Ummy Mwalimu aitetea Serikali kuhusu Lissu

Ummy Mwalimu aitetea Serikali kuhusu Lissu

Status
Not open for further replies.
.Ili serikali iweze kushiriki, ni lazima yawepo maombi ya kufanya hivyo.

Mke wa Lissu akiandika barua ya maombi tu, lazima kuna press releases kama tatu (Ikulu, Bunge, CCM kwa Polepole) zitatolewa kuujulisha Umma wa Watanzania. Well, ifike mahali familia iombe tu maana Uhai kwanza na hizi ''prides'' baadae.
 
Ni sawa kabisa utaratibu huu upo hata kwa watumishi wengine usipofuata mfumo Wa serikali ujigharamie hata awe rais. Mabadiriko hayawezi kuanza kwa lissu lazima utaratibu ufuatwe huku tukizingatia kubana matumizi

We always say "break the rule to accommodate customer(s)". Kwa critical condition kama ile si vyema sana kushikilia bureaucratic procedures of the government unless you are after death. Kwa maoni yangu hata ingekuwa kiongozi yoyote wa nchi yetu imetokea vile au hata ajali mbaya ya gari au chombo chochote cha usafiri lazima baadhi ya taratibu inabidi zisifuatwe ili kuoko maisha yake. Ndio mana hata issue ya PF3 wananchi walitoa maoni wakati fulani kuwa kusubiri majeruhi apate pf3 huku akiwa Hali mbaya sio vyema, tuangalie kuokoa uhai kwanza.
 
Mh Waziri nafikiri fanyeni kwa Busara bila kutaka kujiondoa kwenye lawama kwa nguvu. Mlipieni mgonjwa kwa sababu ni Mtanzania na yuko kwenye ajira ya Bunge. Anastahiki.

Haya mengine ya kuwa alijitoa kwenye mfumo wa serikali ni urasimu husio na maana. Angalau Mh Sitta Hakuwa mbunge au kwenye ajira yoyote ya serikali. Mnachofanya sasa mnauthibitishia ulimwengu kauli ya rais wetu aliyoitoa huko Ugunja akimulaumu Mh Shein kwa kumpeleka Maalimu Saif kwa matibabu. Msaidieni Rais haya mambo ili yeye ashughulike na mambo makubwa.

Mh Lissu hapo Dodoma Hakuwa katika hali ya kuamua chochote. Na ilikuwa Busara tu kuchukua maamuzi ambayo yangesaidia kuokoa uai wake unless hii haikuwa priority!

Very logical point. Ndicho kilichotakiwa kufanywa. Je ufuate urasimu mtu afe useme tulikuwa tunafuata taratibu au kuvunje taratibu ili kuokoa uhai wa mtu? Uhai kwanza taratibu badae
 
Dada Ummy umeshanawa mikono, wenye akili timamu wamekuelewa vyema.

Mungu akujalie uvumilivu, maana kila kitu kwa sasa kinatazamwa kwenye fikra potofu za kisiasa.
 
We always say "break the rule to accommodate customer(s)". Kwa critical condition kama ile si vyema sana kushikilia bureaucratic procedures of the government unless you are after death. Kwa maoni yangu hata ingekuwa kiongozi yoyote wa nchi yetu imetokea vile au hata ajali mbaya ya gari au chombo chochote cha usafiri lazima baadhi ya taratibu inabidi zisifuatwe ili kuoko maisha yake. Ndio mana hata issue ya PF3 wananchi walitoa maoni wakati fulani kuwa kusubiri majeruhi apate pf3 huku akiwa Hali mbaya sio vyema, tuangalie kuokoa uhai kwanza.
Nyie hamweleweki mnayemlalamikia Leo ndio Huyo mumemtuhumu kapiga risasi afu hamna imani naye sijui kama mngeruhusu hizo taratibu zifuatwe? Lakini kwani kuna ubaya gani kutibiwa na chama? Wangeona kunaulazima Wa serikali wangefuata utaratibu kwanini usumbuke na mtu asiyekuamini? Sikuona hata sababu mtu Fulani kutangaza hadharani kuwa serikali haikuchangia wakati hamuiamini mi kama ninhekuwa rais ningezuia serikali isiongelee masuala ya lissu
 
Very logical point. Ndicho kilichotakiwa kufanywa. Je ufuate urasimu mtu afe useme tulikuwa tunafuata taratibu au kuvunje taratibu ili kuokoa uhai wa mtu? Uhai kwanza taratibu badae
Mbona hawasemi aliyegharamia matibabu ya awali Dodoma na walishauliwa nini na madaktari Wa dodoma
 
Kaa na uccm wako... Lodilofa weee[emoji16] [emoji16] [emoji16]
Sina chama namsapoti baba jesca na mungu aendeleee kumweka hai. Na ninamwombea sana lissu na sipendi kuona tatizo LA mwenzetu linazungumzwa kivyama ni ujinga na ulofa kama naouna kwako
 
wakuu hapo juu wote mnaongea kwa hasira, uchungu na gubu. Ila ndio iko hivyo. ni serikali hiyo ni dudu kubwa ambalo halina aibu lina system a procedures. hauzifuati wala haikuangalii


..Mbona familia ilimuomba Waziri na Spika kwamba wampeleke Nairobi badala ya Muhimbili
na wakakataa?
 
Naona ni heri mara kumi mhe. waziri wa afya angekaa tu kimya kiliko kujitahidi kuitetea serikali kwa maneno yanayoumiza mioyo ya Watanzania wengi. Je, ni kweli kwamba viongozi wa nchi hii wamekosa utu kiasi kwamba wakimwona Mtanzania mgonjwa au mwenye tatizo lolote nje ya nchi viongozi hao wataagiza serikali isimsaidie kwa sababu tu familia yake haijaomba rasmi serikalini?

Je, spika Ndugai ialipotibiwa nje ya nchi familia yake ilikuwa imeomba serikali imtibu? Kama viongozi wa nchi hii kweli walikuwa wanamjali Lissu na wakawa wanataka atibiwe kwa nini hawakupeleka michango ya wabunge kwenye hospitali Lissu anapotibwa? Mambo serikali iliyoyafanya tangu Lissu ashambuliwe yamewafanya Watanzania wengi sana waumizwe mioyo sana.

Kulikuwa na sababu gani ya kuwazuia wapenzi wa Lissu wasimwombee? Kulikuwa na sababu gani ya kukamata vijana waliokuwa wanasaidia kutoa damu kwa sababu tu walikuwa wamevaa fulana za "tumwombee Lissu"? Je, ina maana waliokataza Lissu asiombewe walikuwa hawataki Lissu aombewe ili apone?
 
Kwa hiyo Mzee Sitta naye alikuwa mbunge? Nijuavyo na kwa kumbukumbu zangu mzee Sitta amefarki akiwa siyo mbunge.
 
Ni sawa kabisa utaratibu huu upo hata kwa watumishi wengine usipofuata mfumo Wa serikali ujigharamie hata awe rais. Mabadiriko hayawezi kuanza kwa lissu lazima utaratibu ufuatwe huku tukizingatia kubana matumizi
Of course logic ya serikali kutogharamia matibabu ya Lisu ipo japo hawiweki wazi, eti unaanzaje kumtibia mtu ambaye mara kadhaa umesema hastahili kuishi????
 
Ni mwendelezo uleule wa dhihaka kwa mgonjwa na kwa watanzania. naye ni binadamu kuna siku ataonja machungu fulani.
 
Akili yako imejaa chuki na uuaji , unawezaje kulinganisha tukio la Tindu Lissu la kupigwa risasi na ugonjwa wa mzee Sitta???!!!
 
Kauli za sirikale ya umi. Ona hapa:
1. Huyu Lissu ni mchochezi
2. Huyu Lissu hana nia njema na taifa
3. Huyu Lissu amesababisha Bombadier ikamatwe Canada
4. Huyu ni msaliti vitani na hastahili kuishi kabisa
5. Pole Lissu kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana
6. Lissu hatuwezi kumtibu nje ya nchi hadi Muhimbili washindwe na watupatia rufaa
7. Lissu yupo nje ya utaratibu wa serikali hivyo hatuna cha kumsaidia
8. Watu wanaochangia matibabu ya Lissu wapo hatarini kutapeliwa
9. Tupo tayari kumtibu Lissu popote pale ili mradi tu familia yake ituandikie barua ya maombi.
10. Hatuwezi kumtibu Lissu aliyeenda Nairobi kinyume na utaratibu wa serikali.

Tunasubiri keshoUmmy atasemaje, maana mzee wake kule Arusha kasema alisukumizwa tu kwenye hicho cheo alichonacho. Tuwalaumu waliomsukumiza. Ni akina Lubuva, Januari, Bashite, n.k.
 
Mawaziri wengine sijui hata wameokotwa wapi. Huyu waziri wa afya alithubutu mwaka jana kuita waandishi habari kwa lengo moja tu: kukanusha habari za upungufu wa dawa katika hospitali za umma!

Fikiria ubashite wa kiwango hicho! Siku chache baadaye Makamu wa Rais akapata nafasi ya kurekebisha hiyo kauli ya kipuuzi. Waziri anayejua dhamana aliyonayo wala asingezungumzia hadharani hili suala la serikali kugharamia matibabu ya Lissu wakati huu ambapo imechelewa sana. Badala yake, hili ni suala dogo tu la maafisa wa wizara kwenda kuzungumza na familia ya Lissu na kukubaliana kuhusu matibabu kwa gharama ya serikali; fullstop.
 
Ni sawa kabisa utaratibu huu upo hata kwa watumishi wengine usipofuata mfumo Wa serikali ujigharamie hata awe rais. Mabadiriko hayawezi kuanza kwa lissu lazima utaratibu ufuatwe huku tukizingatia kubana matumizi
kama ingekuwa ishu ni hiyo, basi mbona wala tusingekuwa tunaongelea haya? maana barua ingeandikwa siku ile ile na serikali inge-take over. lakini walikataa kabisa, na ndio maana hawajakanusha hilo. haya maelezo yanakuja baadaye baada ya kuumbuka
 
Ni sawa kabisa utaratibu huu upo hata kwa watumishi wengine usipofuata mfumo Wa serikali ujigharamie hata awe rais. Mabadiriko hayawezi kuanza kwa lissu lazima utaratibu ufuatwe huku tukizingatia kubana matumizi
Kwani kupayuka kule kuna MTU aliwaomba msaada wa matibabu wao serikali...!!!? Wananchi tutamtibia wenyewe na hela yetu ya vitumbua wenyewe waendelee na uwongo wao majukwaani...shame on you Ummy
 
..kichwa cha habari hapo juu kinahusika.

..Mh.Ummy Mwalimu ndiye aliyetoa uamuzi kwamba serikali haitalipia ndege wale matibabu ya TL Nairobi.

..Sijui kama Ummy Mwalimu aliweza kumwangalia usoni mke wa Tundu Lissu usiku ule pale uwanja wa ndege Dodoma. Na kama alimwangalia sijui alijisikia vipi.

..Je, hakuguswa na hali aliyokuwa nayo Tundu Lissu? Je nafsi yake ilimtuma kwamba taratibu ni muhimu kuliko maisha ya mtu?

..Ule ulikuwa ni uamuzi mbaya. Huenda Mh.Ummy Mwalimu aliogopa KUTUMBULIWA kama angechukua uamuzi kwa niaba ya serikali kulipia usafiri na matibabu ya TL Nairobi.

..Kwa maana hiyo Mh.Ummy Mwalimu aliona ni bora kulinda cheo chake kuliko kuokoa maisha ya mbunge mwenzake, mwanasheria mwenzake, Tundu Antipas Lissu.

..Sasa haitoshi Mh.Ummy Mwalimu kujitokeza baada ya wiki mbili na "KUTENGUA" uamuzi wake wa awali kuwa serikali haitahusika na kumsafirisha wala kumtibu Tundu Lissu Nairobi.

..Si vizuri kuiweka familia ya TL katika mvutano huu baina ya serikali na CDM. Mh.Ummy Mwalimu muonee huruma Mama Alicia Lissu, mke wa TL. Kabla ya kumuamrisha Mama Alicia Lissu akuandikie barua ya maombi ya matibabu ya mumewe ni vizuri ukaweka sawa mahusiano ya serikali na CDM[wanaomhudumia TL mpaka sasa hivi].

..Ombi langu ni hili: MHESHIMIWA UMMY MWALIMU OMBA RADHI. SAY THAT YOU MADE A BAD DECISION AND YOU ARE SORRY.

CC Nguruvi3, BAK, Nyani Ngabu, Mbase1970 , Mag3, @
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom