Ukweli wa tuhuma za Pinda huu hapa

Ukweli wa tuhuma za Pinda huu hapa

hivi hakuna wa kuiba hiyo ripoti akaipandisha humu jukwaani kabla haijachakachuliwa?mbona mitihani inaibiwa kirahisi na watoto wa shule!
Tulishaomba kitambo hata hiyo Bank statement iwekwe humu lakini imeshindikana. Nina hakika hata ukiipandisha itashushwa ndani ya sekunde kadhaa. Today's JF isn't what it used to be.
 
Wakuu habari za asubuhi .Kile kinachoonekana kuwa ni kuchafuliwa kwa eaziri mkuu mh. Mizengo Pinda hivi karibuni kimebainika.
Vigogo wasaka urais na Wabunge mbalimbali kama David Kafulila, Sendeka, Serukamba na Ligola wakiwa wamelishika sakata la bilioni 200 za Escrow na wengine wakiwa wanataka Pinda ang'olewe katika nafasi yake ya waziri mkuu.

Imefahamika kuwa si kweli kuwa mtoto huyu wa mkulima anahusika. Bali ni vita kati ya wabunge, baadhi ya mawaziri na Urais 2015.Mivutano ifuatayo ndiyo inayomtia kitanzini mzee wa kimyakimya.

VITA YA WABUNGE :Inasemekana David Kafulila anatumiwa na mh. Mbunge tajiri Nimrod Mkono. Mkono ana ugomvi mkubwa na TANESCO kutokana na malipo yake ya mamilioni ya dola aliyokua analipwa na serikali kila mwezi kupitia TANESCO kusitishwa na Muhongo na katibu mkuu wake Maswi.

Malipo haya tata yalikuwa ni ya kazi ya Mkono kama mwanasheria wa TANESCO. Hoja hapa ilikua ni kubainika kuwa malipo hayo yalikuwa mkubwa sana na yaligubigwa na giza katika kiwango cha malipo. Hivyo Mkono anataka Prof Muhongo ang'olewe katika wizara ya nishati na madini kama kisasi.

Ndipo David Kafulila akapewa kazi hiyo kupitia ESCROW na anakula pesa za Mkono kwa kazi hii.

CHRISTOPHER OLE SENDEKA:

Huyu ni Mbunge wa Simanjiro na rafiki kipenzi wa Reginald Mengi wa IPP. Mtakumbuka vita ya mzee Mengi na Muhongo juu ya vitalu vya gesi hivi karibuni. Wawili hawa walichapana sana hadharani na kwenye makongamano huku Muhongo akidai kuwa Mengi ni dalali na sio mfanyabiashara. Hasira za Mengi zimeelekezwa katika kumng'oa prof Muhongo katika kiti chake cha uwaziri.

Hii ilibainika wakati wa kupitisha bajeti ya prof Muhongo mwaka huu. Baadhi ya wabunge wanasemekana kuhongwa ili wamshambulie Muhongo na kukwamisha bajeti yake. Kazi hii inafanyika sasa kupitia sakata la ESCROW. Ole Sendeka anasemekana kutumiwa na bilionea Mengi kumchapa Muhongo kama kisasi cha sakata la vitalu lililomvua nguo Mengi.

SERUKAMBA,FILIKUNJOMBE:

Wabunge hawa wanaongoza kundi la wabunge wa kambi ya mgombea Urais mmoja wa CCM mwenye nywele nyeupe. Hawa nia yao hasa ni kumchapa Pinda. Wanatumwa na kupewa fedha ili kuhakikisha kwa gharama yoyote wanatumia vuguvugu hili kama fursa ya kumsafishia njia mgombea wao kwa kumuhusisha Waziri Mkuu Pinda na sakata la ESCROW.

Lengo hapa ni kumuondoa madarakani japo hahusiki ili ionekane kuwa hata mgombea wao aliwajibika kisiasa tu na hivyo kumsafishia njia nywele nyeupe. Aidha katika siku za karibuni Pinda anasemekana tangu kuanza kutajwa kugombea Urais amepata kuungwa mkono sana na kuvuna wapambe wengi wa wagombea wengine akiwemo Nywele nyeupe.

Pinda ameonekana kuwapiku wenzie walioanza mbio hizi mapema kutokana na uadilifu wake na kuwa ni mtu anayependa watu, asiye na majivuno na aliyekuwa karibu sana na baba wa taifa hayati mwalimu Nyerere . Hivyo ni lazima ashughulikiwe apunguzwe kasi na ikiwezekana ajiuzulu kabisa ili kufanya safari ya nywele nyeupe kuwa nyepesi.

BARAZA KUU UVCCM :

Juhudi za kumchafua Pinda zimeendelea pia wakati wa vikao vya BARAZA KUU la UVCCM Dodoma. Kazi hii inaratibiwa na kada mmoja wa CCM mwenye asili ya Somalia akiwa ameweka kambi Dodoma. Kada huyu ameleta kundi la vijana zaidi ya 30 wasiokua wajumbe wala watumishi wa CCM kutoka sehemu mbalimbali.

Vijana hawa walikua Dodoma wakila na kunywa na kulipwa posho Kazi yao kubwa ikiwa ni kurandaranda katika baa na kumbi zote za Dodoma usiku na mchana kufuatilia wafuasi wa Pinda wamekaa na nani na namna bora ya kumchafua Waziri Mkuu kwa kumuhusisha na ugawaji wa pesa. Kundi hili lilizagaa Dodoma kama paka wa baa kunusa kila mahali na kuandika mitandaoni kumchafua mzee Pinda.

Inasemekana posho yao ilikua kati ya sh 100,000 na 200,000 kulingana na taarifa unayopeleka kwa kada huyo Msomali. Uroho wa pesa uliwafanya vijana hao kupeleka taarifa za uongo mradi wapate kula yao.Hii ndio hali halisi wakuu juu ya mambo haya ambayo nimeyafanyia kazi
kwa kina.

Pinda anaonekana ni tishio kwa wataka Urais ndani ya CCM.

Swali la uelewa,, ela ya escrow imeliwa au haikuliwa?
 
Ray Jay inaelekea wewe ni mchunguzi binafsi mwenye uwezo wa kufanya uchunguzi na kuleta uzi mtandaoni. Ninakutaka utujulishe baada ya kufanya uchunguzi wako vile vile kama hiyo hela ya escroll account imeingia kwenye mifuko ya nani na kila mmoja amekula kiasi gani, kama huwezi hilo basi nawe ni shabiki wa kisisas unachumia tumbo.
 
Mleta mada kwani team pinda unacheza namba ngapi maana unataka ushindi kabla ya matokeo subiri ripoti tujue ukweli
 
Wow mkuu Sana Chabruma umerudi??

Habari za kazi na masahibu mengi?

Ktk sakata la ESCROW hakuna nisichokijua maana mie ni miongoni mwa vidagaa tunaohangaishwa maofisini kuziba matundu boma lisibomoke....

Mimi naangalia kweli... Kweli tupu ndio maana siangalii nasaba...imani au itikadi ya MTU ktk utoaji Wa maoni isipokuwa content....

Swali la kizushi: Kama hili suala ni jepesi na la kitoto mbona ripoti haiwekwi hadharani?

Kama ni jepesi hivyo tunahangaika nini kiasi cha kukosa usingizi kutafuta Huruma ya wafadhili?

Hizi danadana za nini?

Achana nae huyo!Laana ya kumshambulia Warioba bado inamtafuna.Kajifumbia macho.
 
Last edited by a moderator:
Jay jay uliyosema hayaingii akilini, huo ni mchezo wa kisiasa, umejitahidi kutunga tungo nzuri BUT we need a REPORT ya CAG kuhusu akauti ya ESCROW hapo tutajua pumba ni zipi aliyeonewa ni nani?
 
hivi hakuna wa kuiba hiyo ripoti akaipandisha humu jukwaani kabla haijachakachuliwa?mbona mitihani inaibiwa kirahisi na watoto wa shule!

Pinda kaificha kisumbawanga-sumbawanga, kama siyo mtu wa kamati huwezi kuiona japo iko peupe ofisini kwake.
 
As much as I hate ccm,but nimeshangazwa sana na namna anavyoshughulikiwa Mh. Pinda,inaonekana kuna movie ya hatari na ya pamoja... yaani habari mbaya kumhusu pinda utazikuta magazeti kadhaa yale yale kila siku na kwa maudhui yale yale ... inavyoonekana kuna watu wamepewa kazi moja tu ya kudeal nae....
 
Wakuu habari za asubuhi .Kile kinachoonekana kuwa ni kuchafuliwa kwa eaziri mkuu mh. Mizengo Pinda hivi karibuni kimebainika.
Vigogo wasaka urais na Wabunge mbalimbali kama David Kafulila, Sendeka, Serukamba na Ligola wakiwa wamelishika sakata la bilioni 200 za Escrow na wengine wakiwa wanataka Pinda ang'olewe katika nafasi yake ya waziri mkuu.

Imefahamika kuwa si kweli kuwa mtoto huyu wa mkulima anahusika. Bali ni vita kati ya wabunge, baadhi ya mawaziri na Urais 2015.Mivutano ifuatayo ndiyo inayomtia kitanzini mzee wa kimyakimya.

VITA YA WABUNGE :Inasemekana David Kafulila anatumiwa na mh. Mbunge tajiri Nimrod Mkono. Mkono ana ugomvi mkubwa na TANESCO kutokana na malipo yake ya mamilioni ya dola aliyokua analipwa na serikali kila mwezi kupitia TANESCO kusitishwa na Muhongo na katibu mkuu wake Maswi.

Malipo haya tata yalikuwa ni ya kazi ya Mkono kama mwanasheria wa TANESCO. Hoja hapa ilikua ni kubainika kuwa malipo hayo yalikuwa mkubwa sana na yaligubigwa na giza katika kiwango cha malipo. Hivyo Mkono anataka Prof Muhongo ang'olewe katika wizara ya nishati na madini kama kisasi.

Ndipo David Kafulila akapewa kazi hiyo kupitia ESCROW na anakula pesa za Mkono kwa kazi hii.

CHRISTOPHER OLE SENDEKA:

Huyu ni Mbunge wa Simanjiro na rafiki kipenzi wa Reginald Mengi wa IPP. Mtakumbuka vita ya mzee Mengi na Muhongo juu ya vitalu vya gesi hivi karibuni. Wawili hawa walichapana sana hadharani na kwenye makongamano huku Muhongo akidai kuwa Mengi ni dalali na sio mfanyabiashara. Hasira za Mengi zimeelekezwa katika kumng'oa prof Muhongo katika kiti chake cha uwaziri.

Hii ilibainika wakati wa kupitisha bajeti ya prof Muhongo mwaka huu. Baadhi ya wabunge wanasemekana kuhongwa ili wamshambulie Muhongo na kukwamisha bajeti yake. Kazi hii inafanyika sasa kupitia sakata la ESCROW. Ole Sendeka anasemekana kutumiwa na bilionea Mengi kumchapa Muhongo kama kisasi cha sakata la vitalu lililomvua nguo Mengi.

SERUKAMBA,FILIKUNJOMBE:

Wabunge hawa wanaongoza kundi la wabunge wa kambi ya mgombea Urais mmoja wa CCM mwenye nywele nyeupe. Hawa nia yao hasa ni kumchapa Pinda. Wanatumwa na kupewa fedha ili kuhakikisha kwa gharama yoyote wanatumia vuguvugu hili kama fursa ya kumsafishia njia mgombea wao kwa kumuhusisha Waziri Mkuu Pinda na sakata la ESCROW.

Lengo hapa ni kumuondoa madarakani japo hahusiki ili ionekane kuwa hata mgombea wao aliwajibika kisiasa tu na hivyo kumsafishia njia nywele nyeupe. Aidha katika siku za karibuni Pinda anasemekana tangu kuanza kutajwa kugombea Urais amepata kuungwa mkono sana na kuvuna wapambe wengi wa wagombea wengine akiwemo Nywele nyeupe.

Pinda ameonekana kuwapiku wenzie walioanza mbio hizi mapema kutokana na uadilifu wake na kuwa ni mtu anayependa watu, asiye na majivuno na aliyekuwa karibu sana na baba wa taifa hayati mwalimu Nyerere . Hivyo ni lazima ashughulikiwe apunguzwe kasi na ikiwezekana ajiuzulu kabisa ili kufanya safari ya nywele nyeupe kuwa nyepesi.

BARAZA KUU UVCCM :

Juhudi za kumchafua Pinda zimeendelea pia wakati wa vikao vya BARAZA KUU la UVCCM Dodoma. Kazi hii inaratibiwa na kada mmoja wa CCM mwenye asili ya Somalia akiwa ameweka kambi Dodoma. Kada huyu ameleta kundi la vijana zaidi ya 30 wasiokua wajumbe wala watumishi wa CCM kutoka sehemu mbalimbali.

Vijana hawa walikua Dodoma wakila na kunywa na kulipwa posho Kazi yao kubwa ikiwa ni kurandaranda katika baa na kumbi zote za Dodoma usiku na mchana kufuatilia wafuasi wa Pinda wamekaa na nani na namna bora ya kumchafua Waziri Mkuu kwa kumuhusisha na ugawaji wa pesa. Kundi hili lilizagaa Dodoma kama paka wa baa kunusa kila mahali na kuandika mitandaoni kumchafua mzee Pinda.

Inasemekana posho yao ilikua kati ya sh 100,000 na 200,000 kulingana na taarifa unayopeleka kwa kada huyo Msomali. Uroho wa pesa uliwafanya vijana hao kupeleka taarifa za uongo mradi wapate kula yao.Hii ndio hali halisi wakuu juu ya mambo haya ambayo nimeyafanyia kazi
kwa kina.

Pinda anaonekana ni tishio kwa wataka Urais ndani ya CCM.

Na wewe umejiPinda kuandika haya yote kwa sababu ni kibaraka wa TIMU PINDA unacheza namba ipi...?????????
 
Chonde chonde viongozi wetu wapendwa suala la kuusaka urais ndani ns nje ya ccm lisije kuipasua nchi mjue uongozi utoka kwa mungu
 
N a safari hii Zito kawaamualia kweli mlimtumia mkamuharibia yake, mkamshauri aende mahakamani ili aendelee kuwa mbunge mkijua atabaki kwenye kamati iliafiche uozo wenu eee, kwa hela mlizokuwa mnampa mpaka Muhongo akamuonea wivu bora mngeacha aukose na huo ubunge, sasa mtakoma kama mbwai iwe mbwai tu, na nyie mkimbilie mahakamani muwe mawaziri wa mahakama, mlibwatuka weeee, Kwanini chadema imfukuze zito mkijua mnamfurahisha eeeee! imekula kwenu. Zito mwaya sema sema usiogope sema wamekutumia wale panya waoneshe wewe sumu manina.
 
p.mb.vu unadhani huu ni wakati wa kudanganya watu wenye akili?? nijibu kwanini wafadhiri wamekata misaada??,
Wakuu habari za asubuhi .Kile kinachoonekana kuwa ni kuchafuliwa kwa eaziri mkuu mh. Mizengo Pinda hivi karibuni kimebainika.
Vigogo wasaka urais na Wabunge mbalimbali kama David Kafulila, Sendeka, Serukamba na Ligola wakiwa wamelishika sakata la bilioni 200 za Escrow na wengine wakiwa wanataka Pinda ang'olewe katika nafasi yake ya waziri mkuu.

Imefahamika kuwa si kweli kuwa mtoto huyu wa mkulima anahusika. Bali ni vita kati ya wabunge, baadhi ya mawaziri na Urais 2015.Mivutano ifuatayo ndiyo inayomtia kitanzini mzee wa kimyakimya.

VITA YA WABUNGE :Inasemekana David Kafulila anatumiwa na mh. Mbunge tajiri Nimrod Mkono. Mkono ana ugomvi mkubwa na TANESCO kutokana na malipo yake ya mamilioni ya dola aliyokua analipwa na serikali kila mwezi kupitia TANESCO kusitishwa na Muhongo na katibu mkuu wake Maswi.

Malipo haya tata yalikuwa ni ya kazi ya Mkono kama mwanasheria wa TANESCO. Hoja hapa ilikua ni kubainika kuwa malipo hayo yalikuwa mkubwa sana na yaligubigwa na giza katika kiwango cha malipo. Hivyo Mkono anataka Prof Muhongo ang'olewe katika wizara ya nishati na madini kama kisasi.

Ndipo David Kafulila akapewa kazi hiyo kupitia ESCROW na anakula pesa za Mkono kwa kazi hii.

CHRISTOPHER OLE SENDEKA:

Huyu ni Mbunge wa Simanjiro na rafiki kipenzi wa Reginald Mengi wa IPP. Mtakumbuka vita ya mzee Mengi na Muhongo juu ya vitalu vya gesi hivi karibuni. Wawili hawa walichapana sana hadharani na kwenye makongamano huku Muhongo akidai kuwa Mengi ni dalali na sio mfanyabiashara. Hasira za Mengi zimeelekezwa katika kumng'oa prof Muhongo katika kiti chake cha uwaziri.

Hii ilibainika wakati wa kupitisha bajeti ya prof Muhongo mwaka huu. Baadhi ya wabunge wanasemekana kuhongwa ili wamshambulie Muhongo na kukwamisha bajeti yake. Kazi hii inafanyika sasa kupitia sakata la ESCROW. Ole Sendeka anasemekana kutumiwa na bilionea Mengi kumchapa Muhongo kama kisasi cha sakata la vitalu lililomvua nguo Mengi.

SERUKAMBA,FILIKUNJOMBE:

Wabunge hawa wanaongoza kundi la wabunge wa kambi ya mgombea Urais mmoja wa CCM mwenye nywele nyeupe. Hawa nia yao hasa ni kumchapa Pinda. Wanatumwa na kupewa fedha ili kuhakikisha kwa gharama yoyote wanatumia vuguvugu hili kama fursa ya kumsafishia njia mgombea wao kwa kumuhusisha Waziri Mkuu Pinda na sakata la ESCROW.

Lengo hapa ni kumuondoa madarakani japo hahusiki ili ionekane kuwa hata mgombea wao aliwajibika kisiasa tu na hivyo kumsafishia njia nywele nyeupe. Aidha katika siku za karibuni Pinda anasemekana tangu kuanza kutajwa kugombea Urais amepata kuungwa mkono sana na kuvuna wapambe wengi wa wagombea wengine akiwemo Nywele nyeupe.

Pinda ameonekana kuwapiku wenzie walioanza mbio hizi mapema kutokana na uadilifu wake na kuwa ni mtu anayependa watu, asiye na majivuno na aliyekuwa karibu sana na baba wa taifa hayati mwalimu Nyerere . Hivyo ni lazima ashughulikiwe apunguzwe kasi na ikiwezekana ajiuzulu kabisa ili kufanya safari ya nywele nyeupe kuwa nyepesi.

BARAZA KUU UVCCM :

Juhudi za kumchafua Pinda zimeendelea pia wakati wa vikao vya BARAZA KUU la UVCCM Dodoma. Kazi hii inaratibiwa na kada mmoja wa CCM mwenye asili ya Somalia akiwa ameweka kambi Dodoma. Kada huyu ameleta kundi la vijana zaidi ya 30 wasiokua wajumbe wala watumishi wa CCM kutoka sehemu mbalimbali.

Vijana hawa walikua Dodoma wakila na kunywa na kulipwa posho Kazi yao kubwa ikiwa ni kurandaranda katika baa na kumbi zote za Dodoma usiku na mchana kufuatilia wafuasi wa Pinda wamekaa na nani na namna bora ya kumchafua Waziri Mkuu kwa kumuhusisha na ugawaji wa pesa. Kundi hili lilizagaa Dodoma kama paka wa baa kunusa kila mahali na kuandika mitandaoni kumchafua mzee Pinda.

Inasemekana posho yao ilikua kati ya sh 100,000 na 200,000 kulingana na taarifa unayopeleka kwa kada huyo Msomali. Uroho wa pesa uliwafanya vijana hao kupeleka taarifa za uongo mradi wapate kula yao.Hii ndio hali halisi wakuu juu ya mambo haya ambayo nimeyafanyia kazi
kwa kina.

Pinda anaonekana ni tishio kwa wataka Urais ndani ya CCM.
 
Wow mkuu Sana Chabruma umerudi??

Habari za kazi na masahibu mengi?

Ktk sakata la ESCROW hakuna nisichokijua maana mie ni miongoni mwa vidagaa tunaohangaishwa maofisini kuziba matundu boma lisibomoke....

Mimi naangalia kweli... Kweli tupu ndio maana siangalii nasaba...imani au itikadi ya MTU ktk utoaji Wa maoni isipokuwa content....

Swali la kizushi: Kama hili suala ni jepesi na la kitoto mbona ripoti haiwekwi hadharani?

Kama ni jepesi hivyo tunahangaika nini kiasi cha kukosa usingizi kutafuta Huruma ya wafadhili?

Hizi danadana za nini?
Kaka Lusungo namshukuru Mungu kukurudishia ufahamu. Dumu hivyo hivyo maana ulikuwa unapotea bro.
Ndaga fijo nkhulumba.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hatulazimishwi kusoma ulichoandika. Ifike wakati mjue kuwa wasomaji wenu sio wajinga kama mnavyo fikiri. Umeandika haya kwa msukumo gani? Unajaribu kutuhamisha kutoka wapi kwenda wapi! Je unadhani umeandika nini kiasi cha kuamini kuwa ni kikubwa kuliko tunachokijua?.
 
Siyo BURE. Mleta mada lazima utakuwa umerogwa na mchawi wako amekwisha faliki. Ni bayana kabisa kuwa unawaza na kufikiri kwa kutumia MAKALIO. Na waliyokuta hao MAFISADI WA KIMYA KIMYA, wambie wajipange upya kwan Watz cku hizi hawapo CHEAP KIASI HICHO.
 
Back
Top Bottom