Uliona wapi bidhaa inajitembeza mitaani kusifu mnunuzi wake?

Uliona wapi bidhaa inajitembeza mitaani kusifu mnunuzi wake?

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,814
Reaction score
40,420
Mkiambiwa tumerudi enzi za Sultani Mangungo wa Msovero muwe mnakubali, msibishe maana mnayoyafanya hayana tofauti na enzi hizo. Tumesoma kwenye vitabu vya historia kwamba Waafrika wenzetu waliokuwa na nafasi enzi hizo za utumwa waliwapigia Debe matajiri wanunuzi wa Watumwa na kuwapa sifa za uzuri wa America kusini na maeneo mengine walikokuwa wanapelekwa. Kwa namna hiyo Watumwa wengine walijipeleka wenyewe na kuuzwa Kwa Hiari ili wakafaidi maisha Ulaya.

Sisi Wenye Mali ndo tumeuza au basi tukubali tumewakodisha DPW bandari zetu. Iweje Sisi ndo tunazunguka duniani kueleza uzuri wa DP-World badala ya wao au nchi nyingine ambayo iliwahi kuingia nao mkataba ijitokeze kutueleza uzuri wao?

Hebu wafungaji nisaidieni, unakwenda mnadani kuuza Ng'ombe wa familia, anatokea mnunuzi lakini Hana fedha taslimu anaomba umkopeshe na wewe unakubali unamwachia Ng'ombe. Unaporudi nyumbani unaanza kulaumiwa na ndugu zako unaanza kumsifia mnunuzi ambaye umeonana naye mnadani Kwa mara ya Kwanza?

Bora basi wauzaji waliowahi kufanya naye Biashara wangejitokeza kumsifu lakini eti wewe kuwathibitishia ndugu zako unakwenda nyumbani Kwa mkopaji unawapigia simu ndugu zako unaweka simu loud speaker halafu mkopaji anaanza kujisifu jinsi alivyo mwaminifu na mlipaji mzuri wa madeni? Hao ndugu zako wakikubaliana na huo usanii basi haziwatoshi.

Screenshot_2023-06-21-12-41-30-463_com.twitter.android.jpg
 
Kila mtu anongelea kitu asichokijua.
Waziri kila siku anatoa maelezo hadharani, wautu wameshikilia pale pale kuwa tumeuzwa,
Waziri anasema Mkataba unaihusu Bandari Salam tuu
Tena Gati 1,2,3,4,5,6,7 tuu
Tena Gati ya Mafuta haimo,
Yadi ya Magar na container haimo,
Bandari zote zikochini ya TPA pamoja na DSM bali Uendeshaji ndio utakuwa chini ya DP World.
Sasa sijui watu wanataka nini tena.
Serikali ilifanya mambo memngine kimkakati iwe siri kwa sababu Kenya, na Msumbiji wanania kama ya kwetu kuwekeza katika secta ya Bandari ili kuboresha usafirishaji kwa nchi za kaiikati.
Anaye wahi kawahi.
Lakini Watanzania yetu ni Porojona Ujuaji mwingi.

Mkapa kaipa Bandari yetu campuni TSCAN kwa miaka 22 iliyopita na kiwango hakikupanda sana lakini kiliongeza ufanisi kiasi fulani.
sasa leo tunaboresha watu Fye fye fe.
Uzwazwa umetushika na woga wa kijinga.
Kila mtu kawa Mtaalamu
 
Hii safari ya Dubai Kuna uwezekano mkubwa ikawa imefadhiliwa na wakubwa wanaopush mkataba ili wazidi kutulainisha watz.

Kadili wanavyotumia nguvu kubwa kuzidi kutuaminisha watanzania kuhusu hii inshu ya DP world ndivyo inavyokuwa rahisi kuzidi kubaini kwamba hapa Kuna harufu ya ufisadi na u-chief mangungo.

Ila huyu kitenge...
 
Hebu msikilizeniwaziri kisha niambieni tatizo liko wapi?
Au tunajazba za kuburuzwa tuu
 

Attachments

  • __UFAFANUZI_KUHUSU_UWEKEZAJI_WA_BANDARI_ZA_TANZANIA_BARA_NA_ZANZIBAR,_WAZIRI_MBARAWA_AELEZA(36...mp4
    13.8 MB
Kila mtu anongelea kitu asichokijua.
Waziri kila siku anatoa maelezo hadharani, wautu wameshikilia pale pale kuwa tumeuzwa,
Waziri anasema Mkataba unaihusu Bandari Salam tuu
Tena Gati 1,2,3,4,5,6,7 tuu
Tena Gati ya Mafuta haimo,
Yadi ya Magar na container haimo,
Bandari zote zikochini ya TPA pamoja na DSM bali Uendeshaji ndio utakuwa chini ya DP World.
Sasa sijui watu wanataka nini tena.
Serikali ilifanya mambo memngine kimkakati iwe siri kwa sababu Kenya, na Msumbiji wanania kama ya kwetu kuwekeza katika secta ya Bandari ili kuboresha usafirishaji kwa nchi za kaiikati.
Anaye wahi kawahi.
Lakini Watanzania yetu ni Porojona Ujuaji mwingi.

Mkapa kaipa Bandari yetu campuni TSCAN kwa miaka 22 iliyopita na kiwango hakikupanda sana lakini kiliongeza ufanisi kiasi fulani.
sasa leo tunaboresha watu Fye fye fe.
Uzwazwa umetushika na woga wa kijinga.
Kila mtu kawa Mtaalamu
Kwani DP yupo pekee yake duniani anayetoa huduma hiyo? Aje mwekezaji mwingine, do tumemkataa.
 
Back
Top Bottom