Ukiwa na tabia hizi, jiandae kuwa middle class na kuteseka ki uchumi!

Wadau, hasa vijana wenzangu,

Ushauri kwa vijana wenzangu. Ukiona wewe kwanza ndiyo umepata kazi, ukaanza kwa kununua gari la kutembelea, baada ya hapo ukanunua kiwanja na ukaanza kujenga ujue wewe utaishia kuwa middle class na kuteseka ki uchumi katika maisha yako yote. Ninaposema kuteseka ki uchumi namaanisha kila ikihitajika laki moja wewe kuitoa mpaka ukope au ukitoa unaishiwa. Vijana wengi wanapenda kuishi maisha ya luxury wakati hawana sifa ya kuwa na luxury, unakuta ndani kwake kajaza vifaa expensive wakati hana rasilimali ya kumpa kipato, wengi wanafanya hivyo ili waonekane wako na maisha safi kwa jamii, kumbe wanajichimbia kaburi

Asilimia kubwa ya middle class walieanza kwa ku invest kwenye mambo yasiyozalisha, mfano nyumba ya kuishi mwenyewe au gari, ukianza, ukianza kwa kujenga nyumba ya kuishi wewe ndio mbaya kabisa. Watu tunaowaita matajiri, walianza kwa ku invest kwenye kitu kinachozalisha pesa then gari la kutembelea, nyumba vikaja baadae. Huo ni ushauri wangu kwa vijana wenzangu

haha utakua una gross ya laki 3!!

tafuta hela wewe mwanadamu!!!
 
Huo ni ukweli mtupu, mfano wewe unatumia milioni 60 kujenga nyumba ndani ya miaka 4, ukimaliza hiyo nyumba haizalishi chichote, unaishi mwenyewe, vipi kama hiyo 60 kama ungewekeza mfano kwenye ufugaji wa kuku, kama uko serious hao kuku wangekupa hata milioni 4 kwa mwezi na ukajenga kirahisi

Unajenga nyumba unatumia kama dhamana, hao kuku wakipata mafua ya ndege? biashara kuanza nayo ina risk kubwa kuliko kujenga nyumba ambayo utaitumia kama dhamana. Mimi nadhani option zote ni sawa na usimlimit mtu kwenye option moja tu wanasema "the end justifies the means"
 
Nimependa sana ushauri wako, ni kweli kabisa, Kuanza kwa kujenga nyumba ya kuishi ni sawa na kuzika pesa,

nIMEPENDAS
Ame graduate at 25 akaajiriwa na kupanga nyumba ya 150,000

At 30 ana familia na amejaliwa watoto wa 2 aendelee kupanga nyumba ya 300,000?asijenge!

Unafananisha us/uk kwenye 'nhc' nyingi na zile apartment binafsi hamna manyanyaso
 
umeona eeh!! kuna watu kwanza mshahara wao mwezi mmoja tu ni gharama ya vitz mpya. kwanini asijivutie zake usafiri huku anajipanga zaidi na life.

watu wanafikiri wote apa tunalipwa laki saba saba....wengine iyo ni airtime ya mwezi mzima!!!atafute helaaa
 
mi naona kuanza kwa kujenga nyumba ni muhimu sana, nyumba ni asset. kuliko kuendelea kupata gharama za kulipa wenye nyumba kodi bora uwe na kwako uokoe gharama za kodi.


nyumba zenyewe basi ziwe hata mtu unajenga mwenge au sinza basi...mtu anajenga magore,mbezi mpiji sijui wapi huko..kutoka kwako hadi ofisin masaa 6 si bora upange mjini usake mahela town?......walahi nikijenga sihamii hadi uzeeni.period!!nitabak hapa hapa city center...chakufia!!!
 
Ame graduate at 25 akaajiriwa na kupanga nyumba ya 150,000

At 30 ana familia na amejaliwa watoto wa 2 aendelee kupanga nyumba ya 300,000?asijenge!

Unafananisha us/uk kwenye 'nhc' nyingi na zile apartment binafsi hamna manyanyaso
mimi binafs nashauri vijana wakipata tu kazi wakimbilie kununua kiwanja na kujenga fasta. maisha yanaenda mbele hayarudi nyuma. wakati unasema uanze kuivest kwenye business kumbuka umri nao unaenda. muda wa kuwa na familia umefika hauna mahali unapomiliki pa kuweka ubavu. mara watoto hao, majukumu yanazidi kuongezeka huku upo nyumba ya kupanga. anzeni kujenga, mkishindwa tafuteni japo viwanja huku mnajipanga mdogo mdogo.
 
hivi umemuelewa mtoa mada? yeye anakwambia ukianza kwa kujenga utaishia kuwa middle class, maisha hayana formular. mbona wapo walioanza na biashara na matokeo yake biashara zimekufa na nyumba za kuishi hawana. hii kitu haina guarantee bali ni wewe mwenyewe utakavyojipanga kukabiliana na maisha.

Maisha yana formula sana tu, hiyo formula wanayo matajiri (They have their own secret that middle class can't see). Kuhusu biashara kufa ni sehemu ya kuanguka, kuanguka ni jambo la kawaida kwa matajiri, ni sawa na kula cake, swala la msingi jifunze katika kuanguka kwako na uendelee
 
For your information! The richest investor in the world Warren Buffet alianza kujenga nyumba yake before hajaanza biashara alikuwa ameajiliwa wakati huo.
Nawashauri vijana in their 20's to build their career rather than entering into debts.

nashukuru kwa hii comment!
 
mimi binafs nashauri vijana wakipata tu kazi wakimbilie kununua kiwanja na kujenga fasta. maisha yanaenda mbele hayarudi nyuma. wakati unasema uanze kuivest kwenye business kumbuka umri nao unaenda. muda wa kuwa na familia umefika hauna mahali unapomiliki pa kuweka ubavu. mara watoto hao, majukumu yanazidi kuongezeka huku upo nyumba ya kupanga. anzeni kujenga, mkishindwa tafuteni japo viwanja huku mnajipanga mdogo mdogo.

thumb Up
 
mimi binafs nashauri vijana wakipata tu kazi wakimbilie kununua kiwanja na kujenga fasta. maisha yanaenda mbele hayarudi nyuma. wakati unasema uanze kuivest kwenye business kumbuka umri nao unaenda. muda wa kuwa na familia umefika hauna mahali unapomiliki pa kuweka ubavu. mara watoto hao, majukumu yanazidi kuongezeka huku upo nyumba ya kupanga. anzeni kujenga, mkishindwa tafuteni japo viwanja huku mnajipanga mdogo mdogo.

Mimi nawashauri vijana, anza kwa ku invest ili upate muda mrefu wa kuanguka, kuanguka itakuwa fundisho kwako, ukija kufika wa kuwa na watoto wawili tayari asset yako inakuzalishia milioni 40 kwa mwaka na hautatishwa na kodi ya 150,000, na utajenga kilaini kabisa
 
Wadau, hasa vijana wenzangu,

Ushauri kwa vijana wenzangu. Ukiona wewe kwanza ndiyo umepata kazi, ukaanza kwa kununua gari la kutembelea, baada ya hapo ukanunua kiwanja na ukaanza kujenga ujue wewe utaishia kuwa middle class na kuteseka ki uchumi katika maisha yako yote. Ninaposema kuteseka ki uchumi namaanisha kila ikihitajika laki moja wewe kuitoa mpaka ukope au ukitoa unaishiwa. Vijana wengi wanapenda kuishi maisha ya luxury wakati hawana sifa ya kuwa na luxury, unakuta ndani kwake kajaza vifaa expensive wakati hana rasilimali ya kumpa kipato, wengi wanafanya hivyo ili waonekane wako na maisha safi kwa jamii, kumbe wanajichimbia kaburi

Asilimia kubwa ya middle class walieanza kwa ku invest kwenye mambo yasiyozalisha, mfano nyumba ya kuishi mwenyewe au gari, ukianza, ukianza kwa kujenga nyumba ya kuishi wewe ndio mbaya kabisa. Watu tunaowaita matajiri, walianza kwa ku invest kwenye kitu kinachozalisha pesa then gari la kutembelea, nyumba vikaja baadae. Huo ni ushauri wangu kwa vijana wenzangu
kuna mshkaji alishwa wahi kuja na mchanganuo flani wakiuchumi kwa vijana wanaokimbilia kujenga badala ya kuinverst nilimwelewa kwa kiasi chake..
 
Maisha yana formula sana tu, hiyo formula wanayo matajiri (They have their own secret that middle class can't see). Kuhusu biashara kufa ni sehemu ya kuanguka, kuanguka ni jambo la kawaida kwa matajiri, ni sawa na kula cake, swala la msingi jifunze katika kuanguka kwako na uendelee

wewe ni tajiri au middle class?
 
But all of all,NO SPECIAL FORMULAE CAN BE APPLICABLE IN 3RD WORLD COUNTRIES,btx rich & poor, poor can became rich quickly at wonder ways and rich can became poor imediately|| ooh! my god!
 
Yeah mimi naona vyote vinapaswa kwenda pamoja gari ni kama simu kwa-maisha ya mjini sasa hivi ni muhimu sana ukiikosa kuna cost nyingi tu utaziingia tena kwa miji yenye shida ya usafiri hivi gari ni muhimu afu ni soo cheap to afford uki compare na Nyumba ukiwa na gari linaweza kukusaidia ku monitor investments zako. Mtu ambaye anabeza mwenzie kwa kununua gari namshangaa mimi nasoma chuo ila natamani na ninamwomba Mungu kabla sijamaliza kwanza kitega uchumi hata 2million hivi second kiwanja third gari yaaani namwomba Mungu once I reach my 25 I should have those things wether all or 2 of them and not only 1
 
Mimi nawashauri vijana, anza kwa ku invest ili upate muda mrefu wa kuanguka, kuanguka itakuwa fundisho kwako, ukija kufika wa kuwa na watoto wawili tayari asset yako inakuzalishia milioni 40 kwa mwaka na hautatishwa na kodi ya 150,000, na utajenga kilaini kabisa

wewe jamaa sijui vipi. yaani hiyo ndio sababu ya kushauri watu waaanze kwa kuinvest? hivi unajielewa unachotushauri lakini? millioni 40 kwa mwaka ina maaana ni milioni 3 laki 3 na kitu hivi kwa mwezi. sasa investment yenye return ya million 3 kwa mwezi ni bado ni poor investment na hujatoka kwenye umiddle class. acha kupotosha watu mkuu.
 
ukosahihi kiongozi nina nyumba mbili lakini nikama ninashida sana katika hali yangu kiuchumi

una nyumba mbili na bado una shida ya kiuchumi. ungekuwa umepanga hali yako ingekuwa mbaya zaidi. waone consultants.
 
Back
Top Bottom