Ulinitesa sana, sababu nilikupenda

Ulinitesa sana, sababu nilikupenda

Mr Bean

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2018
Posts
206
Reaction score
178
Habari wadau,

Leo jioni nimepokea simu kutoka kwa aliekua mpenzi wangu wa zamani, amenipigia simu na kuniomba msamaha kwa alionifanyia miaka 5 ilopita.

nilimpenda sana kuliko hata nilivyojipenda mwenyewe ila alinitesa sana,, nilivumilia mateso yake kwa sababu penzi langu kwake lilikua kubwa kuliko maumivu aliyokua ananipa.

kuna siku moja alihamaki kisa sikuwa na pesa ya kumnunulia viatu alivyokua anataka, tulivyorudi nyumbani nikamwambia anipe muda nipambane ili siku moja nkipata pesa nkamnunulie hivyo viatu.

Ila hakutaka kusikia chochote, akaanza kunitukana na kuniambia mimi ni boya na mzigo kwake, sina mchango wowote katika maisha yake zaidi ya kumpotezea muda tu. akaniambia rafiki zake wote wapenzi wao wanawanunulia vitu vizuri.

Aliponiambia hivyo niliumia sana moyoni, nikajikuta nimemwambia "basi na wewe nenda kwa hao rafiki zako wakutafutie mwanamme tajiri" .. baada ya kumwambia hivyo akanizaba kibao. akaniambia "usnitafute tena".

nililia sana siku hiyo hadi nikaishiwa na machozi, nikawa sina furaha tena, nilikua naona bora nife tu ili nipate kujipumzikia.

baada ya miezi 3, kidogo kidogo nikaanza kumsahau, nikaanza kutabasamu na kucheka tena. ilikua hadi nisha sahau namna ya kucheka, siku nacheka nilijihisi kama nipo ndotoni.

miaka 5 imepita, na leo ndio ameamua kunipigia simu na kuniomba msamaha na kuniambia anataka turejeane. nikamwambia nimekusamhe ila sitaweza kuwa nawe maana ninae mke ambae nampenda nae ananipenda, ameniambia hakutegemea kama nitamsamehe ila nimemwambia kuwa nilikuwa nimekusamehe tangia siku ulipo ondoka, akaanza kulia,,, akniambia hata pata mwanamme mwingine ataempenda sana kama mimi.
 
Akakuzaba kibao? Huko alikotegemea atapata pumziko kumemtenda sivo ndio mana amerudi, kwa kua umemsamehe sawa lakini me ningekua ni wewe ningemsamehe huku namtakia kila heri kimoyomoyo maisha yaende tu,
 
Hahaha yani hapo ulipo kubali kuzabwa kibao na huyo mwanamke ndipo ulipo ni kera...alijua wewe ni mjinga mjinga ndio maana alio akupige....Hivi unaanzaje kupigwa vibao na mwanamke na wewe una angalia tuu..... Hayo mapenzi ya kizungu yana waponza sana.....
Mwanamke anacho penda zaidi kwa mwanaume ni pale tuu mwanaume anapokuwa imara kiuchumi....
 
Kwenye mapenzi hutokea kuwa, yule ambaye unampenda sana halafu ukamfanyia ubaya ndo anakuwa alikupenda kwa dhati.

Sijui hii inakuwaje watu wengi hawaioni.
 
Hahaha yani hapo ulipo kubali kuzabwa kibao na huyo mwanamke ndipo ulipo ni kera...alijua wewe ni mjinga mjinga ndio maana alio akupige....Hivi unaanzaje kupigwa vibao na mwanamke na wewe una angalia tuu..... Hayo mapenzi ya kizungu yana waponza sana.....
Mwanamke anacho penda zaidi kwa mwanaume ni pale tuu mwanaume anapokuwa imara kiuchumi....
mkuu sasa kibao ndio kilikua kishanipata shavuni, ningefanyaje unadhani? ingekua nimekiona kikija ningeki kwepa, sikua nkitegemea kama siku atanizaba kibao.
 
Ndo ilivyo hivyo,all those years itakuwa ilikuwa inamuuma.
 
Maisha bhana,

Ni kwamba hakuw na hisia na wewe completely,

Alikuwa na mtu ambaye aliwekeza hisia zake kule

Haya mambo magumu sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom