hhhhj
Member
- Oct 5, 2016
- 41
- 68
NI KWELI WALIMU WAMEMPIGA MWANAFUNZI KINYAMA HUKO MKOANI MBEYA LAKINI KIJUE CHANZO KILICHOSABABISHA KUPIGWA KWAKE
Na Mathias Canal
Majira ya asubuhi hapo jana nilianza kuiona kanda ya sekunde 38, ambayo tangu nilipoiona kabla ya kujua serikali itafanya maamuzi gani kwa Walimu waliofanya unyama huo mimi niliwatazama takribani watu hao watano wakiwa wanaonekana kumshambulia mvulana mmoja ambaye ni Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya kutwa ya Mbeya ambaye baadaye alianguka chini kwa kupigwa ngumi pamoja na mateke.
Hakika tangu jana nimekuwa nikihangaika kujua chanzo cha Walimu kuwa na hasira za aina hiyo kama Chui Mwenye njaa, Machache haya nimebaini.
KISA CHA KUPIGWA...!
Mwanafunzi huyo kabla ya kuonekana kwenye kanda hiyo alikataa kuchapwa wala kuchuchumaa pamoja na kwamba wenzake wote ambao hawakufanya zoezi darasani.
Aliipohojiwa akamjibu vibaya mwalimu ambapo Mwalimu yule alitaka kumuadhibu kwa kumchapa viboko kama adhamu ya kuimarisha nidhamu yake.
Mwalimu alipojaribu kutaka kumchapa ghafla mwanafunzi huyo alirusha ngumi nzito ambayo ilituama kwenye mdomo wa Mwalimu huyo.
Baada ya kadhia hiyo ambayo haikumaliza hata sekunde moja walimu wengine walioshuhudia tukio hilo waliamua kumchukua mwanafunzi huyo ili kumpelekea ofisini huku Mwalimu aliyepigwa ngumi akiwa ameamua kurudi darasani kutuliza wanafunzi wengine ambao walitaka kufanya vurugu kwa sababu ya kukerwa na Matukio ya ubabe yanayofanywa na Mwanafunzi huyo na Alipoona wanafunzi hao wametulia alianza kurudi ofisini.
Baada ya Mwanafunzi huyo kufikishwa ofisini akaona Walimu wamebaki wawili tu aliwapiga ngumi kiasi kwamba Walimu hawakuwa na namna ya kumkabili.
Mwanafunzi huyo baada ya kuwamudu Walimu wale wawili Akaanza kutoka nje ya ofisi huku akiwa anakimbia yule mwalimu ambaye alipigwa ngumi ya mdomo na akaenda kuwatuliza wanafunzi darasani akamuona mwanafunzi huyo akiwa ametoka anakimbia ndio alipomuwahi kukawa na majibizano ya ngumi na mateke kidogo.
Mwalimu alifanikiwa kumudu majibizano ya kipigo na hatimaye akafanikiwa kumrudisha ofisini kwa walimu wengine hapo ndio kila mmoja akajikuta anahitaji kumaliza hasira zake. Kumbuka Walimu walikuwa na hasira za Kupigwa tena na mwanafunzi wao...! Na kubaki wakiwa wanaugulia maumivu.
TAARIFA NYINGINE MPENYEZO
Mwanafunzi huyu yeye aliridhia kichapo alichopewa na walimu hao baada ya kufanikiwa kummudu akiwa kwenye ofisi ya walimu ndio maana siku 11 toka tukio limetokea hakwenda kuripoti mahala popote, yaaani Hata nyumbani kwao hakwenda kusema kwakuwa anakesi tatu nzito na aliwahi kumjibu hovyo baba yake mbele ya walimu alipokuwa ameenda kutetea asifukuzwe shule.
Achilia mbali hayo Mwanafunzi huyo alishawahi kuvunja TV ya baba yake nyumbani kwao kama wiki mbili zilizopita.
Pamoja na mambo yote hayo Wiki hili amekamatwa na walimu akiwa anavuta bangi shuleni na wenzake. baba yake mzazi hamtaki huyo Mwanafunzi lakini hana namna ya kumkabili.
MTAZAMO YAKINIFU
Serikali umefanya Kazi Mkubwa kwanza kubaini hiyo video imerekodiwa katika shule gani na Walimu hao ni kina nani, hakika ni jambo la kupongezwa sana lakini imesahau kwamba maamuzi yote yaliyofanyika dhidi ya Walimu yameshindwa kuzingatia chanzo Chake Bali imejikita kukabili matokeo, Wahenga walisema Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo lakini wakaenda mbali zaidi kwa kusema Samaki mkunje angali mbichi. Mwanafunzi huyu ni samaki aayetaka kukunjwa akiwa amekauka Kamwe haiwezekani.
Watanzania, Wanafunzi, jamii kwa ujumla itambue kuwa binafsi nimesikitishwa sana na kadhia hiyo iliyofanywa na walimu karibu wa tano kwa mujibu wa Video iliyosambaa mtaani tena imenikera mno mno lakini vyema zaidi kama tutajikita kuhangaika na chanzo cha tatizo ili kumaliza mzizi wake kuliko kukabili matokeo huku tukiacha mambo hayo yaendelee kukutikana mitaani.
Kuteleza si kuanguka lazima tukiri kwa pamoja kwamba hapo tumeteleza kabla hatujaanguka basi vyema tukatazama mahala pa Kushika ili kuhakikisha hatuanguki Tunapotoa maamuzi ni vyema sana tuangalie mambo kwa ujumla wake tusitazame tu wapi kumesisimua Jamii...?
Tutambue kuwa tukio hilo la Mbeya ni la wanafunzi wa Chuo kumchangia na kumpiga mwanafunzi wa shule ya kutwa ya Sekondari Mbeya tukiwaita Walimu maana yake tutajadili pia Chama Cha Walimu Mkoa wa Mbeya (CWT) kinafanya Kazi gani...?
Kuna mwandishi mmoja huwa anasema hawezi kuwa adui kwa kusema Ukweli nami sitarajii hilo.
Naaam, Ni Neno La Wakati Mwema
Mathias Canal (Sauti ya Wanyonge)
0756413465
Igunga-Tabora
Na Mathias Canal
Majira ya asubuhi hapo jana nilianza kuiona kanda ya sekunde 38, ambayo tangu nilipoiona kabla ya kujua serikali itafanya maamuzi gani kwa Walimu waliofanya unyama huo mimi niliwatazama takribani watu hao watano wakiwa wanaonekana kumshambulia mvulana mmoja ambaye ni Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya kutwa ya Mbeya ambaye baadaye alianguka chini kwa kupigwa ngumi pamoja na mateke.
Hakika tangu jana nimekuwa nikihangaika kujua chanzo cha Walimu kuwa na hasira za aina hiyo kama Chui Mwenye njaa, Machache haya nimebaini.
KISA CHA KUPIGWA...!
Mwanafunzi huyo kabla ya kuonekana kwenye kanda hiyo alikataa kuchapwa wala kuchuchumaa pamoja na kwamba wenzake wote ambao hawakufanya zoezi darasani.
Aliipohojiwa akamjibu vibaya mwalimu ambapo Mwalimu yule alitaka kumuadhibu kwa kumchapa viboko kama adhamu ya kuimarisha nidhamu yake.
Mwalimu alipojaribu kutaka kumchapa ghafla mwanafunzi huyo alirusha ngumi nzito ambayo ilituama kwenye mdomo wa Mwalimu huyo.
Baada ya kadhia hiyo ambayo haikumaliza hata sekunde moja walimu wengine walioshuhudia tukio hilo waliamua kumchukua mwanafunzi huyo ili kumpelekea ofisini huku Mwalimu aliyepigwa ngumi akiwa ameamua kurudi darasani kutuliza wanafunzi wengine ambao walitaka kufanya vurugu kwa sababu ya kukerwa na Matukio ya ubabe yanayofanywa na Mwanafunzi huyo na Alipoona wanafunzi hao wametulia alianza kurudi ofisini.
Baada ya Mwanafunzi huyo kufikishwa ofisini akaona Walimu wamebaki wawili tu aliwapiga ngumi kiasi kwamba Walimu hawakuwa na namna ya kumkabili.
Mwanafunzi huyo baada ya kuwamudu Walimu wale wawili Akaanza kutoka nje ya ofisi huku akiwa anakimbia yule mwalimu ambaye alipigwa ngumi ya mdomo na akaenda kuwatuliza wanafunzi darasani akamuona mwanafunzi huyo akiwa ametoka anakimbia ndio alipomuwahi kukawa na majibizano ya ngumi na mateke kidogo.
Mwalimu alifanikiwa kumudu majibizano ya kipigo na hatimaye akafanikiwa kumrudisha ofisini kwa walimu wengine hapo ndio kila mmoja akajikuta anahitaji kumaliza hasira zake. Kumbuka Walimu walikuwa na hasira za Kupigwa tena na mwanafunzi wao...! Na kubaki wakiwa wanaugulia maumivu.
TAARIFA NYINGINE MPENYEZO
Mwanafunzi huyu yeye aliridhia kichapo alichopewa na walimu hao baada ya kufanikiwa kummudu akiwa kwenye ofisi ya walimu ndio maana siku 11 toka tukio limetokea hakwenda kuripoti mahala popote, yaaani Hata nyumbani kwao hakwenda kusema kwakuwa anakesi tatu nzito na aliwahi kumjibu hovyo baba yake mbele ya walimu alipokuwa ameenda kutetea asifukuzwe shule.
Achilia mbali hayo Mwanafunzi huyo alishawahi kuvunja TV ya baba yake nyumbani kwao kama wiki mbili zilizopita.
Pamoja na mambo yote hayo Wiki hili amekamatwa na walimu akiwa anavuta bangi shuleni na wenzake. baba yake mzazi hamtaki huyo Mwanafunzi lakini hana namna ya kumkabili.
MTAZAMO YAKINIFU
Serikali umefanya Kazi Mkubwa kwanza kubaini hiyo video imerekodiwa katika shule gani na Walimu hao ni kina nani, hakika ni jambo la kupongezwa sana lakini imesahau kwamba maamuzi yote yaliyofanyika dhidi ya Walimu yameshindwa kuzingatia chanzo Chake Bali imejikita kukabili matokeo, Wahenga walisema Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo lakini wakaenda mbali zaidi kwa kusema Samaki mkunje angali mbichi. Mwanafunzi huyu ni samaki aayetaka kukunjwa akiwa amekauka Kamwe haiwezekani.
Watanzania, Wanafunzi, jamii kwa ujumla itambue kuwa binafsi nimesikitishwa sana na kadhia hiyo iliyofanywa na walimu karibu wa tano kwa mujibu wa Video iliyosambaa mtaani tena imenikera mno mno lakini vyema zaidi kama tutajikita kuhangaika na chanzo cha tatizo ili kumaliza mzizi wake kuliko kukabili matokeo huku tukiacha mambo hayo yaendelee kukutikana mitaani.
Kuteleza si kuanguka lazima tukiri kwa pamoja kwamba hapo tumeteleza kabla hatujaanguka basi vyema tukatazama mahala pa Kushika ili kuhakikisha hatuanguki Tunapotoa maamuzi ni vyema sana tuangalie mambo kwa ujumla wake tusitazame tu wapi kumesisimua Jamii...?
Tutambue kuwa tukio hilo la Mbeya ni la wanafunzi wa Chuo kumchangia na kumpiga mwanafunzi wa shule ya kutwa ya Sekondari Mbeya tukiwaita Walimu maana yake tutajadili pia Chama Cha Walimu Mkoa wa Mbeya (CWT) kinafanya Kazi gani...?
Kuna mwandishi mmoja huwa anasema hawezi kuwa adui kwa kusema Ukweli nami sitarajii hilo.
Naaam, Ni Neno La Wakati Mwema
Mathias Canal (Sauti ya Wanyonge)
0756413465
Igunga-Tabora