Ulianzaje kuipenda timu unayoishabikia?

Natafuta Ajira

JF-Expert Member
Mar 25, 2020
4,425
9,822
Ulifata mkondo wa wazazi /ndugu, ulivutiwa na mchezaji wa timu husika, kuna tukio la kufurahisha au kuuzunisha lililikufanya uipende timu yako?

Binafsi nimeanza kufatilia mpira nikiwa na miaka 6 mwaka 1998 kipindi cha world cup. Kabla ya hapo sikua shabiki wa kuangalia mpira ingawa nilikua naucheza na marafiki mtaani na shuleni. Ule mkusanyiko wa watu na vibe wakati wa mechi nami nikawa najumuika ndipo nakaanza kuwa shabiki wa soka

Baada ya world cup kuisha nikawa nafuatilia zaidi ligi ya uingereza kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa majumbani nimesahau chanel gani ila ni DTV au CTN, nilikua nawafatilia zaidi wachezaji waliokuwepo kwenye world cup kama beckham, owen, henry, berkamp n.k.

Wachezaji waliovuma world cup ila hawachezi ligi ya uingereza kama Ronaldo de lima, Zidane, Rivaldo n.k nilikua nawafatilia kupitia uefa champions league kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa ITV. Timu ninazoshabia kwa sasa ni Yanga na Manchester United. Nilianzaje kuzipenda izo timu?

YANGA: Miaka ya 90 mwishoni kuelekea 2000 kuna binamu yangu alitoka kijijini kuja dar tukawa tunaishi nae nyumbani, alikua anaipenda sana simba kila mechi ya simba au yanga lazima asikilize redioni kila siku jioni anasikiliza kipindi cha michezo redio 1 kilikua kinatangazwa na Maulid Kitenge. Kipindi kinaanza na kibwagizo utasikia "maulid baraka wa kitenge jezi nambari 9 mgongoni alalalala goooooo".

Nikajenga mazoea ya kusikiliza nae mpira redioni katika mechi za yanga nilikua nasikia sana jina la Lunyamila kuashiria anawapeleka puta mabeki uko uwanjani, ilifika hatua nikawa nasikiliza mechi za Yanga nisikie tu namna anavyowatesa wapinzani. Lunyamila ndie alinifanya niipende Yanga ingawa nilikua namsikia redioni tu sikua namjua hata kwa muonekano, azam tv haikuwepo kipindi hicho

MANCHESTER UNITED: Ilikuaje nikaanza kuipenda hii timu? Usiku wa fainali ya champions league msimu wa 1998/1999 kati ya bayern Munich vs Man u. Mpaka kufikia hii siku sikua shabiki wa timu yoyote ulaya, bayern walitangulia kupata goli, tukiwa tumekusanyika mtaa mzima nyumbani kwa jirani yetu tunaangalia iyo game sebure nzima kulikua na huzuni kubwa sana nakumbuka wachezaji wa bayern kule benchi walishainuka wamepanga mstari huku wamekumbatiana mabegani kujiandaa na shangwe la ubingwa, furaha ilirudi pale sebureni baada ya Sosha kuchomoa goli dakika za mwisho kila mtu akijua game inaenda 120, Sosha akaweka cha pili. Nakumbuka refa alikua Collina muitary fulani hivi ananyoa kipara, nakumbuka beki wa bayern munich kufor alivyokua analia huku akipiga ngumi uwanja. Lile shangwe pale sebureni kwa jirani na mtaani baada ya mechi kuisha sitakuja kulisahau na ndio siku niliyoanza kuipenda manchester united.
 
Simba niliipenda kwa sababu kaka yangu alikuwa shabiki wa Simba.

Arsenal nakumbuka nikiwa mdogo nilisikia siku kwenye redio anawaita "washika bunduki wa England"

Basi nikavutiwa tu na hilo jina washika bunduki, nikawa naona ni kama jina fulani la watu hatari sana. Nikaipenda Arsenal hadi leo.
 
Arsenal 2006
Nilikua namkubali sana Theo Walcott, kipindi hicho ndo kanaingia asenali ni kadogo afu kahb kinoma, na mimi enzi za utoto nilikua najifananisha nae maana nilikuq nasifiwa kwa uhb(hata hivyo hatufanani hata kodogp). Basi ndo ukawa mwanzo wa kuipenda.

Na sababu nyingine ni bro wangu kuipenda sana Man U na mimi sikutaka kua nae tim moja mi nikachagua asenali.

Bongo ni Yanga
Hii enzi za utoto kwenye kucheza mpira tuligawana wanaoipenda simba huko na yanga kule. Enzi hizo wadogo kweli hizo timu tunaziskia tu kwa wakubwa.

Basi lila dogo akachagua upande na mpaka leo toka ile siku aliechagua simba ni simba mpaka leo na aliechagua yanga ni yanga mpaka leo.

Simba na yanga zilitutesa sana udogoni, tukaanza kuzifatilia na uhasama, visasi na tuvita twa kitoto twa usimba na uyanga vikafanya tuwe mashabiki kindakindaki.
 
Simba ilikuwa ikifunga sana isitoshe ni timu ya familia yetu nakumbuka watu walikuwa wanawamwagia vikopo vya mkojo yanga kisa wamefungwa
 
Dar young Africa kule Manchester united.... Yanga hata cjui yan imekuja automatic tu ila man united ule unyama wa Beckham enzi hizo anafuga nywele ulinifanya niwe shabik
 
Simba ilipoikimbiza Zamalek kwenye mvua enzi za kina Joseph Kaniki nikasema Yes hii ndo timu
 
George masatu na Hussein Aman Masha walivyohamia Simba kutoka pamba ya mwanza! Masatu alikuwa mpangaji wetu nikiwa na miaka 7
 
Inshu ya simba ni familia zaidi kuna wakati nilijarbu kuishabikia ynga mwaka 98 nikiwa std 3 waliposhinda dhidi ya wale jamaa wa uganda changamoto ilikuja kila mnyama anapokuwa anacheza akishambuliwa moyo unakosa utulivu hapo nikagundua najilazimisha na vitu visivyonihusu kuhusu manchester ni class of 92
 
Ulifata mkondo wa wazazi /ndugu, ulivutiwa na mchezaji wa timu husika, kuna tukio la kufurahisha au kuuzunisha lililikufanya uipende timu yako?

Binafsi nimeanza kufatilia mpira nikiwa na miaka 6 mwaka 1998 kipindi cha world cup. Kabla ya hapo sikua shabiki wa kuangalia mpira ingawa nilikua naucheza na marafiki mtaani na shuleni. Ule mkusanyiko wa watu na vibe wakati wa mechi nami nikawa najumuika ndipo nakaanza kuwa shabiki wa soka

Baada ya world cup kuisha nikawa nafuatilia zaidi ligi ya uingereza kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa majumbani nimesahau chanel gani ila ni DTV au CTN, nilikua nawafatilia zaidi wachezaji waliokuwepo kwenye world cup kama beckham, owen, henry, berkamp n.k.

Wachezaji waliovuma world cup ila hawachezi ligi ya uingereza kama Ronaldo de lima, Zidane, Rivaldo n.k nilikua nawafatilia kupitia uefa champions league kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa ITV. Timu ninazoshabia kwa sasa ni Yanga na Manchester United. Nilianzaje kuzipenda izo timu?

YANGA: Miaka ya 90 mwishoni kuelekea 2000 kuna binamu yangu alitoka kijijini kuja dar tukawa tunaishi nae nyumbani, alikua anaipenda sana simba kila mechi ya simba au yanga lazima asikilize redioni kila siku jioni anasikiliza kipindi cha michezo redio 1 kilikua kinatangazwa na Maulid Kitenge. Kipindi kinaanza na kibwagizo utasikia "maulid baraka wa kitenge jezi nambari 9 mgongoni alalalala goooooo".

Nikajenga mazoea ya kusikiliza nae mpira redioni katika mechi za yanga nilikua nasikia sana jina la Lunyamila kuashiria anawapeleka puta mabeki uko uwanjani, ilifika hatua nikawa nasikiliza mechi za Yanga nisikie tu namna anavyowatesa wapinzani. Lunyamila ndie alinifanya niipende Yanga ingawa nilikua namsikia redioni tu sikua namjua hata kwa muonekano, azam tv haikuwepo kipindi hicho

MANCHESTER UNITED: Ilikuaje nikaanza kuipenda hii timu? Usiku wa fainali ya champions league msimu wa 1998/1999 kati ya bayern Munich vs Man u. Mpaka kufikia hii siku sikua shabiki wa timu yoyote ulaya, bayern walitangulia kupata goli, tukiwa tumekusanyika mtaa mzima nyumbani kwa jirani yetu tunaangalia iyo game sebure nzima kulikua na huzuni kubwa sana nakumbuka wachezaji wa bayern kule benchi walishainuka wamepanga mstari huku wamekumbatiana mabegani kujiandaa na shangwe la ubingwa, furaha ilirudi pale sebureni baada ya Sosha kuchomoa goli dakika za mwisho kila mtu akijua game inaenda 120, Sosha akaweka cha pili. Nakumbuka refa alikua Collina muitary fulani hivi ananyoa kipara, nakumbuka beki wa bayern munich kufor alivyokua analia huku akipiga ngumi uwanja. Lile shangwe pale sebureni kwa jirani na mtaani baada ya mechi kuisha sitakuja kulisahau na ndio siku niliyoanza kuipenda manchester united.
Manchester united enzi za ruud van nestory na mdg wake ronaldo
 
Niliipenda Arsenal nikiwa mdogo sana , nakumbuka kuna mgeni alikuja nyumbani akiwa kavaa fulana yenye maandishi ikisomeka "Arsenal"

Basi Kila muda nikawa namuangalia kwani ulimpendeza sana, ndipo alipogundua na kuniambia,

Vipi dogo umeipenda hii eeeh,
Mimi ni shabiki wa hii timu inayopatikana Uingereza.

Ndipo nilipoipenda hii timu tangia hapo huku nikaanza kuifuatilia.

Kuhusu Yanga,
Kwanza sikuwa na mahaba ya mpira wa kibongo, ila nikiwa chuoni , Wana wengi walikuwa Simba, Mimi nikaona kwanini wote tuwe upande mmoja lazima tutofautiane ili kuleta ladha ya ushabiki.

Kule Real Madrid nilimkubali
Raul Gonzalez, ndiyo nikazama mazima
 
Niliota baba ni shabiki wa Yanga tena wa kufa na kupona. Basi katika maisha yote niliipenda yanga nikijua fika kuwa baba ni mjangwani. Hiyo ndoto niliota hata darasa la kwanza bado. Nilivyofika darasa la 7 siku moja najitapa kuwa mimi ni mjangwani na baba ni mjangwani kaaangu akaniambia mzee ni mwana simba na kadi anayo ndo basi nikawa nimeuziwa timu ndotoni hivyo
 
Chelsea 2003 nikiwa na miaka 7.

Kwa kuwa nimejaaliwa kipaji cha uchoraji, niliokota kipande cha gazeti chenye picha ya Frank Lampard nikachora na kupata pongezi za kutosha toka kwa watu mbalimbali. Rasmi nilianza kumpenda na kujikuta nashabikia timu yake. Until today I'm a die hard fan
 
Kuna kaka mtaani alikuwa mkorofiiii, bangi mtu. Ni mgomvi mtaa mzima then anajitapa ni mwanasimba. Nikachukulia watu wa simba ni wendawazimu then nikajikuta tu naipenda yanga.
 
Ulifata mkondo wa wazazi /ndugu, ulivutiwa na mchezaji wa timu husika, kuna tukio la kufurahisha au kuuzunisha lililikufanya uipende timu yako?

Binafsi nimeanza kufatilia mpira nikiwa na miaka 6 mwaka 1998 kipindi cha world cup. Kabla ya hapo sikua shabiki wa kuangalia mpira ingawa nilikua naucheza na marafiki mtaani na shuleni. Ule mkusanyiko wa watu na vibe wakati wa mechi nami nikawa najumuika ndipo nakaanza kuwa shabiki wa soka

Baada ya world cup kuisha nikawa nafuatilia zaidi ligi ya uingereza kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa majumbani nimesahau chanel gani ila ni DTV au CTN, nilikua nawafatilia zaidi wachezaji waliokuwepo kwenye world cup kama beckham, owen, henry, berkamp n.k.

Wachezaji waliovuma world cup ila hawachezi ligi ya uingereza kama Ronaldo de lima, Zidane, Rivaldo n.k nilikua nawafatilia kupitia uefa champions league kwa kipindi hicho ilikua inaoneshwa ITV. Timu ninazoshabia kwa sasa ni Yanga na Manchester United. Nilianzaje kuzipenda izo timu?

YANGA: Miaka ya 90 mwishoni kuelekea 2000 kuna binamu yangu alitoka kijijini kuja dar tukawa tunaishi nae nyumbani, alikua anaipenda sana simba kila mechi ya simba au yanga lazima asikilize redioni kila siku jioni anasikiliza kipindi cha michezo redio 1 kilikua kinatangazwa na Maulid Kitenge. Kipindi kinaanza na kibwagizo utasikia "maulid baraka wa kitenge jezi nambari 9 mgongoni alalalala goooooo".

Nikajenga mazoea ya kusikiliza nae mpira redioni katika mechi za yanga nilikua nasikia sana jina la Lunyamila kuashiria anawapeleka puta mabeki uko uwanjani, ilifika hatua nikawa nasikiliza mechi za Yanga nisikie tu namna anavyowatesa wapinzani. Lunyamila ndie alinifanya niipende Yanga ingawa nilikua namsikia redioni tu sikua namjua hata kwa muonekano, azam tv haikuwepo kipindi hicho

MANCHESTER UNITED: Ilikuaje nikaanza kuipenda hii timu? Usiku wa fainali ya champions league msimu wa 1998/1999 kati ya bayern Munich vs Man u. Mpaka kufikia hii siku sikua shabiki wa timu yoyote ulaya, bayern walitangulia kupata goli, tukiwa tumekusanyika mtaa mzima nyumbani kwa jirani yetu tunaangalia iyo game sebure nzima kulikua na huzuni kubwa sana nakumbuka wachezaji wa bayern kule benchi walishainuka wamepanga mstari huku wamekumbatiana mabegani kujiandaa na shangwe la ubingwa, furaha ilirudi pale sebureni baada ya Sosha kuchomoa goli dakika za mwisho kila mtu akijua game inaenda 120, Sosha akaweka cha pili. Nakumbuka refa alikua Collina muitary fulani hivi ananyoa kipara, nakumbuka beki wa bayern munich kufor alivyokua analia huku akipiga ngumi uwanja. Lile shangwe pale sebureni kwa jirani na mtaani baada ya mechi kuisha sitakuja kulisahau na ndio siku niliyoanza kuipenda manchester united.
Nyumbani Baba ni Yanga, Mama ni Simba.

Siku ambazo Yanga ilikuwa ikishinda, nyumba nzima tunaletewa zawadi, kuanzia watoto mpaka Mama. Kama ulikuwa na kosa unaasamehewa na siku hiyo hulazimishwi kulala mchana. Nyumbani tulikuwa na kuku alipewa jina la Sekilojo Chambua, ilo jina alipewa tangia akiwa kifaranga mpaka akawa Jogoo.

Kiufupi Yanga kushinda, tafsiri inayonijia ni Kwa namna gani familia yetu ilikuwa na furaha back in the days. Now days kila mmoja yuko anapopajua yeye, maisha ya utafutaji yametutawanya. Nyumbani kabaki Baba na Mama kama walivyoanza.
 
Back
Top Bottom