Ulaya pamenishinda narudi bongo

Ulaya pamenishinda narudi bongo

Status
Not open for further replies.
Mim mwehu ndama kijana wa kitanzania niliwah kuandika uzi kuomba msaada kuhusu jinsi yakupata visa yakuingia nchini Sweden, na nashukuru Kwa maoni ya baadhi ya wadau nilifanikiwa kufuata ushauri nakufanikiwa kutia maguu ndani ya bara la uropa.

Lakini tangu nilipotoka bongo nakufika hapa ughaibuni huku kichwani nikiwa na lengo la kujilipua nakubaki huku moja Kwa moja maisha yamekua tofauti na nilivyo fikiria..
Ukizingatia mwenyeji wangu nayeye anaishi hapa kiujanja ujanja.

Niliomba visa ya wiki 3 na bahati nzuri baada yakufika hapa na nlipokaribia KUMALIZA muda wangu waliniongeza miezi mingine 3.

Lakini sasa sioni kinachobadilika katika maisha yangu zaidi yakupata huduma nzuri ya chakula nakuvuta hewa Safi hapa Uppsala .

Kiukweli maisha ya hapa yanazidi kuwa magumu Kwa upande wangu sababu nimejaribu kuanzisha mahusiano na mabinti, wanawake watu wazima Hadi vikongwe ili kusudi atakae jaa nioe ili niweze kupata makaratasi lakini nawao wamekuwa wagumu.

Sitaki kujivika status za kikimbizi maana nahisi ntaaribu kabisa mpangilio wote wa maisha yangu nakuitendea ubaya elimu yangu niliyoipata Kwa shida bongo land.

Nimekua mzururaji na cha ajabu hata zile KAZI za kubeba box nilizokua nazisikia zikisemwa Sana na wadau humu jf sizipati.

Kwa kifupi uchumi wangu umedidimia mara 100 zaidi ya hata nilivyokua bongo , mpaka najuta Kwa nini nilitumia pesa yangu nlioichanga Kwa shida kama nauli yakuja huku uzunguni pasipo na manufaa ya kiuchumi kwangu.

Hapa navyoongea nimeshawasilisha ombi la msaada wa nauli ya kurudi nyumbani katika kanisa naloSali hapa Uppsala.

Kwa kifupi narudi nyumbani na nikifika hapo Kwa mkuu jiwe naenda moja Kwa moja kijijini kwetu namanditi songea kulima.

Bye bye wabongo mliopo Sweden mim maisha yamenishinda narudi nyumbani.

View attachment 1389715View attachment 1389716

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana, angalau umethubutu kukiri mapema kuwa ughaibuni hapajakufaa, wazamiaji wengine hawasemi lolote hukomaa kibishi wakati wakiwa na maisha magumu tu. Mkataa kwao ni mtumwa, we rudi tu home ilimradi usije kutuongezea Corona hapa nyumbani.

Kutamani kwako kurudi hakutukatishi tamaa sie wengine wenye ndoto za kuja ughaibuni, tutakuja tu! Maana hapa maisha sio kabisa. Sie hatuamini kama huko ni pagumu, labda ni fikra zako za kupambana zimefikia ukomo. Hao mademu na vibibi ulivyotongoza ndani ya miezi mitatu ni vingapi!? Yaani ilitoka bongo, weapon yako kubwa ikiwa ni mb*o... Na haijakupa matumaini yoyote ndani ya kipindi cha miezi mitatu! Uliamini wanaume walioko huko wote ni vibamia, kwamba umekwenda kuwakomboa kina mama na vibibi kwa kutofikishwa Uhuru peak!? Acha uboya mwana!! Komaa!! Mawazo ya kurudi bongo ni uchuro kabisa, bora hata awamu hii ingekuwa inafika ukingoni. Ukirudi utajuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unataka utuletee Corona?
Corona ilishatia maguu, mkuu ni hatari sana sijui tutakimbilia wapi,mtanzania mmoja aliyewasili nchini kutokea ubelgiji alitembelea Sweden na denmark baada ya kufanyiwa vipimo na kugundulika na covid 19.serikali inachukua tahadhari ya hali ya juu kuzuia maambukizi.
By ummy mwalimu waziri wa afya.
 
Mwanaume komaa.Cheza hata kiduku weka bakuli la pesa wapo watakaokuchangia.Ina maana miezi mitatu humo kanisani hujapata rafiki wa kizungu wa kubadilishana nae mawazo.
 
Mkuu bora urudi,,,ulaya ni kupoteza muda,,Mimi Nina week tangia nifanye maamuzi ya kurudi kutoka France,,, ulaya yote sasa imajaa waarabu na watu weusi wengi wao wakiiingia kwa njia za panya kutokea Libya na Morocco...kupitia BAHARI...ukitokea Libya unaitafuta Italy,,,wanaotokea Morocco wanaibukia Spain,,makundi kwa makundi,,, mkuu ulaya ya Leo sio ile ya zamani .ULAYA YA LEO KUNA ROBA ZA MBAO,,,.now kazi za box hakuna,,,rudi nyumbani mkuu,,usipoteze muda wako..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna fursa gani huko ya kuwekeza kama nikija na milioni 10 za kibongo. Naomba uzoefu mwehu ndama
Mkuu, yaani unataka kutumia pesa za Kitanzania(Tsh) kuwekeza kwenye nchi za watu walio mbele kimaendeleo? Siku zote huwa naona watu wanatoa pesa kwenye nchi zilizoendelea kuwekeza nchi zinazoendelea( Developing countries).

Na kama utataka kutumia pesa zako katika nchi zilizoendelea labda iwe kununua bidhaa za kuuza nyumbani.

Uwekezaji katika nchi zilizoendelea unahitaji mtaji mkubwa na innovation ya hali ya juu. Maana hiyo milioni 10 kwa mfano, Sweden ni sawa na around SEK 45,000. Hii pesa ni ndogo kuwekeza katika nchi iliyoendelea kama Sweden. Hiyo pesa ni sawa na mshahara wa Lecturer wa Chuo Kikuu kwa mwezi mmoja tu. Pesa ambayo ni ya kawaida sana.

Nchi za wenzetu hakuna mambo sijui ya kuanza kidogokidogo unajiegesha mahala. Kama umepanga kuwekeza ni uwekezaji kweli siyo kubabaisha.!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom