Niambie hiyo Aya nikasome kwamba Mtume Muhammad alitangaza kuwa Ijumaa iwe siku ya Sala. Yaani kama ni kweli Nabatizwa na ww.
KWAKUWA WEWE NI MAAMUMA, YAWEZEKANA UISLAMU UMEUKUTA KWENYE FAMILIA AU UKOO,HIVO UMERITHI
basi ngoja nikusaidie kuhusu ibada ya IJUMAA ilipoanzia ,
NITANUKUU VITABU VYENU NA QURAN....
Ibada ya siku ya ljumaa mwanzo
wake umebainishwa kupitia
maelezo yanayopatikana katika
kitabu kimojawapo cha elimu ya
Uislam kama ifuatavyo:-
Historia ya mtume Muhammad
(s.a.w)
Muhammad Abdallah Riday Ansaar
Muslim
Youth Organization uk. No 47.
Hebu tuone maelezo mafupi katika
ukurasa huo wa kitabu chiko
kinachotumiwa zaidi na jamii ya
Waislam wa Kiansar, katika
kipengele chenye kichwa cha habari
kisemacho:-
Ijumaa ya kwanza aliyoswali mtume.
Mtume aliondoka Qubaa kwenda
Yathriba ilikuwa ni ljumaa, na
jua lilipochomoza alifika katika
maskani ya Bani Salim bin Awf;
katika Wangwa wa Ronunaa, hapo
ndipo Muhammad aliposwali
swala ya ljumaa kwa mara ya
kwanza katika Uislam
Hivyo ndivyo kitabu hicho cha
historia ya maisha ya mtume
kinavyosema kuwa kumbe ibada ya
ijumaa ilianzishwa rasmi na mtume
Muhammad katika kipindi hicho cha
safari ya Muhammad toka mji wa
Makka kwenda mji wa madina, na
ieleweke kuwa huo ulikuwa ni
mwaka 622 Hijra. BK.
Je’ ibada ya ijumaa inasimama
mahali pa Sabato(Jumamosi)?
Mkazo mkubwa wa Umma wa
Kiislam juu ya siku ya ljumaa
unaanzia katika tukio hilo, lakini
maandiko ya Qur-an yanaonyesha
wazi kuwa kabla ya hapo hata
Muhammad mwenyewe alikuwa
akifuata kawaida na mfumo wa
ibada uliyotumiwa na Wayahudi.
Qur an 2:144
Kwa yakini tukiona
unavyogeuzageuza uso wako
mbinguni. Basi tutakugeuza kwenye
kibla ukipendacho. Basi geuza uso
wako upande wa Msikiti Mtakatifu
(Al-kaaba) ……..
Soma ufafanuzi wa aya hiyo ya 144
hapo chini.
Muhammad kwa takriban zaidi ya
mwaka mmoja na nusu naye
alikuwa akiabudu kwa kuangalia
Baytil Muqaddas
(Yerusalemu). (Qur-an 2:144
fafanuzi uk 34).
Andiko hilo linaonyesha kuwa kipindi
fulani katika ibada Muhammad
alionekana akihangaika kwa
kugeuzageuza uso wake kama
ishara ya kutafuta sehemu mpya ya
kutazama wakati wa ibada, lakini
kabla ya hayo kipindi chote taklibani
mwaka mmoja na nusu aliangalia
Yerusalemu (Palipo na msikiti sasa
huitwao Baitul Muqaddas).
Toka mfanano wa ibada na
wayahudi hadi mfumo mpya wa
ibada wa Uislam.
Kadri ya uchambuzi hapo juu
tumeona namna Muhammad
alivyotekeleza ibada zake ambapo
kwa sehemu zikiwa na mfanano na
Wayahudi hasa kwa tendo hilo la
kuangalia mji wa Yerusalemu wakati
wa sala.
Reje: Daniel 6;10 Yohana 4;20-21
Pamoja na hayo historia inaonyesha
kuwa chanzo kikubwa zaidi cha
mabadiliko katika mwenendo na
mfumo wa kidini wa Muhammad
kinatokana na tukio la mwaka 610
BK ambapo katika mwaka huo
Muhammad alipokea mafunuo
mapya katika mapango ya Jabal ilaa.
Maisha ya Muhamadi uk 16 shekhe
Farsy).
Mafunuo hayo baadhi yake
yalionekana kuwa tofauti na
mafundisho ya Kibiblia
yaliyofahamika na Wayahudi na
hivyo kupelekea Wayahudi
kupingana na Muhammad kwa
kiwango ambacho kiliibua uadui
mkubwa baina yao.
Rejea maelezo ya sura hii ya Qur an.
Qur an 5:82
Hakika utawakuta walio madui zaidi
kuliko watu (wengine) kwa Waislam
ni Mayahudi na wale
mushirikina…….
Kimsingi hali hiyo ya uadui ndiyo
mzizi mkubwa wa mtengano huu
wa kiibada, ili kupata picha zaidi
hebu tusome maelezo ya sura
nyingine ya Qur an..
Qur an 2;145
Na hao walipewa kitabu, hata
ukiwaletea hoja za kila namna ,
hawatafuata kibla chako, wala wewe
hutafuata kibla chao……..na kama
ukifuata matamanio yao baada ya
kukufikia ilimu, utakuwa miongoni
mwa madhalimu…….
Kinachoripotiwa katika aya hii ni
mavutano baina ya makundi mawili
yaani Muhammadi na kundi la
Wayahudi miongoni mwa walopewa kitabu, mvutano huo ulihusiana na nani amfate mwenzake katika mfumo wa ibada ambapo kama utakumbuka vizuri hapo awali Muhammad alienda sambamba na Wayahudi kwa kuangalia Yerusalemu kwa mwaka mmoja na nusu.
Hivyo kile kinachoonekana katika
aya hii ni mabadiliko yaliyotokea
katika mwenendo wa kidini wa
Muhammad pale alipojitoa ghafra na kubadilisha muelekeo wa ibada kwa kuangalia makka badala ya kibla cha Yerusalemu