Sijui sisi watu wa Kagera tuliwakosea nini serikali?
Pamoja na kuwa na kila kitu ila serikali imeufanya mkoa wa Kagera kuja na kuchuma mapato na kuutelekeza
Serikali ipo kutawala na kunyonya mkoa wetu bila kuwekeza chochote
Mkoa wetu unazalisha mazao kama kahawa, ndizi, maharage n k
Tuna madini, uvuvi n k
Mkoa wa Kagera umetoa wasomi na wataalam wengi lakini ni sehemu ambayo imekosa wawakilishi wa kuitetea
1. Huduma za jamii
Ukifika Mleba, Buharamulo, Kyerwa, Bukoba vijijini Kuna sehemu hakuna madarasa, Zahanati, barabara wala maji
2 Usalama
Mkoa wa Kagera tunapakana na nchi 3 yaani Burundi, Rwanda, na Uganda. Ni mkoa ambao una wahamiaji haramu wengi na mapori ya kutisha kama Kasindaga na Kimisi
Serikali iboreshe sehemu hizi
3, Miundo mbinu na mawasiliano.
Mkoa wa Kagera una barabara nyingi za vumbi, huduma ya mawasiliano Iko duni sana na mtandao maeneo mengi haukamati.
Serikali haijajenga barabara za kuunganisha wilaya ya Ngara na Karagwe, Kyerwa na Karagwe, Misenyi na Bukoba
4. Afya
Hospital ya mkoa ukifika utasikitika sana
Wananchi hukimbilia hospital binafsi hasa za kanisa
5. Maji
Serikali imeutelekeza mkoa wetu. Kuna shida kubwa ya maji watu hutembea sio chini ya km 10 kupata ndoo ya maji, Na dumu huuzwa sh 1000 ndoo 1, licha ya kuwa tumepakana na ziwa victoria, mto Kagera, Ziwa Burigi, mto Ruvuvu, Bwawa la Chamchuzi na mabwawa mengine mengi
6. Stend ya mkoa.
Ile stend ya mkoa iliyojengwa mpya ukifika ni vumbi na chafunna ni ovyo sana
7.Serikali imeua sekta ya utalii mkoa wa Kagera
Magufuli alituibia hifadhi yetu ya Burigi na kuita Burigi Chato hivo kulipeleka mkoa wa Geita,
Serikali haitangazi vivutio vyeti vingine vya Ibanda n.k
8 sekta ya madini.
Kuna migodi ya Kabanga nickel na Machimbo ya tin Kyerwa lakini haya yote hawanufaishi wazawa
9. Uvuvi na ufugaji
Sekta ya uvuvi imejifia na mifugo hatuna pa kuchungia
Serikali utazame mkoa wetu Kwa hicho la huruma
Soma Pia: Anguko la uchumi wa mkoa wa Kagera