PreGE2025 Ulega ambana Mkandarasi barabara kuelekea Makao Makuu ya Jeshi (JWTZ), amtaka akabidhi barabara Disemba 2025

PreGE2025 Ulega ambana Mkandarasi barabara kuelekea Makao Makuu ya Jeshi (JWTZ), amtaka akabidhi barabara Disemba 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amemtaka Mkandarasi Kampuni ya CHICO kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kikombo – Chololo - Mapinduzi (Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi-TPDF) yenye urefu wa kilometa 16.4 kwa kiwango cha lami ifikapo mwezi Disemba, 2025.

Ulega ametoa maelekezo hayo jijini Dodoma, Juni 01, 2025 akiwa ameongozana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax na kukagua barabara hiyo ambayo utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua kwa sababu ya upungufu wa wafanyakazi na mitambo ya ujenzi.
WhatsApp Image 2025-06-01 at 20.49.56_51208456.jpg

WhatsApp Image 2025-06-01 at 20.50.01_0dad5b04.jpg
“Tumekagua barabara hii, Sijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wake sasa nitoe maelekezo mahususi kwa barabara hii, Mkandarasi afanye kazi usiku na mchana, aongeze vifaa na mitambo ya ujenzi lakini pia azalishe ajira kwa wakazi wa maeneo haya ili barabara hii ikamilike kwa viwango na muda tuliompa kimkataba”, amesisitiza Ulega.

Waziri Ulega amemuagiza Mkandarasi CHICO kuhakikisha anaboresha mpango kazi wake ili aweze kukamilisha kazi zilizobakia zikiwemo ujenzi wa makalvati pamoja na madaraja katika barabara hiyo.

Aidha, Waziri Ulega amebainisha kuwa Serikali hivi sasa ipo katika hatua za mwisho za manunuzi za kumpata Mkandarasi wa kujenga barabara ya njia nne na sita kuanzia Chamwino Ikulu hadi katikati ya jiji la Dodoma.
WhatsApp Image 2025-06-01 at 20.50.03_72536b0e.jpg

WhatsApp Image 2025-06-01 at 20.50.00_6151b9ed.jpg
Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax ameeleza kuwa ni matumaini yake ujenzi wa barabara hiyo utakamilika kwa muda uliopangwa na ikiwa na ubora na viwango vinavyotakiwa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj. Jabir Shekimweri amewashukuru Mawaziri hao kwa kufika na kukagua hatua za barabara hiyo kwani lengo la barabara hiyo ni kuleta muunganiko na ukaribu kati ya Wilaya za Dodoma Mjini na Chamwino hivyo utachochea maendeleo katika maeneo husika.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi wa miradi kutoka TANROADS, Mhandisi Japherson Nnko amewahakikishia Mawaziri hao kuusimamia kwa karibu utekelezaji wa ujenzi wa barabara hiyo ili ikamilike kwa muda uliopangwa ambapo hadi sasa umefikia asilimia 51.
 
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amemtaka mkandarasi anayejenga barabara ya Kikombo – Chololo - Mapinduzi inayokwenda kwenye Makao Makuu mapya ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kukamilisha kazi hiyo ifikapo Desemba mwaka huu.

Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 16.4 kwa kiwango cha lami umekuwa ukisuasua kutokana kwa kile kinachoelezwa kuwa ni upungufu wa wafanyakazi na mitambo ya ujenzi.

Ulega ametoa maelekezo hayo jijini Dodoma wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo akiwa amefuatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax pamoja na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali Salum Haji Othman na watendaji wengine wa wizara yake.

“Tumekagua barabara hii na sijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wake. Natoa maelekezo mahususi kwa barabara hii, mkandarasi afanye kazi usiku na mchana, aongeze vifaa na mitambo ya ujenzi lakini pia azalishe ajira kwa wakazi wa maeneo haya ili barabara hii ikamilike kwa viwango na muda tuliompa kimkataba”, amesema Ulega.

Waziri Ulega amemuagiza mkandarasi ambaye ni kampuni ya CHICO kuhakikisha anaboresha mpango kazi wake ili aweze kukamilisha kazi zilizobakia zikiwemo ujenzi wa makalvati pamoja na madaraja katika barabara hiyo.

 
Ulega mikwara mingi lakini vitendo ni zero kabisa. Wakandarasi washamfanya shamba la babu, kila siku anafoka lakini hachukui hatua yoyote ya serious ili kuwafanya wakandarasi wengine waogope.

Hawa wakandarasi ambao wanaifanya Tanzania shamba la bibi, kuna nchi za serious ambazo wanaziogopa na kuziheshimu kama vile Rwanda, Kenya nk. Huko hawawezi kuthubutu kusua sua katika miradi yao maana wanafahamu fika kitachowakuta.

Miradi ya BRT inamiaka zaidi ya mitatu sasa haijafika hata 50%. Miradi ya DMDP toka tumetangaziwa mpaka leo hakuna cha maana kinachofanyika.
 
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amemtaka Mkandarasi Kampuni ya CHICO kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kikombo – Chololo - Mapinduzi (Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi-TPDF) yenye urefu wa kilometa 16.4 kwa kiwango cha lami ifikapo mwezi Disemba, 2025.

Ulega ametoa maelekezo hayo jijini Dodoma, Juni 01, 2025 akiwa ameongozana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax na kukagua barabara hiyo ambayo utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua kwa sababu ya upungufu wa wafanyakazi na mitambo ya ujenzi.
“Tumekagua barabara hii, Sijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wake sasa nitoe maelekezo mahususi kwa barabara hii, Mkandarasi afanye kazi usiku na mchana, aongeze vifaa na mitambo ya ujenzi lakini pia azalishe ajira kwa wakazi wa maeneo haya ili barabara hii ikamilike kwa viwango na muda tuliompa kimkataba”, amesisitiza Ulega.

Waziri Ulega amemuagiza Mkandarasi CHICO kuhakikisha anaboresha mpango kazi wake ili aweze kukamilisha kazi zilizobakia zikiwemo ujenzi wa makalvati pamoja na madaraja katika barabara hiyo.

Aidha, Waziri Ulega amebainisha kuwa Serikali hivi sasa ipo katika hatua za mwisho za manunuzi za kumpata Mkandarasi wa kujenga barabara ya njia nne na sita kuanzia Chamwino Ikulu hadi katikati ya jiji la Dodoma.
Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Tax ameeleza kuwa ni matumaini yake ujenzi wa barabara hiyo utakamilika kwa muda uliopangwa na ikiwa na ubora na viwango vinavyotakiwa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj. Jabir Shekimweri amewashukuru Mawaziri hao kwa kufika na kukagua hatua za barabara hiyo kwani lengo la barabara hiyo ni kuleta muunganiko na ukaribu kati ya Wilaya za Dodoma Mjini na Chamwino hivyo utachochea maendeleo katika maeneo husika.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi wa miradi kutoka TANROADS, Mhandisi Japherson Nnko amewahakikishia Mawaziri hao kuusimamia kwa karibu utekelezaji wa ujenzi wa barabara hiyo ili ikamilike kwa muda uliopangwa ambapo hadi sasa umefikia asilimia 51.
Jeshi watumie kikosi chao cha ujenzi wa madaraja.
 
Back
Top Bottom