Swali zuri sana.
Nilianza kuishabikia Yanga mwaka 1969 wakati Simba bado inaitwa Sunderland. Wakati huo timu kubwa Dar zilikuwa ni Yanga, Sunderland, na Cosmopolitan (hii sijui iliishia wapi). Siku hiyo Yanga ilikuwa inacheza robo fainali ya kombe la Ubingwa wa Afrika dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana, wakatoka droo ya 1-1 ikabidi zipigwe penalti ambapo yanga ilikosa penalti mbili huku Asante Kotoko ikikosa penalty moja tuy na hivyo wao kuibuke kidedea. Golikipa wa Yanga wakati huo aliyekuwa akiitwa Elias Michael alikuwa golikipa aliyeonyesha uwezo wa juu sana- alikuwa kivutio changu cha kwanza kwani hata mimi huko mtaani nilikuwa golikipa wa mtaa. Halafu wachezaji wakina Kitwana Manara, Maulid dilunga, Salehe Zimbwe, Leonard Chitete, Omar Kapera na wengineo walinifurahisha sana nikawa mwana Yanga kuanzia pale.
Mchezo wa Simba Vs Yanga pale Nyamagana pia nilikwenda kuuona kwa treni pamoja na kaka yangu. Gibsona Sembuli, na Sunday Manara walituvutia sana, ila kivutio kikubwa alikuwa ni Leodgar Tengan kwani tuliamabiwa alikuwa ansoma Engineering hapo Chuo Kikuu cha Dar. Kwa vile utotoni nnilikuwa nnaota sana Uhandisi, basi Tenga akaongeza kunivutia sana Yanga.
Kuna wakati nilipoteza stimu miaka ya sabini tulipofungwa 5-0 na simba baada ya timu kuwa imevunjika katika makundi mawili ya Pan-African (Raizon) na Yanga-Afrikan (kandambili).
Hata hivyo sijaacha kuipenda Yanga hata inapokuwa matatizoni