Ulikuwa unafanya nini ukiwa na miaka 16?

Ulikuwa unafanya nini ukiwa na miaka 16?

Nilikuwa Mbalizi -Tarafani namenya viazi vya chips nalipwa mia tatu na sahani ya kiepe kwa dada Rukia
 
Nilikuwa kidato cha kwanza Ifunda Technical Sec. School enzi za TANU
 
Nilikuwa namaliza form 4 hapo Nina mawazo ya uinjinia tu. Pia Nilikuwa nashinda shamba usiku mchana shule muda wa mavuno [emoji16]
 
Nilikuwa makongo sec tunafukuzana na afande miraji(R.I.P)
 
Hahaha.

Na mnavyokuwaga na madharau sasa viongozi wa UKWATA wa kike.

Hata usemeshwe..utongozwe utamwangalia mtu kwa dharau huku ukisonya kwa vifungu vya Biblia. Utafikiri mpo Mbinguni.
[emoji23][emoji23][emoji23] sasa wewe unaanzaje kumtongoza mpakwa mafuta wa Bwana?
 
Hahaha.
Na mnavyokuwaga na madharau sasa viongozi wa UKWATA wa kike.
Hata usemeshwe..utongozwe utamwangalia mtu kwa dharau huku ukisonya kwa vifungu vya Biblia. Utafikiri mpo Mbinguni.
hawa viongozi baadhi yao walitakiwa kutunukiwa vyeti vya unafki mashuleni. Kuna maboya walitunyima zile karatasi za TYCS kisa huwa hatuhudhurii vipindi vya jioni.
 
Dah aiseeeeeee nilikuwa nakamuwa maziwa ya mbuz kwenye kisoda nimpelekee mbwa wang,, cha ajabu yanakauka kabla sijayafikisha
 
Back
Top Bottom