Umeshawahi kunusurika kifo? Tuelezane ilivyokuwa, kama njia ya kumshukuru Mungu

Mimi ya kwangu hii iIikuwa mwaka 2007 kipindi hicho nipo form two katika mojawapo ya mikoa ya nyanda za juu kusini, siwezi kusahau radi ilivyokosa kunitoa uhai mimi pamoja na baadhi ya wanafunzi wenzangu. Nakumbuka siku hiyo ilikua tupo kwenye foleni ya kupata chakula cha mchana na siku hiyo mvua ilikua inanyesha kubwa sana ambayo ilikua inaambatana na radi kama kuna wenyeji wa hiyo mikoa hasa Njombe wanaweza kuwa mashahidi kule huwa kuna radi za hatari sana.

Wakati nipo kwenye foleni ninachokumbuka niliona mwanga mkali uliombatana na mngurumo wa radi, nilihisi kupigwa na kitu kizito kifuani na kurushwa kutoka pale nilipokua kwenda umbali wa mita kadhaa, baada ya hapo kilicho endelea sikuweza kufahamu zaidi ya kujikuta nipo hospital na drip za maji, nilikaa pale hospital kwa siku mbili nikiendelea kuongezewa maji mwilini pamoja na sindano tena nakumbuka hizi sindano nilikua nachomwa kwenye mishipa ya mikononi na jina lake ni kristapeni, sindano zinauma hizi kamwe siwezi kusahau.

Hili tukio siwezi kulisahu kiukweli sababu mpaka leo ile radi imeniachia baadhi ya makovu hasa maeneo ya kifuani kwa sababu ni kama ilinichubua nikawa na vidonda, nakumbuka walikua wanakuja watu kutoka maeneo jirani kunipa pole kwa sababu ilikua ni kama bahati kusikia mtu amenusurika baada ya kupigwa na radi lakini pia siku hiyo hiyo mimi nilipopigwa radi kuna sehemu ndani ya mkoa huo huo iliua watu wengine wakiwa shambani.

Nakumbuka nilvyorudi shuleni kila mtu hakuwa anaamini kama ningeweza kupona, samahani kwa uandishi mbovu nimeona nijaribu kufupisha sababu ni mengi siwezi kuandika yote hapa.
Pole Sana.haukupata ulemavu wowote?
 
Acha kabisa! Kwanza kumbukumbu huwa hazinitoki jinsi ile siku ilivyoanza toka asubuhi, tulivyoanza kucheza, tulivyoachana na mchezo wa kwanza na kuamua kwenda kuoga. Njia tuliyopita, uchangamfu wa mtoto alionesha siku zile kwa sababu nakumbuka wakati tunaenda, njiani kulikuwa na madimbwi but mtoto alikuwa akiruka hadi tunamsifia, alikuwa na furaha sana kumbe ndio ilikuwa safari ya mwisho.
Tulirudi nyumbani tukiwa wapweke, si watatu kama tulivyoenda bali wawili.
Tulivyofika kwa dada, mwenzangu akaingia ndani kutoa taarifa huku mimi nikisikilizia nje dirishani. Dada alilia kwa uchungu hadi mimi nikakimbia. Habari ziliposambaa kijijini wakaenda kumtafuta, wakamkuta ashakata roho. Kukujibu swali lako la mwisho, mama yake yupo ni dadangu.
hali ya dada ako ipoje saizi? umeshawahi kuiongea na yeye kuhusu hii ishu
 
Da mi nakumbuka,mwili ulitaka ukate pumzi bila kunitaarifu.kuna dawa za kikohozi za watoto,huwa na rangi ya zambarau afu tamu kinoma huwa naiba za dogo na kupiga fundo Kisha nasepa.age Kama ya 12 ivi,bana we mshua Kuna day akaweka salimia ya kuchua alipata maumivu,baada ya kumaliza si akaweka juu ya kabati.mi sijui hili wala lile nikaipitia na kuchomoa kwenye boksi,nikapiga tarumbeta fasta wasinishtukie.wakuu kilichonitokea Mungu anajua .joto likapanda,jicho likanitoka nikaenda kulala,salimia bado inafanya yake tumboni.ikabid nimchane bi mkubwa .anipeleka hospital wakanipiga mi drip na dawa flan sikumbuki jina.tokea siku ile rangi ya zambarau kwenye chupa Sina hamu nayo
ulinusurika.Mungu Ni Mwema
 
mwaka 2000 sita sahau nilipewa panga nikanoe kwajili ya kukatia mti, wakati nishalinoa narudi home nikawa nalichezea kwa kulitupa chini linaganda kwa kusimama kwenye ardhi,njia nzima ndio ukawa mchezo, ile nakaribia home si nikalitupa tena chini ,,,,,daaa sitasahau panga lile ligonga jiwe likanirudia shingoni, bahaati nzuri likanichapa na upapa kwenye koromeo, nilipata wenge nusu kukata moto....Wiki nzima chakula kikawa hakipiti mwendo wa uji tu' Mungu mkubwa alikunipiga kwenye makali
Mungu Ni Mwema.Pole Sana
 
Ilikua Tarehe 25 ya Mwezi Wa Tano, Sheimh Yahya Husein(R.I.P) alitabiri siku hii ndio itakua simu ya mwisho wa dunia hii.. Kulikua na Bonanza la mpira wa miguu Uwanja wa Social(Staki Shari) Maeneo ya Majumba Sita. Baada ya Bonanza kuisha sjsi wakazi wa Kinyerezi na team yetu tukawa tunajiandaa kuondoka.

Kulikua na Gari aina ya Canter inayobeba maji katika matank makubwa ya lita 1000, Tukiwa tunasubiri matank yajae maji ili tudandie gari ile kwa idadi ile ya watu. Ghafla nikasikia kuitwa kwa mbali ila nikapuuza, Bwana yule alikua kweye gari ndogo akashuka na kunifuata, akanishika bega kisha akaniita kwa jina langu na kuniamuru niongozane nae. Sikumjua yule bwana na sijawahi kumjua mpaka leo. Basi akanipa lifti na stori nyingi sana mpaka nikafika Kinyerezi.

Huku Nyuma gari ilimaliza kujaza maji na vijana wenzangu wakapanda gari ile, Walikua zaidi ya 15. Baada ya gari kutoka haikumaliza hata KM 1 maeneo ya kabla daraja la kinyerezi gari ile ilipata ajali mbaya sana na wenzetu Tisa wakafariki palepale. Ulikua ni msiba mkubwa sana katika viunga vya kinyerezi. Vijana wadogo sana walipoteza maisha na wachache wakasalimika nikiwemo mimi niliyeokolewa na Malaika yule, Namuita malaika kwa maana sikuwahi kumuona kabla na sidhani kama nitamuona tena. Mungu alinioloa na Nashukuru Mungu.
Mungu Ni Mwema Sana
 
Niliwahi kupanda bus nikiwa nimepewa lift na kondakta ambae ni rafki yangu baada ya muda alikuja kunihamisha ile siti niliyokaa, alaf akakakaa dada mmoja ilikua ni ile siti ya staff pale mbele karibu na mlango,,, haikupita dakika 15 bus ikapinduka miongoni mwa abiria walio fariki alikua Ni yule dada niliyempisha sit akakaa,, Kuna zile chuma za pembezon mwa barabara ndo iliingia ndani ya gar ikamchoma akafa palepale,,,,
huyo konda bado rafiki yako?vipi haukumninulia soda?
 
Sitasahau siku nimepanda juu ya mpela kuchuma mapela nikiwa na watoto wenzangu kijijini kwetu tabora ,ambapo baada ya kupanda na kufika juu kabisa ya mti ndipo nikaona joka kubwa sana likinifata kwa kasi huku likitoa ndimi nje,nashukuru mungu nilijiachia kutoka juu ya mti mpaka chini na nikateguka mkono tu.
Pole Sana . Huyo nyoka mlimuua?
 
Mara ya kwanza tulikuwa watatu tukiwa chini ya miaka 7 tulinusurika kufa maji, tulimpoteza mwenzetu wa miaka minne. Ile picha jinsi alivyokuwa anaomba msaada tumsaidie haijafutika kichwani kabisa japo nimevuka 30 lakini kumbukumbu ni kama tukio la juzi tu.
Mara ya pili radi ilipiga kama mita 15 toka nilipo, ile shoti si ya mchezo, sitaisahau.
Sasa kwanini hamkumsaidia na nyinyi!

Kumbe ndio maana watoto wanapaswa kutandikwa sana viboko!
 
Ilikua Tarehe 25 ya Mwezi Wa Tano, Sheimh Yahya Husein(R.I.P) alitabiri siku hii ndio itakua simu ya mwisho wa dunia hii.. Kulikua na Bonanza la mpira wa miguu Uwanja wa Social(Staki Shari) Maeneo ya Majumba Sita. Baada ya Bonanza kuisha sjsi wakazi wa Kinyerezi na team yetu tukawa tunajiandaa kuondoka.

Kulikua na Gari aina ya Canter inayobeba maji katika matank makubwa ya lita 1000, Tukiwa tunasubiri matank yajae maji ili tudandie gari ile kwa idadi ile ya watu. Ghafla nikasikia kuitwa kwa mbali ila nikapuuza, Bwana yule alikua kweye gari ndogo akashuka na kunifuata, akanishika bega kisha akaniita kwa jina langu na kuniamuru niongozane nae. Sikumjua yule bwana na sijawahi kumjua mpaka leo. Basi akanipa lifti na stori nyingi sana mpaka nikafika Kinyerezi.

Huku Nyuma gari ilimaliza kujaza maji na vijana wenzangu wakapanda gari ile, Walikua zaidi ya 15. Baada ya gari kutoka haikumaliza hata KM 1 maeneo ya kabla daraja la kinyerezi gari ile ilipata ajali mbaya sana na wenzetu Tisa wakafariki palepale. Ulikua ni msiba mkubwa sana katika viunga vya kinyerezi. Vijana wadogo sana walipoteza maisha na wachache wakasalimika nikiwemo mimi niliyeokolewa na Malaika yule, Namuita malaika kwa maana sikuwahi kumuona kabla na sidhani kama nitamuona tena. Mungu alinioloa na Nashukuru Mungu.
Hii ilikuwa ni DE jaVu na time traveling.

You travelled from the future to save yourself.
 


Siku ya tarehe 08/12/2018 ilikuwa siku yangu ya mwisho katika dunia lakini Mungu hakuniacha alinipigania.

Kwenye hii video msemaji alipunguza idadi ya watu, tulikuwa watu nane lakini kwa muda mfupi tulibaki watu wawili tu!!

Mungu ni Mwema , sikuchonwa hata nyuzi moja mwilini.

Mr mkiki.
Mungu Ni Mwema
 
Enzi za u teenager Niliwahi kukutana na Cobra mkubwa kijijini kwetu. Nilikuwa natembea huku naangalia chini na njia za kijijini ni nyembaba huku zikipakana na nyasi ndefu.

Nikiwa natembea na huku nimeangalia chini....ghafla kuna kama sauti ikanena akilini mwangu...kama wazo fulani hivi "angalia unakoenda!"

Ile kuangalia mbele tu...hatua yangu iliyokuwa inafatia nilikuwa naenda kumkanyaga huyu Cobra. Kumbe yeye alikuwa anavuka njia, na aliponiona nazidi kwenda alipo yeye, akasimama.

Ile nimesimama tu, nikiwa na butwaa na sijui cha kufanya, akasimama usawa wa urefu wangu, kichwa chake kikawa kinaangaliana na changu.

Cha kushangaza ni kuwa ile butwaa, au niseme Mungu alini control. Sikuogopa kabisa, akawa ananiangalia kama dakika 3 hivi. Na mimi namuangalia.

Alipoona sifanyi chochote....akaanza kushuka chini taratibu sana....halafu akaanza kwenda kwenye nyasi. Hapo ndipo nikawa kama nimezinduka toka usingizini...woga ukaniingia.

Nilitimua mbio si za nchi hii...huku nikipiga mayowe. Wenzangu niliokuwa nimewatangulia kidogo wakaja mbio mbio wakidhani ni nyoka mdogo. Mmoja akamrushia fimbo...hapo ndipo nilipoona Cobra akifanya maajabu.

Akiwa mbali kidogo na tulipo akasimama kwa mkia wake, akapanda hewani kwa urefu wake, akarusha mate uelekeo wetu. Baada ya kumuona jinsi alivyomkubwa, hakuna aliyetaka tena kwenda kumpiga. Tukaondoka.

Leo hii nikirejea hili tukio naona kabisa Mungu aliniokoa na kiumbe yule mjeuri. Naamini ni Mungu alinena nami akilini kuwa niangalie ninakoenda ili nisimkanyage yule nyoka.

Mungu hutenda makuu, yeye hutusikia tuitapo siku ya hatari. Hutuokoa na hila za adui. I came across a deadly snake and yet i prevailed. It was not by my powers or capabilities but by God's grace.
Mungu Ni Mwema
 
1. Nikiwa na miaka 8 nilianguka kwenye mzambarau mrefu sana, bro mmoja akataka kunidaka akavunjika shingo na bega. Mimi sikupata hata mchubuko.

2. Nikiwa darasa la tatu nilikunywa sumu, ilikua yakuulia sisimizi nyumbani, sikufa, sikuumwa tumbo, wala sikuharisha.

3. Nikiwa darasa la tatu hilo hilo dada yangu aliyekua mlokole na amenizidi miaka 7 alinihakikishia kua ipo siku isiyo na jina wala saa atahakikisha mimi ninatangulia ardhini kabla yake. Mpaka leo bado ni mlokole, yupo hai na mimi ndo hivi tena.

4. Nikiwa darasa la tatu hilohilo nilisaga chupa nikanywa sikufa pia, wala sikupata shida yoyote.

5. Nikiwa darasa la sita, siku natoka kwenye mafundisho ya kipaimara, niliokota pakiti ya ngao ya maji ikiwa haijafunguliwa. Niliendanayo nyumbani nikaificha. Saa mbili usiku nikainywa then nikalala. Asubihi nikaamka nabeua ladha ya ngao. Sikuharisha wala kuumwa kwa namna yoyote na sikufa ndomaana leo naandika hapa.

6. Nikiwa form six nilinusurika kufa kwenye pipe za maji. Kuna channel za maji zilijengwa na wamishenari kutoka milimani kuleta maji shuleni. Zile channel zina kipenyo cha urefu wa rula moja na nusu mpaka mbili (45cm - 60). Kuingia kwakwe ni unacroul kama wanajeshi, na kutoka una croul kinyumenyume. Ili uingie humo lazima ukafunge maji kwenye chanzo. Sisi tulifunga maji na mimi nikaingia kwenye pipe kutoa uchafu ulioingia ukawa unazuia maji kufika shule. Nikiwa nimecroul urefu wa almost mita 10 nilishangaa kuona maji yamekuja ghafla. Kumbe kuna mwanakijiji alikua kwenye chanzo na bila kjjua kama yamefungwa on purpose, akafungua. Nilipona japo sijui niliponaje.
atakuwa huyo dada ako mlokole huwa anakuombea
 
Back
Top Bottom