Kwa hiyo suluhisho, la mgogoro uliopo ni kwa cuf kugoma ili wafuatwe kubembelezwa na sio kuwa pro-active kusaka haki?
Sijui kama Shein akishaapishwa anaweza kustep down! Sidhani kama vurugu ni suluhu sahihi kwa both sides!
Ila pia mifano yako haina tija, hakimu anachofanya ni kutusaidia kufanya tafsiri ya vifungu ili kuona uko sahihi au umekosea wapi? Kama sheria ya mita 200 ipo ndani ya sheria zako hakimu hawezi kuificha, na ndio maana ya kudai haki mahakamani, si kusikilizwa matakwa yako!
Ugumu mkubwa kwa wanasiasa wa Tanzania ni kuwa tempted na ujanjaujanja wa ccm nanyi kuujaribu! Definitely vyama tawala duniani vinaweza kupindisha mambo, lkn kama alivyochangia mwenzangu hapo juu mechanisms za kufikia hukumu inaweza kuwa appealed kama haiko sawa! Lkn hata unapo appeal kwa wananchi una ground za kutosha kufanya hivyo!
Kwa case ya znz!
Yes Jecha amezuia matokeo na kuitisha uchaguzi mpya! Kinaweza kuwa kosa, lkn pia anaweza kuwa sahihi!
Seif amejitangaza mshindi jambo ambalo ni kosa kwa sheria za uchaguzi Zanzibar, kitendo kinachoweza hata kumpelekea kufungwa! Lkn Seif pia anaweza kuwa sahihi!
Sasa kipi ni sahihi kati ya hivi, hatuwezi kudebate wananchi, uwe ccm, cuf au chama chochote au huna chama! Ni suala linaloweza kuwa argued na our learned brothers!
Kwanza EU au popote bado ni maana sawa tu, tuna appeal hii issue ktk taasisi tunazohisi zinaweza kutoa maamuzi fulani lkn very unfortunately si EU, US, AU au UN zinazoweza kuhukumu zaidi ya mahakama zetu!
Kama tuna doubt our judicial system basi tujue hatuna nchi na kama hatuheshimu sheria tulizojipangia wenyewe hao EU ndio hatutowaogopa kabisa! Hii ni principle ktk utii wa sheria, tunaanza na kuheshimu taratibu tulizojiwekea kabla ya zile zilizokuwa imposed kwetu!