Nahitaji ushauri wa biashara ya Pharmacy

PYD

Senior Member
Jun 9, 2020
107
151
Habari za muda huu wakubwa.

Mimi ni kijana wa kiume ambae nimebahatika kupata sehemu yangu ya urithi toka kwa wazee wangu ambapo nimepata milioni 30.

Nilikua naomba wazoefu, watu mnaoifanya hii biashara tusaidiane kwenye mambo kadhaa juu ya hii biashara kama eneo, mbinu za kuongeza mauzo, nk.

Kwanini nimeomba ushauri juu ya kufungua pharmacy tu jibu ni sababu ni taaluma yangu(Pharmaceutical Technician), naipenda, nina uzoefu na ujuzi wa kuuza dawa japo sijawahi kufanya biashara yoyote ile ya kwangu ndo nataka kuanza.

Kwasasa nimeajiriwa kwenye community pharmacy flani Tanga Mjini. Nimefanya utafiti wangu kwa huu mji naona kama sitafikia malengo ya mauzo mazuri ukizingatia kuna wingi wa pharmacy za jumla, aina ya wakazi wake wamekariri baadhi ya maduka kua ndio yenye dawa za bei nafuu tu, wingi wa pharmacy mpya katikati ya mji(hapa ikumbukwe Tanga sio kubwa kwa mjini ambapo unaweza ukazunguka kwa masaa kadhaa ukaumaliza).

Kinachoniumiza ni location maana hapa najua hua ni kila kitu katika hii biashara ni wapi niende? Eneo/mkoa gani? Hali ya kiuchumi ya huo mkoa/eneo? Je miundombinu za usafirishaji kwenye hilo eneo/mkoa ukoje kama nikifanya order ya dawa zitachukua mda gani hadi zinifikie? Unafuu wa dawa nk.

Muuzaji nitakua mimi mwenyewe japo nilikua nafikiria kuajiri mtu wa jinsia ya kike mwenye dispensing certificate kubalance gender ili kutokosa baadhi wa wateja ambao hua hawako huru kuelezea tatizo lake hasa la baadhi ya magonjwa kwa mhudumu ambae sio wa jinsia yake.(hili nimelishuhudia mtu anaondoka kabisa kwakuona aibu)

Hivyo gharama kubwa itabaki kwa mfamasia ambae nitatumia cheti chake, mashelf, milango na karabati nyinginezo, kodi pamoja na kuagiza mzigo.

Nawaza hadi kichwa kinapata moto wakuu, nipeni mawili matatu wenye uzoefu na hii biashara hapahapa au hata ikiwa PM pia sawa nitashukuru sana.

Asanteni.

1619256485074.png
 
Mi nakushauri kwa kuwa uko Tanga ni bora uanzia hapo hapo sababu ni mahali ambapo umeshatambua changamoto zake kuliko kuanza eneo au mkoa ambao wewe mwenyewe ni mgeni itakuchukua muda kidogo kujiweka sawa

Dawa kama ilivyo biashara nyingine yeyote inahitaji bidii binafsi na kujituma, nikupongeze kwa hatua hiyo ya uwekezaji

Kila la heri kiongozi
 
Mi nakushauri kwa kuwa uko Tanga ni bora uanzia hapo hapo sababu ni mahali ambapo umeshatambua changamoto zake kuliko kuanza eneo au mkoa ambao wewe mwenyewe ni mgeni itakuchukua muda kidogo kujiweka sawa

Dawa kama ilivyo biashara nyingine yeyote inahitaji bidii binafsi na kujituma, nikupongeze kwa hatua hiyo ya uwekezaji

Kila la heri kiongozi
Shukrani mkuu kwa ushauri wako...labda nitoke nje ya mji kidogo maana kila nikichungiza location, maeneo yote ya karibu na hospital mjini zimeshazibwa, nikicheki big pharmacies na zinazojulikana zilivyoshikilia majina na aina ya watu wa huku kwenda kwa kujuana napo changamoto ingine nayo!
 
Mchawi ni location,yenye watu wengi wanaofanya movements..maana mauzo inabidi yawe vizuri ili uweze kumlipa mfamasia (700k-1m)/month.

Tafuta location ambayo hamna pharmacy nyingi around..then taratibu shawishi watu wanunue kwako kwa kutoa huduma nzuri zenye kuzingatia rational drug use.
 
Mchawi ni location,yenye watu wengi wanaofanya movements..maana mauzo inabidi yawe vizuri ili uweze kumlipa mfamasia (700k-1m)/month.

Tafuta location ambayo hamna pharmacy nyingi around..then taratibu shawishi watu wanunue kwako kwa kutoa huduma nzuri zenye kuzingatia rational drug use.
Shukrani mkuu nauzingatia sana huu ushauri kwa kuendelea kusaka maeneo ya aina hiyo na ambayo kuna hospitali za kubwakubwa/serikali.
 
Mkuu la mwanzo acha woga, biashara ukiwa moga kutisua ngumu.
La pili hapo hapo ulipo na uzoefu napo ndio sehemu nzuri ya kuanzia kazi.
La tatu hakikisha unakaa mwenye dukani, hiyo ideo ya kuajiri mwanamke wa kukusaidia kazi ni nzuri. Ila hakikisha nawewe unakuepo.
 
Habari za muda huu wakubwa.

Mimi ni kijana wa kiume ambae nimebahatika kupata sehemu yangu ya urithi toka kwa wazee wangu ambapo nimepata milioni 30.

Nilikua naomba wazoefu, watu mnaoifanya hii biashara tusaidiane kwenye mambo kadhaa juu ya hii biashara kama eneo,
Mkuu kwanza kwa maelezo yako inaonekana unacho kila kitu cha kuanzia biashara isipokuwa tu labda ni ile hofu ya kawaida ya kuchukua hatua.Sasa Kwa sababu tayari unazo taarifa za msingi swali la kujiliza je Target yako ni Mapato kiasi gani?Mfano kwa Mwezi.

Hii itakusaidia kujua je UANZE na DLDM au uanze na Phamarcy Full.Usiingie kwenye biashara kubwa kwa sababu tu una mtaji mkubwa.

Ni Bora zaidi ufungue DLDM kisha ukue kwa kuzingatia location na malengo yako ya kimapato.
 
Unataka kufanya whole sale ama retail?

Kwenye miji mikubwa kubwa kidogo 30M kwa wholesale haitoshi ila kwenye wilaya zinazochipukia unaweza kufanya kazi vizuri tu.
 
Biashara sio mtaji tu mkuu. Biashara ni uthubutu anza kidogokidogo, kutakua na kuanguka na kunyenyuka ndio kutakupa mwanga wa nini ufanye baadae.
Ukiweza fanya research ya sehem gani uanzie.
 
Unataka kufanya whole sale ama retail?

Kwenye miji mikubwa kubwa kidogo 30M kwa wholesale haitoshi ila kwenye wilaya zinazochipukia unaweza kufanya kazi vizuri tu.
Sio kwamba hata 30m haitoshi kwenye miji midogo pia?
Na je wholesale faida inaizidi vipi retail pharmacy sababu sina uzoefu kwa upande wa pharmacy za jumla.

Nikiangalia asilimia ya faida kwa dawa mojamoja kuna dawa zina faida kubwa sana mpaka mara3 ya price... je kwa wholesale hiyo faida inapatikanaje?si mpaka uwe na wateja wengi wakuwauzia dawa in bulks tu kila siku?
 
Sio kwamba hata 30m haitoshi kwenye miji midogo pia?
Na je wholesale faida inaizidi vipi retail pharmacy sababu sina uzoefu kwa upande wa pharmacy za jumla.

Nikiangalia asilimia ya faida kwa dawa mojamoja kuna dawa zina faida kubwa sana mpaka mara3 ya price... je kwa wholesale hiyo faida inapatikanaje?si mpaka uwe na wateja wengi wakuwauzia dawa in bulks tu kila siku?
Sina uzoefu ila ktk pitapita zangu nimesikia ukiweza wholesale italipa zaidi na zaidi
japo hata retail inalipa Sana nayo pia.
Kuna dawa unanunua 500 Kwa jumla half inauzwa 9,000. yaani
wholesale mchawi ni mzunguko Tu.
 
Back
Top Bottom