Ulevi wa pombe ni hatari kwa afya yako

Ulevi wa pombe ni hatari kwa afya yako

Pombe ni janga linalofungiwa macho na watu wengi Ila linaua vijana wengi sana na limeingiza wengi kwenye umasikini mkubwa wengi pia wamepoteza kazi au biashara zimefilisika Kwa ajili yo pombe.ikikukolea ni addiction mbaya Sanaa Ila inavituo vichache vya kusaidia waathirika
Yaani inatesa wengi.
 
Kitu cha kufurahisha kuhusu Starehe ni kuwa kila mtu anamsimanga mwenzake
1.Mlevi anamnanga mvuta sigara kuwa itamuua
2.Mvuta sigara anatamnanga Mwenda chumvini kuwa si salama
3.Mnywa soda anamnanga Mlevi
4.Mvuta kiko anamnanga mvuta sigara
5.Muhongaji anamnanga AnayeBET
6.Mzinzi anamnanga Mlevi
......
......
...... Kila mtu afanye Starehe yake yatakayomkuta atajua mwenyewe.
 
Natumaini nikimaliza mwezi wa tatu bila kilaji ndio nimeacha hivyo, kuna mdau humu alitoa ushauri mzuri sana juu ya pombe, me bado naiongele na nakaa na walevi sema sigusi kabisa nakula maji tu lengo baada ya muda nione kitu cha kawaida na hakina maana kabisa. Pombe ni mbaya sana nilikosea watu heshima na kuwa mtu wa hovyo sana. Uzi mzuri sana huu.
Sawa, ila usipende kutia mguu bar, na hao marafiki walevi jiepushe nao.
 
Kunywa pombe jenga Taifa lako zini jenga kaburi, mbona mlingano hauwiani;?!
 
Kwa hiyo?!? Maandiko hayo hayo yanasema "ACHENI MASIKINI" wanywe mvinyo wazisahau shida zao.
Wapi imeandikwa hivyo?
Hebu jihurumie na uwahurumie walevi wote wapone.

Usiwatie moyo na andiko fake.
 
Naomba utulie tuli kama maji ya mtungini, ukatae ukubali, siku zote pombe siyo chai.

RIP Marijan Rajabu
 
Nipo napiga BAMBODIER hapa yamwisho mwisho mkuu
 
Kuna mshakaji wangu mmoja laiti angalikuwemo JF basi angekutafuta ulipo akuondoe duniani.

Yeye kauli mbiu yake ni.

"Kijana wangu! Kula maishaaa, maisha ndio haya haya, ukifa unakufa peke yako, hata raba wahuni wanakuvua unazikwa kama mbwa"

Huwa nafurahi sana life style yake. Huwa hawazi kabisa sijui stress za maisha sijui kufa.. Aaahh anakula maisha tu
 
Alcohol may be man's worst enemy, but the bible says love your enemy.” “I drink to make other people more interesting.” “In wine there is wisdom, in beer there is Freedom, in water there is bacteria.” “First you take a drink, then the drink takes a drink, then the drink takes you.”
 
Kuna mshakaji wangu mmoja laiti angalikuwemo JF basi angekutafuta ulipo akuondoe duniani.

Yeye kauli mbiu yake ni.

"Kijana wangu! Kula maishaaa, maisha ndio haya haya, ukifa unakufa peke yako, hata raba wahuni wanakuvua unazikwa kama mbwa"

Huwa nafurahi sana life style yake. Huwa hawazi kabisa sijui stress za maisha sijui kufa.. Aaahh anakula maisha tu
Usimsingizie mshikaji wako, kama unataka kujua nilipo hebu njoo hapa Matejoo utanikuta nimejaa tele,ila usije na smart phone utajuta!!
 
Usimsingizie mshikaji wako, kama unataka kujua nilipo hebu njoo hapa Matejoo utanikuta nimejaa tele,ila usije na smart phone utajuta!!
Haha mimi sipigi mizinga nina mda kidogo nimechill nisome maisha yanavyoenda kwanza
 
Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;
Do not drink wine nor strong drink, thou, nor thy sons with thee, when ye go into the tabernacle of the congregation, lest ye die: it shall be a statute for ever throughout your generations: Walawi 10:9
 
Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu;
Do not drink wine nor strong drink, thou, nor thy sons with thee, when ye go into the tabernacle of the congregation, lest ye die: it shall be a statute for ever throughout your generations: Walawi 10:9
Watafsirie kwa kichaga pls
 
Nashukuru Mungu ni mwezi wa nne sasa tangu niache kunywa shetani nilikuwa na duka la kuuza pombe za jumla nashukuru nimemkataa shetani pamoja na kwamba nimeyumba Mungu ataninyanyua ki vingine PUMBAFU POMBE NENDA ZAKO KUZIMU
Uko wapi mkuu?
 
Back
Top Bottom