Kitambo kidogo kilipita tukiwa tunazungumza, punde niliona sahani zenye vyakula zikiletwa na kuwekwa kwenye meza. Macho yangu yalisimama ilipo sahani iliyokuwa imejaa kuliko zote. Nilijiuliza mbona sahani ile ilikuwa imejaa kuliko zingine. Akili yangu ikaniambia huenda sahani ile ni Baba Mkwe. Kimoyo moyo nikasema Baba Mkwe anafukia duuuh!
Basi Dada mkubwa alianza kwa kuwatengea Baba, na Mama lakini kilichonishtua hakuichukua ile sahani iliyojaa kuliko kawaida. Hapo ikabidi nisubiri nione kijeba anayeweza kufukia msosi wote ule. Niliapa nikimjua nitamheshimu na kumsalimia shikamoo pale pale hata kama ni ukweni.