Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
[h=6]Unafikiri tunaweza kuelezea hali ya kisiasa nchini kuwa ni "ukoloni wa ufisadi"? Yaani tukitofautisha na kutawaliwa na wageni?[/h]Ukoloni wa ufisadi (colonialism of corruption) naweza kuelezea kuwa ni mfumo wa utawala ambao umekuwa imposed on the people na ambao watu hawakuuchagua wala kuukubali lakini unaonekana ukiendesha mifumo mbalimbali ya serikali na kuwanufaisha wachache. Ni mfumo ambao unaendesha karibu njia zote za maisha ya wananchi (kisheria, kiuchumi, na kijamii) huku ukitengeneza kati ya watu kundi la watu wachache wenye kunufaika na mfumo huo (mafisadi, makuwadi wa ufisadi na vikaragosi vya ufisadi) na mamilioni ya watu ambao wanajikuta wakiuhudumia mfumo huo (servicing the system) .
Kama ukoloni wa kisiasa wa kigeni ambao ulikuwa imposed on the people na kuwanufaisha wananchi wachache wa ndani na wengi wa kigeni mfumo wa ukoloni wa kifisadi unaendelea kuwanufaisha wachache wa ndani na wengi wa kigeni. Mifumo yote miwili - ukoloni wa kisiasa na ukoloni wa kifisadi - msingi wake ni dhulma, unyonyaji, ukandamizaji na kutokujali matokeo (impunity)
Kama ilivyokuwa wakati wa ukoloni wa kisiasa mafanikio ya jamii kubwa ya watu wakati ule na ya mtu yeyote yule yalitegemea sana uhusiano wake na wakoloni. Wale waliokuwa karibu na wakoloni au waliopewa ajira na wakoloni walijikuta wananufaika na wengine kufikia mahali pa kujaribu kuutetea ukoloni na mafao yake kwao. Wale ambao hawakuwa na nafasi za kunufaika katika ukoloni walijikuta ni wahanga wa mfumo huo; hawakuwa na nafasi ya kubadilisha sheria, taratibu isipokuwa kulalamikia mfumo huo.
Wapo kati yao ambao waliona njia bora ya kushughulikia mfumo wa ukoloni wa kisiasa ni kufanya nao mazungumzo ya kuona jinsi gani "wakoloni" wangeweza kuboresha hali ya maisha ya wananchi kwenye koloni. Hawa hawakuwa hasa na nia ya kuuondoa mfumo huo bali kuona jinsi gani wangeweza kustawisha maisha yao ndani ya mfumo huo. Leo hii hii chini ya utawala wa ukoloni wa ufisadi wapo ambao wananufaika na mfumo huu kiasi kwamba hawako tayari kuubomoa na kuumong'onyoa kabisa kwani ni kama kuukata mkono unaowalisha.
Tofauti kubwa ni kwamba wakati wa kuukataa mfumo wa ukoloni wa kisiasa wananchi wetu walikuwa pamoja kwani walijua kabisa ni kwa pamoja tu wangeweza kuleta mabadiliko ya kweli. Leo hata hivyo tumegawanywa katika kuukataa mfumo wa ukoloni wa kifisadi. Nyerere alielezea vizuri kuwa wakati wa kupinga ukoloni TANU was the national movement ya kukataa mfumo ule na wananchi toka kila kona ya taifa letu walikuwa nyuma yake (Nyerere na TANU) kukataa ukoloni.
Lakini wakoloni baada ya kuwakataa na kuung'oa mfumo wao waliondoka kurudi makwao; je mafisadi ambao ni wenzetu tunapowakataa na tukiwatoa wanaenda wapi? Na wale waliokuwa wananufaika na mfumo wao watakwenda wapi kama siyo kubakia in the background kusubiria zamu yao tena? Je, tunaweza vipi kuushinda mfumo huu tukiwa tumegawanyika, kugawanyika na kugawanyana? Je twawezi kweli kuungo'a ufisadi bila kujikuta kizazi fulani kinajenga chuki kama kizazi kilichonyang'anywa mirija wakati wa Mwalimu kilivyojenga chuki?
Kama ukoloni wa kisiasa wa kigeni ambao ulikuwa imposed on the people na kuwanufaisha wananchi wachache wa ndani na wengi wa kigeni mfumo wa ukoloni wa kifisadi unaendelea kuwanufaisha wachache wa ndani na wengi wa kigeni. Mifumo yote miwili - ukoloni wa kisiasa na ukoloni wa kifisadi - msingi wake ni dhulma, unyonyaji, ukandamizaji na kutokujali matokeo (impunity)
Kama ilivyokuwa wakati wa ukoloni wa kisiasa mafanikio ya jamii kubwa ya watu wakati ule na ya mtu yeyote yule yalitegemea sana uhusiano wake na wakoloni. Wale waliokuwa karibu na wakoloni au waliopewa ajira na wakoloni walijikuta wananufaika na wengine kufikia mahali pa kujaribu kuutetea ukoloni na mafao yake kwao. Wale ambao hawakuwa na nafasi za kunufaika katika ukoloni walijikuta ni wahanga wa mfumo huo; hawakuwa na nafasi ya kubadilisha sheria, taratibu isipokuwa kulalamikia mfumo huo.
Wapo kati yao ambao waliona njia bora ya kushughulikia mfumo wa ukoloni wa kisiasa ni kufanya nao mazungumzo ya kuona jinsi gani "wakoloni" wangeweza kuboresha hali ya maisha ya wananchi kwenye koloni. Hawa hawakuwa hasa na nia ya kuuondoa mfumo huo bali kuona jinsi gani wangeweza kustawisha maisha yao ndani ya mfumo huo. Leo hii hii chini ya utawala wa ukoloni wa ufisadi wapo ambao wananufaika na mfumo huu kiasi kwamba hawako tayari kuubomoa na kuumong'onyoa kabisa kwani ni kama kuukata mkono unaowalisha.
Tofauti kubwa ni kwamba wakati wa kuukataa mfumo wa ukoloni wa kisiasa wananchi wetu walikuwa pamoja kwani walijua kabisa ni kwa pamoja tu wangeweza kuleta mabadiliko ya kweli. Leo hata hivyo tumegawanywa katika kuukataa mfumo wa ukoloni wa kifisadi. Nyerere alielezea vizuri kuwa wakati wa kupinga ukoloni TANU was the national movement ya kukataa mfumo ule na wananchi toka kila kona ya taifa letu walikuwa nyuma yake (Nyerere na TANU) kukataa ukoloni.
Lakini wakoloni baada ya kuwakataa na kuung'oa mfumo wao waliondoka kurudi makwao; je mafisadi ambao ni wenzetu tunapowakataa na tukiwatoa wanaenda wapi? Na wale waliokuwa wananufaika na mfumo wao watakwenda wapi kama siyo kubakia in the background kusubiria zamu yao tena? Je, tunaweza vipi kuushinda mfumo huu tukiwa tumegawanyika, kugawanyika na kugawanyana? Je twawezi kweli kuungo'a ufisadi bila kujikuta kizazi fulani kinajenga chuki kama kizazi kilichonyang'anywa mirija wakati wa Mwalimu kilivyojenga chuki?