Ulinzi na Usalama wa Kazi zetu

Habibu B. Anga

JF-Expert Member
May 7, 2013
6,557
25,671
Habari wakuu,

Nimejikuta imenibidi kukatisha mfululizo wa makala inayohusu kifo cha Rais JF Kennedy ili kutafakari na kutafuta msaada wa kisheria kutokana na gazeti la RAI kunakili makala hiyo na kuanza kuichapa bila makubaliano yoyote.

Huwa nasema mara kwa mara kwamba hakuna mtu mwenye hati miliki ya kuandika kuhusu tukio fulani, lakini ni kosa kisheria na kitaaluma pale ambapo mtu akifanya utafiti wake na kuandika kwa maneno yake na mtazamo wake kuhusu tukio fulani alafu akaja mtu mwingine akanakili andiko hilo kama lilivyo na kwenda kulitumia pasipo makubaliano au ruhusa.

Hiki ndicho ambacho wamekifanya Gazeti la Rai, wamenakili mfululizo wa makala hii ninayoiandika hapa Jamii Forums na kwenda kuichapa kwenye gazeti lao na tovuti yao huku mwandishi wao akijifanya kuwa yeye ndiye muandishi.

Si hawa tu, pia mtu ninaye muheshimu sana, Eric Shigongo naye kupitia mtandao wake wa vyombo vya habari vya Global Publishers wamenakili makala niliyoandika kuhusu kifo cha Pablo Escobar na kwenda kuichapa kama makala yao.

Changamoto hii pia ilitokea mwaka Jana kwa gazeti la Kisiwa kunakili makala ya "Geranimo" na kwenda kuichapa kwenye gazeti lao pasipo kuwasiliana na mimi (hawa waliomba radhi toleo lililofuata).

Japokuwa nimeanza kutafuta msaada wa kisheria dhidi ya Gazeti la Rai, lakini kinachonifanya nilete mjadala huu kwenu ni kuomba ushauri wa namna gani nzuri ya kuwadhibiti hawa wahuni ili huu mchezo ukome?

Najua kuna suala la kusajili kazi za uandishi, lakini hili suala kidogo linakuwa ni zito kwa watu ambao karibu kila wiki tunaandika makala mpya.... Je, ni njia gani nyingine nzuri zaidi ambayo kisheria inasaidia kuhahakikisha kazi ya ubunifu wa mtu inakuwa salama baada ya kuwekwa Public sehemu kama hii??

Lakini pia ningependa kusikia kutoka kwa Jamii forums, Maxence Melo, Invisible, Paw ni namna gani wanatusaidia kuhakikisha kuwa makala zetu, simulizi, hadithi, chambuzi na mada tunazoandika humu pale zinapotumiwa na watu wengine kwa maslahi yao ya kibiashara tunakuwa na uwezo wa kuwawajibisha kwa msaada wao (Jamii Forums).

Nazingatia kwamba kuna waandishi wengi humu ambao wanaweka mabandiko murua kabisa yenye kukonga nyoyo, nikiwataja wachache; lara 1, mshana jr, CHIEF MKWAWA, barafu, Pascal Mayalla, SteveMollel, ONTARIO na wengineo wengi..

Sasa kama kama hakutokuwa na namna fulani ambayo Jamii Forums mnatusaidia kulinda maandishi haya, tunaweza kujikuta watu hawa wanafanya kazi kubwa sana lakini kuna wahuni fulani huko nje wanafaidi jasho lao...

Wakuu, nimeandika maneno haya kwa uchungu kwa sababu imeniuma mno, kuona kuna watu wananufaika na kazi zetu ambazo sisi tunaweka hapa bure kushea na wanafamilia wenzetu wa Jamii Forums..

Naomba tusaidiane kushauriana kwenye hili.!! Ni namna gani tufanye kuwawajibisha hawa watu?? Tunakomeshaje huu uhuni wa waandishi wa habari makanjanja kuiba maandiko humu na kwenda kuyachapa huko nje kana kwamba ni kazi zao???

1228cadf3bc31a85558f7cea24d95e12.jpg


d0ca3a11c3bd22b98dd9e232c5088481.jpg


c7b52bc61959088571a82c35c24cb5b6.jpg


087cbbe319b831cd5e235823b3c2f56c.jpg

Huu ndio uhuni walioufanta gazeti la Rai kwenye mfululizo wa makala ya kifo cha Kennedy ninayoiandika hapa JF


Hapa chini ni uhuni uliofanywa na Global Publishers kutumia makala yangu ya "Plata O Plomo - kuhusu maisha ya Pablo Escobar"
ce9a7ac5b968b94e47f8d9d69d142f05.jpg


f1220516d93395b5ee3265d40f6acf42.jpg


ffed823fcf81ccecd78e658cf99aa898.jpg


Shukrani sana sana kwa wakuu wote ambao mmenipatiataarifa kuhusu vyombo vya habari wanaonakili maandiko yangu na kuyatumia... elmagnifico, AKILI TATU

Naomba tusaidiane kwenye hili wakuu!!! Tunafanya nii?? Hii inauma sana aisee..
 
Habari wakuu,


Nimejikuta imenibidi kukatisha mfululizo wa makala inayohusu kifo cha Rais JF Kennedy ili kutafakari na kutafuta msaada wa kisheria kutokana na gazeti la RAI kunakili makala hiyo na kuanza kuichapa bila makubaliano yoyote.

Huwa nasema mara kwa mara kwamba hakuna mtu mwenye hati miliki ya kuandika kuhusu tukio fulani, lakini ni kosa kisheria na kitaaluma pale ambapo mtu akifanya utafiti wake na kuandika kwa maneno yake na mtazamo wake kuhusu tukio fulani alafu akaja mtu mwingine akanakili andiko hilo kama lilivyo na kwenda kulitumia pasipo makubaliano au ruhusa.

Hiki ndicho ambacho wamekifanya Gazeti la Rai, wamenakili mfululizo wa makala hii ninayoiandika hapa Jamii Forums na kwenda kuichapa kwenye gazeti lao na tovuti yao huku mwandishi wao akijifanya kuwa yeye ndiye muandishi.

Si hawa tu, pia mtu ninaye muheshimu sana, Eric Shigongo naye kupitia mtandao wake wa vyombo vya habari vya Global Publishers wamenakili makala niliyoandika kuhusu kifo cha Pablo Escobar na kwenda kuichapa kama makala yao.

Changamoto hii pia ilitokea mwaka Jana kwa gazeti la Kisiwa kunakili makala ya "Geranimo" na kwenda kuichapa kwenye gazeti lao pasipo kuwasiliana na mimi (hawa waliomba radhi toleo lililofuata).


Japokuwa nimeanza kutafuta msaada wa kisheria dhidi ya Gazeti la Rai, lakini kinachonifanya nilete mjadala huu kwenu ni kuomba ushauri wa namna gani nzuri ya kuwadhibiti hawa wahuni ili huu mchezo ukome?

Najua kuna suala la kusajili kazi za uandishi, lakini hili suala kidogo linakuwa ni zito kwa watu ambao karibu kila wiki tunaandika makala mpya.... Je, ni njia gani nyingine nzuri zaidi ambayo kisheria inasaidia kuhahakikisha kazi ya ubunifu wa mtu inakuwa salama baada ya kuwekwa Public sehemu kama hii??


Lakini pia ningependa kusikia kutoka kwa Jamii forums, Maxence Melo, Invisible, Paw ni namna gani wanatusaidia kuhakikisha kuwa makala zetu, simulizi, hadithi, chambuzi na mada tunazoandika humu pale zinapotumiwa na watu wengine kwa maslahi yao ya kibiashara tunakuwa na uwezo wa kuwawajibisha kwa msaada wao (Jamii Forums).

Nazingatia kwamba kuna waandishi wengi humu ambao wanaweka mabandiko murua kabisa yenye kukonga nyoyo, nikiwataja wachache; lara 1, mshana jr, CHIEF MKWAWA, barafu, Pascal Mayalla, SteveMollel, ONTARIO na wengineo wengi...

Sasa kama kama hakutokuwa na namna fulani ambayo Jamii Forums mnatusaidia kulinda maandishi haya, tunaweza kujikuta watu hawa wanafanya kazi kubwa sana lakini kuna wahuni fulani huko nje wanafaidi jasho lao...


Wakuu, nimeandika maneno haya kwa uchungu kwa sababu imeniuma mno, kuona kuna watu wananufaika na kazi zetu ambazo sisi tunaweka hapa bure kushea na wanafamilia wenzetu wa Jamii Forums..

Naomba tusaidiane kushauriana kwenye hili.!! Ni namna gani tufanye kuwawajibisha hawa watu?? Tunakomeshaje huu uhuni wa waandishi wa habari makanjanja kuiba maandiko humu na kwenda kuyachapa huko nje kana kwamba ni kazi zao???

1228cadf3bc31a85558f7cea24d95e12.jpg


d0ca3a11c3bd22b98dd9e232c5088481.jpg


c7b52bc61959088571a82c35c24cb5b6.jpg


087cbbe319b831cd5e235823b3c2f56c.jpg

Huu ndio uhuni walioufanta gazeti la Rai kwenye mfululizo wa makala ya kifo cha Kennedy ninayoiandika hapa JF


Hapa chini ni uhuni uliofanywa na Global Publishers kutumia makala yangu ya "Geranimo"
ce9a7ac5b968b94e47f8d9d69d142f05.jpg


f1220516d93395b5ee3265d40f6acf42.jpg


ffed823fcf81ccecd78e658cf99aa898.jpg




Shukrani sana sana kwa wakuu wote ambao mmenipatiataarifa kuhusu vyombo vya habari wanaonakili maandiko yangu na kuyatumia... elmagnifico, AKILI TATU




Naomba tusaidiane kwenye hili wakuu!!! Tunafanya nii?? Hii inauma sana aisee..
Pole sana nikiwa kama mwandishi wa riwaya matatizo haya yalinikuta hasa humu mitandaoni ila nikajua kuwa hakimiliki ndiyo kitu pekee kinachoweza kulinda haki ya mtu. The Bold kama wewe ni mwanachama wa COSOTA sajili kila andiko lako kule, ukiona limetumika bila ridhaa wape taarifa COSOTA.

Watakutajirisha wenyewe kwa faini wanazozitoa kwa wizi wao, hiyo ni intellectual property ikatie Copyright upate namna ya kuwashtaki. Ukiwafanyia hivyo wenye makampuni wawili tu, wataziogopa kazi zako kama ukoma.
 
Mkuu pole kwa Yale yanayokukuta, binafsi nimsomaji mzuri sana Wa makala zako, na ninaona nna unavyo umia hasa kwa hili LA kunakili kazi zako,

Anyway ngoja nishauri japo kidogo,kwanza kabula ya yote wasiliana(rai na global) ili kujua kwa nini wametumia maandiko yako bila kibali chako? Hiyo inaitwa natural justice...

Pili nenda pale idara ya habari maelezo,sina uhakika kama ni wao ila huwa wanapokea malalamiko pia ya watu ambao huandikwa au kunukuliwa au vinginevyo tofauti na matakwa yao..

Tatu, ipo misingi ya uandishi Wa makala, moja wapo ni kuitambua kwa jina hyo makala na vyanzo vya uandishi Wa makala au habari/ hivyo kwa kutumia Mwanasheria kwenye weredi Wa kiundishi, muombe akupe muongozo Wa namna ya kuwafikia waandishi Wa makala hizo ili waseme vyanzo vya makala kwa vielelezo.

NNE si kwa umhim , zungumza na watu habari hasa akina tido au charles hilal kujua uzoefu wao hasa kwenye wizi Wa makala/au habari...

Zingatia hiki habari ni huru ila kusema chanzo cha habari ni bora sana, mfn mashirika yetu ya ndani hunukuu habari kutoka mashirika makubwa kama BBC, DW, CNN n.k ila hutoa creditability kwa hyo watu...


Na hata hayo mashirika yakiwa na habari ambayo inatoka kwenye nchi husika husema chanzo kuwa ni radio/TV Fulani..

Nakushauri fuata utaratibu, pamoja na wadau kuongezea utapata solution,

Kila changamoto inamlango Wa kutokea... Pole The BOLD..
 
Kumbe hao waandishi ni vilaza eeh wanachukuaje kazi ya mtu bila taarifa?. Basi taarifa wasitoe hata credit pia kusema tu hii makala kaandika fulani wanashidwa, Mkuu tafuta wanasheria kama kuna sheria za haya mambo wakupe haki yako.
 
Pole sana nikiwa kama mwandishi wa riwaya matatizo haya yalinikuta hasa humu mitandaoni ila nikajua kuwa hakimiliki ndiyo kitu pekee kinachoweza kulinda haki ya mtu. The Bold kama wewe ni mwanachama wa COSOTA sajili kila andiko lako kule, ukiona limetumika bila ridhaa wape taarifa COSOTA.

Watakutajirisha wenyewe kwa faini wanazozitoa kwa wizi wao, hiyo ni intellectual property ikatie Copyright upate namna ya kuwashtaki. Ukiwafanyia hivyo wenye makampuni wawili tu, wataziogopa kazi zako kama ukoma.

The Bold,hili ndio suluhisho pekee.
 
Pole sana Mkuu The bold , wakuu wengi wameshatoa ushauri, kwahiyo sasa hivi funika kwanza makabrasha yako, hangaikia haki yako, I hope utajiri ndio huo sasa umejileta wenyewe, mpaka mwakani am sure utakua umeshafungua "media house" yako hapo mikocheni kupitia hii kesi, Mungu akutangulie, msalimie mwenzetu Nifah
 
mkuu The bold pole sana.
Nina ushauri mdogo kwako, ukiupokea na kuufanyia kazi sawa,ukiuupuza sawa.

kama umeamua kufanya uandishi wa makala za kitafiti katika mitandao ya kijamii kuwa ni kazi yako ya kudumu,basi una kila sababu ya kuanza kutumia verified ID(jina lako la kiserikali)achana na hiyo ID unayotumia sasa.ibaki kama alias name.

nalisema hili kwasababu endapo utaamua kuwashitaki wanaoiba kazi zako ambazo umezi-post kwa kutumia ID ya the bold,mahakamani watataka utoe vithibisho vinavyotambulika kisheria kuwa wewe ni the bold wa jf.

nadhani wanaoiba makala zako wamengundua hiyo weakness kiasi kwamba wanajiamini hata ukiwashtaki wa najua watakubana wapi ili uachane nao.

Mimi sio mwanasheria,ila sina shaka wanasheria wanaweza kukushauri vizuri katika hili.jaribu ku-consult nao.kuna yule mwanasheria anayesimamia kazi za mwana fa na AY.yupo vizuri sana ktk hizi mambo.
 
Gazeti la Rai lilipata kuwa 'kubwa' sana enzi za waliolianzisha. Ni aibu kwamba wanafanya faulo ya kizembe namna hii. Wao Pia ni wahanga wa uharamia wa Sanaa, inashangaza kuwa hawaheshimu kazi za wenzao.

Ushauri: Watanzania wengi wqnachukulia poa uharamia wa Sanaa. Wanadhani sio kosa kivile. Nenda ofisini kwao kule Sinza. Ongea nao uwasikilize wanajiteteaje. Kama ni wabishi na hawataki kufika bei ndipo utafute msaada wa kisheria. Nazingatia ukweli kuwa mambo ya kisheria yana urasimu na gharama.

Pia kwa kuwa wewe unaandika makala kila wiki, ni vyema ukawa na Mwanasheria ambaye kazi yake ni kulinda maslahi yako. Mfano Albert Msando amejipambua kama Mwanasheria mwanaharakati wa haki za Sanaa. Naamini anaweza akachukua commission kwa kila violation.
 
Back
Top Bottom