Ulianzaje kuipenda timu unayoishabikia?

Ulianzaje kuipenda timu unayoishabikia?

Arsenal
Fainali ya UEFA 2006 against Barcelona
Niliona kama wameonewa.
Kipa alipewa red card dakika za mwanzo tu kwa kuucheza mguu wa Etoo.

Nikawaonea huruma nikaanza kuwashabikia
Arsenal walipoteza kwa kufungwa 2-1

Arsenal ile ilikua ya akina Henry, Ebue n.k

Wakati barcelona ina akina Dinho, Etoo n.k
Naikumbuka ile game bila ile red cad ingekua bonge la game. Gunnerz alikua wa moto kabla ya fainali kampeleka nje real madrid na villareal ya requelme
 
Simba ilipoikimbiza Zamalek kwenye mvua enzi za kina Joseph Kaniki nikasema Yes hii ndo timu
Naikumbuka hii mkuu. Ingawa kipindi hicho mpira wa bongo tulikua tunasikiliza redioni. Big up sana bakhresa [emoji3][emoji3][emoji3] kwa kutuletea azam tv
 
Nilianza kufuatilia mpira mwaka 2004. Sikua na team ya kushabikia, nilikua naenjoy tu kuangalia mbungi inavyopigwa!

Mambo yalibadilika mwaka 2006, nilipomshuhudia nabii wa mwisho wa soka wa kuitwa Ronaldinho Gaucho. Hajawahi kutokea na hatokaa atokee mchezaji aliekamilika kumzidi Gaucho. Baada ya ile fainali, nikasilimu rasmi nakua shabiki wa Barcelona.

Mikoba ya Gaucho ikaja kurithishwa kwa mchawi wa kuitwa Leonel Andres Messi a.k.a Cuccitini. There was no turning back. Siku hizi hata mechi za EPL naangalia mara mojamoja sana. Ila mechi za Barcelona na Laliga kwa ujumla ndio sterehe yangu!
 
Nilianza kufuatilia mpira mwaka 2004. Sikua na team ya kushabikia, nilikua naenjoy tu kuangalia mbungi inavyopigwa!

Mambo yalibadilika mwaka 2006, nilipomshuhudia nabii wa mwisho wa soka wa kuitwa Ronaldinho Gaucho. Hajawahi kutokea na hatokaa atokee mchezaji aliekamilika kumzidi Gaucho. Baada ya ile fainali, nikasilimu rasmi nakua shabiki wa Barcelona.

Mikoba ya Gaucho ikaja kurithishwa kwa mchawi wa kuitwa Leonel Andres Messi a.k.a Cuccitini. There was no turning back. Siku hizi hata mechi za EPL naangalia mara mojamoja sana. Ila mechi za Barcelona na Laliga kwa ujumla ndio sterehe yangu!
Kabla ya ile red card ya jens lehman barca alikamatwa. Bila ya red card huenda ingekua bonge la game.
 
Kabla ya ile red card ya jens lehman barca alikamatwa. Bila ya red card huenda ingekua bonge la game.
Yes, ile game bila red card arsenal wangeshinda.

Robert Pires, Antonio Reyes, Fredrik Ldjumberg, Thierry Henry, Kolo Toure, Emmanuel Eboue. Sidhani kama ipo siku Arsenal watakua na team kama ile!
 
Nyumbani Baba ni Yanga, Mama ni Simba.

Siku ambazo Yanga ilikuwa ikishinda, nyumba nzima tunaletewa zawadi, kuanzia watoto mpaka Mama. Kama ulikuwa na kosa unaasamehewa na siku hiyo hulazimishwi kulala mchana. Nyumbani tulikuwa na kuku alipewa jina la Sekilojo Chambua, ilo jina alipewa tangia akiwa kifaranga mpaka akawa Jogoo.

Kiufupi Yanga kushinda, tafsiri inayonijia ni Kwa namna gani familia yetu ilikuwa na furaha back in the days. Now days kila mmoja yuko anapopajua yeye, maisha ya utafutaji yametutawanya. Nyumbani kabaki Baba na Mama kama walivyoanza.
Umenikumbusha maisha ya nyumbani, msosi wa kengele, hekaheka za bimkubwa,
Mikwara ya Mzee,
Dah tumetoka mbali sana
 
Arsenal
Fainali ya UEFA 2006 against Barcelona
Niliona kama wameonewa.
Kipa alipewa red card dakika za mwanzo tu kwa kuucheza mguu wa Etoo.

Nikawaonea huruma nikaanza kuwashabikia
Arsenal walipoteza kwa kufungwa 2-1

Arsenal ile ilikua ya akina Henry, Ebue n.k

Wakati barcelona ina akina Dinho, Etoo n.k
Kumbe bado dogo sana kijana
 
Yes, ile game bila red card arsenal wangeshinda.

Robert Pires, Antonio Reyes, Fredrik Ldjumberg, Thierry Henry, Kolo Toure, Emmanuel Eboue. Sidhani kama ipo siku Arsenal watakua na team kama ile!
Barca nae alikua kamili. Deco, gaucho, eto'o, zambrota yupo pembeni, puyol anamaliza nyuma alafu messi yupo benchi enzi bado ana mpira wa shule ule wa kupiga chenga timu nzima
 
Naikumbuka hii mkuu. Ingawa kipindi hicho mpira wa bongo tulikua tunasikiliza redioni. Big up sana bakhresa [emoji3][emoji3][emoji3] kwa kutuletea azam tv
Mi nilijikuta tu Moyo unadunda mechi inapoendelea mara uzungushe antenna ya redio
 
Nimezaliwa nimekuta Wazazi wangu wote ni mashabiki lia lia wa Simba na sisi watoto wote tukafuata mkondo huo huo.Kifupi familia yetu hakuna anaeshabikia Yanga mpaka watoto wetu.

Chelsea nilivutiwa na uchezaji wa Juan Sebastian Veron kipindi hicho kahamia Chelsea kutokea Man U.Mpaka leo mimi ni Simba damu na Chelsea
 
Sijawahi kuelewa mtu anakuwaje mshabiki wa Yanga. Mazingira ya makuzi yangu 'yalinishape' hivyo
 
LIVERPOOL
Ni Ile fainal na A.C Milan na Liverpool.. kipindi cha Kwanza liver alipigwa Goli tatu bila, kipindi cha pili Liverpool akasawazisha na baadae kushinda Kwa matuta.. Ndo mechi Bora zaidi kwenye michuano ya ulaya UEFA champions League.. Hadi wazungu wameibatiza jina la "instanbul miracle"

YANGA
Nilianza kuipenda kipindi cha Ivo Mapunda maana Mimi pia nilikua golikipa namba moja shuleni kwetu na Ivo ndo alikua role model wangu. Enzi hizo walikua wananiita "Tony Silver" huyu alikua golikipa wa Senegal enzi zile walitisha Sana world cup...
 
hatukumbuki ni lini,,kwanini na ilikuaje tukaanza kuipenda dar young africans
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom