Da'Vinci
JF-Expert Member
- Dec 1, 2016
- 35,690
- 106,830
Vizuri sana mkuu.. nimejifunza kitu.Baada ya kumaliza chuo yeye alipata kazi dar mimi nikapata mkoani. Mwana yupo alishaoa na ana Watoto wawili kwa Sasa..alikujapata mke Mrembo sana. Wakati wakiwa wachumba nilibahatika kukutana nao mlimani city... Baada ya kunitambulisha tu mwana akanivuta pembeni akaniambia...mwana huyu ndo nataka kuweka ndani pls usifanye kama yule mwingine. Nikamjibu...ondoa shaka mwana...mpaka harusi yao nilihudhuria na mwana alitaka niwe best man wake mimi nikakataa.
Tuliendelea kuwa karibu...kila nikija dar nilikuwa nawatembelea maana makazi yangu yalikuwa dar. Badae nilipunguza tabia ya kuwatembelea sana maana kuna kitu nilihisi kinaweza kutokea.
Kimsingi mimi na mwana ni rika moja ila mwana ana utoto Fulani na mimi nilikuwa naonekana nimepevuka zaidi yake. Kwa hyo tukiwa Kwenye mazungumzo mimi nilikuwa nasikilizwa zaidi. Hata mke wake alikuwaga anayapa attention sana mazungumzo yangu. Kwa hyo nikahisi kinaweza tokea kitu..ikabidi nipunguze mawasiliano nao.
Badae mimi nilihamia mkoa kabisa kwa hyo kukitana nikawa haipo tena...tunawasiliana kwa simu tu...ila nikifika dar huwa nawatembelea
Mwana bado ni kitombi na hata mke wake anajua...sema mke anampenda na anapenda familia yake kwa hyo vitu vingine anavumilia tu.
Napenda sana watu wakae kirafiki.. Hongera sana