Umasikini wa Watanzania ni wa kujitakia

Umasikini wa Watanzania ni wa kujitakia

William-123

Senior Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
197
Reaction score
94
Sasa nimeamini kuwa umasikini wa Watanzania walio wengi ni wa kujitakia.
Nasema hivi kwa kuangalia jinsi kampeni za uchaguzi zilivyokuwa na jinsi
matokeo yanavyoendelea kutangazwa. Niliamini kuwa sisi watanzania tumetambua
chanzo cha umasikini wetu ni CCM na viongozi wake. Na hii ndio imefanya uchaguzi
wa mwaka huu kuwa wa msisimko mkubwa na hata kuwapa kazi kubwa wazee wa CCM
waliostaafu, vijana wa CCM waliobahatika kupata mrija wa kupata chochote chini
ya CCM na hata wasanii wetu waliolipwa mamilioni ya pesa ili kuwashawishi
masikini waendelee kuichagua CCM. Niliamini tunajitambua na tunaelewa haki yetu ni
nini. Lakini kwa jinsi matokeo yanavyotangazwa, nimeamini kuwa umasikini wetu ni
wa kujitakia.
Ushauri Wangu:
(1) Kama ni kweli hizi kura ni za haki. Kwa kweli mtu yeyote akija kukuomba msaada
kwa maelezo yake kuwa maisha ni magumu. Mtu kama huyu hafai kusaidiwa kabisaaaaaa!
Maana mijini unaweza kutana na mtu anakuomba nauli au pesa ale. Mtu kama huyu
unaweza mfukuza tuu akaombe ofisi za kata.


(2) Vijana wengi wakilalamika kuwa hakuna Ajira. Kwa kweli nitabaki kuwaaangalia na
kuwa support wakiwa kwenye vigenge wanacheza bao.


(3)Wanafunzi wa vyuo wakilalamika mikopo inachelewa. Watu kama hawa unatakiwa kuwaangalia
tuu.


(4)Watu wakisema hamna madawa mahospitalini watu wanalala chini. Ni kuwaangalia na kuwaambia
mmejitakiwa wenyewe kwa kurudisha utawala ambao umeshindwa kuwa support miaka 54.


Kwa ujumla ni kwamba Umasikini wetu utakaoendelea kuwepo Tanzania ni wa kujitakia.
Na nchi itaendelea kunyonywa na kuwafanya wachache kuwa mabepari na matajiri na wengine
kuendelea kuwa masikini. Inasikitishaa sanaa.
Maoni yangu::::
 
Niko Ulaya kwa miaka 12 sasa. Ninafanya kazi yenye kipato kizuri sana. Mara nyingi nimekuwa nikitoa misaada kwa watu mbalimbali wanaoniomba kwa kuwa wana maisha magumu. Nasikitika kusema kuwa tangu sasa nasitisha misaada hiyo rasmi! Watanzania wanajitakia dhiki wao wenyewe.
 
Wote tunafia humohumo? Lakini sio mbaya maake watanzania wengi bado ni wajinga twaazibuni tu, nipo Ruvuma huku naona ndo misukule ya CCM hawajielewi hata kidogo, Kama kuna wanaruvuma waliokomboka akili zao huko washaurini waje wawaelimishe ndugu zao maana ni aibu tu kwa maisha wanayo ishi na kura walizozitoa kwa CCM.
 
Ngudu Croach sijui COARTEM ..!! Nadhani hujanielewa point yangu. Sio kwamba kumsaidia
mtu kulikuwa ni kuwa force wachague chama fulani. Mimi sina chamaaa !!! Maana ya sentensi
zangu hapo juu ni kwamba watu wengi wamekuwa wakilalamika maisha magumu, Mishara midogo,
hamna madawa hospitalini, huduma za afya mbovu, Maji na umeme hakuna sehemu nyingi Tanzinia..
Na hata vikiwepo ni vya katakata mtu akijisikia..!!
Kampeni za mwaka huu watu wameelezwa ukweli kuwa miaka 54 ulitakiwa kuwa hapa na sasa uko hapa.
Angalia huyu ameshachota chake na maisha yake ni mazuri na watoto wake..!! Wewe bado unaendelea
kushabikia hao hao wanaokufanya uishi kwa shida!! Na ndio maana nikasema umasikini ni wa kujitakia.
Kwa wale wote waliokuwa na hali mbaya kimaisha na still kushabikia wanao waumiza..!! Hiyo ndio point
hapa. Wewe kama kiongozi au una mrija sehemu usijiangalie wewe angalia maisha ya watu kwa ujumla
hasa vijijini. Hope umesoma na unauelewa...!!!
 
Sasa nimeamini kuwa umasikini wa Watanzania walio wengi ni wa kujitakia.
Nasema hivi kwa kuangalia jinsi kampeni za uchaguzi zilivyokuwa na jinsi
matokeo yanavyoendelea kutangazwa. Niliamini kuwa sisi watanzania tumetambua
chanzo cha umasikini wetu ni CCM na viongozi wake. Na hii ndio imefanya uchaguzi
wa mwaka huu kuwa wa msisimko mkubwa na hata kuwapa kazi kubwa wazee wa CCM
waliostaafu, vijana wa CCM waliobahatika kupata mrija wa kupata chochote chini
ya CCM na hata wasanii wetu waliolipwa mamilioni ya pesa ili kuwashawishi
masikini waendelee kuichagua CCM. Niliamini tunajitambua na tunaelewa haki yetu ni
nini. Lakini kwa jinsi matokeo yanavyotangazwa, nimeamini kuwa umasikini wetu ni
wa kujitakia.
Ushauri Wangu:
(1) Kama ni kweli hizi kura ni za haki. Kwa kweli mtu yeyote akija kukuomba msaada
kwa maelezo yake kuwa maisha ni magumu. Mtu kama huyu hafai kusaidiwa kabisaaaaaa!
Maana mijini unaweza kutana na mtu anakuomba nauli au pesa ale. Mtu kama huyu
unaweza mfukuza tuu akaombe ofisi za kata.


(2) Vijana wengi wakilalamika kuwa hakuna Ajira. Kwa kweli nitabaki kuwaaangalia na
kuwa support wakiwa kwenye vigenge wanacheza bao.


(3)Wanafunzi wa vyuo wakilalamika mikopo inachelewa. Watu kama hawa unatakiwa kuwaangalia
tuu.


(4)Watu wakisema hamna madawa mahospitalini watu wanalala chini. Ni kuwaangalia na kuwaambia
mmejitakiwa wenyewe kwa kurudisha utawala ambao umeshindwa kuwa support miaka 54.


Kwa ujumla ni kwamba Umasikini wetu utakaoendelea kuwepo Tanzania ni wa kujitakia.
Na nchi itaendelea kunyonywa na kuwafanya wachache kuwa mabepari na matajiri na wengine
kuendelea kuwa masikini. Inasikitishaa sanaa.
Maoni yangu::::

Mjinga ni yule aliyekuwa anaamini Lowassa atamletea kula, Maendeleo yako yataletwa na ww mwenyewe hao viongozi kazi yao ni kukuboreshea miundombinu ya ww kutafuta pesa,
 
Ni kweli kabisa nchii hii mamamuma ni wengi sana shauri yao si wengine alhamudilah maisha yanaendaaa sasa nisikie mgonjwaa ananiambia hana Hela ya kununua dawa nitamchana live
 
Ka ulikua unategemea EL akuletee msoc unajidanganya, yule jamaa hawezi endesha nchi, anaumwa sana jamaa, anasahau sahau kila kitu. Ukawa walikua na tamaa sana kumsimamisha jamaa, wangemsimamisha mtu mwingine msafi angeweza pita kirahisi mno..

Kitu nalaumu watanzania mimi ni kuwapa wabunge wengi sana CCM, ningependa kuona rais Magufuli alafu wabunge wote UKAWA ili apewe challenge ya kutosha.. Sasa wabunge majority wakiwa CCM tunabaki kulekule, watakua wanapeana support wenyewe kwa wenyewe bungeni.
 
Mjinga ni yule aliyekuwa anaamini Lowassa atamletea kula, Maendeleo yako yataletwa na ww mwenyewe hao viongozi kazi yao ni kukuboreshea miundombinu ya ww kutafuta pesa,

Hao viongozi wa fisiem na serekali yao ndo wameshindwa kuboresha hiyo miundombinu ya watu kutafuta pesa, ndio mana Tanzania ni moja kati ya nchi maskini sana duniani kwa kuangalia kipato cha wananchi wake....hata kama wamefanya lakini muda ya miaka 50 hauwiyani na kiwango cha maendeleo waloyaleta.....
 
Wote mnaomuunga mkono mtoa mada ni mambumbumbu hasa. Hivi upinzani huu kweli unaweza kuiletea nchi yetu maendeleo? Hivi nyie mnaijua ccm kweli? Hivi nyie mnamjua Lowassa na madhara aliyoiletea ccm? Hicho mnachokiikita MFUMO mnakielewa? Je, kweli mnadhani Mbowe na genge lake wanadhamira njema na nchi hii? Mnawafahamu walio nyuma ya wapinzani hawa na nia yao? Je, mnajua ni kwanini Lowassa tangu enzi ya Nyerere anakataliwa? Tafuteni kuzijua siasa za Tz.
 
Hao viongozi wa fisiem na serekali yao ndo wameshindwa kuboresha hiyo miundombinu ya watu kutafuta pesa, ndio mana Tanzania ni moja kati ya nchi maskini sana duniani kwa kuangalia kipato cha wananchi wake....hata kama wamefanya lakini muda ya miaka 50 hauwiyani na kiwango cha maendeleo waloyaleta.....

Ww sio Mtanzania ila ni asylum seeker.
Mana =maana
Hauwiyani =hauwiani
Waloyaleta =waliyoyaleta
Kati ya hiyo miaka 50 hakuna kiongoz aliyewahi kutokea kama Dr Magufuri
 
William123 and people alike. Watanzania ni watu we ye upeo mkubwa sana na kwa taarifa yenu hawadanganyiki. Chadema na cuf kwa aina ya viongozi walionao leo huwezi kuwalinganisha na magufuli kwa vipimo vyovyote vile. Kama ni umaskini basi magufuli yuko juu sana. Lowasa na wapambe wake hawawezi kutuondolea umaskini zaidi sana watatuongezea umaskini.
 
Ka ulikua unategemea EL akuletee msoc unajidanganya, yule jamaa hawezi endesha nchi, anaumwa sana jamaa, anasahau sahau kila kitu. Ukawa walikua na tamaa sana kumsimamisha jamaa, wangemsimamisha mtu mwingine msafi angeweza pita kirahisi mno..

Kitu nalaumu watanzania mimi ni kuwapa wabunge wengi sana CCM, ningependa kuona rais Magufuli alafu wabunge wote UKAWA ili apewe challenge ya kutosha.. Sasa wabunge majority wakiwa CCM tunabaki kulekule, watakua wanapeana support wenyewe kwa wenyewe bungeni.
Kama wamewapa wabunge wengi hivi ni nani basi ukawa ingemuweka akashinda? hivi una afiki kafulila,wenje,mkosa mali,machali hawa watu kazi waliyoifanya hawakustahili kurudi bungeni? mara mia wote kama si kafulila escrow tungeijua? hii nchi robo tatu ya wananchi wake hawana elimu, hawajitambui na bado hawajui siasa ni nini katika maisha. wewe ukiwa mmoja wao mnashangaza sana. kama EL hawezi kuleta msosi magufuri ndo atakuletea. toka uzaliwe ulishaletewa msosi hata na diwani?
 
mwanaccm yeyote atakayekuja na vishida vya kujitakia jibu litakuwa.........''Hapa kazi tu ...upate hela''
 
Umenena mleta mada. Inaonyesha dhahiri uliko kidhiri umaskini ndipo wanakoendelea kung'ang'ania Ccm. Duuuuuuuh!wadanganyika bana.
 
Niko Ulaya kwa miaka 12 sasa. Ninafanya kazi yenye kipato kizuri sana. Mara nyingi nimekuwa nikitoa misaada kwa watu mbalimbali wanaoniomba kwa kuwa wana maisha magumu. Nasikitika kusema kuwa tangu sasa nasitisha misaada hiyo rasmi! Watanzania wanajitakia dhiki wao wenyewe.
.

Safi sana. Pia na subiri mtu yeyote atoke huko aseme ccm oyeee halafu aniombe pesa ya kula.
 
Back
Top Bottom