Ukonga Kumekucha: Waendesha bodaboda wamtimua Waitara

Ukonga Kumekucha: Waendesha bodaboda wamtimua Waitara

Kama wanaweza kumwapisha waende wakamwapishe lakini wasitusumbue wana Ukonga eti tupange foleni tena kumchagua yule yule tuliyemchagua jana tena kwa gharama ya mabilioni na muda pia. Waitara usituchoshe. Vinginevyo leta hizo fedha ulizopewa tujengee hizi barabara zinazotusumbua kila siku. Asubirie tu kupata cheo cha kuteuliwa yaani kupewa mezani cheo kama wenzake akina Kafulila, Katambi, Kitila, Shonza/funza, Wampamba, n.k.
 
Ndugu nimekuwa nafuatilia sana post zako na haina shaka wewe ni mwanachama wa CHADEMA. Takupa udhaifu mmoja hai mmoja unaokikumba chama chenu na amini kabisa ninachokuambia.

Unakumbuka katika mkoa wa Shinyanga halmashauri ya Msalala mlikuwa na diwani mmoja tu wa CHADEMA aliyekuwa kata ya BUGARAMA BULYANHULU, huyu pamoja na kuwa peke yake kukibeba chama chenu si Mbowe wala kiongozi yoyote aliyewahi kwenda japo kumsikiliza changamoto zake za kisiasa hata zile za kifamilia (uchumi) ukizingatia alikuwa peke yake na hivyo chama kingemuona kama mtu muhimu na sioni sababu hata kwa nini viongozi wote wangelikuja hata siku moja kumsalimia na kumtia nguvu lkn hakuna lolote lililofanyika hadi akazidiwa nguvu na kuamua kuunga juhudi za Jiwe. Si hivyo tu soon hata mwenyekiti wa kijiji cha Kakola ulipo mgodi wa Bulyanhulu atajiunga hivi karibuni maana hana msaada wowote wa chama isipokuwa viongozi wako Dar tu wanakula bata. CHADEMA ya sasa ni dhaifu mno na inaishi kwa kulalamika tu kwani kila siku napata updates za kinachoendelea. Amini Waitara atapita kwa kura nyingi tu kwani CCM haitegemei kura za majukwaani yenyewe inazifuata nyumba kwa nyumba kupitia mabalozi
si rahisi kumchunga binadamu , hivi Waitara alinyimwa ushirikiano au Mtatiro aliyepewa hadi uenyekiti naye alinyimwa ushirikiano ?
 
si rahisi kumchunga binadamu , hivi Waitara alinyimwa ushirikiano au Mtatiro aliyepewa hadi uenyekiti naye alinyimwa ushirikiano ?
Naomba uweke kumbukumbu katika hii komenti yangu. CCM huwa wanaumia sana kuona sehemu ilipo migodi mikubwa kama Bulyanhulu ikiongozwa na upinzani narudia tena CCM huwa wanaumia sana kuona sehemu ilipo migodi mikubwa kama Bulyanhulu ikiongozwa na upinzani. Suala la sehemu pekee inayoshikiliwa na CHADEMA ulipo mgodi wa Bulyanhulu kijiji cha Kakola ni suala la muda tu utasikia
 
Naomba uweke kumbukumbu katika hii komenti yangu. CCM huwa wanaumia sana kuona sehemu ilipo migodi mikubwa kama Bulyanhulu ikiongozwa na upinzani narudia tena CCM huwa wanaumia sana kuona sehemu ilipo migodi mikubwa kama Bulyanhulu ikiongozwa na upinzani. Suala la sehemu pekee inayoshikiliwa na CHADEMA ulipo mgodi wa Bulyanhulu kijiji cha Kakola ni suala la muda tu utasikia
Wala sijakubishia mjomba , kama Alinunuliwa Dr Slaa atakuwa Mwenyekiti wa kijiji ?
 
Hawa mbuzi wanaomuunga mguu jiwe kwa tamaa ya vipande thelasini laiti wangekua wanaujua mwisho wao, wasingekua wanathubuti kufanya upumbafu,

Hapa boda ya wajanja baada ya madiwani watano wa cdm kuuza utu wao kwa ma fisiem mkurugenzi akishirikiana na shetani wenzake wakafanya figisu wakasema wamepita bila kupingwa, sasa kilicho na kinachowakuta hawa madiwani batili wanajuta wanaishi kama digi digi, mmoja alipita eneo panaitwa kisimani, wakamsabahi "jambo diwani wa viti maalumu" basi akapaniki " nani diwani wa viti maalumu? Viti maalumu ni kwa ajiri ya wanawake" wakasema umejibu vizuri sasa wewe umepigiwa kura? Si umepitishwa tu? Wakaongezea ulikua unavaa gwanda sasa unavuliwa ch.pi .

Nakwambia aliondoka analia mtu mzima.
 
Back
Top Bottom