Dunia Ina mengi sana ya ajabu.....
Nakumbuka miaka kadhaa nyuma nimeenda kutembea kijijini....
Siku moja usiku mkubwa nikasikia mbwa wanabweka isivyo kuwa kawaida....kwa watu wa kijijini au waliowahi kufuga mbwa watakuwa wamenielewa!!!....
Kelele kali za zikanilazimu nitoke nje usiku nikiwa na panga na gongo moja zito sana!!!....nilitoka nikijua labda ni mnyama wa porini ameingia mitaa hiyo kimakosa hivyo nilitoka kwenda kumkimbiza!!!......
Nikawa naelekea usawa wa kule walipo mbwa.....
Mbwa waliponiona wakanikimbilia huku wakibweka!!!.....nikasogea kidogo nikaona kuna kitu mbele mfano wa mtoto mdogo sana!!!....naweza kusema kwa udogo wake ni kama wa miezi nane au tisa....lakini akiwa amevaa nguo!!!.....
Nilisisimka mwili lakini nikajipa ujasiri nikawa nasogelea pale kilipokaa!!!.....
Muda wote huo mbwa wanabweka lakini nyuma yangu tu hawathubutu kusogea pale karibu!!!....
Nilipofika karibu nikakaona kamejiinamia huku kakiwa kamevaa uniform za shule......lakini kalikuwa ni kadogo sana kiasi huwezi kusema ni mbilikimo au ni mtoto wa chekechea!!!....
Nikasimama mbele yake huku kakiwa kamejiinamia tu.....
Baada kama ya dakika 3 kakasimama kanatembea....nikasema Ngoja nikafuate nione kataingia nyumba gani....kalivyoniacha hatua kama kumi hivi kakapiga kona.,...nilivyokuja sikukaona tena......
Nikarudi ndani kulala.....asubuhi niliamka kichwa kikiwa kinauma vibaya sana!!....yale maumivu sikuwahi kuyapata tangu nazaliwa....mpaka nilipoenda kwa mtaalamu....akaniambia nilikutana na kitu kibaya usiku wa juzi....na akanichanja dawa fulani kwenye Paji la uso na kichwa kikapoa hapo hapo......!!!
Dunia Ina mengi....