nemulo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 1,589
- 441
Habarini wadau,
Leo nimekumbuka hili na kuona sii vibaya tukashare:
Wimbo wa "Malaika" ni wimbo unaofahamika sanaaa sio Afrika tu bali hata katika mabara mengine,nakumbuka mwaka 2011 nikiwa chuoni walikuja wanafunzi kutoka Asia na waliusikia huo wimbo kwenye laptop ya mtu na mmojawapo (mkorea) aliweza kuuimba nusu na kuonesha kuupenda sana.
Mwaka huo huo mwishoni nikiwa nasikiliza kipindi cha miziki ya zamani na historia zake nilisikia kuwa wimbo wa malaika ulitungwa na kuimbwa kwa mara ya kwanza kabisa mkoani Arusha(eneo la kaloleni ya leo) kabla kabisa ya uhuru,nilitafituli zaidi kwa kuwauliza baadhi ya wazee wapenda miziki nikaambiwa huu wimbo uliimbwa na kijana aliyekuwa akichunga mbuzi karibu na maghorofa ya wahindi kipindi hicho kumwimbia binti mmoja mwenye asili ya Asia,na kurekodiwa na binti huyo kwenye redio yake ndogo.
Baada ya hapo binti yule alikuwa na uhusiano na kijana yule Ila uhusiano wao ulikatishwa na wazazi pamoja na ndugu wa binti.Binti yule alihifadhi ile rekodi ya wimbo na kuja kuirudisha kwa muimbaji naye akawapa baadhi ya watu,
Baada ya hapo studio za kwanza kabisa Arusha kama Radio Habari Maalum(RHM) zikaanza kuupiga wimbo huo pamoja na kwaya za mwanzoni na kukubalika sana.
Leo hii wimbo huu bado ni maarufu sana na ulirudiwa kuimbwa na mwimbaji maarufu Miriam Makeba (Mama Afrika) na wengine. Binafsi naupenda huu wimbo.
Leo nimekumbuka hili na kuona sii vibaya tukashare:
Wimbo wa "Malaika" ni wimbo unaofahamika sanaaa sio Afrika tu bali hata katika mabara mengine,nakumbuka mwaka 2011 nikiwa chuoni walikuja wanafunzi kutoka Asia na waliusikia huo wimbo kwenye laptop ya mtu na mmojawapo (mkorea) aliweza kuuimba nusu na kuonesha kuupenda sana.
Mwaka huo huo mwishoni nikiwa nasikiliza kipindi cha miziki ya zamani na historia zake nilisikia kuwa wimbo wa malaika ulitungwa na kuimbwa kwa mara ya kwanza kabisa mkoani Arusha(eneo la kaloleni ya leo) kabla kabisa ya uhuru,nilitafituli zaidi kwa kuwauliza baadhi ya wazee wapenda miziki nikaambiwa huu wimbo uliimbwa na kijana aliyekuwa akichunga mbuzi karibu na maghorofa ya wahindi kipindi hicho kumwimbia binti mmoja mwenye asili ya Asia,na kurekodiwa na binti huyo kwenye redio yake ndogo.
Baada ya hapo binti yule alikuwa na uhusiano na kijana yule Ila uhusiano wao ulikatishwa na wazazi pamoja na ndugu wa binti.Binti yule alihifadhi ile rekodi ya wimbo na kuja kuirudisha kwa muimbaji naye akawapa baadhi ya watu,
Baada ya hapo studio za kwanza kabisa Arusha kama Radio Habari Maalum(RHM) zikaanza kuupiga wimbo huo pamoja na kwaya za mwanzoni na kukubalika sana.
Leo hii wimbo huu bado ni maarufu sana na ulirudiwa kuimbwa na mwimbaji maarufu Miriam Makeba (Mama Afrika) na wengine. Binafsi naupenda huu wimbo.