Umeshawahi kunusurika kifo? Tuelezane ilivyokuwa, kama njia ya kumshukuru Mungu

Wakati bado niko mdogo nilikwenda kumtembelea bibi yangu aliekuwa akiishi mkoani Singida maeneo ya saranda.

Bwana kuzoea kidogo pale nikawa na rafiki yeye michezo yake kudandia treni likiwa linakuja mpk litakaposimama ndio anashuka na kujiskia raha/msela.

Sasa bwana sikuhiyo na mimi nikaenda kama siku 2 hivi nilifanikiwa na kuja kujisifu sisi ni masela.

Siku hiyo nakumbuka tumesubiri treni limetoka manyoni linashuka mlima ilikuwa usiku wa saa 2 tumevizia nikakamata chuma nipande weee bwana wee nilitereza miguu ikanasa nikawa nabembea kama tumbili huku chuma imekamata reli mteremko ule asee sijui Mungu aliniponyaje mpka leo sielewi nilijikuta chini ninatoka damu mwili umechubuka vibaya asee nilikaa hospitali muda mrefu ila nilipona. Siku hiyo nilijua ndio mwisho wangu.
Nimecheka kwa sababu bado umzima,pole Sana mkuu.
 
Da mi nakumbuka,mwili ulitaka ukate pumzi bila kunitaarifu.kuna dawa za kikohozi za watoto,huwa na rangi ya zambarau afu tamu kinoma huwa naiba za dogo na kupiga fundo Kisha nasepa.age Kama ya 12 ivi,bana we mshua Kuna day akaweka salimia ya kuchua alipata maumivu,baada ya kumaliza si akaweka juu ya kabati.mi sijui hili wala lile nikaipitia na kuchomoa kwenye boksi,nikapiga tarumbeta fasta wasinishtukie.wakuu kilichonitokea Mungu anajua .joto likapanda,jicho likanitoka nikaenda kulala,salimia bado inafanya yake tumboni.ikabid nimchane bi mkubwa .anipeleka hospital wakanipiga mi drip na dawa flan sikumbuki jina.tokea siku ile rangi ya zambarau kwenye chupa Sina hamu nayo
 
Nilopokua form two nilikkswa koswa na gari kubwa kama si kujiongeza ungekuta nshasahaulika mudaaaa,nilikua na wenzangu watatu kama mnavyojua morogoro road ya zamani two way alafu service road ndogoo sa Mimi nilikua pemben natembea ubavuni kuna Yale machuma ya kuzuia gari lisiende bondeni wait tunatembea tulikua wanne majamaa wote wakahama site waaenda nne ya chuma mi nikabak natembea ndani Mara gafla nikasikia Lori linapiga honi nyingi kwa nyuma kugeuka bahat nzur niligeuka mwili mzima huku nimeegemea lile chuma, kuangalia naona Lori lipo spid limewasha full alafu linaikwangua ile chuma no space ,niajikuta tu ninebinuka nje ya chuma miguu juu lori likapita na moto wake,

Ila niliumia kiuno maana nilidondokea kwenye vile vitofali hadi leo nahis maumivu kwa mbaali ,wenzangu walishika kichwa mpaka tukasahau kama tulikua tunatoka shule au tunaenda shule,sitoisahau ile siku na lile eneo ni mbezi stendi mita kidog stendi mpya, Na ni mahali watu wamekufa sana hapo

Bado tena kati ya wale jamaa zangu nae alikoswa koswa na lori ubungo yale yanayoelekea chuo kikuu ,ilikua ni kama cm 10 tu bro mmoja akamfuta shaaap kama mshale bila vile tairi zilikua zimpitie
 
Dah! Nimekujibu kwa urefu Bushmamy but comment haijatokea, naona uvivu kurudia, kwa ufupi narudia.
Tukiwa chini ya miaka 7, mimi na watoto wa dada tulishauriana tukaoge mtoni wakati wazazi wetu wakiwa shambani.
Kwa bahati mbaya kina cha maji kiliongezeka kutokana na mvua. Tulipofika mtoni, ile sehemu ambayo huwa tunaingilia tukaona maji ni mengi zaidi halafu yana kasi.
Tukamwambia dogo ambaye alikuwa na miaka minne hivi abakie pale pale, kisha sisi tuzunguke upande wa pili kupitia daraja.
Sasa wakati tumezunguka upande wa pili, ile furaha ya kumwona dada yake na mjomba wake (mimi) upande wa pili, ikamfanya aingie kwenye maji ili atufate.
Sehemu aliyoingia ilikuwa na kina kirefu kwa siku ile kama nilivyosema kutokana na mvua.
Tulishuhudia akiomba tumsaidie huku akienda, alipojaribu kusimama maji yalimpiga ngwala hadi akapotea. Tulitamani tusogee but ilikuwa ni hatari zaidi kwetu. Tukachukua tu nguo zake tukaenda nyumbani kutoa taarifa.
Kumbukumbu huwa hazinipotei kabisa kwa sababu alikuwa ndugu na rafiki.
Jamani, sasa maiti ilipatikana? Na nyumbani hilo swala walilipokea Vip? Mamake na huyo mtoto yupo?
 
Aisee sitasahau nikiwa kijana wa miaka 20hivi nihitimu kidato Cha nne nikiwa mtaa tu nasubiri matokeo damu ikiwa inachemka , nagegeda mabinti Kama Nina pepo hivi , Mara nikampa ujauzito mtoto wa watu , wazazi ni moto Atari natafutwa kila Kona, issue ushafika adi polisi, nikaanza maisha ya kukimbia kimbia , nkapoteza dila kabisa, ela Sina adi nkafikia hatua ya kuanza kuunza nguo zangu ili ni survive, niliuza nguo zote nikabaki na kaptura ambayo mwanzo ilikua suruali kabla ya kukatwa km ujuavyo mitoko ya vijana wa mtaan nikiwa pamoja no t short moja tu kuu kuu pamoja na yebo yebo,

Bs sikuhiyo baada ya kutoka pango nililokua nimelala mida ya saa kumi hivi mapema ili watu wasinikute maana nilikua nalala kwenye kibanda flani ambachp hua wanauza nyanya na mazaga mengine, asubuhi hiyo niliwaza kwenda kufua nguo hizo nilizovaa adi zikauke kwenye mto wa jirani , kwa kua sikua nafahamu njia nzuri za kufika nilijikuta nakatisha kwenye nyumba za watu , bahati mbayaa njia niliopita mbele ilikua haiwez kukutoa nkajikuta kwenye geti la mtu, fasta nataka kurudi nilikotoka nakutana na watu wanakuja upande ule nilikokwama nikasikia mmoja akisema mwingine si huyu alijificha huyuu nilijiesemea tu MUNGU NITANGULIE, waliniweka mtu Kati na kuamsha majirani wengine, nilijitetea Sana adi kulia machozi mengi huku nikishikilia miguu ya Mama mmoja hivi nikimuomba anisamehe mm si mwizi nilipotea njia tu, watu walianza kurusha ngumi lakini Yule mama alinionea huruma na kuanza kulia kua wasinipige ikabidi nitaje adi shule niliosoma nilitaja adi walimu na mkuu wa shule pamoja na vilanja bs walinichapa MAKOFI tu na kuniacha niende zangu MUNGU MWEMA sitosahau hii ishu.
Mwisho wa siku ikawaje sasa? Na yule mtoto aliezaliwa ulishawahi kumuona?
 
Da mi nakumbuka,mwili ulitaka ukate pumzi bila kunitaarifu.kuna dawa za kikohozi za watoto,huwa na rangi ya zambarau afu tamu kinoma huwa naiba za dogo na kupiga fundo Kisha nasepa.age Kama ya 12 ivi,bana we mshua Kuna day akaweka salimia ya kuchua alipata maumivu,baada ya kumaliza si akaweka juu ya kabati.mi sijui hili wala lile nikaipitia na kuchomoa kwenye boksi,nikapiga tarumbeta fasta wasinishtukie.wakuu kilichonitokea Mungu anajua .joto likapanda,jicho likanitoka nikaenda kulala,salimia bado inafanya yake tumboni.ikabid nimchane bi mkubwa .anipeleka hospital wakanipiga mi drip na dawa flan sikumbuki jina.tokea siku ile rangi ya zambarau kwenye chupa Sina hamu nayo
 
Mwambie aokoke kabisa atoke humo kwenye michanganyo...maana anaupako huyo sema akiendelea huko atanyonywa upako .
 
Boss hii gari inayochomoka tyre kila wakati ni gari hiyo hiyo? Je ni zile zinaitwa Prado mchaga?
Mkatoliki, sema pia yupo chama fulani cha kitume wakatoliki wanaita "Karismatiki" hawa hawatofautiani sana na walokole namna ya kusali kwao ingawa ipo kwenye ukatoliki.
Kifupi ni mtu wa dini sana.
Fanya services mara kwa mara uzembe wa kutembelea gari mbovu utakuua. Mie naendesha gari mwaka wa 20 sijawahi kuchomokewa tyre
Hacha ujuaji ndugu mambo mengi sio ya ulimwengu huu wanatafutwa na roho za mauti.Ukiona upatwi na hayo maswaiba mshukuru Mungu na ukatoe sadaka ya shukrani kanisani.
 
Ndio mzee nae dini sana (familia yetu na ukoo kiujumla) tunaye hadi Askofu Mkatoliki (japo sitapenda kumtaja jina) kifupi familia na ukoo karibu wote dini tumeishika sana, japo mimi kuna muda hua nateleza as you know ujana una changamoto zake lakini hofu ya Mungu naweza sema ni kubwa sana (nimetumikia utumishi wa altareni zaidi ya miaka 10) huu ndio ulinisaidia kumjua Mungu sana, ilibaki kidogo niende upadri bahati mbaya balehe ikanizidi nguvu
Uokoke Sasa...
 
Jamani, sasa maiti ilipatikana? Na nyumbani hilo swala walilipokea Vip? Mamake na huyo mtoto yupo?
Acha kabisa! Kwanza kumbukumbu huwa hazinitoki jinsi ile siku ilivyoanza toka asubuhi, tulivyoanza kucheza, tulivyoachana na mchezo wa kwanza na kuamua kwenda kuoga. Njia tuliyopita, uchangamfu wa mtoto alionesha siku zile kwa sababu nakumbuka wakati tunaenda, njiani kulikuwa na madimbwi but mtoto alikuwa akiruka hadi tunamsifia, alikuwa na furaha sana kumbe ndio ilikuwa safari ya mwisho.
Tulirudi nyumbani tukiwa wapweke, si watatu kama tulivyoenda bali wawili.
Tulivyofika kwa dada, mwenzangu akaingia ndani kutoa taarifa huku mimi nikisikilizia nje dirishani. Dada alilia kwa uchungu hadi mimi nikakimbia. Habari ziliposambaa kijijini wakaenda kumtafuta, wakamkuta ashakata roho. Kukujibu swali lako la mwisho, mama yake yupo ni dadangu.
 
Mimi ya kwangu hii iIikuwa mwaka 2007 kipindi hicho nipo form two katika mojawapo ya mikoa ya nyanda za juu kusini, siwezi kusahau radi ilivyokosa kunitoa uhai mimi pamoja na baadhi ya wanafunzi wenzangu. Nakumbuka siku hiyo ilikua tupo kwenye foleni ya kupata chakula cha mchana na siku hiyo mvua ilikua inanyesha kubwa sana ambayo ilikua inaambatana na radi kama kuna wenyeji wa hiyo mikoa hasa Njombe wanaweza kuwa mashahidi kule huwa kuna radi za hatari sana.

Wakati nipo kwenye foleni ninachokumbuka niliona mwanga mkali uliombatana na mngurumo wa radi, nilihisi kupigwa na kitu kizito kifuani na kurushwa kutoka pale nilipokua kwenda umbali wa mita kadhaa, baada ya hapo kilicho endelea sikuweza kufahamu zaidi ya kujikuta nipo hospital na drip za maji, nilikaa pale hospital kwa siku mbili nikiendelea kuongezewa maji mwilini pamoja na sindano tena nakumbuka hizi sindano nilikua nachomwa kwenye mishipa ya mikononi na jina lake ni kristapeni, sindano zinauma hizi kamwe siwezi kusahau.

Hili tukio siwezi kulisahu kiukweli sababu mpaka leo ile radi imeniachia baadhi ya makovu hasa maeneo ya kifuani kwa sababu ni kama ilinichubua nikawa na vidonda, nakumbuka walikua wanakuja watu kutoka maeneo jirani kunipa pole kwa sababu ilikua ni kama bahati kusikia mtu amenusurika baada ya kupigwa na radi lakini pia siku hiyo hiyo mimi nilipopigwa radi kuna sehemu ndani ya mkoa huo huo iliua watu wengine wakiwa shambani.

Nakumbuka nilvyorudi shuleni kila mtu hakuwa anaamini kama ningeweza kupona, samahani kwa uandishi mbovu nimeona nijaribu kufupisha sababu ni mengi siwezi kuandika yote hapa.
 
Acha kabisa! Kwanza kumbukumbu huwa hazinitoki jinsi ile siku ilivyoanza toka asubuhi, tulivyoanza kucheza, tulivyoachana na mchezo wa kwanza na kuamua kwenda kuoga. Njia tuliyopita, uchangamfu wa mtoto alionesha siku zile kwa sababu nakumbuka wakati tunaenda, njiani kulikuwa na madimbwi but mtoto alikuwa akiruka hadi tunamsifia, alikuwa na furaha sana kumbe ndio ilikuwa safari ya mwisho.
Tulirudi nyumbani tukiwa wapweke, si watatu kama tulivyoenda bali wawili.
Tulivyofika kwa dada, mwenzangu akaingia ndani kutoa taarifa huku mimi nikisikilizia nje dirishani. Dada alilia kwa uchungu hadi mimi nikakimbia. Habari ziliposambaa kijijini wakaenda kumtafuta, wakamkuta ashakata roho. Kukujibu swali lako la mwisho, mama yake yupo ni dadangu.
Uchungu sana Jamanii, Uwiiii
 
Mie ni last year msiba wa Ruge. .nilienda home kwa wazazi nikanunua dawa moja ya kusafishia tiles na sinks...ni dawa moja Kali sana...iko kwa chupa ya pink hivi...
Kupuuzia MAELEZO mie nikamwaga chini kwa tiles jumba zima..bas nikasema Leo lazima tiles ing'ae coz ilikua imefubaa...msukuma Mimi sikuvaa barakoa puan Wala magotini kufunga zile safety...!
Nikafanya usafi kwa siku mbili mfululizo..
Siku ya 3 macho yakawa red vibaya Sana...mama akaniambia mbona macho mekundu Sana una nn..na inaonekana umepoozaa..nikamwambia hata sijui Tena najiskia homa Kali Sana..bas nikawa najidunga Panadol inapoa...lakini nikawa naumwa Sana mifupa inapasua balaa...sikua najua kitu..bas nikawa najiuliza inamaana asthma term hii imekuja kwa Kasi namna hii? Bas kila masaa yanavyozidi nazidi kuwa weak. .
Siku anayokufa Kibonde(rip) ndo nilihis kufa...nilimtxt mama saa11 aliamka aje aninyanyue room najisikia vby Sana...akaja saa2! Akanishika mkono ulikua wa Moto kuliko maelezo..akanishangaa Sana..nikawa namwambia sijui naumwa nn...maana nilipatwa flu Kali Sana na kichwa kikawa hakisii dawa...Wala homa kushuka...bas nikajua maza atanipeleka hossy
Bahati mbaya msabato yule akaenda kwenye uinjilist wake..nikabaki na dada wakazi ...dingi akaenda shamba...waliniacha sebulen nashangaa shangaa na msiba wa kibonde...
Aisee niliumwa hata kunyanyuka siwez...nikajitupa chini nipate ubaridi...saa8 nikazinduka..kumbe dada kaniita siitiki..akawa amenimwagia maji mwili wote...nikajitahid kumtxt house boy wetu..nikamwambia njoo unipeleke hossy Nakufa...ndo akawajulisha wazaz wakaja Kasi ..mama alianza kulia...hata kuongea nikawa siwez. (Nachokumbuka nilivalishwa nguo sebuleni..Nilikua natokwa povu Sana..nikafikishwa hosp hawaon ugonjwa..nikimuomba nesi anitundikie drip kkwanza(hapo Nampa ishara tu ..majibu ya damu inaonekana nimekula sumu...Sasa hapo akili ikaconnect na Ile dawa..nkajitahid kumwelezea dk nimefanya nn week Hili hom akaelewa akanianzishia sindano na drips nyingi mno! Mle room mama alikua analia ananiask y umekunywa sumu mwanangu nn shida( akaita wasabato wenzake waniombee) nikawaomba msinitingishe Wala kugusa mwili maana mifupa ilikua inapasua mno machizi yanatokea tu balaa.. maana mwili ungeacha roho....lol...dk aliniambia dada ww ulikua unakufa! Since then sitaki kusikia Ile dawa...naisahau jina...!
Sitaki kugusa dawa yenye kiambato Cha sumu teena!
"...bas nikajua maza atanipeleka hossy
Bahati mbaya msabato yule akaenda kwenye uinjilist wake..nikabaki na dada wakazi ..." hii line imenitia hasira sana ingawa ni mama yako.
 
Mimi ya kwangu hii iIikuwa mwaka 2007 kipindi hicho nipo form two katika mojawapo ya mikoa ya nyanda za juu kusini, siwezi kusahau radi ilivyokosa kunitoa uhai mimi pamoja na baadhi ya wanafunzi wenzangu. Nakumbuka siku hiyo ilikua tupo kwenye foleni ya kupata chakula cha mchana na siku hiyo mvua ilikua inanyesha kubwa sana ambayo ilikua inaambatana na radi kama kuna wenyeji wa hiyo mikoa hasa Njombe wanaweza kuwa mashahidi kule huwa kuna radi za hatari sana.

Wakati nipo kwenye foleni ninachokumbuka niliona mwanga mkali uliombatana na mngurumo wa radi, nilihisi kupigwa na kitu kizito kifuani na kurushwa kutoka pale nilipokua kwenda umbali wa mita kadhaa, baada ya hapo kilicho endelea sikuweza kufahamu zaidi ya kujikuta nipo hospital na drip za maji, nilikaa pale hospital kwa siku mbili nikiendelea kuongezewa maji mwilini pamoja na sindano tena nakumbuka hizi sindano nilikua nachomwa kwenye mishipa ya mikononi na jina lake ni kristapeni, sindano zinauma hizi kamwe siwezi kusahau.

Hili tukio siwezi kulisahu kiukweli sababu mpaka leo ile radi imeniachia baadhi ya makovu hasa maeneo ya kifuani kwa sababu ni kama ilinichubua nikawa na vidonda, nakumbuka walikua wanakuja watu kutoka maeneo jirani kunipa pole kwa sababu ilikua ni kama bahati kusikia mtu amenusurika baada ya kupigwa na radi lakini pia siku hiyo hiyo mimi nilipopigwa radi kuna sehemu ndani ya mkoa huo huo iliua watu wengine wakiwa shambani.

Nakumbuka nilvyorudi shuleni kila mtu hakuwa anaamini kama ningeweza kupona, samahani kwa uandishi mbovu nimeona nijaribu kufupisha sababu ni mengi siwezi kuandika yote hapa.
Mizimu inayokusimamia ipo imara sana
 
Aisee sitasahau nikiwa kijana wa miaka 20hivi nihitimu kidato Cha nne nikiwa mtaa tu nasubiri matokeo damu ikiwa inachemka , nagegeda mabinti Kama Nina pepo hivi , Mara nikampa ujauzito mtoto wa watu , wazazi ni moto Atari natafutwa kila Kona, issue ushafika adi polisi, nikaanza maisha ya kukimbia kimbia , nkapoteza dila kabisa, ela Sina adi nkafikia hatua ya kuanza kuunza nguo zangu ili ni survive, niliuza nguo zote nikabaki na kaptura ambayo mwanzo ilikua suruali kabla ya kukatwa km ujuavyo mitoko ya vijana wa mtaan nikiwa pamoja no t short moja tu kuu kuu pamoja na yebo yebo,

Bs sikuhiyo baada ya kutoka pango nililokua nimelala mida ya saa kumi hivi mapema ili watu wasinikute maana nilikua nalala kwenye kibanda flani ambachp hua wanauza nyanya na mazaga mengine, asubuhi hiyo niliwaza kwenda kufua nguo hizo nilizovaa adi zikauke kwenye mto wa jirani , kwa kua sikua nafahamu njia nzuri za kufika nilijikuta nakatisha kwenye nyumba za watu , bahati mbayaa njia niliopita mbele ilikua haiwez kukutoa nkajikuta kwenye geti la mtu, fasta nataka kurudi nilikotoka nakutana na watu wanakuja upande ule nilikokwama nikasikia mmoja akisema mwingine si huyu alijificha huyuu nilijiesemea tu MUNGU NITANGULIE, waliniweka mtu Kati na kuamsha majirani wengine, nilijitetea Sana adi kulia machozi mengi huku nikishikilia miguu ya Mama mmoja hivi nikimuomba anisamehe mm si mwizi nilipotea njia tu, watu walianza kurusha ngumi lakini Yule mama alinionea huruma na kuanza kulia kua wasinipige ikabidi nitaje adi shule niliosoma nilitaja adi walimu na mkuu wa shule pamoja na vilanja bs walinichapa MAKOFI tu na kuniacha niende zangu MUNGU MWEMA sitosahau hii ishu.
pole sana.vipi kuhusu huyo demu uliyempa mimba?
 
Sitasahau mwaka 2017 Kuna siku tulienda kuogelea , hotel Fulani ya Kinondoni nimesahau jina kunasweaming pool.
Kufika pale tukakutana na watu, wengine wako pembeni ya pool wachache ndo wanaogelea.

Mimi nikafika nakurukia pool, nisichokijua kumbe lile sweaming pool linakina kirefu hatari. Yani nilizama chini naibuka, naona watu pembeni lakini nikiita sijui ndo hawasikii. Nazama chini naibuka Hadi Mara ya mwisho ndo pumzi imekata kabisa Yani naona nakufaaa.

Ghafla naona watu wawili wamenikamata hapo nishakata tamaa maana Kila nikijaribu kuomba msaada nazamishwa chini. Wakanidaka na kuniweka pembeni, Pumzi ilikuwa ishakata nahema kwa shida. Ule kwangu Ni ushuhuda nilimuona Mungu kwa macho yangu.

Hadi Leo sitaki kuona mto, bahari wala sweaming pool. Yani hata kwenye Tv nikiona natetemeka.
ulipata wapi ujasiri wa kujirusha sweeming pool wakati kuogelea huwezi?
 
Acha kabisa! Kwanza kumbukumbu huwa hazinitoki jinsi ile siku ilivyoanza toka asubuhi, tulivyoanza kucheza, tulivyoachana na mchezo wa kwanza na kuamua kwenda kuoga. Njia tuliyopita, uchangamfu wa mtoto alionesha siku zile kwa sababu nakumbuka wakati tunaenda, njiani kulikuwa na madimbwi but mtoto alikuwa akiruka hadi tunamsifia, alikuwa na furaha sana kumbe ndio ilikuwa safari ya mwisho.
Tulirudi nyumbani tukiwa wapweke, si watatu kama tulivyoenda bali wawili.
Tulivyofika kwa dada, mwenzangu akaingia ndani kutoa taarifa huku mimi nikisikilizia nje dirishani. Dada alilia kwa uchungu hadi mimi nikakimbia. Habari ziliposambaa kijijini wakaenda kumtafuta, wakamkuta ashakata roho. Kukujibu swali lako la mwisho, mama yake yupo ni dadangu.
duh!!!! sister hali yake vipi now?? umeshawahi kuongra naye kuhusu hiyo issue?
 
Back
Top Bottom