Ulaya wamgomea Magufuli

Ulaya wamgomea Magufuli

Mahakama zipi sasa?au unazungumzia hizi zilizopewa maagizo ya kuhukumu chap chap ?
hivi jecho angelikuwa mwenyekiti wa marefa ikatokea marefa wakatishia kuzichapa katikati ya mechi moja
basi suluhisho ni kufuta ligi nzima!
 
Kwa hiyo suluhisho, la mgogoro uliopo ni kwa cuf kugoma ili wafuatwe kubembelezwa na sio kuwa pro-active kusaka haki?
Sijui kama Shein akishaapishwa anaweza kustep down! Sidhani kama vurugu ni suluhu sahihi kwa both sides!
Ila pia mifano yako haina tija, hakimu anachofanya ni kutusaidia kufanya tafsiri ya vifungu ili kuona uko sahihi au umekosea wapi? Kama sheria ya mita 200 ipo ndani ya sheria zako hakimu hawezi kuificha, na ndio maana ya kudai haki mahakamani, si kusikilizwa matakwa yako!
Ugumu mkubwa kwa wanasiasa wa Tanzania ni kuwa tempted na ujanjaujanja wa ccm nanyi kuujaribu! Definitely vyama tawala duniani vinaweza kupindisha mambo, lkn kama alivyochangia mwenzangu hapo juu mechanisms za kufikia hukumu inaweza kuwa appealed kama haiko sawa! Lkn hata unapo appeal kwa wananchi una ground za kutosha kufanya hivyo!
Kwa case ya znz!
Yes Jecha amezuia matokeo na kuitisha uchaguzi mpya! Kinaweza kuwa kosa, lkn pia anaweza kuwa sahihi!
Seif amejitangaza mshindi jambo ambalo ni kosa kwa sheria za uchaguzi Zanzibar, kitendo kinachoweza hata kumpelekea kufungwa! Lkn Seif pia anaweza kuwa sahihi!
Sasa kipi ni sahihi kati ya hivi, hatuwezi kudebate wananchi, uwe ccm, cuf au chama chochote au huna chama! Ni suala linaloweza kuwa argued na our learned brothers!
Kwanza EU au popote bado ni maana sawa tu, tuna appeal hii issue ktk taasisi tunazohisi zinaweza kutoa maamuzi fulani lkn very unfortunately si EU, US, AU au UN zinazoweza kuhukumu zaidi ya mahakama zetu!
Kama tuna doubt our judicial system basi tujue hatuna nchi na kama hatuheshimu sheria tulizojipangia wenyewe hao EU ndio hatutowaogopa kabisa! Hii ni principle ktk utii wa sheria, tunaanza na kuheshimu taratibu tulizojiwekea kabla ya zile zilizokuwa imposed kwetu!

Hivi hamuoni ni jambo zuri sababu Cuf wamejitoa katika uchaguzi na mtashinda bila ya kutupiga mambomu!!?.Tatizo lipo wapi!!!?,tumewaachia kiroho safi kabisa nchi yenu mtawale kwa raha hamuoni huo ni uungwana !!?.Hatukuwa tukijua 'Machotara' hawana chao ktk ardhi ya mababu na mabibi zao ...
 
Unajuwa hapa ndipo penye utamu wote wa hii Oscar winning movie ya Jecha. Ikiwa Jecha atalazimisha CUF na vyama vyengine kuviweka kwenye polling card, legally watakuwa wameshiriki uchaguzi japokuwa watakuwa hawana wakala kama ilivyokuwa kwa vyama vyengine vidogo vilivyokuwa havina uwezo wa kuweka wakala kila kituo. Kwa maana hiyo wataweza kupeleka malalamiko yao mahakamani na kupinga matokeo ya uchaguzi.

Scenario ya pili ambayo Jecha & co hawaipendelei ni kuwatoa kwenye polling process CUF na vyama vyengine vilokataa kushiriki. Lakini hata kama hawatakuwa wameshiriki basi wanayo haki ya kwenda kupinga matokeo mapya mahakamani kwa vile hakukuwa na uhalali wa kufutiwa matokeo yao ya Oct 2015. Wa kwenda mahakamani alikuwa Jecha kuomba kufutwa kwa matokeo yale kwa vile ni mahakama pekee ndio ilikuwa yenye uwezo wa kubadilisha matokeo na alikuwa hana legal auyhority ya kufuta yale matokeo na kwa maana hiyo kauli yake kisheria ilikuwa haisihi. Ufahamu ya kwamba CUF hawatokwenda kupinga matokeo ya uchaguzi hapa, watakachokwenda kupigania ni uhalali wa matokeo yao, na sio kuweka pingamizi ya matokeo ya uchaguzi kwa vile Jecha kaamua kutoa hati za udiwani na uwakilishi mara mbili, jee ipi ni halali? Huwezi kuuza nyumba yako kwa watu wawili tofauti kwa wakati tofauti. Obviously mauzo ya mara ya pili yatakuwa legally void kwa vile ulipouza mara ya pili ulikuwa unauza kitu si chako, na hicho ndicho anachofanya Jecha!
Kwenda maakaman cuf nisawa na kesi yanyan umpelekee tumbili
 
Sielewi kwa nini cuf kama wanaamini kuwa zec imekosea, si waende mahakamani ili haki ipatikane. Wanaogopa nini kwenda mahakamani?
Mahakama hiyo iko mbinguni?mahakimu wanatokea wapi?hawa waliopokea amri ya mkuu wa kaya siku ile ya Law?
 
Back
Top Bottom