Ulishawahi kununua kitu baadaye ukagundua umeuziwa bei kubwa?

LA7

JF-Expert Member
Aug 26, 2019
457
1,725
Kuna wakati huwa inauma sana, baada ya kununua kitu halafu ukirudi mtaani mtu akikuuliza bei uliyonunulia ukamtajia halafu akakwambia mbona umeuziwa bei kubwa hivo na wakati zinauzwa tu bei rahisi.

Nimewahi kutana na mambo Kama haya kwa nyakati tofauti.

Nimewahi uziwa begi Kariakoo 40 baada ya kufika nyumbani kuna jirani akaniambia kuwa huwa zinauzwa 25 tu

Pia nimewahi katiwa tiketi na madalali kwa 25 baadae nikaona abiria wengine wakikatiwa kwenye basi kwa 15 kutoka itula to tabora mjini.

Funzo:
Hii ipo hasa kwenye biashara mfano. Mwaka jana nilitoka kijijini kwenda mjini kwa ajili ya kufanya manunuzi ya vifaa vya umeme vya mteja wangu, nikiwa ndo kazi yangu ya Kwanza ya wring ya umeme.

Basi nikaenda duka la Kwanza kuulizia menu switch jamaa akaniambia 80 mwisho 70.

Nikashtuka baada ya kuona mbona hela haitatosha kabisa kununua vitu vingine, maana niliulizia kwa mtu mmoja jumla ya pesa aliyotoa kusukiwa umeme, akaniambia alitoa 180 wring ya taa 3 na soketi 1 basi bhana nikaenda duka la pili.

Jamaa akaniambia ni 25 dah! Nikawaza sana ni watu wangapi hufanyiwa hivo, nikagundua ni wengi ila pia mfanyabiashara wa aina hiyo ni ngumu kufanikiwa zaidi kibiashara.

Fikiria angeweza kunifanya mm kuwa mteja wake wa kudumu ila yeye akanifukuza mazima.

Tusiwe na tamaa kwani waweza muona mtu hajui kitu ila siku akijua hutamuona tena, na sio kila mteja huwa ni mpita njia was siku moja tu. Hapana tujitahidi kutoa huduma nzuri.

Mimi ni fundi electronics najitahidi kutoa huduma isiyokandamizi, ndo maana nimeweza kutengeneza wateja wa kudumu.
 
Wewe unafuatilia bei ya nini wakati ulishatatua shida yako?
Umetoka kununua simu maybe kwa 250k then unakutana na mtu anauza simu kama hiyohiyo kwa 150k unaanza kujilaumu bila kujua sometimes things happens for the reason, Pengine hiyo simu ya 150k safari yake ya kuwa hai ni kesho asubuhi labda inapaswa kuanguka na kukanyagwa na gari? Au labda imepangwa itamilikiwa na fulani ambae sio wewe ndo ile unashangaa umeporwa na wahuni anaenda kuuziwa mtu ambae ilipaswa yeye ndo aimiliki.

Ni hayo tu kama umenielewa baridi.
 
Nilishanunua G SHOCK kwa 120k,halafu kuna jamaa nikamkuta anayo kali kuliko yangu,ina compass,gps,water resistance nk...
nilipomuuliza bei,akanambia amenunua 65k halafu mtumba..
 
Wewe unafuatilia bei ya nini wakati ulishatatua shida yako?
Umetoka kununua simu maybe kwa 250k then unakutana na mtu anauza simu kama hiyohiyo kwa 150k unaanza kujilaumu bila kujua sometimes things happens for the reason, Pengine hiyo simu ya 150k safari yake ya kuwa hai ni kesho asubuhi labda inapaswa kuanguka na kukanyagwa na gari? Au labda imepangwa itamilikiwa na fulani ambae sio wewe ndo ile unashangaa umeporwa na wahuni anaenda kuuziwa mtu ambae ilipaswa yeye ndo aimiliki.

Ni hayo tu kama umenielewa baridi.
Unaongea vitu kinadharia Sana. Sio lazima ufuatilie bei ndio ujue kuwa umepigwa mfano kwenye hiyo ishu ya bei ya tiketi hakuwa anafuatilia ila akagundua amepigwa! Hizo habari kwamba huenda iliyouzwa bei ndogo ikaharibika kesho hazina mashiko, unaweza ukauziwa bei kubwa Leo na kesho kikaharibika vile vile!
 
Kuna wakati huwa inauma sana, baada ya kununua kitu halafu ukirudi mtaani mtu akikuuliza bei uliyonunulia ukamtajia halafu akakwambia mbona umeuziwa bei kubwa hivo na wakati zinauzwa tu bei rahisi,

Nimewahi kutana na mambo Kama haya kwa nyakati tofauti,

Nimewahi uziwa begi kariakoo 40 baada ya kufika nyumbani kuna jirani akaniambia kuwa huwa zinauzwa 25 tu

Pia nimewahi katiwa tiketi na madalali kwa 25 baadae nikaona abiria wengine wakikatiwa kwenye basi kwa 15 kutoka itula to tabora mjini,

Funzo:
Hii ipo hasa kwenye biashara mfano. Mwaka jana nilitoka kijijini kwenda mjini kwa ajili ya kufanya manunuzi ya vifaa vya umeme vya mteja wangu, nikiwa ndo kazi yangu ya Kwanza ya wring ya umeme,

Basi nikaenda duka la Kwanza kuulizia menu switch jamaa akaniambia 80 mwisho 70,

Nikashtuka baada ya kuona mbona hela haitatosha kabisa kununua vitu vingine, maana niliulizia kwa mtu mmoja jumla ya pesa aliyotoa kusukiwa umeme, akaniambia alitoa 180 wring ya taa 3 na soketi 1 basi bhana nikaenda duka la pili,

Jamaa akaniambia ni 25 dah! Nikawaza sana ni watu wangapi hufanyiwa hivo, nikagundua ni wengi ila pia mfanyabiashara wa aina hiyo ni ngumu kufanikiwa zaidi kibiashara,

Fikiria angeweza kunifanya mm kuwa mteja wake wa kudumu ila yeye akanifukuza mazima

Tusiwe na tamaa kwani waweza muona mtu hajui kitu ila siku akijua hutamuona Tena, na sio kila mteja huwa ni mpita njia was siku moja tu. Hapana tujitahidi kutoa huduma nzuri,

Mm ni fundi electronics najitahidi kutoa huduma isiyokandamizi, ndo maana niwmeweza kutengeneza wateja wa kudumu.
Hapo kwenye vifaa vya umeme kuna feki na original, so usikomae na bei tu
 
Asa unaumia nini mfamo,umekamata hela ngapi maishani mwako,na aliyekurangua hafiki popote,maana ni mwizi
 
Unakutana na madalali wanakuwa sio wamiliki wa hayo maduka

Nilishawajulia nikiulizwa nina shilingi ngapi, nashusha bei chini sana mpaka aje mwenye duka mwenyewe

usiende kununua kitu hujui bei, lazima uulize bei kitaani kwanza
 
Unaongea vitu kinadharia Sana. Sio lazima ufuatilie bei ndio ujue kuwa umepigwa mfano kwenye hiyo ishu ya bei ya tiketi hakuwa anafuatilia ila akagundua amepigwa! Hizo habari kwamba huenda iliyouzwa bei ndogo ikaharibika kesho hazina mashiko, unaweza ukauziwa bei kubwa Leo na kesho kikaharibika vile vile!
so then what ukishajua uliuziwa bei kubwa?, Alafu kama hujui chochote kuhusu nadhararia niliyoisema huwezi kunielewa, Sometimes dig deep kwanza, Jifunze na utafakari zaidi kuhusu maisha ndo uwe unajibu deep thoughts kama hizi.
 
Main switch ya 25,000 inakuwa na ubora gani hiyo au ni ndogo. Huwa sinunui kitu cha bei ya chini sana kulingana na bei ya soko, najua kuna walakini hasa kama kipo technical, kiafya au kina sheria nyuma yake. Mimi sio mjinga, najua biashara fulani haiwezi lipa kwa bei hii, ili hii bei ifikiwe lazima quality au quantity iwe compromised.
Siwezi enda mjini let's say Kariakoo kwa mamantilie aniuzie wali wa 2,000 najua kwa uhalisia wa sasa hiyo bei haimlipi ili iweze kumlipa lazima afanye kitu ambacho matokeo yake hasi nitayaona.

Alafu sipendi kujilinganisha na watu, lengo langu kwenye manunuzi ni kuwa satisfied sio kushindana na wanunuzi wengine. Nikiwa na shida ya dawa ya jino, ukanipa kwa 40,000 na nikapona, I don't give a damn fck ukimpa mwingine dawa hiyohiyo kwa 25,000. Lengo langu halikuwa ligi ya kununua dawa, lilikuwa kupona jino na limetimia. Na hela nilitoa sababu niliimudu na nimeridhika.

Huwa sipo price sensitive sana huwa nazingatia quality na after sales service kama warranty na servicing.

Mambo mengine ni kujua range ya bei ya unachotaka kabla haujaenda kununua na kujiuliza justification ya bei ya huduma au bidhaa, kuna vitu huwa nakataa kununua nikijiuliza justification yake hata kama nitapewa ofa. Kitu hakina craftsmanship, high-end technology nyuma kwamba inahitaji research kubwa na certification, kipo simple to manufacture alafu kinauzwa bei na sio cha lazima sinunui. Kitu kingine nakinunua kwa appreciation ya nguvu iliyotumika nyuma.
Cheni iliyoundwa na sonara kwa mkono wake nitainunua ghali kuliko cheni iliyofyatuliwa kiwandani China. Hii imeundwa kwa siku nzima, nyingine ni mojawapo ya cheni 12,000 zilizofyatuliwa siku moja. Navaa nikijua kuna skills zilizokuwa mastered kwa miaka, jasho la mtu na dedication yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom