Ukizaa na mume wa mtu funga domo lako

Katika pitapita huku na kule jamaa akajikuta amezaa na mchepuko, jamaa akamwambia mtu wake"nitamjengea nyumba mtoto tutapangisha ili pesa za matumizi na mambo mengine zitoke huko na pia huo utakuwa ndio urithi wake, kwasababu mimi nina familia sitoweza kumtambulisha huyo mtoto kwenye familia yangu, nitasababisha misukomisuko kwenye ndoa yangu.

Mchepuko ukashukuru sana na ukaahidi kutunza siri maisha yote,nyumba ikajengwa wakapata mpangaji l50K kwa mwezi, wakakubaliana hiyo pesa ya pango iwekwe benki kwa ajii ya kumsomeshea mtoto atakapokuwa amefikisha umri wa kuanza shule.

Kwahiyo jamaa akawa anatoa pesa za matumizi kila mwezi,yule bibie akanogewa na zile huduma akajisahau na kujihisi naye ni mke wa jamaa, akaanza"Hooo huyu ni mtoto wa fulani hoooo baba yake anamjali sana kamjengea nyumba maneno kedekede.

Hizi habari zikamfikia mke wa jamaa ,ugomvi mkubwa ndani ya nyumba, ikabidi Yf apeleke mashtka kwa wakweze kikao cha usuluhishi kikakaa Jamaa mbele ya wazazi wake na nduguze akakiri mtoto ni wake na nyumba kamjengea kweli, kikao kikaamua mtoto atambulishwe rasmi kwenye familia na nyumba aliyojengewa itakuwa ya familia nzima, mkewe naye akawa tayari kumlea mtoto wa mumewe bila ubaguzi Ila tu mumewe amhakikishie kutoendelea tena na mahusiano na mchepuko, jamaa akafanya hivyo kwa kiapo.

Baada ya mchepuko kuambiwa maamuzi ya kikao amekubaliana na suala moja tu la kumchukua mtoto,ila kuhusu nyumba anataka iendelee kuwa ya huyo mtoto wake tu kama walivyokubaliana awali,kwa madai kwamba hata yeye ana watoto wengine ambao siku za usoni watahitaji msaada wa kifedha kutoka kwenye hiyo nyumba.

Jamaa amegoma amemwambia mdomo wake umesababisha hayo yatokee,lakini ukweli ni kwamba yeye Mchepuko hakuchangia chochote kwenye ujenzi.

Kimenuka huko hakuna cha pesa ya matumizi wala pesa kwenda benki, Mchepuko anataka aolewe na jamaa awe mke mdogo amlee mwanaye yeye mwenyewe, jamaa naye anasema hana uwezo huo wa kuoa wake wawili na sio kuoa tu hata kuchepuka hataki tena,punguzeni midomo hizo tambo zinawaharibia.


Kisicho riziki hakilikagi!
 
Mwanaume kusema Eti anachepuka lakini huku anampenda mke wake wa ndoa ni uongo na unafiki!

Ukimpenda mtu huwezi tafuta kumfanyia jambo ambalo unajua mwenzi wako akijua utakuwa umeumiza moyo wake Kwa makusudi.

Kuchepuka ni jambo la makusudi na linalopangwa na kuratibiwa vilivyo.

Kwa hiyo ni makusudi mazima na wala si jambo la bahati mbaya.
We ni mwanaume?
Kama ndio, umeoa?
 
Kwa vipi?

Hivi maana ya upendo inaeleweka vizuri miongoni mwa wanandoa kweli ?

Kama unampenda mtu utamfanyia jambo la kuumiza moyo wake ?
Huwezi kumfanyia jambo la kuumiza moyo,ndio maana ukichepuka unajificha,ndio maana unampa masharti mchepuko wako ili asije akakuharibia kwa unayempenda.
 
Mwanaume kusema Eti anachepuka lakini huku anampenda mke wake wa ndoa ni uongo na unafiki!

Ukimpenda mtu huwezi tafuta kumfanyia jambo ambalo unajua mwenzi wako akijua utakuwa umeumiza moyo wake Kwa makusudi.

Kuchepuka ni jambo la makusudi na linalopangwa na kuratibiwa vilivyo.

Kwa hiyo ni makusudi mazima na wala si jambo la bahati mbaya.
Wewe sio mwanaume..huwezi elewa kitu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Huwezi kumfanyia jambo la kuumiza moyo,ndio maana ukichepuka unajificha,ndio maana unampa masharti mchepuko wako ili asije akakuharibia kwa unayempenda.



Sizani!

Mbona hata wezi wanapoibia watu huwa wanajificha Kwa namna mbalimbali?

Ni tabia ya Mhalifu tu kutaka kujificha Kwa namna fulani na wala sio kusema sababu ya kumpenda mtu wala nini!

Unajua ni Kwanini wahalifu hutafuta kujificha wawafanyiapo uhalifu watu?

Hebu fikiria kidogo!
 
Sizani!

Mbona hata wezi wanapoibia watu huwa wanajificha Kwa namna mbalimbali?

Ni tabia ya Mhalifu tu kutaka kujificha Kwa namna fulani na wala sio kusema sababu ya kumpenda mtu wala nini!

Unajua ni Kwanini wahalifu hutafuta kujificha wawafanyiapo uhalifu watu?

Hebu fikiria kidogo!
Waharifu wanajificha ili kukwepa mkono wa sheria,na sisi wasaliti tunajificha ili tusiwaumize wapendwa wetu,ndio maana simu zetu wasaliti bila password haiwezekani.
 
Back
Top Bottom