Umasikini unaambukizwa, tuweni makini?

Umasikini unaambukizwa, tuweni makini?

Niwe mkweli , mimi ni mtu wa kipato cha kati. Niliwahi kuoa mwanamke kutoka katika familia ya kipato cha chini. Ilikuwa sipati nafasi hata mara moja ya kukaa mimi na mke wangu tule pamoja mchana. Lazima shemeji ua mama mdogo au baba mdogo lazima waje kumtembelea mke wangu wakati wa kula. Hakuwahi hata siku moja ndugu yangu mimi kuna kwa wakati huo. Ishatokezea mimi mwenye nyumba kukosa chakula kwa sababu ndugu wa mke wangu walikuja wengi kwa pamoja. Na wakitaka kuondoka lazima waombe na nauli. Ninachotaka kusema kila mtu aoe katika daraja yake

huyo mke bado unaye??
 
umaskini ni kushindwa kukidhi mahitaji ya msingi

maana za umaskini ni nyingi ila hiyo ndo inafaa kwa muktadha wa hii mada

ndio maskini hawaachi shule kwasababu ya hela tu, ila hizo sababu zingine nyingi zinahusiana na umaskini

ndio sio wote wanaosoma ni matajiri ila sijasema maskini wote hawasomi

elewa umaskini ni suala mtambuka

mpe shule
 
Niwe mkweli , mimi ni mtu wa kipato cha kati. Niliwahi kuoa mwanamke kutoka katika familia ya kipato cha chini. Ilikuwa sipati nafasi hata mara moja ya kukaa mimi na mke wangu tule pamoja mchana. Lazima shemeji ua mama mdogo au baba mdogo lazima waje kumtembelea mke wangu wakati wa kula. Hakuwahi hata siku moja ndugu yangu mimi kuna kwa wakati huo. Ishatokezea mimi mwenye nyumba kukosa chakula kwa sababu ndugu wa mke wangu walikuja wengi kwa pamoja. Na wakitaka kuondoka lazima waombe na nauli. Ninachotaka kusema kila mtu aoe katika daraja yake
Duh mzee ni balaa.
 
Wakuu,,

Umasikini ni sawa na Ukimwi, fungus, kaswende au Ebola au ugonjwa wa kuambukizwa.

Umasikini unaambukizwa kuweni makini. Kama wewe ni masikini kamwe usifungamane na masikini wala kuoa masikini maana mtaambukizana upele tena kama ni mwanaume utakuwa masikini mara mbili kama tujuavyo wakwe wa mke watakuwa wanakuangalia na wazazi wako na ndugu zako pia.

Tuwe makini, tujikinge na mahusiano tunayoanzisha au tunaooa au kukutana na kushinda nao.

Ni hayo tu kwa leo
Sasa usifungamane na masikini mwenzio ili msiambukizane, je tajiri atakubali umuambukize huo umaskini?
 
Hii ni mada uliyoichukulia kirahisi bila kushirikisha kichwa. Ratio ya maskini na matajiri ni ngapi?
Maskini mara nyingi huwa wanaoana na maskini wenzao. Sasa wewe so called "tajiri" unaogopa kuwa na maskini au kuoa maskini basi utajiri wako sio utajiri bali ni uwezo tu wa kula milo 3 kwa siku.

Tajiri hawezi kuwa na wasiwasi na kuwasaidia upande wa wakwe zake na ukiona una ubahili huo basi wewe sio tajiri ni mbadilisha mboga tu.
🤣🤣🤣
 
Wote viumbe hakuna anayejua hatma yake...Hakuna tajiri pasi kuwepo tabaka la masikini...Kama mnataka kutengana hizo biashara zenu fanyenu wenyewe.

Maskini kama umempenda mwenyewe utaona pamoja na kumfuata ,kwanza maskini hawana shobo kwa sanaa....Matajiri wengi mnajishtukua hamna cha maana.

Sipend kukaa na matajiri kwanza wengi washamba ..
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Wakuu,,

Umasikini ni sawa na Ukimwi, fungus, kaswende au Ebola au ugonjwa wa kuambukizwa.

Umasikini unaambukizwa kuweni makini. Kama wewe ni masikini kamwe usifungamane na masikini wala kuoa masikini maana mtaambukizana upele tena kama ni mwanaume utakuwa masikini mara mbili kama tujuavyo wakwe wa mke watakuwa wanakuangalia na wazazi wako na ndugu zako pia.

Tuwe makini, tujikinge na mahusiano tunayoanzisha au tunaooa au kukutana na kushinda nao.

Ni hayo tu kwa leo
thank you!!,kwa ivo unanishauri niachane na hii kampani yangu ya kugida minazi????,,,manake wengi choka mbaya!!
 
Back
Top Bottom