Ukweli juu ya nafsi(roho) kuendelea kuishi baada ya kufa kwa mujibu wa biblia

Undava King

JF-Expert Member
Aug 11, 2017
3,205
5,332
"Matunda ya kila mti wa bustani unaweza kula mpaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula,utakufa hakika" (mwanzo 2:16,17)

Lakini je kuna sehemu fulani ya mwanadamu inayoendelea kuishi baada ya mtu kufa?

Biblia inasema "Mungu hawezi kamwe kusema uongo" (waebrania 6:18) ukweli ni kwamba shetani ndiye alisema uongo alipomwambia Hawa hivi "Hakika hamtakufa" mwanzo 3:4.

Hivyo basi swali ni; ikiwa fundisho la kutokufa kwa nafsi ni uongo ni nini hutokea mtu anapokufa?

"Yehova Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai,naye mtu akawa nafsi hai" usemi "nafsi hai" unatokana na neno la kiebrania ne'phesh, likimaanisha kiumbe anayepumua.Mwanzo2:7

Hivyo biblia haielezei kuwa mwanadamu hakuumbwa akiwa na "nafsi isiyoweza kufa" badala yake ni "nafsi hai"

Ni kina nani basi walioleta fundisho la nafsi kutokufa kama siyo Mungu mwenyewe?

Wamisri walikuwa kikundi cha kwanza,wakifuatiwa na wababiloni na wagiriki walioeneza mafundisho hayo kuenea katika himaya nzima ya ugiriki katika mwaka wa utawala wa Aleksanda Mkuu 332W.K,

Baadae madhehebu ya kiyahudi ya waesene na mafarisayo, yalianza kufundisha kutokufa kwa nafsi kwa kupokea mawazo ya Plato" ilikuwa rahisi kuunganisha falsafa ya Plato na ukristo sababu ya nadharia ya Plato kwamba mwanzoni nafsi zetu zilikuwa mahali pazuri na sasa zinaishi ulimwengu uliopotoka"

Mtume Paulo analiongeleaje,"...vipindi vya nyakati za mwisho wengine wataanguka kutoka kwenye imani, wakisikiliza maneno yaliyoongozwa kwa roho yenye kupotosha na mafundisho ya roho waovu"(1Timotheo 4:1) Hivyo basi biblia haiungi mkono fundisho hilo na chanzo chake ni falsafa na dini za kale za kipagani.

Yesu anasema" Nanyi mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru" (Yohana 8:32)
Yesu kristo alisali hivi kwa Mungu; "uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli na juu ya yule uliyemtuma,yesu kristo"

Je wafu wako wapi? Wafu wako kaburini wakingojea ufufuo (Yohana) hawateseki au kuhisi maumivu yoyote, kwa sababu "wafu hawajui lolote kamwe" (mhubiri 9:5)-(mhubiri 9:10) hata hivyo, kupitia ufufuo, Mungu atakishinda kifo milele. 1 Wakorintho 15:24,55;ufunuo 21:4
Kauli tata; ijapokuwa mwili hurudi udongoni, roho humrudia Mungu.(Mh.12:7)

Utatuzi wake; kufuatana na sulemani, katika kifo, hakuna tofauti ya roho za wanyama na za wanadamu, wote huenda pamoja (mh.3:19-21). Anachomaanisha kuwa kinamrudia Mungu ni ile cheche ya uhai (mwa.2:7)

Imani ya kuongea na wafu(spiritualism) ikiwa wafu hawana ufahamu, je wanaongea huwa na akina nani?

Imani ya kuongea na wafu imeanzia kwenye uongo wa awali wa shetani kwa Hawa."Hakika hamtakufa"(mwa.3:4) Maneno hayo yalikuwa hubiri la kwanza (linaloendelea hivi sasa) juu ya kutokufa kwa roho(nafsi)

Roho itendayo dhambi itakufa(Eze.18:20)imebadilishwa kimtizamo kuwa "roho hata ikitenda dhambi itaendelea kuishi milele"

Hivyo utamaduni wa mafundisho haya umejenga imani yenye dhana yakubatilisha ukweli nakutimiliza matakwa ya shetani. Na kila haaminiye nakutimiliza matendo yakiimani katika njia hii ujinasibu mwishoni kuwa yu mungu au mwenye nguvu juu yake mwenyewe zakuumba nakuponya kujua kabla na baada ya,kutoa na kutwaa nakujitukuza mwenyewe sawa na ahadi ya babaye shetani "mtakuwa kama miungu"(Mwa.3:5)
 
So mchizi aliyekufa kabla ya yesu na yeye bado anangojea ufufua mpaka leo mika elf 2 na kedekede!!? Nikifika hapa nakua mzito kumini hizi ngano! Kuna akina daud nao wanangojea ufufua sijui ni mika elf ngapi mpaka sasa!! Acha nijipitie kushoto tu🚶‍♂️🚶‍♂️
 
So mchizi aliyekufa kabla ya yesu na yeye bado anangojea ufufua mpaka leo mika elf 2 na kedekede!!? Nikifika hapa nakua mzito kumini hizi ngano! Kuna akina daud nao wanangojea ufufua sijui ni mika elf ngapi mpaka sasa!! Acha nijipitie kushoto tu🚶‍♂️🚶‍♂️
The dead have no sense of time. Sekunde utakayokufa wewe ndiyo hiyo hiyo utakayofufuliwa kwa maana kuwa you won't be able to detect that lapse of time between the time of your death and that of your ressurrection.
Tuseme kwa mfano, ukiwafufua leo baadhi ya watu waliokufa hata miaka 2000 iliyopita, wanaweza kukuambia kuwa wamepitiwa usingizi sekunde moja tu, yaani imepita hata sekunde moja wakiwa hawana ufahamu, wakati mtu alifariki miaka 2000 iliyopita. Sijui kama unanielewa ninachosema hapa.

Ndiyo maana mimi huwa nawashangaa sana nikimsikia mtu anasema Yesu amechelewa kurudi. Yesu hachelewi kurudi as long as utakufa hata kama amebakiza miaka million mbili mbele halafu ndiyo arudi kwa sababu siku ukifa kabla hajarudi, huo muda wa miaka million mbili kwako aliokuwa amebakiza ndiyo arudi halafu ikatokea wewe ukafa kabla hajafanya hivyo, muda huo kwa wewe utakayekuwa upo kaburini, utabadilika na kuwa kama sekunde tu, ila wakaoendelea kuwa wako hai hao ndiyo watakaoweza kuuhesabu muda huo kwa miaka hiyo million mbili, katika vipindi vyao tofauti tofauti vya uhai wao, kila mtu kwa wakati wake kipindi akiwa yuko uhai hapa duniani.

Kwa hiyo Yesu anachelewa kurudi tu iwapo mtu atalazimika kutokufa na kumsubiri hadi arudi ila kwwa wale wote wanaokufa, kwao ni kama Yesu tayari alisharudi.

Ikitokea kwa mfano tuseme leo Roho Mtakatifu akaja kwako na kukuambia kuwa hautakufa mpaka Yesu atakaporudi, na wakati tuseme Yesu atakuwa amebakiza miaka million mbili ndiyo arudi, hapo angalau wewe unaweza kusema kuwa Yesu anachelewa kurudi, au bado yuko mbali kidogo, ila kwa wale wanaokufa, Yesu hachelewi hata kama atakuwa amebakiza miaka billion kumi ( huu ni mfano tu, na si kweli) mbele ndiyo arudi. The moment you die, the moment He returns, hata kama utakaa mabillion ya mabillion kaburini. The dead have no sense of time.
 
Mwanzo 2:7

BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Ukiangalia ;

Mwanzo 1:27

Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

Mungu alianza kuumba roho , baada ya roho tunaona Mungu akafanya mwili wa mavumbi sasa, baadae Mungu akapulizia pumzi ya uhai, tunaona mtu akawa nafsi hai . Nafsi ni matokea ya Mwili na Roho kuwa na puzmia ya uhai ndio ikaja nafsi kwa kugha nyepesi kuna ufufuno wa nafsi baada ya hiyo acts. Ila tunaona mtu akifa, mwili hurudi mavumbini, roho na nafsi hutoki, vinaenda palipo na ( roho iliyokuwa iki zi control ), kama Roho Mtakatifu basi vitaenda paradise na kama roho zidanganyazo basi itaenda kwa hizo roho zidanganyazo. Nafai ni muhimu sana, dunia itakufaidi nini kama ukapata kila kitu ila nafsi ikaenda motoni
 
The dead have no sense of time. Sekunde utakayokufa wewe ndiyo hiyo hiyo utakayofufuliwa kwa maana kuwa you won't be able to detect that lapse of time between the time of your death and that of your ressurrection.
Tuseme kwa mfano, ukiwafufua leo baadhi ya watu waliokufa hata miaka 2000 iliyopita, wanaweza kukuambia kuwa wamepitiwa usingizi sekunde moja tu, yaani imepita hata sekunde moja wakiwa hawana ufahamu, wakati mtu alifariki miaka 2000 iliyopita. Sijui kama unanielewa ninachosema hapa.

Ndiyo maana mimi huwa nawashangaa sana nikimsikia mtu anasema Yesu amechelewa kurudi. Yesu hachelewi kurudi as long as utakufa hata kama amebakiza miaka million mbili mbele halafu ndiyo arudi kwa sababu siku ukifa kabla hajarudi, huo muda wa miaka million mbili kwako aliokuwa amebakiza ndiyo arudi halafu ikatokea wewe ukafa kabla hajafanya hivyo, muda huo kwa wewe utakayekuwa upo kaburini, utabadilika na kuwa kama sekunde tu, ila wakaoendelea kuwa wako hai hao ndiyo watakaoweza kuuhesabu muda huo kwa miaka hiyo million mbili, katika vipindi vyao tofauti tofauti vya uhai wao, kila mtu kwa wakati wake kipindi akiwa yuko uhai hapa duniani.

Kwa hiyo Yesu anachelewa kurudi tu iwapo mtu atalazimika kutokufa na kumsubiri hadi arudi ila kwwa wale wote wanaokufa, kwao ni kama Yesu tayari alisharudi.

Ikitokea kwa mfano tuseme leo Roho Mtakatifu akaja kwako na kukuambia kuwa hautakufa mpaka Yesu atakaporudi, na wakati tuseme Yesu atakuwa amebakiza miaka million mbili ndiyo arudi, hapo angalau wewe unaweza kusema kuwa Yesu anachelewa kurudi, au bado yuko mbali kidogo, ila kwa wale wanaokufa, Yesu hachelewi hata kama atakuwa amebakiza miaka billion kumi ( huu ni mfano tu, na si kweli) mbele ndiyo arudi. The moment you die, the moment He returns, hata kama utakaa mabillion ya mabillion kaburini. The dead have no sense of time.
Yes, u have a point!

Ila tukifa hatukai makaburini. Tuliomwamini Yesu ni moja kwa moja peponi (paradise). Kusubiri kuingia kwenye mbingu mpya na nchi mpya (Yerusalemu mpya)

Wanaokufa hawajamwamini Yesu wao moja kwa moja ni kuzimu wakisubiri hukumu ya mwisho kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto wa kiberiti (hii ndio mauti ya pili)


YESU NI MWOKOZI
 
"Matunda ya kila mti wa bustani unaweza kula mpaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula,utakufa hakika" (mwanzo 2:16,17)

Lakini je kuna sehemu fulani ya mwanadamu inayoendelea kuishi baada ya mtu kufa?

Biblia inasema "Mungu hawezi kamwe kusema uongo" (waebrania 6:18) ukweli ni kwamba shetani ndiye alisema uongo alipomwambia Hawa hivi "Hakika hamtakufa" mwanzo 3:4.

Hivyo basi swali ni; ikiwa fundisho la kutokufa kwa nafsi ni uongo ni nini hutokea mtu anapokufa?

"Yehova Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai,naye mtu akawa nafsi hai" usemi "nafsi hai" unatokana na neno la kiebrania ne'phesh, likimaanisha kiumbe anayepumua.Mwanzo2:7

Hivyo biblia haielezei kuwa mwanadamu hakuumbwa akiwa na "nafsi isiyoweza kufa" badala yake ni "nafsi hai"

Ni kina nani basi walioleta fundisho la nafsi kutokufa kama siyo Mungu mwenyewe?

Wamisri walikuwa kikundi cha kwanza,wakifuatiwa na wababiloni na wagiriki walioeneza mafundisho hayo kuenea katika himaya nzima ya ugiriki katika mwaka wa utawala wa Aleksanda Mkuu 332W.K,

Baadae madhehebu ya kiyahudi ya waesene na mafarisayo, yalianza kufundisha kutokufa kwa nafsi kwa kupokea mawazo ya Plato" ilikuwa rahisi kuunganisha falsafa ya Plato na ukristo sababu ya nadharia ya Plato kwamba mwanzoni nafsi zetu zilikuwa mahali pazuri na sasa zinaishi ulimwengu uliopotoka"

Mtume Paulo analiongeleaje,"...vipindi vya nyakati za mwisho wengine wataanguka kutoka kwenye imani, wakisikiliza maneno yaliyoongozwa kwa roho yenye kupotosha na mafundisho ya roho waovu"(1Timotheo 4:1) Hivyo basi biblia haiungi mkono fundisho hilo na chanzo chake ni falsafa na dini za kale za kipagani.

Yesu anasema" Nanyi mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru" (Yohana 8:32)
Yesu kristo alisali hivi kwa Mungu; "uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli na juu ya yule uliyemtuma,yesu kristo"

Je wafu wako wapi? Wafu wako kaburini wakingojea ufufuo (Yohana) hawateseki au kuhisi maumivu yoyote, kwa sababu "wafu hawajui lolote kamwe" (mhubiri 9:5)-(mhubiri 9:10) hata hivyo, kupitia ufufuo, Mungu atakishinda kifo milele. 1 Wakorintho 15:24,55;ufunuo 21:4
Kauli tata; ijapokuwa mwili hurudi udongoni, roho humrudia Mungu.(Mh.12:7)

Utatuzi wake; kufuatana na sulemani, katika kifo, hakuna tofauti ya roho za wanyama na za wanadamu, wote huenda pamoja (mh.3:19-21). Anachomaanisha kuwa kinamrudia Mungu ni ile cheche ya uhai (mwa.2:7)

Imani ya kuongea na wafu(spiritualism) ikiwa wafu hawana ufahamu, je wanaongea huwa na akina nani?

Imani ya kuongea na wafu imeanzia kwenye uongo wa awali wa shetani kwa Hawa."Hakika hamtakufa"(mwa.3:4) Maneno hayo yalikuwa hubiri la kwanza (linaloendelea hivi sasa) juu ya kutokufa kwa roho(nafsi)

Roho itendayo dhambi itakufa(Eze.18:20)imebadilishwa kimtizamo kuwa "roho hata ikitenda dhambi itaendelea kuishi milele"

Hivyo utamaduni wa mafundisho haya umejenga imani yenye dhana yakubatilisha ukweli nakutimiliza matakwa ya shetani. Na kila haaminiye nakutimiliza matendo yakiimani katika njia hii ujinasibu mwishoni kuwa yu mungu au mwenye nguvu juu yake mwenyewe zakuumba nakuponya kujua kabla na baada ya,kutoa na kutwaa nakujitukuza mwenyewe sawa na ahadi ya babaye shetani "mtakuwa kama miungu"(Mwa.3:5)
Umeongea mambo meengi, ila cha kusikitisha hujui kuwa kuna tofauti ya roho na nafsi.

roho(conscience, intuition, communion)

nafsi(mind, will, emotion)

Hii inadhihirisha hukijui ulichokiandika.


YESU NI BWANA.
 
Yes, u have a point!

Ila tukifa hatukai makaburini. Tuliomwamini Yesu ni moja kwa moja peponi (paradise). Kusubiri kuingia kwenye mbingu mpya na nchi mpya (Yerusalemu mpya)

Wanaokufa hawajamwamini Yesu wao moja kwa moja ni kuzimu wakisubiri hukumu ya mwisho kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto wa kiberiti (hii ndio mauti ya pili)


YESU NI MWOKOZI
Mungu akubariki na azidi kukutunza.
 
Mwanzo 2:7

BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Ukiangalia ;

Mwanzo 1:27

Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

Mungu alianza kuumba roho , baada ya roho tunaona Mungu akafanya mwili wa mavumbi sasa, baadae Mungu akapulizia pumzi ya uhai, tunaona mtu akawa nafsi hai . Nafsi ni matokea ya Mwili na Roho kuwa na puzmia ya uhai ndio ikaja nafsi kwa kugha nyepesi kuna ufufuno wa nafsi baada ya hiyo acts. Ila tunaona mtu akifa, mwili hurudi mavumbini, roho na nafsi hutoki, vinaenda palipo na ( roho iliyokuwa iki zi control ), kama Roho Mtakatifu basi vitaenda paradise na kama roho zidanganyazo basi itaenda kwa hizo roho zidanganyazo. Nafai ni muhimu sana, dunia itakufaidi nini kama ukapata kila kitu ila nafsi ikaenda motoni
3 (Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu, Na roho ya Mungu i katika pua yangu
Ayubu 27:3

7 Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo 2:7

Kwa vifungu hivi ina maana roho = pumzi!
Kwa hiyo ili mtu afe pumzi hiyo ndio hutoka siyo?
(7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
Mhubiri 12:7)

Sasa kama Mungu alikupa pumzi ya uhai (roho) ukawa nafsi hai,ukaishi duniani ukatrnda mema na maovu halafu leo hiyo pumzi ya uhai (roho) inatoka na kumrudia Mungu aliyeitoa unakuwa mfu usiyejua chochote kama hapo kabla hunapokea pumzi ya uhai;

1. Kwa hiyo usemacho ni kuwa pumzi za watenda mema huenda paradise?
2. Pumzi za watenda mabaya huenda Kwa roho zidanganyazo?
3. Mbona biblia imesema zote humrudia Mungu aliyezitoa?
4. Lakini pia mbona mhubiri 3:19-21 inasema kitu tofauti na ulichosema?

19 Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
Mhubiri 3:19

20 Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.
Mhubiri 3:20

21 Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?
Mhubiri 3:21
 
The dead have no sense of time. Sekunde utakayokufa wewe ndiyo hiyo hiyo utakayofufuliwa kwa maana kuwa you won't be able to detect that lapse of time between the time of your death and that of your ressurrection.
Tuseme kwa mfano, ukiwafufua leo baadhi ya watu waliokufa hata miaka 2000 iliyopita, wanaweza kukuambia kuwa wamepitiwa usingizi sekunde moja tu, yaani imepita hata sekunde moja wakiwa hawana ufahamu, wakati mtu alifariki miaka 2000 iliyopita. Sijui kama unanielewa ninachosema hapa.

Ndiyo maana mimi huwa nawashangaa sana nikimsikia mtu anasema Yesu amechelewa kurudi. Yesu hachelewi kurudi as long as utakufa hata kama amebakiza miaka million mbili mbele halafu ndiyo arudi kwa sababu siku ukifa kabla hajarudi, huo muda wa miaka million mbili kwako aliokuwa amebakiza ndiyo arudi halafu ikatokea wewe ukafa kabla hajafanya hivyo, muda huo kwa wewe utakayekuwa upo kaburini, utabadilika na kuwa kama sekunde tu, ila wakaoendelea kuwa wako hai hao ndiyo watakaoweza kuuhesabu muda huo kwa miaka hiyo million mbili, katika vipindi vyao tofauti tofauti vya uhai wao, kila mtu kwa wakati wake kipindi akiwa yuko uhai hapa duniani.

Kwa hiyo Yesu anachelewa kurudi tu iwapo mtu atalazimika kutokufa na kumsubiri hadi arudi ila kwwa wale wote wanaokufa, kwao ni kama Yesu tayari alisharudi.

Ikitokea kwa mfano tuseme leo Roho Mtakatifu akaja kwako na kukuambia kuwa hautakufa mpaka Yesu atakaporudi, na wakati tuseme Yesu atakuwa amebakiza miaka million mbili ndiyo arudi, hapo angalau wewe unaweza kusema kuwa Yesu anachelewa kurudi, au bado yuko mbali kidogo, ila kwa wale wanaokufa, Yesu hachelewi hata kama atakuwa amebakiza miaka billion kumi ( huu ni mfano tu, na si kweli) mbele ndiyo arudi. The moment you die, the moment He returns, hata kama utakaa mabillion ya mabillion kaburini. The dead have no sense of time.
haya yote umeyajuaje??
 
Tofauti ya nafsi na roho ni nini?
Hahahaaa! "Au mwadhani ya kwamba maandiko yasema bure? Huyo roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?(Yakobo 4:5)
Soma alichowasilisha Mkuu Able man kafafanua vizuri kibiblia kuwa vyote hivyo vyamaanisha kitu kimoja na havitengani kwa maana ya mwanadamu alipuliziwa pumzi ya uhai ambayo ni Roho toka kwa Mungu ndani yake akawa nafsi hai yaani akawa na ile roho ndani yake iishiyo, hivyo nafsi ndiyo hiyohiyo roho yenyewe iishiyo ndani mwetu nakutupa uhai na fahamu zetu.
 
Mimi ni mkristo tena kindaki ndaki,lakini hua nina kigugumizi kikubwa sana ya story za maisha badala ya kifo, binafsi ninahisi na kuona wazi kwamba:-

1. Hakuna maisha baada ya kifo zaidi ya kutishana ili tustaarabiane hapa Duniani

2. Hakuna moto wa milele hata kidogo,nao ni uongo ili watu tustaarabiane tusilipe visasi na kutenda mabaya

3. Kwa mbaaaali nakua naamini yamkini baada ya kifo uhai huhamia kwenye kasha jingine lenye limezaliwa punde

4. Hakuna mwisho wa dunia isipokua pale tu mtu anapokufa
 
umejuaje kama hiyo njia ni sahihi
Vya rohoni huwa ni sahihi kwa yule anayevipokea, vinaweza visiwe sahihi kwako. Ulishawahi kulala usingizi halafu ukaota ndoto? Je, akija mtu akakwambia kuwa unadanganya huwa huoti, wakati ukweli ni kuwa kweli huwa unaota, mtu huyu unaweza ukamthibitishiaje kwamba kweli wewe huwa unaota?
 
Vya rohoni huwa ni sahihi kwa yule anayevipokea, vinaweza visiwe sahihi kwako. Ulishawahi kulala usingizi halafu ukaota ndoto? Je, akija mtu akakwambia kuwa unadanganya huwa huoti, wakati ukweli ni kuwa kweli huwa unaota, mtu huyu unaweza ukamthibitishiaje kwamba kweli wewe huwa unaota?
ndo unaweza ukaota ila ukweli wa hiyo ndoto ndio ukawa invalid,yani kwakuwa rohoni umeota utakwenda marekani kesho sio kwamba utakwenda kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom