Ukweli ni upi kuhusu tukio la Scorpion wa Buguruni?

View attachment 415577

Kama ambavyo raia wengine walivyoshtushwa na tukio zima la kusisimua kuhusu bwana Salim Njwete 'Scorpion', kumnyofoa macho ndugu Said, nami ndivyo nilivyopata mshangao na butwaa juu.

Sitaki kurejea tena sakata hilo kwa kuwa kila mtu analifahamu. Badala yake nitajikita zaidi kwenye kile nilichokifahamu baada ya tukio. Sitaongeza wala kupunguza neno.

Usiku wa tarehe 9/10/2016, siku chache baada ya tukio hili kutokea, nilifika eneo la tukio kuokoteza mawili matatu kuhusu ishu nzima.

Magazeti, Televisheni na mitandao ya kijamii ilinilisha taarifa za kutosha, lakini ziliniacha na maswali ambayo nisingeweza kupata majibu isipokuwa kwa kufika mwenyewe eneo la tukio na kuuliza. Hivyo nikaenda.

Shauku ilinipa sababu za kuhoji. Nikahoji kuanzia barabarani kwa wafanyabiashara ninaofahamiana nao pale. Nikaenda kuhoji mtaani kwetu nilipokuwa nikiishi zamani (niliwahi kuishi Buguruni miaka ya 2010 kurudi nyuma), mwisho nikamalizia kuhoji kwa waendesha bajaj na bodaboda ninaowafahamu. Hawa wote wapo katika kitovu cha eneo ambako tukio hili lilitokea, nikaonyeshwa mpaka meza ya nyama ambako ndiko tukio hili ulifanyika...

Tuendelee..

Nilielezwa kuwa, huyu scorpion amekuwa ni mwenyeji wa eneo la Buguruni kwa Mnyamani kwa kipindi kirefu kidogo. Hupatikana zaidi maeneo ya Hotel ya Popex iliyopo mkabala na mataa ya Barabara ya Mandela, pembeni kidogo ya Bar maarufu ya Kimboka. Anafahamika kama mlinzi wa eneo lile hasa nyakati za jioni. Si mgeni, kila mtu anamjua.

Pale Kimboka kwa machangudoa, pamekuwa pakilalamikiwa uwepo wa vibaka na vijana wahuni ambao hukaba na kupora watu wanaofika kufanya manunuzi. Vibaka hawa huwapora abiria mikoba yao wanaopita na pikipiki pamoja na mali nyingine kama simu na kadhalika.

Sasa wakazi wote nilobahatika kuzungumza nao, wamekiri kuwa Scorpion amekuwa msaada mkubwa sana kwa wakazi wa pale hasa nyakati za jioni na usiku, kwa kuweza kutokomeza tatizo la wizi na uporaji. Hapa nilishtuka na kushangaa sana! Scorpion huyu huyu?

Si hivyo tu, wapo walioeleza kuwa licha ya kuonekana ni mtu mwenye manguvu, Scorpion hakuwahi kufanya tukio lolote baya la kuiba, kupora wala uvamizi, zaidi ya kujishughulisha na masuala ya usalama wa maeneo hayo, hivyo tukio hili la kumtoa macho kijana Said limemwacha kila mtu mdomo wazi na kubakisha maswali mengi mpaka hivi sasa.

Mshangao mwingine, huu unatoka kwa dereva wa Bajaj aliyenirudisha kwenye makazi yangu, alisema anashangazwa kuwa baada ya tukio, ilipita wiki nzima na Scorpion aliendelea kuwepo mtaani akiendelea na mishe zake kama kawaida bila kukamatwa mpaka alipoamua kwenda kujisalimisha.

Lingine, wapo wanaodhani tukio hili ni la kisasi kati ya Said na Scorpion, ama inawezekana Scopion 'alitumwa' kumshughulikia Said. Hata hivyo, zote hizi ni dhana tu ambazo hazina budi kufanyiwa kazi.

Kwa ufupi, tunaweza kukubaliana kuwa unyama aliofanyiwa ndugu Saidi ni wa kukemewa kwa nguvu zote na sheria ifuate mkondo wake ipasavyo, lakini tusiache kutafuta majibu ya maswali ya msingi kuhusu tukio zima.

Unaniona mtetezi? Nenda Buguruni kaulize..
Mkuu..toka hii habari ivume,kwa tunaofikiri nje ya box tunasemaga story haibalance..
Tukiacha ushabik,hili swala la scorpion na full story nzima hielewek flan mkuu yaan n waz kna ktu knajfchajfcha..
In all,alchofanyiwa jamaa kutobolewa macho n cha kukemea sana,whether n scorpion au mtu mwngne ndo almchoma.....
 
Scorpion yupo chini ya ulinzi wa police na kwakuwa amemtoboa mwenzie macho basi Kaanza ale kisago huku akitoa maelezo yalionyooka,hapo ndipo tutapata ukweli wa Kila kitu.asanten
 
mimi napata mashaka sana ule ukimya wa tangu siku ya tukio hadi media kulibumburua na scorpion kuswekwa rumande...ktk zile siku za ukimya nn kilikua kinaendelea hasa upande wa Said??....
 
Hata mimi imenishangaza kidogo. Kama lilikuwa ni tukio lililofanyika tena eneo la wazi (pia Buguruni Polisi siyo mbali) bila shakalilivuta Watu, na kama taratibu zilivyo angepitishwa Polisi ili kupata PF3 kwa ajili ya matibabu na baadaye kuchukuliwa maelezo.

Lakini unaona ni kama tukio la ghafla lakini taarifa zake zimechelewa kutoka. Kuna nini?
Naomba usikilize ile clip aliyokuwa anahojiwa kwani kaeleza yote.Alisema alisaidiwa na raia mwema na ikatokea gari ya polisi na alichukuliwa na hiyo gari ya polisi na mtuhumiwa akiwa mita chache pembeni.Alipelekwa moja kwa moja polisi na kuchukuliwa maelezo na akapewa PF3.
 
Siyo wizi wa Kawaida, inaweza kuwa ni visasi vya kwenye dili chafu au ni visasi vinavyotokana na mambo ya mapenzi au scorpion ni psychiatric patient.
 
Hata mimi imenishangaza kidogo. Kama lilikuwa ni tukio lililofanyika tena eneo la wazi (pia Buguruni Polisi siyo mbali) bila shakalilivuta Watu, na kama taratibu zilivyo angepitishwa Polisi ili kupata PF3 kwa ajili ya matibabu na baadaye kuchukuliwa maelezo.

Lakini unaona ni kama tukio la ghafla lakini taarifa zake zimechelewa kutoka. Kuna nini?
Hili tukio linamaswali nengi sana kuliko majibu...
 
Binafsi najiuliza kwanini amtoboe macho.. Na huyu jamaa alietobolewa macho alikua kinyozi.. Hivyo kwa kuangalia tu hakua na Fedha nyingi.. Alikua na maisha ya kawaida.. Na huyu kinyozi inaonyesha anamjua scorpion...
Au alichukua nywele zake kwa kufanyia ushirikina scorpion kugundua akaamua kufanya vile.
 
Characteristic moja ya vinyozi ni wanyoaji wazuri maeneo hata yasiyo wahusu.... Rejea wimbo wa spea tairi maneno aliyo yazungumza mpoki wakati anampiga mkwara mzito matonya.
Huyo jamaa kafanya kitu na mhanga ka retaliate kwa ku hire assassin. Sema nafikiri aliemtuma skopioni alitoa maelekezo ya kumyofoa gogozi kifaa ambacho kilianzisha tamaa ya mhanga ili asiendelee kutamani mali ya mtu mwingine.
Mambo ambayo yanaweza kusababisha ukang'olewa macho, ukaliwa 0714, ukatolewa roho etc
1-Usingizi wa mwanaume mwenzio, pumziko la moyo wake
2-Dhuluma na utapeli.
NB :Hii nimeifikiria kwa sauti tu na haina tofauti na hoja za Darwin.
 
Sasa mimi unajua nipo busy nashugulikia nyumba yangu unajua nina nyumba mpya najenga cha msingi tuonane nikupe nondo zote uende mahakaman ukasimamame shaid wa mlemavu haki lazima itendeke mkuuu
acha visingizio hiyo nyumba unajenga masaa 24? Nenda polisi ukatoe ushahidi
 
Hata mimi imenishangaza kidogo. Kama lilikuwa ni tukio lililofanyika tena eneo la wazi (pia Buguruni Polisi siyo mbali) bila shakalilivuta Watu, na kama taratibu zilivyo angepitishwa Polisi ili kupata PF3 kwa ajili ya matibabu na baadaye kuchukuliwa maelezo.

Lakini unaona ni kama tukio la ghafla lakini taarifa zake zimechelewa kutoka. Kuna nini?
Kama ulimsikiliza Said alivyoelezea, alisema kuna msamalia mwema alimuokota pale chini barabarani, akampeleka polisi kuchukua PF3 then akapelekwa Amana, then akakimbizwa Muhimbili
 
Back
Top Bottom