Ukweli juu ya nafsi(roho) kuendelea kuishi baada ya kufa kwa mujibu wa biblia

Mpaka sasa tatizo la duniani ni kifo na kutokuwa na uwezo wa kutatua chamgamoto za magonjwa na matatizo mengine. Ila raha zipo na furaha ipo tena ya kutosha kwa mtu asiye na maradhi na mwenye uwezo wa kutatua chamgamoto za maisha.

Raha ya shida ni iwe na utatuzi. Raha ya njaa uwe na chakula au ujue pa kukipata chakula, raha ya changamoto yoyote ni iwe na utatuzi.

Mbinguni kama hakuna kusikia njaa, hakuna kiu, hakuna kuoa wala kuolewa, hakuna kujenga nyumba nzuri, hakuna viwanda vya magari ukanunua gari upendalo, unafahamu vipi kuwa kuna raha? Raha ni nn mbinguni?

Je binadamu wote wanataka hiyo aina ya raha? Au ni vile kama huitaki basi unachomwa hivyo unakuwa huna jinsi? Ts either raha ya kulazimishiwa au moto.

Unahisi raha ni kula na kunywa pombe, uzinzi, kuendesha vitu,kumiliki mali, kuagiza chochote unachokitaka na unakipata, kuwa na afya njema,kuwa na familia n.k

Siyo kweli hiyo siyo raha kamili kwa sababu utakubaliana nami kuwa hakuna raha duniani yakudumu kila kitu tunakipata duniani kwa limitation fulani na lazima penye raha kuwepo na uchungu fulani tukiachana na hilo la furaha ya kidunia ambayo kamwe hata ikiwa asilimia 100 bado ahikidhi kuitwa furaha kamili,

Hii ndiyo sababu ya baadhi ya watu ku-meditate kuitafuta hiyo furaha ya peponi isiyo na mfano wake yaani hali ya kujihisi kutoitaji kitu kingine cha ziada kukamilisha furaha yako mfano uraibu,hisia,pesa,nguvu,afya,mali,michezo,fahari nakadhalika,

Kuhusu kufikia mpaka kuchomwa moto siwezi lielezea zaidi maana siyo uonevu ni haki kabisa kwa kuwa mkaidi hiyo ndo adhabu ikufaayo,pia usijisaulishe kuwa huyo unayempinga ni kwa sababu yake upo na unaexist na kwa kuwa anakupenda anakutakia mema tu.
 
Mleta mada atakuwa ni Muadventista msabato au Jehova whiteness!

Maana hayo madhehebu mawili ndio yanafuata doctrine hiyo kwamba mtu akifa anapotea tu na kuwa mavumbi huku roho yake tu ndio inayomrudia Mungu.

Lakini madhehebu mengine yote yaliyobakia ya kikristo yanaamini kuna maisha baada ya kifo, na biblia inalithibitisha hili.

Kama hakuna maisha baada ya kifo, na kama mtu akifa anakuwa hajui lolote;

Swali:: pale juu ya mlima wa kugeuka sura, Yesu alipotokewa na Musa na Eliya, wale walikuwa wakina nani wakati Mussa alishakufa miaka zaidi ya elfu moja iliyopita?! MARKO 9:2

Yesu aliwaambia Mimi ndio huo ufufuo wa wafu na uzima, mtu akiniamini mimi hatakufa kabisa hata akifa atakuwa anaishi YOHANA 11:25


Yesu akawaambia kwanini mnamwita Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo,,, kwani Mungu ni Mungu wa walio hai sio Mungu wa wafu?!


Pale msalabani Yesu alisulubiwa pamoja na wahalifu wawili mmoja upande wa kushoto na mmoja upande wa kulia, yule muhalifu wa kulia alimwomba Yesu, kisha nae Yesu akamjibu akamwambia,"amin, amin nakwambia jioni ya Leo utakuwa nami peponi" LUKA 23: 42-43. Kama mtu akifa tu anapotea Yesu angemwambiaje yule mwalifu jioni ya Leo utakuwa nami Peponi???!!!

Yesu alipokufa makaburi yalifunuka na wafu walipita mjini Jerusalem na kuonekana na watu, sasa kama watu wakifa hawajui lolote wale wafu waliofufuka na kujionesha Jijini Jerusalem walitoka wapi na walienda wapi?! MATHAYO 27:51-53.
SOMA VIZURI BIBLIA YAKO.....

Katika Biblia hakuna mtu ye yote aliyewahi kuzikwa harafu ikasemekana ameenda mbinguni. Enoki alipaa, Musa alikufa akafufuka (Yuda 1:9); na hata hivyo Musa hakuzikwa na mtu ye yote, Eliya alipaa, Yesu alifufuka kwanza ndipo akapaa. Hakuna mtu aliyekufa akazikwa harafu akaenda mbinguni bila kufufuka kwanza. Yesu katika mfano wa tajiri na Lazalo amemtaja Ibrahimu kama mfano tu, kuwakilisha “mbinguni.” na ametaja neno kuzimu/kaburi kuwakilisha “jehanamu ya moto”.

Hivyo mfano huo haupaswi kuchukuliwa kiuhalisi; kwa maana kama Yesu angelimaanisha kweli kwamba tajiri alipokufa alienda moja kwa moja motoni, na Lazalo alienda moja kwa moja mbinguni, hii ingemfanya kujichanganya katika maneno yake; kwa maana Lazalo alipokufa, Yesu mwenyewe alisema Lazalo amelala [Yohana 11:11].

Mfano wa tajiri na Lazaro pia unatuonyesha kuwa ni jinsi gani isivyowezekana kwa mtu kutoka kwa wafu kuja huku duniani kwa walio hai; maana katika mfano Lazaro hakuruhusiwa kabisa kurudi kwa walio hai. Hivyo mizuka yote inayoibuka na kudanganya watu kwamba imetoka kwa wafu ni mapepo na uongo. Na hii hajilishi kwani hata huko nyakati za nyuma kuna pepo moja lilichukua sura ya nabii Samweli kisha likamtokea Sauli, na hivyo haishangazi leo kama pepo hili likichukua sura ya bikira Maria na kuwatokea watu, maana hiyo ni kazi ya shetani tangu zamani kwani; Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” 2 Wakorinto 11:14,15.
 
Yes, u have a point!

Ila tukifa hatukai makaburini. Tuliomwamini Yesu ni moja kwa moja peponi (paradise). Kusubiri kuingia kwenye mbingu mpya na nchi mpya (Yerusalemu mpya)

Wanaokufa hawajamwamini Yesu wao moja kwa moja ni kuzimu wakisubiri hukumu ya mwisho kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto wa kiberiti (hii ndio mauti ya pili)


YESU NI MWOKOZI
HUU UONGO HATA WEWE , MAPADRI, WACHUNGAJI, KINA MWAMPOSA WANAOUFUNDISHA... WAKIUMWA HATA HOMA , WANAOGOPA KIFO...KWANINI MSIFE MUENDE PARADISO? SOTE TUNAJUA NI KUZURI


NI DHAHIRI MNAPOTOSHA WATU


huo si ukweli, pumzi peke yake tu bila mwili haiwezi kwenda jehanum.

Yesu anatusaidia kuona ukweli huu anaposema,

“…mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum” Mathayo 10:28. Mungu atawangamiza watu katika jehanum huku wakiwa na mwili pamoja na roho pia, kudai kwamba roho pekee iko jehanum ni sawa na kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu!

Baadhi ya watu wemeniuliza swali kwamba, “Kama unafundisha kwamba roho za wafu haziko hai mbinguni pamoja na Yesu, Je hao watakatifu wengine unaosema wako mbinguni ni akina nani?”

Ninajibu kwamba, “Watakatifu walio mbinguni ninaomaanisha hapa ni Henoko na Eliya, ambao walipaa mwili na roho kwenda mbinguni, na Musa; ambaye alikufa, hata hivyo hakuzikwa na mtu yeyote, baadaye Yesu alikuja akamfufua na kwenda naye mbinguni (Yuda 1:9). Watakatifu wengine walio mbinguni sasa ni wale waliofufuka wakati wa tetemeko kipindi Yesu anakufa.)
 
SOMA VIZURI BIBLIA YAKO.....

Katika Biblia hakuna mtu ye yote aliyewahi kuzikwa harafu ikasemekana ameenda mbinguni. Enoki alipaa, Musa alikufa akafufuka (Yuda 1:9); na hata hivyo Musa hakuzikwa na mtu ye yote, Eliya alipaa, Yesu alifufuka kwanza ndipo akapaa. Hakuna mtu aliyekufa akazikwa harafu akaenda mbinguni bila kufufuka kwanza. Yesu katika mfano wa tajiri na Lazalo amemtaja Ibrahimu kama mfano tu, kuwakilisha “mbinguni.” na ametaja neno kuzimu/kaburi kuwakilisha “jehanamu ya moto”.

Hivyo mfano huo haupaswi kuchukuliwa kiuhalisi; kwa maana kama Yesu angelimaanisha kweli kwamba tajiri alipokufa alienda moja kwa moja motoni, na Lazalo alienda moja kwa moja mbinguni, hii ingemfanya kujichanganya katika maneno yake; kwa maana Lazalo alipokufa, Yesu mwenyewe alisema Lazalo amelala [Yohana 11:11].

Mfano wa tajiri na Lazaro pia unatuonyesha kuwa ni jinsi gani isivyowezekana kwa mtu kutoka kwa wafu kuja huku duniani kwa walio hai; maana katika mfano Lazaro hakuruhusiwa kabisa kurudi kwa walio hai. Hivyo mizuka yote inayoibuka na kudanganya watu kwamba imetoka kwa wafu ni mapepo na uongo. Na hii hajilishi kwani hata huko nyakati za nyuma kuna pepo moja lilichukua sura ya nabii Samweli kisha likamtokea Sauli, na hivyo haishangazi leo kama pepo hili likichukua sura ya bikira Maria na kuwatokea watu, maana hiyo ni kazi ya shetani tangu zamani kwani; Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” 2 Wakorint

Umeandika maelezo marefu ambayo hata sijayanukuu, hakuna mahali popote ambapo nilinukuu mfano wa Ibrahim na Lazaro! Wala hakuna popote kwenye maelezo yangu ambapo niliwahi kueleza kisa cha mfalme Sauli kwenda kuwa mwanamke muaguzi pepo ampandishie Nabii Samweli!!! Sijui kwanini unaniwekea maelezo ambayo sijawahi kuyanukuu popote!

Pengine hukuelewa maelezo yangu!

Narudia tena! Musa alikufa AKAZIKWA NA MUNGU, MWILI WAKE (MAITI YAKE IKAGOMBANIWA KATI YA MALAIKA NA SHETANI) lakini malaika akamwambia shetani Bwana na akukemee akamzika yeye! Hivyo hakuna ubishi kuwa Nabii Mussa ALIKUFA NA ALIZIKWA
(Kumbukumbu la Torati 34:5-6)

Swali ambalo hukujibu Bali umekimbilia mifano ya Ibrahim na Lazaro na sauli na samweli, ambayo sijainukuu popote ni hili, kama Musa tunasoma kwamba alikufa akazikwa na Mungu (kumbukumbu la torati 34:5-6), na Mtu akifa umesema anapotea na kuwa mavumbi, sasa Yule Mussa aliyemtokea Yesu pale mlimani alitokea wapi??????

Umesema hakuna mtu ambaye hakwenda mbinguni bila kufufuka nipe andiko mstari gani unasema kuwa Musa aliwahi kufufuka????
MARKO 9:2


Pili umeshindwa kunijibu kuwa; Yesu aliwaambia wayahudi kuwa Mungu ni Mungu wa waliyo hai sio Mungu wa wafu, kwanini Mnamwita Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo wakati wote hao ni marehemu?! Wayahudi wakashindwa kumjibu swali hili???? Ni jibu wewe?????? Na kama wako hai wapi waliwahi kufufuka???!


Tatu, Yesu alipomfufua Lazaro alimwambia dadayake Martha kuwa "Mimi ndimi huo uzima na ufufuo, mtu akiniamini Mimi hatakufa kamwe bali ajapokufa atakuwa anaishi!" Nini maana ya HATAKUFA KAMWE HATA AJAPOKUFA ATAKUWA ANAISHI, (Yohana 11:25)


Nne, Yesu alimwambia yule muhalifu pale msalabani upande wake wakulia kwamba "Amin, Amin nakwambia Jioni ya Leo utakuwa nami Peponi" (luka 23:42-43)

Yesu alisema JIONI YA LEO UTAKUWA NAMI PEPONI, NI PEPO GANI WAKATI YESU ALIKUFA SAA TISA ALASIRI YA MCHANA????!!! na umesema mtu akifa anakuwa mavumbi kaburini??? kuna pepo kaburini wakati wanakuwa mavumbi???? Kama mtu akifa anapotea na kuwa mavumbi (kwa mujibu wa maelezo yako) basi Yesu ni mwongo??? Hiyo pepo aliyomwahidi yule muhalifu jioni ya Siku ile ile waliposulubiwa ilikuwa pepo ipi???? Na kama peponi ni mbinguni na umesema mtu haendi peponi bila kwanza kufa na kufufuka, ilikuwaje Yesu amwahidi yule muhalifu watakuwa wote "JIONI YA LEO" ilihali akijua atafufuka siku ya tatu???? Na hakuna popote (andiko) panapo tuonyesha kuwa yule muhalifu alifufuka na kwenda peponi jioni ile ile?????
(LUKA 23:42-43.)




NB:
Naomba jibu haya maswali yangu, na tafadhali usiruke swali hata moja, jikite kwenye kile nilicho uliza kwa kunukuu maandiko kuliko kunipeleka kwa Ibrahim na Lazaro au sauli na samweli ambako hata sijawahi kunukuu popote!
 
Umeandika maelezo marefu ambayo hata sijayanukuu, hakuna mahali popote ambapo nilinukuu mfano wa Ibrahim na Lazaro! Wala hakuna popote kwenye maelezo yangu ambapo niliwahi kueleza kisa cha mfalme Sauli kwenda kuwa mwanamke muaguzi pepo ampandishie Nabii Samweli!!! Sijui kwanini unaniwekea maelezo ambayo sijawahi kuyanukuu popote!

Pengine hukuelewa maelezo yangu!

Narudia tena! Musa alikufa AKAZIKWA NA MUNGU, MWILI WAKE (MAITI YAKE IKAGOMBANIWA KATI YA MALAIKA NA SHETANI) lakini malaika akamwambia shetani Bwana na akukemee akamzika yeye! Hivyo hakuna ubishi kuwa Nabii Mussa ALIKUFA NA ALIZIKWA
(Kumbukumbu la Torati 34:5-6)

Swali ambalo hukujibu Bali umekimbilia mifano ya Ibrahim na Lazaro na sauli na samweli, ambayo sijainukuu popote ni hili, kama Musa tunasoma kwamba alikufa akazikwa na Mungu (kumbukumbu la torati 34:5-6), na Mtu akifa umesema anapotea na kuwa mavumbi, sasa Yule Mussa aliyemtokea Yesu pale mlimani alitokea wapi??????

Umesema hakuna mtu ambaye hakwenda mbinguni bila kufufuka nipe andiko mstari gani unasema kuwa Musa aliwahi kufufuka????
MARKO 9:2


Pili umeshindwa kunijibu kuwa; Yesu aliwaambia wayahudi kuwa Mungu ni Mungu wa waliyo hai sio Mungu wa wafu, kwanini Mnamwita Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo wakati wote hao ni marehemu?! Wayahudi wakashindwa kumjibu swali hili???? Ni jibu wewe?????? Na kama wako hai wapi waliwahi kufufuka???!


Tatu, Yesu alipomfufua Lazaro alimwambia dadayake Martha kuwa "Mimi ndimi huo uzima na ufufuo, mtu akiniamini Mimi hatakufa kamwe bali ajapokufa atakuwa anaishi!" Nini maana ya HATAKUFA KAMWE HATA AJAPOKUFA ATAKUWA ANAISHI, (Yohana 11:25)


Nne, Yesu alimwambia yule muhalifu pale msalabani upande wake wakulia kwamba "Amin, Amin nakwambia Jioni ya Leo utakuwa nami Peponi" (luka 23:42-43)

Yesu alisema JIONI YA LEO UTAKUWA NAMI PEPONI, NI PEPO GANI WAKATI YESU ALIKUFA SAA TISA ALASIRI YA MCHANA????!!! na umesema mtu akifa anakuwa mavumbi kaburini??? kuna pepo kaburini wakati wanakuwa mavumbi???? Kama mtu akifa anapotea na kuwa mavumbi (kwa mujibu wa maelezo yako) basi Yesu ni mwongo??? Hiyo pepo aliyomwahidi yule muhalifu jioni ya Siku ile ile waliposulubiwa ilikuwa pepo ipi???? Na kama peponi ni mbinguni na umesema mtu haendi peponi bila kwanza kufa na kufufuka, ilikuwaje Yesu amwahidi yule muhalifu watakuwa wote "JIONI YA LEO" ilihali akijua atafufuka siku ya tatu???? Na hakuna popote (andiko) panapo tuonyesha kuwa yule muhalifu alifufuka na kwenda peponi jioni ile ile?????
(LUKA 23:42-43.)




NB:
Naomba jibu haya maswali yangu, na tafadhali usiruke swali hata moja, jikite kwenye kile nilicho uliza kwa kunukuu maandiko kuliko kunipeleka kwa Ibrahim na Lazaro au sauli na samweli ambako hata sijawahi kunukuu popote!
UNATAFSIRI MAANDIKO KWA AKILI YAKO , NITAKUWEKEA AYA HALAFU UTANIAMBIA NI ZAUONGO AU UTAJUA ULIKUWA HUJUI

KUHUSU mus
Umeandika maelezo marefu ambayo hata sijayanukuu, hakuna mahali popote ambapo nilinukuu mfano wa Ibrahim na Lazaro! Wala hakuna popote kwenye maelezo yangu ambapo niliwahi kueleza kisa cha mfalme Sauli kwenda kuwa mwanamke muaguzi pepo ampandishie Nabii Samweli!!! Sijui kwanini unaniwekea maelezo ambayo sijawahi kuyanukuu popote!

Pengine hukuelewa maelezo yangu!

Narudia tena! Musa alikufa AKAZIKWA NA MUNGU, MWILI WAKE (MAITI YAKE IKAGOMBANIWA KATI YA MALAIKA NA SHETANI) lakini malaika akamwambia shetani Bwana na akukemee akamzika yeye! Hivyo hakuna ubishi kuwa Nabii Mussa ALIKUFA NA ALIZIKWA
(Kumbukumbu la Torati 34:5-6)

Swali ambalo hukujibu Bali umekimbilia mifano ya Ibrahim na Lazaro na sauli na samweli, ambayo sijainukuu popote ni hili, kama Musa tunasoma kwamba alikufa akazikwa na Mungu (kumbukumbu la torati 34:5-6), na Mtu akifa umesema anapotea na kuwa mavumbi, sasa Yule Mussa aliyemtokea Yesu pale mlimani alitokea wapi??????

Umesema hakuna mtu ambaye hakwenda mbinguni bila kufufuka nipe andiko mstari gani unasema kuwa Musa aliwahi kufufuka????
MARKO 9:2


Pili umeshindwa kunijibu kuwa; Yesu aliwaambia wayahudi kuwa Mungu ni Mungu wa waliyo hai sio Mungu wa wafu, kwanini Mnamwita Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo wakati wote hao ni marehemu?! Wayahudi wakashindwa kumjibu swali hili???? Ni jibu wewe?????? Na kama wako hai wapi waliwahi kufufuka???!


Tatu, Yesu alipomfufua Lazaro alimwambia dadayake Martha kuwa "Mimi ndimi huo uzima na ufufuo, mtu akiniamini Mimi hatakufa kamwe bali ajapokufa atakuwa anaishi!" Nini maana ya HATAKUFA KAMWE HATA AJAPOKUFA ATAKUWA ANAISHI, (Yohana 11:25)


Nne, Yesu alimwambia yule muhalifu pale msalabani upande wake wakulia kwamba "Amin, Amin nakwambia Jioni ya Leo utakuwa nami Peponi" (luka 23:42-43)

Yesu alisema JIONI YA LEO UTAKUWA NAMI PEPONI, NI PEPO GANI WAKATI YESU ALIKUFA SAA TISA ALASIRI YA MCHANA????!!! na umesema mtu akifa anakuwa mavumbi kaburini??? kuna pepo kaburini wakati wanakuwa mavumbi???? Kama mtu akifa anapotea na kuwa mavumbi (kwa mujibu wa maelezo yako) basi Yesu ni mwongo??? Hiyo pepo aliyomwahidi yule muhalifu jioni ya Siku ile ile waliposulubiwa ilikuwa pepo ipi???? Na kama peponi ni mbinguni na umesema mtu haendi peponi bila kwanza kufa na kufufuka, ilikuwaje Yesu amwahidi yule muhalifu watakuwa wote "JIONI YA LEO" ilihali akijua atafufuka siku ya tatu???? Na hakuna popote (andiko) panapo tuonyesha kuwa yule muhalifu alifufuka na kwenda peponi jioni ile ile?????
(LUKA 23:42-43.)




NB:
Naomba jibu haya maswali yangu, na tafadhali usiruke swali hata moja, jikite kwenye kile nilicho uliza kwa kunukuu maandiko kuliko kunipeleka kwa Ibrahim na Lazaro au sauli na samweli ambako hata sijawahi kunukuu popote!
MBONA UNATAFSIRI MAANDIKO KWA AKILI YAKO? Lini Ibrahimu , yakobo na isaka wapo hai ? je biblia inajipinga?

DAUDI, IBRAHIMU, YAKOBO , ISAKA.... WALISHAKUFA JAPOKUWA WANAUNGOJA UZIMA WA MILELE.....
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa Mkono wangu wa Kuume. Hata nitakapoweka adui zako chini ya miguu yako. Daudi, alifariki na akazikwa.[ Matendo.2:29-39].

Mzee wetu Ibrahimu hakuahidiwa mbingu bali nchi. Naye Aliamini kwa kuutegemea Mji wenye misingi ambao Mwenye Kuubuni Na Mwenye Kuujenga Ni Mungu Baba [Ebr.11:10].

KUHUSU MUSA NIMEKUPA AYA YUDA 1;9

Yuda 1:9 SRUV​

Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

YESU kusema Ujapokuwa umekufa huu hai, ni kwa wale tu waliokufa ktk BWANA... hao wakifufuliwa wataurithi uzima wa milele
Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni " BWANA" , ( YESU NI BWANA NA NI KRISTO: Mdo 2:36; 5:42; 9:22; 17:3; 18:5,28), Na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, Utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.( Rum.10:9,10; Yohana.20:29-31).

Yesu hakumaanisha kwamba Lazaro alikuwa amepumzika. Yesu akaendelea kusema: “Lazaro amekufa.” (Yohana 11:11-14) Kwa hiyo Yesu alilinganisha kifo na usingizi. Hakusema kwamba Lazaro alikuwa mbinguni au pamoja na watu wa familia yake waliokufa zamani. Wala hakusema Lazaro anateseka katika moto wa mateso au amezaliwa upya akiwa mwanadamu au mnyama. Alimaanisha kwamba ni kama Lazaro alikuwa amelala usingizi mzito. Maandiko mengine hufananisha kifo na usingizi mzito. Biblia inasema kwamba Stefano alipouawa, ‘alilala usingizi katika kifo.’ (Matendo 7:60) Pia, mtume Paulo aliandika kwamba baadhi ya Wakristo walikuwa “wamelala usingizi katika kifo.”—1 Wakorintho 15:6.


Ukweli ni kwamba Bwana wetu Yesu Kristo alipomwambia yule mhalifu aliyetubu ya kwamba , leo hivi utakuwa pamoja Nami peponi

[ Luka.23:42], Hakuwa na maana ya kwamba siku ile ile [leo hivi] alipanda na Bwana wetu Yesu Kristo kwenda peponi mbinguni. Alimhakikishia yule mhalifu ni " UZIMA WA MILELE". Ya kwamba tangu siku ile kwa " KUTUBU", sasa amepata uzima wa milele tangu saa ile ile, kama Maandiko yasemavyo:
Amini, amini, nakwambia, Yeye alisikiaye Neno Langu Na Kumwamini Yeye Aliyenipeleka " YUNA UZIMA WA MILELE"; Wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautuni na kuingia uzimani [ Yohana.5:24]. Kwa kuwa Mapenzi Yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana Na Kumwamini Yeye ( Kama yule mhalifu akiyetubu), Awe na uzima wa milele, " NAMI NITAMFUFUA SIKU YA MWISHO". [ Yohana.6:40].

Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu; Hivyo wote tutasubiri siku ya hukumu pamoja na yule mhalifu aliyetubu.( Ila Siku ile kwa watakatifu wote pamoja na yule mhalifu aliyetubu, wao hawataingia hukumu, bali wao wataingia moja kwa moja kwenye kuurithi uzima wa milele). Waebrania.9:27,28; Mathayo.24:29-31,46; 25:31-34,41,46.
 
Umeandika maelezo marefu ambayo hata sijayanukuu, hakuna mahali popote ambapo nilinukuu mfano wa Ibrahim na Lazaro! Wala hakuna popote kwenye maelezo yangu ambapo niliwahi kueleza kisa cha mfalme Sauli kwenda kuwa mwanamke muaguzi pepo ampandishie Nabii Samweli!!! Sijui kwanini unaniwekea maelezo ambayo sijawahi kuyanukuu popote!

Pengine hukuelewa maelezo yangu!

Narudia tena! Musa alikufa AKAZIKWA NA MUNGU, MWILI WAKE (MAITI YAKE IKAGOMBANIWA KATI YA MALAIKA NA SHETANI) lakini malaika akamwambia shetani Bwana na akukemee akamzika yeye! Hivyo hakuna ubishi kuwa Nabii Mussa ALIKUFA NA ALIZIKWA
(Kumbukumbu la Torati 34:5-6)

Swali ambalo hukujibu Bali umekimbilia mifano ya Ibrahim na Lazaro na sauli na samweli, ambayo sijainukuu popote ni hili, kama Musa tunasoma kwamba alikufa akazikwa na Mungu (kumbukumbu la torati 34:5-6), na Mtu akifa umesema anapotea na kuwa mavumbi, sasa Yule Mussa aliyemtokea Yesu pale mlimani alitokea wapi??????

Umesema hakuna mtu ambaye hakwenda mbinguni bila kufufuka nipe andiko mstari gani unasema kuwa Musa aliwahi kufufuka????
MARKO 9:2


Pili umeshindwa kunijibu kuwa; Yesu aliwaambia wayahudi kuwa Mungu ni Mungu wa waliyo hai sio Mungu wa wafu, kwanini Mnamwita Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo wakati wote hao ni marehemu?! Wayahudi wakashindwa kumjibu swali hili???? Ni jibu wewe?????? Na kama wako hai wapi waliwahi kufufuka???!


Tatu, Yesu alipomfufua Lazaro alimwambia dadayake Martha kuwa "Mimi ndimi huo uzima na ufufuo, mtu akiniamini Mimi hatakufa kamwe bali ajapokufa atakuwa anaishi!" Nini maana ya HATAKUFA KAMWE HATA AJAPOKUFA ATAKUWA ANAISHI, (Yohana 11:25)


Nne, Yesu alimwambia yule muhalifu pale msalabani upande wake wakulia kwamba "Amin, Amin nakwambia Jioni ya Leo utakuwa nami Peponi" (luka 23:42-43)

Yesu alisema JIONI YA LEO UTAKUWA NAMI PEPONI, NI PEPO GANI WAKATI YESU ALIKUFA SAA TISA ALASIRI YA MCHANA????!!! na umesema mtu akifa anakuwa mavumbi kaburini??? kuna pepo kaburini wakati wanakuwa mavumbi???? Kama mtu akifa anapotea na kuwa mavumbi (kwa mujibu wa maelezo yako) basi Yesu ni mwongo??? Hiyo pepo aliyomwahidi yule muhalifu jioni ya Siku ile ile waliposulubiwa ilikuwa pepo ipi???? Na kama peponi ni mbinguni na umesema mtu haendi peponi bila kwanza kufa na kufufuka, ilikuwaje Yesu amwahidi yule muhalifu watakuwa wote "JIONI YA LEO" ilihali akijua atafufuka siku ya tatu???? Na hakuna popote (andiko) panapo tuonyesha kuwa yule muhalifu alifufuka na kwenda peponi jioni ile ile?????
(LUKA 23:42-43.)




NB:
Naomba jibu haya maswali yangu, na tafadhali usiruke swali hata moja, jikite kwenye kile nilicho uliza kwa kunukuu maandiko kuliko kunipeleka kwa Ibrahim na Lazaro au sauli na samweli ambako hata sijawahi kunukuu popote!
NAKUJIBU TENA ,NA PIA NITAOMBA UNIJIBU,

TWENDE tararatibu
1.NAKUSWALIKA Kuna haja Gani ya ufufuo kama waliokufa wanakwenda mbinguni baada ya kufa.?

“Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.” Ufu. 22:12. “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko,… nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza… na hivyo tutakuwa na Bwana milele.” 1 Thes. 4:16,17. “Sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua,… na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu… Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa. Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika…” 1 Kor. 15:51-53.

2.KWANINI kama mtu akifa anaenda mbinguni , why mkiumwa au kifo kikiwasogelea... kama malaria, corona, n.k mtakimbilia hata INDIA , kwanini msife muende mbinguni ? je ni kubaya? mbona maandiko yanasema ni kuzuri sana

Yohana anaandika kuwa jiji hilo ni umbali wa maili 1,400 kwa urefu, na ni pana mithiri ya mchemraba mkamilifu (Ufunuo 21: 15-17). Mji pia utakuwa wa kuvutia kwa kila njia. Unaangazwa na utukufu wa Mungu (Ufunuo 21:23). Misingi yake kumi na miwili, yenye jina la mitume kumi na wawili, "umepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani" (Ufunuo 21: 19-20). Una milango kumi na miwili, kila mmoja ukiwa wa lulu, yenye majina ya makabila kumi na mawili ya Israeli (Ufunuo 21:12, 21). Barabara zitakuwa za dhahabu (Ufunuo 21:21).
 
Kwanini wanaofundisha tukifa tunaenda mbinguni, wao ni waoga balaa wa kifo? hata wakiumwa mafua watakimbilia india

au huko mbinguni kubaya?

HII NI DHAHIRI HILO FUNDISHO LA UONGO
 
Sasa mtumishi wa Mungu swali:- kwa kuwa umesema roho/pumzi hurudi kwa Mungu aliyoitoa, hiyo pumzi/roho inarudi na mwili mpya au inarudi ndani ya mwili wa Mungu? Anaivuta kama hewa?
Sijasema Mimi ni biblia
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
Mhubiri 12:7
Mwanzo ilitolewa na Mungu ikiwa pumzi tupu kwenye mwili uliokuwa mavumbi tupu
7 Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo 2:7
Sasa Mungu alipoitoa pumzi hakupungukiwa na uhai na anaposema inarudi kwake sio ndani yake ila dhamana ya uhai wako tena inabaki mikononi mwake maana yeye ndiye chanzo cha uhai wa mwanadamu.

Na si kweli kwamba kuna mahala anatunza vifurushi vya pumzi za watu ila akitaka uwe hai ataagiza pumzi kuja ndani yako nawe utakuwa hai

9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.
Ezekieli 37:9

10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.
Ezekieli 37:10
 
Sasa kama amelala, anarudi kuwa mavumbi, ataamka vipi wakati mwili haupo tena?
Wafu watafufuliwa kwa neno la Mungu si kwa sababu miili yao haijaoza! Fikiria watu waliokufa tangu Adamu Hadi leo si walishaoza kabisa...ila Kwa neno lake watafufuliwa wote

28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
Yohana 5:28

29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
Yohana 5:29

Angalia pia Ezekiel 37:1-15
 
The dead have no sense of time. Sekunde utakayokufa wewe ndiyo hiyo hiyo utakayofufuliwa kwa maana kuwa you won't be able to detect that lapse of time between the time of your death and that of your ressurrection.
Tuseme kwa mfano, ukiwafufua leo baadhi ya watu waliokufa hata miaka 2000 iliyopita, wanaweza kukuambia kuwa wamepitiwa usingizi sekunde moja tu, yaani imepita hata sekunde moja wakiwa hawana ufahamu, wakati mtu alifariki miaka 2000 iliyopita. Sijui kama unanielewa ninachosema hapa.

Ndiyo maana mimi huwa nawashangaa sana nikimsikia mtu anasema Yesu amechelewa kurudi. Yesu hachelewi kurudi as long as utakufa hata kama amebakiza miaka million mbili mbele halafu ndiyo arudi kwa sababu siku ukifa kabla hajarudi, huo muda wa miaka million mbili kwako aliokuwa amebakiza ndiyo arudi halafu ikatokea wewe ukafa kabla hajafanya hivyo, muda huo kwa wewe utakayekuwa upo kaburini, utabadilika na kuwa kama sekunde tu, ila wakaoendelea kuwa wako hai hao ndiyo watakaoweza kuuhesabu muda huo kwa miaka hiyo million mbili, katika vipindi vyao tofauti tofauti vya uhai wao, kila mtu kwa wakati wake kipindi akiwa yuko uhai hapa duniani.

Kwa hiyo Yesu anachelewa kurudi tu iwapo mtu atalazimika kutokufa na kumsubiri hadi arudi ila kwwa wale wote wanaokufa, kwao ni kama Yesu tayari alisharudi.

Ikitokea kwa mfano tuseme leo Roho Mtakatifu akaja kwako na kukuambia kuwa hautakufa mpaka Yesu atakaporudi, na wakati tuseme Yesu atakuwa amebakiza miaka million mbili ndiyo arudi, hapo angalau wewe unaweza kusema kuwa Yesu anachelewa kurudi, au bado yuko mbali kidogo, ila kwa wale wanaokufa, Yesu hachelewi hata kama atakuwa amebakiza miaka billion kumi ( huu ni mfano tu, na si kweli) mbele ndiyo arudi. The moment you die, the moment He returns, hata kama utakaa mabillion ya mabillion kaburini. The dead have no sense of time.
Upo sahihi sana, hakuna mda kwenye kifo..hata billion years, ukiamshwa utaona umelala a second tu, ..ht usiku tukilala hamna muda, ndio mfano wa kifo
 
Upo sahihi sana, hakuna mda kwenye kifo..hata billion years, ukiamshwa utaona umelala a second tu, ..ht usiku tukilala hamna muda, ndio mfano wa kifo
That overnight time you normally spend at your bed, and of which you sometimes feel its apparent length in terms of second rather than hours, whether you fell asleep at around 2100hrs and woke up at aound 0600hrs (a total of complete 9 hours), might be longer billions of times than the time you will feel to have your body spent in the grave. Those apparent few seconds which replace the 9 hours of your daily sleep, are actually longer billions of times, as compared to the time your body will stay in the grave before ressurection, and regardless of the time your body will spend burried in the grave. Hata kama mwili wako utakaa mabillion ya miaka kaburini, those billions of years will seem to be just microsecnds.
 
hakuna mizmu wala nini mkuu, ile ni mishetani
Makao ya shetani pamoja na malaika wake wote ni kuzimu, huku duniani huwa wanakuja kufanya fujo tu, wakishirikiana na binadamu ambao walishabakiza maumbile ya kibinadamu tu ila roho zao ni za kuzimu na za kishetani. Kwa hiyo mizimu ni kiumbe yeyote anayeishi kuzimu, shetani akiwa mmoja wao
 
Makao ya shetani pamoja na malaika wake wote ni kuzimu, huku duniani huwa wanakuja kufanya fujo tu, wakishirikiana na binadamu ambao walishabakiza maumbile ya kibinadamu tu ila roho zao ni za kuzimu na za kishetani. Kwa hiyo mizimu ni kiumbe yeyote anayeishi kuzimu, shetani akiwa mmoja wao

Kuna jambo umelitamka ila mpaka leo lina utata yaani 'kuzimu' ni wapi? na hao viumbe wasiyo na ubinadamu bali roho za kuzimu ukiachilia mbali washirikina kuna mauhusiano ya ukaribu na wanameditation pia?
 
Kuna jambo umelitamka ila mpaka leo lina utata yaani 'kuzimu' ni wapi? na hao viumbe wasiyo na ubinadamu bali roho za kuzimu ukiachilia mbali washirikina kuna mauhusiano ya ukaribu na wanameditation pia?
Kwani wewe ukiulizwa duniani ni wapi utajibuje? Duniani ni hapa ulipo wewe ila si makazi pekee ya viumbe wote wanaoishi. Kuna viumbe vingine ambavyo haviishi hapa duniani, vinaishi kuzimu. Sina details zaidi za kuzimu kwa sababu hainisadii sana kujua mambo ya kuzimu, inanisadia zaidi kujua ya hapo nilipo. Muhimu tu ni kwamba kila lisilo jema unalokumbana nalo asili yake ni kuzimu. Hata Corona pia imetokana na roho iliyotokea kuzimu
 
Kwani wewe ukiulizwa duniani ni wapi utajibuje? Duniani ni hapa ulipo wewe ila si makazi pekee ya viumbe wote wanaoishi. Kuna viumbe vingine ambavyo haviishi hapa duniani, vinaishi kuzimu. Sina details zaidi za kuzimu kwa sababu hainisadii sana kujua mambo ya kuzimu, inanisadia zaidi kujua ya hapo nilipo. Muhimu tu ni kwamba kila lisilo jema unalokumbana nalo asili yake ni kuzimu. Hata Corona pia imetokana na roho iliyotokea kuzimu
Baada ya kunijibu utaona ni jinsi gani ni muhimu kujua huko kuzimu ni wapi, maana kama unadai majanga mengi yanayotukabili kiroho na kiafya hapa duniani uanzia kuzimu kwanini tusiondoe vichwani mwetu huo ujinga wakutokujua lolote kuhusu kuzimu?

Simaanishi kwenda au kufanya ya kuzimu bali kuwa na ufahamu kuwa kuzimu ni kitu gani, nini ufanyika huko na kipi tuepuke tusiende huko.

Pengine kutokujua ya huko labda ndo chanzo cha viumbe vya huko kutunyanyasa sisi au kutuvuruga katika dunia iliyo mahali petu salama pa kuishi.

Maana masimulizi na michoro mbalimbali ya kuzimu uashiria kuzimu kuwa sehemu fulani chini ya dunia ambapo mimi na wewe tutakubaliana kuwa hamnaga chini ya dunia bali kuna katikati ya kipenyo cha duara lake ambapo tunakutana na mantle then core na hapo hutawaliwa na jotoridi kali na sifa za ki-volcano "pengine hapo ndo kuzimu kwenyewe"

au ni nje ya dunia "kwenye uso wa ardhi tunapoishi sisi au angani sehemu fulani tusiyoweza iona kwa macho" all in all kuzimu ni wapi? Labda wachangiaji nao watakuja na majibu.
 
Baada ya kunijibu utaona ni jinsi gani ni muhimu kujua huko kuzimu ni wapi, maana kama unadai majanga mengi yanayotukabili kiroho na kiafya hapa duniani uanzia kuzimu kwanini tusiondoe vichwani mwetu huo ujinga wakutokujua lolote kuhusu kuzimu?

Simaanishi kwenda au kufanya ya kuzimu bali kuwa na ufahamu kuwa kuzimu ni kitu gani, nini ufanyika huko na kipi tuepuke tusiende huko.

Pengine kutokujua ya huko labda ndo chanzo cha viumbe vya huko kutunyanyasa sisi au kutuvuruga katika dunia iliyo mahali petu salama pa kuishi.

Maana masimulizi na michoro mbalimbali ya kuzimu uashiria kuzimu kuwa sehemu fulani chini ya dunia ambapo mimi na wewe tutakubaliana kuwa hamnaga chini ya dunia bali kuna katikati ya kipenyo cha duara lake ambapo tunakutana na mantle then core na hapo hutawaliwa na jotoridi kali na sifa za ki-volcano "pengine hapo ndo kuzimu kwenyewe"

au ni nje ya dunia "kwenye uso wa ardhi tunapoishi sisi au angani sehemu fulani tusiyoweza iona kwa macho" all in all kuzimu ni wapi? Labda wachangiaji nao watakuja na majibu.
Pale Misri tu, yaani hapa hapa tulipo duniani, kuna vitu vipo vinaonekana kwa macho lakin hadi leo, hatujui asili yake na wala hatuwezi kujua nani alivijenga, mapiramidi ya Misri. Leo wewe unataka uje uwe mtaalamu wa mambo ya kuzimu? By the way of what use? Cha msingi unachotakiwa kujua kuhusiana na kuzimu ni ile namna ya kujikinga na majanga yanayotokana na nguvu za huko tu basi. Hizi details zingine ni irrelevant kwako. Wewe ya kwako hapana duniani tu huyawezi, uende tena extra mile kuwa expert wa mambo ya kuzimu kwa kudai kuwa unataka kutokuonekana mjinga?

Actually unaonekana mjinga zaidi kwa kuanza kuchimba mambo ya kuzimu na kuacha kushughulika na mambo yako ya msingi hapa duniani
 
Pale Misri tu, yaani hapa hapa tulipo duniani, kuna vitu vipo vinaonekana kwa macho lakin hadi leo, hatujui asili yake na wala hatuwezi kujua nani alivijenga, mapiramidi ya Misri. Leo wewe unataka uje uwe mtaalamu wa mambo ya kuzimu? By the way of what use? Cha msingi unachotakiwa kujua kuhusiana na kuzimu ni ile namna ya kujikinga na majanga yanayotokana na nguvu za huko tu basi. Hizi details zingine ni irrelevant kwako. Wewe ya kwako hapana duniani tu huyawezi, uende tena extra mile kuwa expert wa mambo ya kuzimu kwa kudai kuwa unataka kutokuonekana mjinga?

Actually unaonekana mjinga zaidi kwa kuanza kuchimba mambo ya kuzimu na kuacha kushughulika na mambo yako ya msingi hapa duniani
Ili ujikinge na tatizo mfano magonjwa au majanga lazima ujue chanzo na namna ya kuliepuka ndipo hapo research au laboratory experiments au study ufanywa kupata majawabu,, sasa leo hii kuzimu ndo chanzo halafu hauruhusu idea ya kuichunguza au kuichambua kuzimu kuja na majibu unafikiri utaweza kutokomeza tatizo au utabakia kutibu symptoms na kujikinga na usichokijua au

pengine kuzimu ni hofu yako tu, ninaweza sema hii mindset yetu wenda ndo udhaifu unaotufanya miaka nenda rudi tushindwe kumdhibiti adui yetu shetani au tuendelee kurithishana hofu na matarajio kizazi mpaka kizazi.

sasa hili la kiroho au kuzimu jenyewe lina sababu gani hata lisichunguzwe au kudadisiwa ili lijulikane?
mf; unaongelea mapiramidi ambayo wajenzi wake kwenye vitabu vya dini au historia wanajulikana

labda swali lisilo na jibu hapo ni kwamba walifikiria vipi kama wanaweza jenga kitu kama hicho? Ukiwauliza swali kama hilo nami ntakuuliza binadamu wa leo aliwaza nini hata akaunda ndege?
 
Ili ujikinge na tatizo mfano magonjwa au majanga lazima ujue chanzo na namna ya kuliepuka ndipo hapo research au laboratory experiments au study ufanywa kupata majawabu,, sasa leo hii kuzimu ndo chanzo halafu hauruhusu idea ya kuichunguza au kuichambua kuzimu kuja na majibu unafikiri utaweza kutokomeza tatizo au utabakia kutibu symptoms na kujikinga na usichokijua au

pengine kuzimu ni hofu yako tu, ninaweza sema hii mindset yetu wenda ndo udhaifu unaotufanya miaka nenda rudi tushindwe kumdhibiti adui yetu shetani au tuendelee kurithishana hofu na matarajio kizazi mpaka kizazi.

sasa hili la kiroho au kuzimu jenyewe lina sababu gani hata lisichunguzwe au kudadisiwa ili lijulikane?
mf; unaongelea mapiramidi ambayo wajenzi wake kwenye vitabu vya dini au historia wanajulikana

labda swali lisilo na jibu hapo ni kwamba walifikiria vipi kama wanaweza jenga kitu kama hicho? Ukiwauliza swali kama hilo nami ntakuuliza binadamu wa leo aliwaza nini hata akaunda ndege?
Sources of knowledge, how many are they? You are talking of Empirical Knwoledge ambayo inaendana na empirical research. Kuzimu iko kwenye dimension ya an unseen world where empirical tools cannot work. Use empirical tools for emperical research only. Au pengine empirical research huwa inatumika popote hata kwenye spritual realm nako pia tools zake zinafanya kazi? Empiricism yenyewe imesemje kuhusu hilo?
You need to know the several types of knowledge existing and the tools used in research in each of them. Do not use empirical research /tools everywhere. Kuna vitu vingine ni miracles /mysteries ambavyo empirical tools will not work to explain anything substantial
 
Sources of knowledge, how many are they? You are talking of Empirical Knwoledge ambayo inaendana na empirical research. Kuzimu iko kwenye dimension ya an unseen world where empirical tools cannot work. Use empirical tools for emperical research only. Au pengine empirical research huwa inatumika popote hata kwenye spritual realm nako pia tools zake zinafanya kazi? Empiricism yenyewe imesemje kuhusu hilo?
You need to know the several types of knowledge existing and the tools used in research in each of them. Do not use empirical research /tools everywhere. Kuna vitu vingine ni miracles /mysteries ambavyo empirical tools will not work to explain anything substantial
Ni kweli kwa ulichokisema nakubaliana nacho kabisa kuhusu sayansi na ukomo wake, ila linapokuja suala la uchunguzi wa jambo lisilokuwepo kisayansi au linalosemekana kuwapo moja kwa moja

mwanadamu ujaribu kutumia fikra,uzoefu,historia,mahesabu,maono,milango ya fahamu,taarifa,sources both oral&written,practises,hisia,makisio n.k lengo likiwa lile lile kutumia njia yeyote ile iwezekanavyo kupata majibu (both idealistic na materialistic au practical)

Swali ni je, ikiwa suala la kuzimu halionekani kwa macho ya kawaida wala hatupaswi kujua yaliyomo wewe umelijuaje?

Na je huyo aliyekudokeza kuwa huko hakukufai udili na yanayokuhusu uwezi kumtumia pia kujua alichokuficha?

Kama kuna wanadamu wenzetu tiyari wapo au wana access yakuingia nakutoka katika dimension ya unseen world na tuko nao huoni kama kuna ubinafsi katika kupeana taarifa na siyo kwamba hatuwezi kujua?

Naamini katika kila jambo linalotukabili
huwa kuna njia ya kutokea tukiamua kutaka kujua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom