Ulimaji wa vitunguu

Itategemeana na eneo ulilolopo, vitunguu vinachukua miezi 5-6 tangu kusia mbegu kitaluni mpaka kuvuna, hivyo kama utapanda mwezi wa 8 maana yake utavuna mwezi wa 12, sasa hapo itategemea na sehemu uliyopo, kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Kutoka iringa, njombe, ruvuma, mbeya na katavi) miezi hiyo masika huanza, hivyo kama uko maeneo hayo vitunguu vitakuharibikia tu shambani coz ya mvua.


Heshima kwenu ndugu zangu..
Me napenda kuuliza hivi siwezi anza kulima vitunguu kipindi hiki..?
Kuanzia mwezi huu
 
Mbegu kuna red cleole ya south Africa,red Bombay ya Holland hata ya kibo sio mbaya,kuna high breed km jambari F1. Kwa ushauri wangu usitumie mbegu za kienyeji wanazootesha watu.. Zina usumbufu wake,production yake sio kubwa na pia hushambuliwa sana na wadudu na magonjwa.

Kuhusu soko lima na uvune kipindi ambacho demand is high kuliko supply utapiga hela. Kitunguu kinalimwa kwenye ardhi isiyotuamisha maji. All the best
 
Itategemeana na eneo ulilolopo, vitunguu vinachukua miezi 5-6 tangu kusia mbegu kitaluni mpaka kuvuna, hivyo kama utapanda mwezi wa 8 maana yake utavuna mwezi wa 12, sasa hapo itategemea na sehemu uliyopo, kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Kutoka iringa, njombe, ruvuma, mbeya na katavi) miezi hiyo masika huanza, hivyo kama uko maeneo hayo vitunguu vitakuharibikia tu shambani coz ya mvua.
Vipi Morogoro mikumi/kilosa hali yake huwa vipi kipindi hiki
 
Morogoro kitunguu kinakubali anzia maeneo ya magubike, magole, dakawa, dumila na kilosa pia, kikubwa uhakikishe una maji , mwezi wa 6 after masika kukata ndipo mashamba ya vitunguu huanza kuandaliwa, ili kuvuna november-december

Kama unaanza, anza na mbegu aina ya OPV kama hizo Red cleorel, Red Bombay, ili upate uzoefu kidogo anza hata na nusu eka kwanza, kisha badae ndipo uje utumie hizo hybrid kama Neptune F1 etc, Usije kupanda Jambari F1 zinasumbua sana sokoni maana ni vinene mnoo.

Vipi Morogoro mikumi/kilosa hali yake huwa vipi kipindi hiki
 
ni pazuri mkuu kuanzia mwezi wa nne hadi mwezi wa 6 ndiyo mida ya kupanda mbegu baada ya kutoka kitaluni
 
Morogoro kitunguu kinakubali anzia maeneo ya magubike, magole, dakawa, dumila na kilosa pia, kikubwa uhakikishe una maji , mwezi wa 6 after masika kukata ndipo mashamba ya vitunguu huanza kuandaliwa, ili kuvuna november-december

Kama unaanza, anza na mbegu aina ya OPV kama hizo Red cleorel, Red Bombay, ili upate uzoefu kidogo anza hata na nusu eka kwanza, kisha badae ndipo uje utumie hizo hybrid kama Neptune F1 etc, Usije kupanda Jambari F1 zinasumbua sana sokoni maana ni vinene mnoo.
Nashkuru mkuu...sema mm nataka limia mikumi na ndo nataka kuanza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom