Ulinzi wa geti kwenye biashara

Ulinzi wa geti kwenye biashara

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,197
Reaction score
14,890
Habari zenu Wakuu,

Mimi ni mfanya biashara na nina fremu yangu mahali, sasa kuna jirani yangu amevunjiwa fremu yake na wezi na imepelekea na sisi wafanyabiashara wengine tuwe na wasiwasi kuhusu hilo tukio.

Yeye alievunjiwa ni ana geti na huwa anafunga na kufuri tu, lakini wamekata zile tundu za kuingizia kufuli na kuingia Dukani kwake.

Hapa shop kwangu namimi nina geti kama lake, sasa nilikuwa nafikiria kuweka kitasa kwenye geti langu ili niwe nafunga na kufuli pamoja na kitasa.

Wakuu nikiweka kitasa cha geti kitasaidia, au na hicho wezi wanambinu ya kukivunja?

NITASHUKURU MKINIJIBU
 
Wezi ni watu wabaya, jirani hapa kuna mageti na katika harakati za kubomoa na walikate waya wa umeme na kusababisha shoti, mafrem matatu yaliungua na hakikuokolewa hata kitu.

Maana hakuna mlinzi, alfajiri watu wapita njia ndiyo waliona.
 
Wezi ni wabaya, kwangu nawaweka daraja moja na wachawi tu.
Mtu mwizi simpendi kiukweli.

Hapo ufanye mpango wa mlinzi tu, pigeni donation(donee) kila mtu akitoa sh 30 kwa mwezi, mnamuungia jamaa anawalindia.
Upo sahihi, na asante kwa mchango wako Mkuu.
 
Habari zenu Wakuu,

Mimi ni mfanya biashara na nina fremu yangu mahali, sasa kuna jirani yangu amevunjiwa fremu yake na wezi na imepelekea na sisi wafanyabiashara wengine tuwe na wasiwasi kuhusu hilo tukio.

Yeye alievunjiwa ni ana geti na huwa anafunga na kufuri tu, lakini wamekata zile tundu za kuingizia kufuli na kuingia Dukani kwake.

Hapa shop kwangu namimi nina geti kama lake, sasa nilikuwa nafikiria kuweka kitasa kwenye geti langu ili niwe nafunga na kufuli pamoja na kitasa.

Wakuu nikiweka kitasa cha geti kitasaidia, au na hicho wezi wanambinu ya kukivunja?


NITASHUKURU MKINIJIBU
Wana master key
 
Weka kitasa kwa ndani alafu na nje unafunga kwa makufuli mazito
Kitasa ndio ilikuwa option kwang, lakini kuna mchangiaji mmoja hapo kasema kuwa wezi wanatumia Master Key

Dah! Ni mtihani kwakweli.
 
Hii mbaya sana, kijana anaweza kudhurika na hao wezi au hata short ya umeme.. sio vizuri kabisa
Ni kweli pia,

Kuna mkinga tumempangisha aisee duka stoo pia limejaa na analalaga mwenyewe nawazaga likitokea la kutokea itakuwaje

Mungu aepushe,l
 
Upo sahihi Mkuu, lakini inshu ya kuweka mlinzi ni kwamba Fremu zetu zipo mbalimbali, yani ni kila mtu kwenye makazi yake binafsi. Changamoto nyengine ni udogo wa biashara zetu kumuweka mlinzi.
Ulinzi shirikishi ni chief option mkiwapa vijana ten ten wapige doria vibaka wqkijua Kuna ulinzi wanapunguza speed ata kama walinzi wenyewe wanalalaga muda mwingi
 
Wezi ni wabaya, kwangu nawaweka daraja moja na wachawi tu.
Mtu mwizi simpendi kiukweli.

Hapo ufanye mpango wa mlinzi tu, pigeni donation(donee) kila mtu akitoa sh 30 kwa mwezi, mnamuungia jamaa anawalindia.
Mkuu hivi hawa wezi has vibaka wa usiku wanatumia uchawi? Kwasababu sijawahi Sikia wanakamatwa. Na kama kukamatwa mara chache.

Yani ukikaa ufikirie binadamu unatoa wapi ujasiri na kumvamia mtu kumuibia na kuharibu vitu.
 
Back
Top Bottom