Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
CCM imezidi kujidhihirisha zaidi kama chama kinachoongoza kwa kufuata siasa za Umafia. Mfululizo wa viroja vya CCM vya hivi karibuni vinatoa picha ya wazi bila kubakiza shaka yoyote.
Baada ya jaribio la Makamba la siasa za majitaka ya Ngono kupuuzwa na wapiga kura na ku-backfire vilivyo kuwarudia wao wenyewe, sasa CCM wameendelea na mhimili wao mkuu wa Umafia wa kisiasa kutangaza sms za hisia za vita. Shimbo alianzisha hili na sasa limeunganishwa barabara na SMS hizo za kimafia.
Msururu wa vitendo vya kimafia vya CCM dhidi ya wananchi ni mrefu na ulianzia siku nyingi ikiwemo kitendo cha kujaribu kuhusisha kifo cha Chacha Wangwe na CHADEMA. CHADEMA wamejitahidi sana kuirudisha CCM kutoka siasa za maji taka kuwa siasa za kutangaza sera na kulinda maslahi ya Tanzania na kuendeleza nchi. CHADEMA walimudu umafia wa CCM kuhusu kifo cha Chacha Wangwe, pia wamemuda umafia wa siasa za CCM za Ngono, sasa limekuja hili la sms za kimafia.
Umafia ni fani ya CCM na tunajua hawataishia hapo hadi umafia huo utaingia kwenye sanduku la kupiga kura. Na CCM watataka kulazimisha kutangazwa mshindi wa kiti cha uraisi anayetarajiwa kushindwa badala ya Dr. Slaa ambaye amekubalika kwa Wananchi. CCM imekuwa sasa si chama cha siasa bali ni kikundi cha wanyang'anyi.
Lakini nguvu ya umma itaushinda umafia huu wa CCM na Dr. Slaa atakuwa rais wa awamu ya tano kwa uamuzi halali wa wananchi kupitia sanduku la kura.
Baada ya jaribio la Makamba la siasa za majitaka ya Ngono kupuuzwa na wapiga kura na ku-backfire vilivyo kuwarudia wao wenyewe, sasa CCM wameendelea na mhimili wao mkuu wa Umafia wa kisiasa kutangaza sms za hisia za vita. Shimbo alianzisha hili na sasa limeunganishwa barabara na SMS hizo za kimafia.
Msururu wa vitendo vya kimafia vya CCM dhidi ya wananchi ni mrefu na ulianzia siku nyingi ikiwemo kitendo cha kujaribu kuhusisha kifo cha Chacha Wangwe na CHADEMA. CHADEMA wamejitahidi sana kuirudisha CCM kutoka siasa za maji taka kuwa siasa za kutangaza sera na kulinda maslahi ya Tanzania na kuendeleza nchi. CHADEMA walimudu umafia wa CCM kuhusu kifo cha Chacha Wangwe, pia wamemuda umafia wa siasa za CCM za Ngono, sasa limekuja hili la sms za kimafia.
Umafia ni fani ya CCM na tunajua hawataishia hapo hadi umafia huo utaingia kwenye sanduku la kupiga kura. Na CCM watataka kulazimisha kutangazwa mshindi wa kiti cha uraisi anayetarajiwa kushindwa badala ya Dr. Slaa ambaye amekubalika kwa Wananchi. CCM imekuwa sasa si chama cha siasa bali ni kikundi cha wanyang'anyi.
Lakini nguvu ya umma itaushinda umafia huu wa CCM na Dr. Slaa atakuwa rais wa awamu ya tano kwa uamuzi halali wa wananchi kupitia sanduku la kura.