Ulifanya nini baada ya hayo kutokea?

Ulifanya nini baada ya hayo kutokea?

Pyepyepye

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2017
Posts
1,940
Reaction score
3,857
Miaka kadhaa iliyopita, mjomba wangu niliyekuwa nikiishi kwake, aliniahidi kulipa gharama zote za chuo, nilikuwa nashughulikia michakato ya kutafuta uwezesho wa kuendelea na masomo, lakini baada ya kauli ile nikaacha kila kitu na kumsubiri yeye.

Pesa aliyoitegemea ilikuwa ya mkopo, siku ya siku mkopo ukaingia, akaniita akanieleza na kuniambia nimsindikize benki akachukue pesa, tuliongozana hadi benki akachukua pesa, tukarudi home

Siku tatu baadae, niliona mjomba anaboresha sebule kwa kununua samani (ikumbukwe kipindi hicho nilikuwa naishi kwake) na vitu vingine vingi, jioni ya siku ile mjomba aliniita na kuniambia "Natamani sana kukusaidia, lakini siwezi kuharibu mahusiano yangu na mke wangu kwa ajili yako, Mama Japhe ameshauri hizi pesa tununue vitu na kama ulivyoona tumeshanunua, wewe fanya utaratibu mwingine"

Ulishawahi katishwa tamaa na yule uliyemtegemea kabisa?

Hebu tupe uzoefu wako katika hili.
 
duuuuhhh Huyo mjomba wako ni H.I.V nini
yaani ningekuwa mimi ndio wewe sikuhiyo hiyo ningehama ...maana Sikh sinyingi atakwambia kuwa naogopa kumuuzi mke wangu ..amenishauri nikufukuze kwahiyo naomba uondoke...
 
Sijawahi kukatishwa tamaa lakini ningekubaliana na hali hiyo na kufanya michongo mingine maana hamna jinsi wala nisinge mind saana. Ila ungemuuliza kama ungekuwa mtoto wake je angefanya hivyo?.

Ila inaonesha mjomba wako ni bonge la bwege kwa mkewe.
 
Huyo mjomba wako atakuwa ni mwanaccm maana ccm ndiyo wana tabia za namna hiyo
 
Mjomba wako ni Kaa na mkewe naye ni Kaa!waambie wakatae kuwa kaa bora wewe umekuwa chawa
 
Yeah. Mtangazaji fulani hivi wa kituo cha radio, hii ni baada ya kuona uweze wangu mkubwa darasani alikuja kuniahidi kuwa nikimaliza form four atanisomesha chuo. Nilipo maliza tu na sikufanikiwa kuendelea na A level, alikuja kunitia moyo kuwa nitafute chuo chochote ninachokipenda atanilipia kila kitu, nilimaliza pesa yangu yote kwa nauli, lakini alinitelekeza bila kujuma mimi nitafanya nini. Nimepambana kiume mpaka leo hii sitaki hata kumuona kwa alicho nifanyia
 
Matokeo ya mitihani wa kidato cha 4 mwaka 2009, nilipata CCC kwenye combination niliyoipenda... Nilijua Mjomba yupo hakijaaribika kitu, akaniambia kuwa atanipeleka SHULE yeyote. Km sintapata SHULE ya serikali... Sasa selection zikatoka nilikuwa kijijini nikamuambia anichekie km nimepata... Duuuu akaniambia hujapata SHULE and count on your mother for school fees..!! Aiseee huyo maza sasa masikini....!!! Siku 3 baadae mama anapigiwa simu na rafiki yangu eti nimepangiwa weruweru girls.....!!! Naikumbuka ile siku.... Maana nilishaanza mchakato wa kujiunga na mandaka TTC...


Mungu ni mwema.
 
Back
Top Bottom