Umasikini mkoa wa Kagera unaletwa na Serikali

Umasikini mkoa wa Kagera unaletwa na Serikali

Watanzania bhana! Huwa tunaigiza kuwa watu safi lakini chuki zimetujaa ajabu, kinachotubeba kwa kiasi kikubwa kuishi kwa amani ni uoga wetu tu. Tumejawa na ubinafsi, ubaguzi na roho mbaya za kutosha tu ambazo tunawasontea wakazi wa Kagera huku tukijifanya wasafi.

Mkoa wa Kagera na watu wake wanachukiwa ajabu sijapata kuona, ukiuliza sababu ni hizohizo zisizoeleweka. Chuki hizo ni dhahiri kuanzia mitaani hadi mitandaoni. Utasikia ooh wanajivuna/wanaringa/wanajisikia sana! Sasa mtu akijisikia ndo sababu umchukie? kama huna asili ya uchawi wewe tuseme una shida gani nyingine hata uchukie watu kirahisi?

Tazama hapa mtoa mada anazungumzia huduma za kijamii kama afya, maji, umeme, shule, usalama, barabara nk ambazo ni wajibu wa lazima wa serikali kuzifikisha kwa wananchi wote bila ubaguzi wala upendeleo na si hisani. Lakini ukishuka kwenye comments watu wanazungumzia ishu za kurogana, majungu, watu kujifanya matajiri na kutokurudi nyumbani, mara ubinafsi na kujisikia! Yote hayo yanahusiana nini na serikali kutokuwafikishia wananchi huduma muhimu kama afya na elimu kwa ubora kama inavyofanya kwingine ilhali wote ni walipakodi!?

Kwenye nyuzi za mkoa wa Kagera ndipo utawakuta watu wakiitetea na kuikingia kifua serikali kwa kutokutimiza wajibu wake na kufosi kuhamishia makosa kwa wananchi ambao ni wakazi wa mkoa huo.

Baadaye watu hao utawakuta wakijiliza humu na kuilaumu serikali kwa kutokutimiza wajibu wake wa kufikisha huduma hizo katika maeneo mengine! Hapo watakupostia picha za watoto wakisoma chini ya miti au madarasa mabovu ya matope, akina mama wakiteka maji machafu kwenye vidimbwi, barabara mbovu, akina mama wazazi wakilala wanne kitanda kimoja hospitali nk. Hapo serikali itapondwa balaa, sisiem italaaniwa laana zote za ulimwenguni na kuzimu! Sasa jichanganye upost picha za namna hiyo useme za Kagera uone wakazi watakavyogeuziwa kibao na serikali kuonekana haina hatia! Wahenga walisema "kunya anye kuku akinya bata kaharisha"!
ila kwa sisi tuliowahi na ambao bado tunafanya kazi na kuishi na wahaya tunawajua vizuri, ni bora kuishi na fisi kuliko kuishi au kufanya kazi na mhaya, kuna mmoja alikuwa HR hapa kazini,
juzi kamwambia mwenye kampuni ana elimu ndogo ndiyo maana ni mzito kuelewa,
mchagga wa watu akamwambia tu sawa, ngoja nitafute wajinga wenzangu nifanye nao kazi,
Na kazi ikaishia hapo.
 
Kagera imedumazwa na wana Kagera wenyewe! Wamesoma lakini wamejenga mikoa mingine!
 
Hivi unajua kwamba mipango ya Maendeleo ya wilaya inapangwa na Na nani, Ni Baraza la madiwani ndio wanaohusika na sio wateule wa Rais, kazi ya wateule wa Rais ni Kumentain laws and order. Hao Madiwani wenu ndo muwalaum na siyo serikali.
Hiyo mipango haipo wilaya zote ila kwingine Tanzania ndo ipo
 
Kagera imedumazwa na wana Kagera wenyewe! Wamesoma lakini wamejenga mikoa mingine!
Kujenga mikoa mwingine ndo serikali isipeleke Kagera huduma za jamii kama afya, elimu, maji, barabara
 
Huu mkoa pamoja na kuwa na wasomi wengi lakini upo nyuma sana kimaendeleo kulinganisha na mikoa mingine
Hilo ni tatizo kubwa la mkoa huo,kuna maprofesa fulani uko kiziba wanashindana tu kujenga mijengo,lkn kuishi humo hawana mpango wao ni dar au USA baasi,huko kijijini wanaacha watumishi au majirani ndo wawe wanawaangalizia,hakuna uwekezaji wowote hata wa mashine yakusaga unga,ili na wengine wanufaike.
 
Tanzania nzima Serikali yetu kuna mambo haifanyi sawa hasa kupitia watumishi wake ambao wamepewa mamlaka ya kuwasaidia wakulima, wanafanya biashara na na wajasiriamali ambao ndio walipa kodi na chachu ya maendeleo nchi yetu inanuka rushwa na uvivu kwa wanaoisaidia Serikali kutimiza wajibu wake, la mwisho wana Kagera mjitahidi kulima mna vishamba vidogo sana
 
Hilo ni tatizo kubwa la mkoa huo,kuna maprofesa fulani uko kiziba wanashindana tu kujenga mijengo,lkn kuishi humo hawana mpango wao ni dar au USA baasi,huko kijijini wanaacha watumishi au majirani ndo wawe wanawaangalizia,hakuna uwekezaji wowote hata wa mashine yakusaga unga,ili na wengine wanufaike.
Inabidi wabadilike
 
Sijui sisi watu wa Kagera tuliwakosea nini serikali?

Pamoja na kuwa na kila kitu ila serikali imeufanya mkoa wa Kagera kuja na kuchuma mapato na kuutelekeza

Serikali ipo kutawala na kunyonya mkoa wetu bila kuwekeza chochote

Mkoa wetu unazalisha mazao kama kahawa, ndizi, maharage n k

Tuna madini, uvuvi n k

Mkoa wa Kagera umetoa wasomi na wataalam wengi lakini ni sehemu ambayo imekosa wawakilishi wa kuitetea

1. Huduma za jamii
Ukifika Mleba, Buharamulo, Kyerwa, Bukoba vijijini Kuna sehemu hakuna madarasa, Zahanati, barabara wala maji

2 Usalama
Mkoa wa Kagera tunapakana na nchi 3 yaani Burundi, Rwanda, na Uganda. Ni mkoa ambao una wahamiaji haramu wengi na mapori ya kutisha kama Kasindaga na Kimisi
Serikali iboreshe sehemu hizi

3, Miundo mbinu na mawasiliano.
Mkoa wa Kagera una barabara nyingi za vumbi, huduma ya mawasiliano Iko duni sana na mtandao maeneo mengi haukamati.

Serikali haijajenga barabara za kuunganisha wilaya ya Ngara na Karagwe, Kyerwa na Karagwe, Misenyi na Bukoba

4. Afya
Hospital ya mkoa ukifika utasikitika sana
Wananchi hukimbilia hospital binafsi hasa za kanisa

5. Maji
Serikali imeutelekeza mkoa wetu. Kuna shida kubwa ya maji watu hutembea sio chini ya km 10 kupata ndoo ya maji, Na dumu huuzwa sh 1000 ndoo 1, licha ya kuwa tumepakana na ziwa victoria, mto Kagera, Ziwa Burigi, mto Ruvuvu, Bwawa la Chamchuzi na mabwawa mengine mengi

6. Stend ya mkoa.
Ile stend ya mkoa iliyojengwa mpya ukifika ni vumbi na chafunna ni ovyo sana

7.Serikali imeua sekta ya utalii mkoa wa Kagera

Magufuli alituibia hifadhi yetu ya Burigi na kuita Burigi Chato hivo kulipeleka mkoa wa Geita,
Serikali haitangazi vivutio vyeti vingine vya Ibanda n.k

8 sekta ya madini.
Kuna migodi ya Kabanga nickel na Machimbo ya tin Kyerwa lakini haya yote hawanufaishi wazawa

9. Uvuvi na ufugaji
Sekta ya uvuvi imejifia na mifugo hatuna pa kuchungia

Serikali utazame mkoa wetu Kwa hicho la huruma

Soma Pia: Anguko la uchumi wa mkoa wa Kagera
tatizo wakazi wengi wa mkoa wa kagera ni machawa
 
Sijui sisi watu wa Kagera tuliwakosea nini serikali?

Pamoja na kuwa na kila kitu ila serikali imeufanya mkoa wa Kagera kuja na kuchuma mapato na kuutelekeza

Serikali ipo kutawala na kunyonya mkoa wetu bila kuwekeza chochote

Mkoa wetu unazalisha mazao kama kahawa, ndizi, maharage n k

Tuna madini, uvuvi n k

Mkoa wa Kagera umetoa wasomi na wataalam wengi lakini ni sehemu ambayo imekosa wawakilishi wa kuitetea

1. Huduma za jamii
Ukifika Mleba, Buharamulo, Kyerwa, Bukoba vijijini Kuna sehemu hakuna madarasa, Zahanati, barabara wala maji

2 Usalama
Mkoa wa Kagera tunapakana na nchi 3 yaani Burundi, Rwanda, na Uganda. Ni mkoa ambao una wahamiaji haramu wengi na mapori ya kutisha kama Kasindaga na Kimisi
Serikali iboreshe sehemu hizi

3, Miundo mbinu na mawasiliano.
Mkoa wa Kagera una barabara nyingi za vumbi, huduma ya mawasiliano Iko duni sana na mtandao maeneo mengi haukamati.

Serikali haijajenga barabara za kuunganisha wilaya ya Ngara na Karagwe, Kyerwa na Karagwe, Misenyi na Bukoba

4. Afya
Hospital ya mkoa ukifika utasikitika sana
Wananchi hukimbilia hospital binafsi hasa za kanisa

5. Maji
Serikali imeutelekeza mkoa wetu. Kuna shida kubwa ya maji watu hutembea sio chini ya km 10 kupata ndoo ya maji, Na dumu huuzwa sh 1000 ndoo 1, licha ya kuwa tumepakana na ziwa victoria, mto Kagera, Ziwa Burigi, mto Ruvuvu, Bwawa la Chamchuzi na mabwawa mengine mengi

6. Stend ya mkoa.
Ile stend ya mkoa iliyojengwa mpya ukifika ni vumbi na chafunna ni ovyo sana

7.Serikali imeua sekta ya utalii mkoa wa Kagera

Magufuli alituibia hifadhi yetu ya Burigi na kuita Burigi Chato hivo kulipeleka mkoa wa Geita,
Serikali haitangazi vivutio vyeti vingine vya Ibanda n.k

8 sekta ya madini.
Kuna migodi ya Kabanga nickel na Machimbo ya tin Kyerwa lakini haya yote hawanufaishi wazawa

9. Uvuvi na ufugaji
Sekta ya uvuvi imejifia na mifugo hatuna pa kuchungia

Serikali utazame mkoa wetu Kwa hicho la huruma

Soma Pia: Anguko la uchumi wa mkoa wa Kagera
Bukoba = ka Re jenairo😀😀😀
 
Back
Top Bottom