Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hebu chukulia kwamba, una mtoto ambaye umempeleka shule ya kulala au bweni. Huko anaishi hosteli na sio kwenye bweni. Halafu unashangaa kwamba, maendeleo ya mtoto kitaaluma hayako sawa na pia anaonesha kama hajatulia.
Unapoamua kufuatilia shuleni unabaini kwamba mwanao anahudhuria masomo mara chache sana. Lakini mwaya zaidi unabaini kwamba haishi kwenye Hosteli ambayo ulimlipia kuishi, badala yake unabaini kwamba anaishi na shangingi au Gubeli fulani ambalo limejichubua hadi kwenye ukucha.
Hebu niambie kama ni wewe ambaye umebaini jambo kama hili ungefanya nini? Kumbuka mtoto wako bado ni mdogo akiwa hazidi umri wa miaka 17.