransa na Hispania kuhusu kuacha kulipua maeneo ya jiji la Aleppo ili warudi kwenye mazungumzo ya mezani.
Pingamizi hili imeambatana na kura ya Hapana (VETO) kutoka Urusi, hivyo kutupilia mbali kabisa Azimio hilo la Baraza la Ulinzi na Usalama.
Na kibaya zaidi ni kwamba Mrusi naye alileta Azimio lake kuhusu nchi ya Syria lakini nalo likapingwa kwa kutumia kura ya VETO kutoka nchi za Magharibi. Serikali ya Uchina imeamua kutofungamana na upande wowote na kuamua kutopiga kura kabisa.
Ikumbukwe mwaka 2011 Azimio namba 1973 la Umoja wa Mataifa ndilo lilirohusu mataifa ya Magharibi yakiongozwa na NATO kwenda kufunga anga la nchi ya Libya na mwisho wake wote tunajua ni nini kilitokea. Mataifa ya Magharibi yalivuka mipaka na kuanza kulipua hadi chini kitu ambacho ni kinyume kabisa na Azimio.
Kinachoniogopesha ni kauli zisizo za Kidiplomasia ambazo zimetolewa na Mabalozi husika katika kikao hicho. Mfano tu, Balozi wa Uingereza bwana Matthew Rycroft amesema "Normally I begin my statement with, ‘Thank you Mr President’, cannot do this today. his council cannot stand by while such misery is meted out on the people of Aleppo. And yet, thanks to you, Mr President, that is exactly what we are doing. Thanks to your actions today, Syrians will continue to lose their lives in Aleppo and beyond to Russian and Syrian bombing. Please stop now."
Balozi wa Marekani naye kasema "One of us, perversely the president of council, is determined for the killing to continue, and is helping carry it out"
Kilichonishangaza zaidi ni pale ambapo wajumbe wa mataifa ya Marekani, Ufaransa, Uingereza na mengine kuamua kutoka wakati balozi wa nchi ya Syria alipoanza kuzungumza kuhusu huu mgogoro.
Kama hawataki kuwasikiliza wahusika, je watamsikiliza nani kwa sasa?
Ikumbukwe kwamba Baraza la Ulinzi na Usalama la Umoja wa Mataifa ndilo pekee lenye uwezo wa kuidhinisha uvamizi wa nchi yoyote ile kama linahisi kuna uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
Uvamizi kama ule wa George Bush wa mwaka 2003 hauruhusiwi na ndiyo umechangia kuleta mambo kama ISIS, AL-NUSRA na Wimbi la Wakimbizi barani Ulaya.
Najiuliza tu,
- Kwanini haya mataifa ya Magharibi hayajifunzi tu?
- Wakivamia Syria hawataongeza Wakimbizi na Ugaidi kweli?
- Kwanini wahusika wakuu kama Israel, Iran na Syria wanaachwa kwenye vikao muhimu kama hivi?
- Je mataifa ya Magharibi yanaweza kuvamia Syria bila ruhusa ya Baraza la Ulinzi?