KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 18,132
- 32,835
Habari za jumamosi wapendwa.
Bila ya shaka sote tu wazima wa afya na walio na maradhi Mungu awaangazie warudi kwenye afya zao.
Sote tunajua kuwa ukuaji wa teknolojia umeleta manufaa kwenye jamii zetu hata imekuwa rahisi kupashana habari na kurahisisha shughuli mbalimbali za kijamii. Bila ya kusahau ukuaji wa teknolojia kwa kiasi kikubwa kumewafanya watu kuwa karibu na hivyo kuifanya dunia kuwa kama kijiji kimoja.
Lakini kwa upande wa pili ukuaji wa teknolojia umeleta changamoto kwenye suala zima la mahusiano kiasi kwamba kiwango cha uaminifu kwenye ndoa au kwenye mahusiano kimeporomoka tangu kukua kwa teknolojia. Kwa upande mwingine, umeongeza uaminifu ingawa ni kwa wachache.
Je wewe mdau wangu ungependa kushare nasi mara ya kwanza ulipopekua au kuchunguza simu ya mpenzi wako au mkeo uligundua nini na pengine ulichukua hatua gani baada ya tukio hilo?
Karibuni sana
Bila ya shaka sote tu wazima wa afya na walio na maradhi Mungu awaangazie warudi kwenye afya zao.
Sote tunajua kuwa ukuaji wa teknolojia umeleta manufaa kwenye jamii zetu hata imekuwa rahisi kupashana habari na kurahisisha shughuli mbalimbali za kijamii. Bila ya kusahau ukuaji wa teknolojia kwa kiasi kikubwa kumewafanya watu kuwa karibu na hivyo kuifanya dunia kuwa kama kijiji kimoja.
Lakini kwa upande wa pili ukuaji wa teknolojia umeleta changamoto kwenye suala zima la mahusiano kiasi kwamba kiwango cha uaminifu kwenye ndoa au kwenye mahusiano kimeporomoka tangu kukua kwa teknolojia. Kwa upande mwingine, umeongeza uaminifu ingawa ni kwa wachache.
Je wewe mdau wangu ungependa kushare nasi mara ya kwanza ulipopekua au kuchunguza simu ya mpenzi wako au mkeo uligundua nini na pengine ulichukua hatua gani baada ya tukio hilo?
Karibuni sana