Ukweli juu ya kukamatwa magari bandarini

Ukweli juu ya kukamatwa magari bandarini

Uzuri ni kwamba wanaolishana ujinga ni wenyewe kwa wenyewe manake hakuna mtu aliye nje na wao anayeamini hizo drama zao!!
Watu wanataka vyeti yy yupo busy kuibua skendo za kuwasahaulisha watu na Leo wametengeneza movie ingine kati ya Lipumba na maalim Seif.
 
Watanzania wa Safari hii wamekomaa na vyeti vya Daud Bashite hata waje na story gani ni mwendo wa vyeti vyeti vyeti tu.
 
Sterling hapa ni bwana ukwaju
anaweza kuwa kiongozi wa Dili pia anaweka akawa ni wakala wa kutoa mizigo hakuna mwenye uhakika kwa 100% kwa kawaida wakala anaweza asijue mzigo ndani kuna nini kwani huamini kilichoandikwa kwenye documents ikitokea tatizo mwenye msala anatakiwa awe mmiliki wa mzigo.
 
Jawabu la kumaliza tatizo ni kumjua mmiliki wa hizo gari na kila kitu kipo kwa nini hawamtafuti mmiliki? Kwani mwenye mali akionekana ndiyo atasema Ukweli wote.
 
Kaka usibishane na kilichotokea. Sijui lolote kuhusu mambo ya bandari. Tunachotakiwa kujiuliza imewezekanaje gari la transit likapata usajiri zanzibar?
Swali hili ni rahisi sana kwani jawabu lake linapatikana kwa mmiliki wa hiyo gari.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Umuofia kwenu...

Jana nimepata habari za ndani juu ya hili sakata la kukamatwa kwa kontena zikisemekana ni mitumba. Kiufupi hapo zamani watu walidanganya sana nature ya mizigo iliyo ndani ya kontena tena ujanja wao wote walikuwa wakifanya kwa kivuli cha transit cargo.

Ujue transit cargo hapo mwanzo zilikuwa hazilipi VAT na hata ukaguzi wake kwenye scanner ulikuwa hafifu kwani ilikuwa haina maslahi kimapato ingawa hii mizigo ilikuwa inabaki humuhumu.

Ujio wa scanner mpya na msimamo wa JPM kuwa lazima kila mzigo upite scanner ndio umefumua madudu mengi. Kulingana na mtoa taarifa wangu anasema "kweli JPM amefanikiwa kuwapoteza wapiga dili wengi bandarini" kwani pale scanner kuna wanajeshi,TISS,TRA na watu wa bandari. Pia port manager ameweka informers kibao. So ili upige dili hawa wote mpaka uwaweke sawa.

Turudi kwenye mada
Inasenekana huyu Bwana ukwaju aliingiza hizi kontena tangu mwezi wa tisa mwaka jana. Ikumbukwe kuwa hii ilikuwa ni kawaida ya bwana ukwaju kukwepa kodi kwa njia hiyo ya kusingizia mitumba na pia kufanya ni transit. Sasa Bwana ukwaju alimtumia dogo flani aende kwenye kampuni ya clearing( sitaitaja) ili mzigo utolewe mwaka huu February. Ujue agent yeye huwa anafanyia kazi taarifa anazoletewa. Sasa Bill of lading ilionuesha ni mitumba.

Hii bill of lading inajazwa ulaya wakati agent hayupo so hapa udanganyifu umeanzia kwa shipping line. Ok agent akaendelea kufanya kazi yake mpaka akawa amepata release order. Lakini ikaja kugundulika mzigo unadaiwa zaidi ya $80,000 ikiwemo na storage charge(kumbuka mzigo wa tangu September mwaka jana) Bwana Ukwaju alikuwa ameshaanza kunegotiate apunguziwe gharama kwa kuwaandikia TRA bila ya agent kujua.

Sasa TRA wakawasiliana na agent kumjulisha juu ya negotiations alizoanzisha bwana ukwaju. Hapa kengele ya hatari ikalia kwa agent. Kumbuka wakati hili kontena linashughurikiwa tayari bwana ukwaju alishaleta kazi nyingine of the same nature kupitia kwa dogo aliyemtuma mwanzo.

Agent baada ya kuwa na mashaka akamwambia dogo anaomba akutane na mwenye mzigo ndipo bwana ukwaju akaenda kwa agent akamwambia yeye achape kazi tu kwani kila mtu ni wake mle bandarini.

Agent kwa kutotaka kuharibika akawaandikia TRA kuwa anajitoa katika shughuri za kushughurikia huo mzigo na atafutwe agent mwingine. Ikumbukwe haya yote yametokea kabla ya kontena kukamatwa au kupita scanner.

Sasa bwana ukwaju sijui alitafuta agent mwingine au la? Lakini inasemekana mzigo haukupita scanner na tayari alikuwa ameshapanga timu yake ili kutoa mzigo. Nadhani kulikuwa na mazingira ya kuzungukana mzigo ukakamatiwa getini ukiwa katika hatua za mwisho za kutoka. Au ni mainformer ndio walitoa taarifa hilo mie sijui. Ndipo mzigo ukaamuliwa urudishwe scanner na ubainika kumbe sio mitumba bali ni range rover.

Bwana ukwaju alishafanikiwa kutoa gari zingine mfano ile inayoonekana ina namba za zanzibar ilishatolewa ikaenda zanzibar na kupewa namba wakati ile gari documents zilionyesha ni transit to zambia. Ile gari ilikamatiwa zanzibar na inavyoonekana alikuwa anawatumia agents tofauti tofauti. Ile picha inayooshesha gari yenye namba za Zanzibar ni kwenye kituo cha polisi bandari. Kwa hiyo hakuna uongo katika hilo. Sema sio sawa kusema JPM alikamata yale magari. Magari yalikamatwa either kwa kuzungukana kwenye pesa au kwa mamlaka husika kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Kama haya magari yalikamatwa baada ya kuzungukana. Je, nini maana ya kuwa na taasisi nyingi za usalama pale bandari? Inamaana wameamua kujiunga for common interest? Gari ilifanikiwaje kufika geti la kutoka bila ya kupita scanner? This is a home work for JPM.

TUNDU LISSU
Rais wa TLS ameshaingia katika kumtetea Bwana ukwaju. Naomba hili lisichukuliwe kisiasa kwani anatekeleza majukumu yake ya kutetea hata muuaji. Kila mtuhumiwa ana haki ya kutetewa hata akiwa ni muuaji.

Lissu amelalamika kwa nini Bwana ukwaju anashilikiwa na polisi kwa siku 23 bila ya kufikishwa mahakamani au kupata dhamana. Hili nalo ni la msingi ili haki za watuhumiwa zilindwe. Inasemekana Bwana ukwaju ana ukwasi wa kutisha. Inasemekana polisi wananufaika sana na ukaaji wake pale kituoni kwani ukikaa na waridi lazima unukie waridi.

Wasalaam
Ndimu mkata shombo
Habari hii ina ukakasi kidogo na chumvi ni nyingi.
TRA hawawezi kudai storage ya bandarini maana haiwahusu.

Storage, wharfage za bandarini mdai ni THA , hivyo kuna kutunga hii stori.
 
Ukwaju wakati anakamatwa alikuwa na pesa cash dola kadhaa pia wazambia nao walikuwa na cash pesa yote imepigwa na hao watu wa bandarini na Siri ilitoka pindi mgao uliposhindwa kupita kote na wazambia kulalamika kukaa jela wakati wametoa pesa zao nyingi, na kama Lisu kaingia hapo atakuwa kaenda kupeleleza issue ilivyokuwa kisha aanike Ukweli iwe Aibu kwani kama mizigo ni ya toka September na watu wapo jela kwa siku nyingi iweje magufuli adai yy ndiyo kawakata? alitaka afunike Nape na kuwasahaulisha watu juu ya vyeti feki vya makonda Daud Bashite.
We jamaa ulisikia rais alichoambiwa?. Au umehadithiwa?. Raisi hajasema kama yeye ndio kakamata.
Ziara ya raisi ilikua na kuangalia zile container za mchanga alizopiga marufuku zisisafiri. Akiwa bandarini mkuu wa bandari ndio alie mpa jpm taarifa za huo mzigo kwamba dcmnt zinaonesha ni mtumba lakini ndani ni range.
Jpm akatoa pongezi kwa kazi nzuri waliofanya watu wa bandari.
 
kuna njia moja inatumika kukwepa kodi ya magari ya transit na kutumika nchini. Mojawapo ni kutumia reg number za magari yaliyopata ajali na kuuzwa kama scraps. kuna team ya watu wanafanya scouting ya aina mbali mbali za magari yanayochinjwa tandale hasa ya kifahari wananunua file kabla halijarudishwa TRA. Mfano Harrier T 777 DSW imepata ajali na kukatwakatwa, wao wanaenda kununua file la hiyo harrier Nyeupe T777DSW waanagiza gari nje ikiwa under transit ikishaingia nchini inapewa number zile ni chessis number inabadilishwa ama inaachwa.

Kisha inafanyiwa transfer of ownership inauzwa ama inatumika.


wito kwa mamlaka fuatilienni magari ya kifahari yanaoneskana ni ya kisasa lakini yana number za zamani.......
 
Najiuliza kama ushahidi upo wazi hivyo kwanini Bwana Ukwaju anaendelea kupata adhabu ya kukaa mahabusu bila kupelekwa mahakamani kesi yake ikaamuliwa? Ni lini hii nchi itajifunza kutoa haki kwa wakati? Ni wakati sasa wa Ukwaju kufikishwa mahakamani na apate wakili mzuri wa kumtetea ikibidi huyo Lissu afanikishe hili
 
Nina shaka kuna watu wamegeuza kukwepa ni kama hobby.
Pamoja na usumbufu wote wa kujaribu kukwepa sasa hivi bado watu hawaachi!
Mi mwenyewe nikipata nafasi ya kupitisha mzigo wangu kinyemela napitisha tu infact niwe mkweli tu nimeshatumia fursa mara kadhaa.biashara haijui ishu ya uzalendo its about profit and loss,wapemba wengi kkoo wametajirika kwa kuingiza mizigo kimagendo kwa kutumia bandari bubu.
Hai make sense kulipa makodi makubwa makubwa halafu tuliowapa dhamana ya kuzisimamia wanazitapanya hovyo na dharau juu.unanunua gari 1000$ japan alafu linafika bongo wanataka ushuru milioni tisa, si ufala huu,unadai vipi kodi mara nne hadi tano ya bei ya manunuzi,eti wanasingizia uchakavu,sasa gari ya 2004 ina uchakavu gani,kama mnapenda sana mazingira simzuie moja kwa moja yasiletwe nchini kuliko kukomoana na mikodi isiyokuwa na tija.shabaash.
 
Jawabu la kumaliza tatizo ni kumjua mmiliki wa hizo gari na kila kitu kipo kwa nini hawamtafuti mmiliki? Kwani mwenye mali akionekana ndiyo atasema Ukweli wote.
Kwani ukwaju sio mmiliki wa hayo magari?, then anaingiaje hapo?
 
Wanajamvi.
Umuofia kwenu....
Jana nimepata habari za ndani juu ya hili sakata la kukamatwa kwa kontena zikisemekana ni mitumba. Kiufupi hapo zamani watu walidanganya sana nature ya mizigo iliyo ndani ya kontena tena ujanja wao wote walikuwa wakifanya kwa kivuli cha transit cargo.

Ujue transit cargo hapo mwanzo zilikuwa hazilipi VAT na hata ukaguzi wake kwenye scanner ulikuwa hafifu kwani ilikuwa haina maslahi kimapato ingawa hii mizigo ilikuwa inabaki humuhumu. Ujio wa scanner mpya na msimamo wa JPM kuwa lazima kila mzigo upite scanner ndio umefumua madudu mengi.

Kulingana na mtoa taarifa wangu anasema "kweli JPM amefanikiwa kuwapoteza wapiga dili wengi bandarini" kwani pale scanner kuna wanajeshi,TISS,TRA na watu wa bandari. Pia port manager ameweka informers kibao. So ili upige dili hawa wote mpaka uwaweke sawa.

Turudi kwenye mada
Inasenekana huyu Bwana ukwaju aliingiza hizi kontena tangu mwezi wa tisa mwaka jana. Ikumbukwe kuwa hii ilikuwa ni kawaida ya bwana ukwaju kukwepa kodi kwa njia hiyo ya kusingizia mitumba na pia kufanya ni transit.

Sasa Bwana ukwaju alimtumia dogo flani aende kwenye kampuni ya clearing( sitaitaja) ili mzigo utolewe mwaka huu February. Ujue agent yeye huwa anafanyia kazi taarifa anazoletewa. Sasa Bill of lading ilionuesha ni mitumba. Hii bill of lading inajazwa ulaya wakati agent hayupo so hapa udanganyifu umeanzia kwa shipping line.

Ok agent akaendelea kufanya kazi yake mpaka akawa amepata release order. Lakini ikaja kugundulika mzigo unadaiwa zaidi ya $80,000 ikiwemo na storage charge(kumbuka mzigo wa tangu September mwaka jana) Bwana Ukwaju alikuwa ameshaanza kunegotiate apunguziwe gharama kwa kuwaandikia TRA bila ya agent kujua.

Sasa TRA wakawasiliana na agent kumjulisha juu ya negotiations alizoanzisha bwana ukwaju. Hapa kengele ya hatari ikalia kwa agent. Kumbuka wakati hili kontena linashughurikiwa tayari bwana ukwaju alishaleta kazi nyingine of the same nature kupitia kwa dogo aliyemtuma mwanzo.

Agent baada ya kuwa na mashaka akamwambia dogo anaomba akutane na mwenye mzigo ndipo bwana ukwaju akaenda kwa agent akamwambia yeye achape kazi tu kwani kila mtu ni wake mle bandarini.

Agent kwa kutotaka kuharibika akawaandikia TRA kuwa anajitoa katika shughuri za kushughurikia huo mzigo na atafutwe agent mwingine. Ikumbukwe haya yote yametokea kabla ya kontena kukamatwa au kupita scanner.

Sasa bwana ukwaju sijui alitafuta agent mwingine au la? Lakini inasemekana mzigo haukupita scanner na tayari alikuwa ameshapanga timu yake ili kutoa mzigo. Nadhani kulikuwa na mazingira ya kuzungukana mzigo ukakamatiwa getini ukiwa katika hatua za mwisho za kutoka. Au ni mainformer ndio walitoa taarifa hilo mie sijui. Ndipo mzigo ukaamuliwa urudishwe scanner na ubainika kumbe sio mitumba bali ni range rover.

Bwana ukwaju alishafanikiwa kutoa gari zingine mfano ile inayoonekana ina namba za zanzibar ilishatolewa ikaenda zanzibar na kupewa namba wakati ile gari documents zilionyesha ni transit to zambia.

Ile gari ilikamatiwa zanzibar na inavyoonekana alikuwa anawatumia agents tofauti tofauti. Ile picha inayooshesha gari yenye namba za Zanzibar ni kwenye kituo cha polisi bandari. Kwa hiyo hakuna uongo katika hilo.

Sema sio sawa kusema JPM alikamata yale magari. Magari yalikamatwa either kwa kuzungukana kwenye pesa au kwa mamlaka husika kufanya kazi zake kwa ufanisi.
Kama haya magari yalikamatwa baada ya kuzungukana. Je, nini maana ya kuwa na taasisi nyingi za usalama pale bandari? Inamaana wameamua kujiunga for common interest? Gari ilifanikiwaje kufika geti la kutoka bila ya kupita scanner? This is a home work for JPM.

TUNDU LISSU
Rais wa TLS ameshaingia katika kumtetea Bwana ukwaju. Naomba hili lisichukuliwe kisiasa kwani anatekeleza majukumu yake ya kutetea hata muuaji. Kila mtuhumiwa ana haki ya kutetewa hata akiwa ni muuaji. Lissu amelalamika kwa nini Bwana ukwaju anashilikiwa na polisi kwa siku 23 bila ya kufikishwa mahakamani au kupata dhamana.

Hili nalo ni la msingi ili haki za watuhumiwa zilindwe. Inasemekana Bwana ukwaju ana ukwasi wa kutisha. Inasemekana polisi wananufaika sana na ukaaji wake pale kituoni kwani ukikaa na waridi lazima unukie waridi.
Wasalaam

Ndimu mkata shombo

Asante kwa ufafanuzi. Serikali ikifanya mazuri, tuisifie, ikikosea hapo tuikosoe, sio kutetea uhalifu, vita ya wakwepa kodi siyo ya Rais pekee, ni vita yetu wote.
 
Acha bhana!! Kwahiyo amefanikiwa kuwapoteza wapiga dili bandarini na amebaki na watu wanaomwambia kwamba hizi containers zina dhahabu 90% na watu kama mazuzu wanashangilia!!!

Kua makini Bwana! Hadi hapa uzi unassailable fresh sasa wewe unalterable Mzava!
Hiyo 90% ni habari Rasmi? Hadi sasa hatuna taarifa rasmi ya kilichopo kwenye makontena, lkn ninaami Rais anazo Taarifa za ndani zaidi , na hii yote ni kwa usalama wa uChumi wa Taifa.
 
Back
Top Bottom