Ukweli ni kwamba Magufuli alikataa kata kata boti za Azam kwenda ziwa Victoria

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Sio lengo langu kutoa uzi huu kwa kivuli cha kampeni. Najua kuna mengi yanasemwa kuhusu Lowassa ambayo hata mie nakubaliana na baadhi. Hata hivyo, ni vema pia tukayasema ya Magufuli, ili Watanzania waelewe tunatarajia kuwa na viongozi wa aina gani.

Katika maamuzi ya Magufuli ambayo yaliniacha mdomo wazi ni lile la kugoma katakata kupeleka boti za Azam Ziwa Victoria toka Bandari ya Dar, akidai zingeharibu madaraja yetu.

Wakati Magufuli akiweka msimamo huo, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wakati huo, Prof Mwandosya, alijaribu ku-reason naye kwamba boti hizo hazikuwa na uzito wa kuweza kuharibu madaraja, kutokana na data walizokuwa nazo. Mwandosya alisisitiza juu yan umuhimu wa kutatua tatizo la usafiri kwa wananchi wa eneo la ziwa Victoria kwa kutumia boti hizo. Magufuli alikataa katakata na hata kutoa kauli kwamba kama mnataka zikateni vipande vipande hizo boti mkaziunganishe Mwanza, akijua hilo lisingewezekana.

Ilikuwa ni busara na hekima za Prof Mwandosya zilizoleta ufumbuzi kwa suala hili. Mwandosya aliwaendea Wa-Kenya na kuwaeleza tatizo alilokuwa akipata toka kwa Waziri mwenzake. Akawaomba Wakenya boti zisafirishwe kwenda Victoria kwa barabara toka Mombasa. Wakenya waliomba data za boti na wakaona kwamba uzito wa boti usingekuwa tatizo kuzisafirisha kwa barabara na wakakubali boti za Azam zipitie Mombasa kwenda Ziwa Victoria.

Leo hii sidhani kama watu wanakumbuka kwamba uwepo wa hizi boti ziwa Victoria ni busara za Mwandosya.

Na suala jingine linalolingana na hilo ni pale Zambia walipotaka kupeleka mabasi yao marefu (Megabus) Zambia toka bandari ya Dar. Magufuli aliyazuia mabasi haya Kibaha akidai sheria za Tanzania haziruhusu mabasi marefu ya kiwango kile katika barabara zetu. Kwa mara nyingine tena likawa jambo kubwa sana. Magufuli alieleweshwa kwamba haya mabasi yatakuwa transit bila abiria, na hayafikii urefu wa malorikama semitrailers ambazo tunaziruhusu barabarani, lakini akashika msimamo kwamba Wazambia watafute namna nyingine ya kuyapeleka mabasi yao Zambia, sio barabara zetu hata kama hayana abiria yako transit tu. Jambo hili likawa kubwa sana ukizingatia Zambia kutumia bandari yetu, hadi ikabidi ngazi za juu upande wa Zambia na Tanzania ziingilie kati ndipo mabasi yakaruhusiwa kwenda Zambia.

Ndio maana niliwahi kusema, napenda uchapakazi wa Magufuli, lakini katika suala la "rational thinking", mmmh!
 
Sijui nini kimenitokea hizi siku 2-3, ni kama nimepumbazwa ghafla, nimejikuta nazielewa sera za Magufuli, nikijaribu kufigure out naona kama "huyu ndiye niliyekua namsubiri"

Sijui ni mimi peke yangu?

hujakosea nihaki yako naunapaswa kupongezwa. magufuli mfanya kazi. raisi yakitokea majanga hata kama alikuwa kalala anavuta suruali kitaa. siyo raisi hadi achomwe sindano ndipo apate nguvu za kutembea
 
Kama boti zingeharibu barabara mbona malori ndo yanaharibu zaidi?
Hizo barabara zina viwango gani zisiharibiwe na malori au hizo boti?
Mbona Kenya walikubali?
 
Sio lengo langu kutoa uzi huu kwa kivuli cha kampeni. Najua kuna mengi yanasemwa kuhusu Lowassa ambayo hata mie nakubaliana na baadhi. Hata hivyo, ni vema pia tukayasema ya Magufuli, ili Watanzania waelewe tunatarajia kuwa na viongozi wa aina gani.

Katika maamuzi ya Magufuli ambayo yaliniacha mdomo wazi ni lile la kugoma katakata kupeleka boti za Azam Ziwa Victoria toka Bandari ya Dar, akidai zingeharibu madaraja yetu.

Wakati Magufuli akiweka msimamo huo, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wakati huo, Prof Mwandosya, alijaribu ku-reason naye kwamba boti hizo hazikuwa na uzito wa kuweza kuharibu madaraja, kutokana na data walizokuwa nazo. Mwandosya alisisitiza juu yan umuhimu wa kutatua tatizo la usafiri kwa wananchi wa eneo la ziwa Victoria kwa kutumia boti hizo. Magufuli alikataa katakata na hata kutoa kauli kwamba kama mnataka zikateni vipande vipande hizo boti mkaziunganishe Mwanza, akijua hilo lisingewezekana.

Ilikuwa ni busara na hekima za Prof Mwandosya zilizoleta ufumbuzi kwa suala hili. Mwandosya aliwaendea Wa-Kenya na kuwaeleza tatizo alilokuwa akipata toka kwa Waziri mwenzake. Akawaomba Wakenya boti zisafirishwe kwenda Victoria kwa barabara toka Mombasa. Wakenya waliomba data za boti na wakaona kwamba uzito wa boti usingekuwa tatizo kuzisafirisha kwa barabara na wakakubali boti za Azam zipitie Mombasa kwenda Ziwa Victoria.

Leo hii sidhani kama watu wanakumbuka kwamba uwepo wa hizi boti ziwa Victoria ni busara za Mwandosya.

Na suala jingine linalolingana na hilo ni pale Zambia walipotaka kupeleka mabasi yao marefu (Megabus) Zambia toka bandari ya Dar. Magufuli aliyazuia mabasi haya Kibaha akidai sheria za Tanzania haziruhusu mabasi marefu ya kiwango kile katika barabara zetu. Kwa mara nyingine tena likawa jambo kubwa sana. Magufuli alieleweshwa kwamba haya mabasi yatakuwa transit bila abiria, na hayafikii urefu wa malorikama semitrailers ambazo tunaziruhusu barabarani, lakini akashika msimamo kwamba Wazambia watafute namna nyingine ya kuyapeleka mabasi yao Zambia, sio barabara zetu hata kama hayana abiria yako transit tu. Jambo hili likawa kubwa sana ukizingatia Zambia kutumia bandari yetu, hadi ikabidi ngazi za juu upande wa Zambia na Tanzania ziingilie kati ndipo mabasi yakaruhusiwa kwenda Zambia.

Ndio maana niliwahi kusema, napenda uchapakazi wa Magufuli, lakini katika suala la "rational thinking", mmmh!

Mimi nafikiri wewe labda na huyo Mwandosya kama ni kweli alisema ulivyosema ndiyo mna matatizo, kwanza hazikuwa boti za Azam, hilo kwanza likae sawa turudi kwenye mada, kwa kawaida Dunia nzima hizi meli huwa zinakuwa assembled bandarini na huwa hazisafirishwi nzima nzima na Meli zetu zote zinazotumika kwenye Maziwa yetu kuanzia Liemba ya tangu enzi ya Ujerumani ilibebwa vipande vipande ktk Bandarini Dar mpaka Kigoma ndiyo ikejengewa huko na zile zote zilizo kwenye Z.Nyanza (Victoria) na Wazungu walikuwa wanafanya hivyo kwa sababu hiyo aliyoitoa Magufuli ni kwamba zina uzito kuliko uwezo wa Madaraja na Br. zetu sasa ulitaka zikabomowe madaraja halafu ni nani angeyajenga tena? Na kwa fedha gani?

Kiongozi wa namna hii ya Magufuli wa kusimamia sheria kama ilivyo ndiyo anayetakiwa hapa nchini, ikumbukwe TanZania ni masikini siyo kwa sababu hakuna sheria HAPANA bali nchi ni masikini kwa sababu kuna sheria tena nzuri lkn hatuzifuati laiti tungefwata sheria zetu sasa hivi tungekuwa mbali sana kuanzia msd kufikisha Dawa kwenye Zahanati vijijini mpaka ufunguzi wa bar kila kona bila ya kibali! Tuko masikini kwa sababu kila mtu anafanya anavyotaka!

Hivyo hii nchi inahitaji mtu ambaye hatopinda ktk kutekeleza sheria ambazo sisi wenyewe tumeziweka kama sheria inasema hairuhusiwi kujenga ndani ya mita 50 ktk ufukweni basi na ifwatwe kama sheria inasema mita 30 ni hifadhi ya Br. na iwe hivyo...
 
we mleta uzi una elimu gani?
utakua umesoma sanaa, kwa maana ya bachelor of arts in.........
kwaio we kwa mawazo yako unafikiri magufuli aligoma ili kuwakomoa wananchi au?
mbona hajagoma kusimamia barabara?
unajua izo boti zilikua na uzito gani na barabara na madaraja vilikua na uwezo wa kuimili uzito gani?
unajua meli au boti kubwa kwenye inland lakes uwa zinapelekwaje, mfano Mv Victoria ilipelekwa vipi Mwanza?
Acha ujuha, umu kuna wasomi, usifikili wote umu ni mamburura kama wewe! Ndorobooo
Leta hoja na sio vioja. Pumbavu...
 
Sio lengo langu kutoa uzi huu kwa kivuli cha kampeni. Najua kuna mengi yanasemwa kuhusu Lowassa ambayo hata mie nakubaliana na baadhi. Hata hivyo, ni vema pia tukayasema ya Magufuli, ili Watanzania waelewe tunatarajia kuwa na viongozi wa aina gani.

Katika maamuzi ya Magufuli ambayo yaliniacha mdomo wazi ni lile la kugoma katakata kupeleka boti za Azam Ziwa Victoria toka Bandari ya Dar, akidai zingeharibu madaraja yetu.

Wakati Magufuli akiweka msimamo huo, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wakati huo, Prof Mwandosya, alijaribu ku-reason naye kwamba boti hizo hazikuwa na uzito wa kuweza kuharibu madaraja, kutokana na data walizokuwa nazo. Mwandosya alisisitiza juu yan umuhimu wa kutatua tatizo la usafiri kwa wananchi wa eneo la ziwa Victoria kwa kutumia boti hizo. Magufuli alikataa katakata na hata kutoa kauli kwamba kama mnataka zikateni vipande vipande hizo boti mkaziunganishe Mwanza, akijua hilo lisingewezekana.

Ilikuwa ni busara na hekima za Prof Mwandosya zilizoleta ufumbuzi kwa suala hili. Mwandosya aliwaendea Wa-Kenya na kuwaeleza tatizo alilokuwa akipata toka kwa Waziri mwenzake. Akawaomba Wakenya boti zisafirishwe kwenda Victoria kwa barabara toka Mombasa. Wakenya waliomba data za boti na wakaona kwamba uzito wa boti usingekuwa tatizo kuzisafirisha kwa barabara na wakakubali boti za Azam zipitie Mombasa kwenda Ziwa Victoria.

Leo hii sidhani kama watu wanakumbuka kwamba uwepo wa hizi boti ziwa Victoria ni busara za Mwandosya.

Na suala jingine linalolingana na hilo ni pale Zambia walipotaka kupeleka mabasi yao marefu (Megabus) Zambia toka bandari ya Dar. Magufuli aliyazuia mabasi haya Kibaha akidai sheria za Tanzania haziruhusu mabasi marefu ya kiwango kile katika barabara zetu. Kwa mara nyingine tena likawa jambo kubwa sana. Magufuli alieleweshwa kwamba haya mabasi yatakuwa transit bila abiria, na hayafikii urefu wa malorikama semitrailers ambazo tunaziruhusu barabarani, lakini akashika msimamo kwamba Wazambia watafute namna nyingine ya kuyapeleka mabasi yao Zambia, sio barabara zetu hata kama hayana abiria yako transit tu. Jambo hili likawa kubwa sana ukizingatia Zambia kutumia bandari yetu, hadi ikabidi ngazi za juu upande wa Zambia na Tanzania ziingilie kati ndipo mabasi yakaruhusiwa kwenda Zambia.

Ndio maana niliwahi kusema, napenda uchapakazi wa Magufuli, lakini katika suala la "rational thinking", mmmh!
Wewe so msemakweli na ninakushauri kabla ya kuleta hoja hapa jamii forums ni vyema ungefanya kautafiti kidogo ili angalau uwe na kauelew cha unachokisema. Magufuli hakuzuia boti yeyote ya Azam Marine kwenda ziwa Victoria (Mwanza) Bali zile boti zilikuwa Mali ya Mohamed Dewji. Sababu kubwa ya kuzuia boti zile na ni sababu yenye mashiko siyo ya kisiasa ni kutokana na uzito mkubwa wa boti zenyewe lakini pia ni kutokana na upana wa mzigo wenyewe. Kwa kipindi kile pale Ruvu darajani kulikuwa na daraja la muda ambalo lilijengwa kwa Chuma lilikuwa ni daraja jembamba la kutosha kupita gari moja tu kwa wakati mmoja lakini zile boti zilikwa pana sana kiasi cha kwamba zisingeweza kupita pale labda like daraja lingebomolewa ndiyo zingeweza kupenya na pia urefu kwenda juu kwa pale Ruvu daraja la train linaruhusu kupita gari zenye height isizidi 5.5 meters lakini boti zile zilikuwa na urefu wa zaidi ya mita 5.5. He zingepita vipi pale?

Kuhusu Yale mabasi yaliyokuwa yanakwenda Zambia kama ulikuwa hujui Yale mabasi ni mabasi ya Higer saw a saw a kabisa na basis wanalolitumia club ya Azam FC. Kwa sheria namba 10 ya Road Tragic Act ya mwaka 1973 imeonyesha upana, urefu na kimo cha magari makubwa ambayo yanaruhusiwa kupita barabarani na iwapo gari au mzigo wake ukizidi zaidi ya physical dimensions hizo huitwa ABNORMAL WIDE LOAD ambayo inatakiwa kuombewa kibali maalum kutoka Wizara ya Ujenzi na pia inatakiwa waweke Bangor mbele na nyuma lililoandika "abnormal wide load" wawe na escort pamoja na kibali maalum. Sasa hiyo road traffic act.1973 inasema hivi urefu (length)wa rigid vehicle usizidi 12.5 meters, Articulated Vehicles yaani semi trailer ni 17 meters na Combination of two vehicles yaani pulling isizidi 22 meters. Na upana yaani width mwisho ni 2.6 meters kwa magari yote na kimo yaani height mwisho ni 4.6 meters hivyo kwa gari au mzigo wowote unaozidi zaidi ya huyo physical dimensions unaitwa ABNORMAL WIDE LOAD na anatakiwa awe na kibali cha kumruhusu kutembea barabarani. Sasa Yale mabasi mawili yaliyokuwa yanakwenda Zambia yalizuiwa pale Kibaha mizani kwakuwa yalikuwa na urefu yaani length ya 13.5 hivyo ni Abnormal wide load na walitakiwa wawe na Kibali lakini wao hawakuwa na Kibali hivyo hawakuwa na uhalali wa kutembea barabarani. Hiyo ni sheria iliyotungwa na bunge mwaka 1973 kabla hata magufuli hajawa waziri hivyo yeye anatekeleza sheria tu.

Nakushauri mtoa mada uwe unafanya utafiti usiongee kishabiki tu hapa
 
wengi wetu humu huwa tunaongea vitu tusivovijua,, ni watu wa kuponda tu kishabiki kila kitu hata kiwe kizuri vipi ili mradi tu kimefanywa na chama tawala, kusifia kitu hata kiwe cha ovyo vipi kwakua tu wamefanya watu wa mabadiliko!! hiyo sio tabia ya muungwana,,, akijenga barabara wakasema mpongezeni utasikia oooh tumpongeze kwani katoa pesa mifukoni kwake, basi na asipozijenga pia mnatakiwa mjilaum wenyewe kwakua nyie ndo "wenye pesa"!! na watu wa aina hii ndo wakwepaji kodi waliokubuhu
 
Huu ni ukweli...

Huyu jamaa shida pekee aliyonayo ni maamuzi yake ya kibinafsi...

Akiwa rais huyu anapaswa awe na washauri wazuri sana...

Na serikali yake isiwe kama hizi serikali nyoronyoro zilizopita...


Ndio maana niliwahi kusema, napenda uchapakazi wa Magufuli, lakini katika suala la "rational thinking", mmmh!
 
Mimi nafikiri wewe labda na huyo Mwandosya kama ni kweli alisema ulivyosema ndiyo mna matatizo, kwanza hazikuwa boti za Azam, hilo kwanza likae sawa

sababu hiyo aliyoitoa Magufuli ni kwamba zina uzito kuliko uwezo wa Madaraja na Br. zetu sasa ulitaka zikabomowe madaraja halafu ni nani angeyajenga tena? Na kwa fedha gani?

Kiongozi wa namna hii ya Magufuli wa kusimamia sheria kama ilivyo ndiyo anayetakiwa hapa nchini


Okay, labda hazikuwa boti za Azam, lakini angalau unakiri kulikuwa na boti hizo. Suala la kubomoa madaraja sio hoja yenye mshiko. Madaraja mangapi ya Kenya ulisikia yamebomoka kwa sabau hizo boti zilipita barabra za Kenya?

Unasema tunataka mtu wa kufuata sheria, sawa. Ndio maana Magufuli aliambiwa kwamba suala sio uzito tu, bali spread ya uzito kwenda kwenye matairi. Kwamba kuna magari maalum ya kubeba boti yenye tairi nyingi ambayo yana spread pressure kwenye kila tairi (i.e pressure = Force/Area) lakini alikataa katakata sababu za kisayansi toka kwa wataalamu akang'ang'ania uzito wa boti, japo ni mwalimu wa sayansi
 
Wewe so msemakweli na ninakushauri kabla ya kuleta hoja hapa jamii forums ni vyema ungefanya kautafiti kidogo ili angalau uwe na kauelew cha unachokisema. Magufuli hakuzuia boti yeyote ya Azam Marine kwenda ziwa Victoria (Mwanza) Bali zile boti zilikuwa Mali ya Mohamed Dewji.


Kuhusu Yale mabasi yaliyokuwa yanakwenda Zambia kama ulikuwa hujui Yale mabasi ni mabasi ya Higer saw a saw a kabisa na basis wanalolitumia club ya Azam FC. Kwa sheria namba 10 ya Road Tragic Act ya mwaka 1973 imeonyesha upana, urefu na kimo cha magari makubwa ambayo yanaruhusiwa kupita barabarani na iwapo gari au mzigo wake ukizidi zaidi ya physical dimensions hizo huitwa ABNORMAL WIDE LOAD ambayo inatakiwa kuombewa kibali maalum kutoka

Unaongea non-issues kwa sababu wewe umepewa kazi ya kujibu thread hii kwa kila namna ili Magufuli asionekane hakufanya uamuzi usi wa makini. Kumbuka kwamba katika maamuzi hayo mawili aliishia kukwaruzana na Mekyembe na Mwandosya, watu ambao walikuwa pia mawaziri kama yeye, na kila wakati akawa anakimbilia vyombo vya habari kuwadharirisha mawaziri wenzake.

Suala la boti zulikuwa za Dewji sijui nani sio issue ya msingi.
 
Sijui nini kimenitokea hizi siku 2-3, ni kama nimepumbazwa ghafla, nimejikuta nazielewa sera za Magufuli, nikijaribu kufigure out naona kama "huyu ndiye niliyekua namsubiri"

Sijui ni mimi peke yangu?

Ni nani alie kuroga?
 
Okay, labda hazikuwa boti za Azam, lakini angalau unakiri kulikuwa na boti hizo. Suala la kubomoa madaraja sio hoja yenye mshiko. Madaraja mangapi ya Kenya ulisikia yamebomoka kwa sabau hizo boti zilipita barabra za Kenya?

Unasema tunataka mtu wa kufuata sheria, sawa. Ndio maana Magufuli aliambiwa kwamba suala sio uzito tu, bali spread ya uzito kwenda kwenye matairi. Kwamba kuna magari maalum ya kubeba boti yenye tairi nyingi ambayo yana spread pressure kwenye kila tairi (i.e pressure = Force/Area) lakini alikataa katakata sababu za kisayansi toka kwa wataalamu akang'ang'ania uzito wa boti, japo ni mwalimu wa sayansi


Nimekwisha kuelezea sababu ya Magufuli kukataa wewe unakuja na Mifano ya Kenya, sasa haujui kwamba Kenya na TanZania ni nchi mbili tofauti na zenye viongozi tofauti, unajuaje kama Br. za Kenya zinaruhusu kusafirisha uzito wa hizo Meli?

TanZania haijawahi kusafirisha Meli nzima kwa Br. ktk Dar mpka ziwani, na nimeshakupa mifano hata wazungu walikuwa hawafanyi hivyo Meli zote zilizoko kwenye Maziwa yetu zilisafirishwa vipande vipande ktk Dar mpaka Kigoma au Mwanza halafu ndiyo zikajengewe huko na sababu ya Wazungu kufanya hivyo ilikuwa ni kuepusha uharibifu wa br. aambao unachukuwa gharama kubwa kukarabati sasa kama ni kweli huyo Mwandosya alimpinga Magufuli kwa hilo basi nasema Mwandosya naye ni kilaza vile vile kwa maana kuna sababu kwa nini Br. huwa zinaandikwa kibao cha uzito unaoruhusiwa pembeni, au unafikiri Serikali inaingia gharama kubwa kujenga weighing bridge kwa sababu zinaongeza muonekano mzuri wa Barabara?
 
Hivi zile boti zilifikaje Mwanza? Kwani huko Kenya hawana madaraja?

Kukataa ni suhluhisho la kishenzi na kibabe. Hata kama sheria inakataza, muungwana angeweza kutoa ushauri kwa waziri mwenzake na wakapata suluhisho la kiustaarabu. Lakini kumwabia akate boti akaunge Mwanza huoni sio jibu la MSOMI?
nI HIVYO HIVYO ALISEMA KAMA WA KIGAMBONI HAWAWEZI KULIPA SH.200 KWENYE KIVUKO WAPIGE MBIZI. This is stupidity
 
Back
Top Bottom