Miaka kadhaa nyuma nikiwa jobless baada ya kumaliza hii mnayoita elimu ya juu, nikawa naishi kwa braza ili kuangalia namna ya kuendesha maisha.
Ikafika muda wa kumpeleka mtoto wake shule katika mkoa mmoja wa kaskazini mwa hii nchi yetu kubwa. Nikapewa hili jukumu la kumsindikiza huyu dogo shule, ukiwa jobless ukipewa jukumu walau unajisikia vizuri kama mwanajamii.
Basi baada ya kukamilisha taratibu zote, nikawa nipo na dogo kwenye basi Ubungo bus terminal kwa ajili ya kuanza safari. Dakika chache akaingia dada mmoja akiwa na mtoto wa kiume, akanisalimu na kisha walikaa siti ya pembeni yangu tukitengwa na korido.
Tukiwa safarini hawa madogo wakaanza kama kuzoeana hivi kiasi cha kuongea na kuanza kupeana vitu kama biscuits na tambi.
Tukajikuta mimi na huyu dada tunatazamana lakini bila kuongea chochote. Maeneo ya Lugoba basi ikaingia kwenye sehemu ya kupata huduma za chakula na huduma za maliwato.
Dada akaniambia anaomba nimsaidie kuongozana na mtoto aliyekuwa naye kwenye vyoo vya wanaume. Baada ya kumaliza, nikawa nafanya utaratibu wa kununua chakula na vinywaji kwa ajili yangu na kwa ajili ya hawa madogo.
Kurudi kwenye gari nikawapanga hawa madogo kwenye siti mbili za upande mmoja na mimi nikakaa siti moja ya upande mwingine, dada akarudi akiwa na mifuko ya chakula na vinywaji na kukuta nimeshabadili mpago wa kukaa. Hili la kubadili mpango wa kukaa nililifanya kimkakati kabisa.
Akiwa anashangaa nikainuka ili kumpisha apite siti ya dirishani,alinishukuru kisha akasema ''naona watoto wameshazoeana na wameamua kukaa siti moja''.
Kuanzia hapo sasa tukawa kama familia moja, stori mbili tatu nikajua kuwa yule ni mtoto wa dada yake naye pia anamsindikiza shule japo ni shule tofauti.
Baada ya stori mbili tatu tukawa tupo comfortable sana, huku vicheko na vitendo vya kushawishiana vikishamiri, Katika safari mara kadhaa katika mazungumzo dada alikuwa ananilalia na mimi nikajiongeza kwa kucheza na mkono wake huku nikiminyaminya viganja vyake, papasa mgongo mpaka ikafika mahali akaniambia naona unatafuta password. Tukajikuta tunacheka tu.
Hatimaye tulifika jioni kiasi na kukuta wawakilishi wa shule husika wakiwa wanatusubiri. Mimi nikamkabidhi dogo kwa mwakilishi wa shule yake na dada naye akamkabidhi dogo kwa mwakilishi wa shule aliyekuja kumpokea.
Tukabaki tunaangaliana, dada akauliza wewe mwenyeji kidogo hapa. Nikamwambia ndio, kisha nikamuuliza una mpango wa kurudi Dar kesho tufanye mpango wa kukata tiketi kabisa? Dada akajifikiria kisha akasema, hapana mpaka keshokutwa hivi nataka walau nitembee kidogo katika huu mji.
Kwa kuwa nilikuwa naujua vizuri huu mkoa kwa kuwa niliwahi kufika hapa mara kadhaa, nikamwongoza dada mpaka kwenye Lodge moja classic karibu kabisa na stendi. Tumefika mapokezi naona dada ameketi kwenye siti huku akiwa hana habari. Nikafanya malipo ya chumba na kisha nikampa ishara huku tukiongozana na mhudumu.
Kufika room, dada akajitupa kitandani akilalama kuhusu uchovu wa safari lakini pia baridi, mimi nikaingia bafuni kuoga, nimetoka nikabadili nguo, dada naye akaingia bafuni na kuanza kuoga.
Ametoka bafuni akabadili nguo kwa kujifichaficha huku akiniambia ‘’fumba macho usije kuota bure’’.
Tukaenda kupata chakula cha usiku huku dada akisistiza kulipa yeye, tumemaliza kula tukarudi room huku wote tukiwa kimya.
Kufika room kila mmoja akawa anakitamani kitanda, mimi nikatangulia kuingia kwenye blanket baada ya muda dada naye akajisogeza ndani ya blanket akiwa na pajama na tshirt.
Akanipa mgongo ukiwa akiniuliza maswali mawili matatu, baada ya muda akageuka tukawa tunatazama, nikasogeza mkono na kuweka chini ya shavu la huyu binti huku mkono mwingine ukitalii kwenye mgongo wa huyu binti kuelekea kwenye bambataa.
Binti akajisogeza tukaanza kubadilishana mate kwa ufundi wa hali ya juu, huku nikiwa nimehama mgongoni nikipapasa vilima viwili vilivyosimama vyema juu ya kifua cha huyu dada.
Hii michezo iliendelea mpaka tukajikuta tupo watupu na tukifurahia kitendo adhimu cha kupeana raha.
Kwa baridi la ule mkoa kwa kweli zile siku mbili ililkuwa ni furaha tu. Nikajua nimepata mpenzi, binti akaniweka wazi kuwa ameshatolewa mahari.
Tumerudi mjini hapa akaendelea kunipa tunda bila hiyana japo nilikuwa jobless.
Baada ya muda nikajikuta mwenye kundi la whatsapp la send off ya huyu dada nikitambulishwa kama rafiki. Hatimaye binti aliolewa, pazia likafungwa.