Ukiwa kama Great Thinker wa JamiiForums una Fikra gani za Nje ya Box hasa kumhusu huyu Daktari Feki aliyekamatwa Muhimbili na tena Amana?

Ukiwa kama Great Thinker wa JamiiForums una Fikra gani za Nje ya Box hasa kumhusu huyu Daktari Feki aliyekamatwa Muhimbili na tena Amana?

Kwa maelezo ya Mr.Slow slow anasema nyumba ni kama haina mwenye(Hii inaweza kutoa jibu sahihi).Kuna sehemu jamii imeamua mambo yawe vile yatakavyo(Hakuna miongozo,taratibu zote zilizowekwa zinavunjwa ndio maana maadili hakuna tena)
 
Mtu anaongea akiwa na confidence ya kutosha na SI mara ya kwanza kufanya tukio la namna hiyo... Mbaya zaidi ni eneo hilo hilo with the same scenario

Is it a coincidence?

MOI na Team yako mjitathmini kama kuna jambo mlilifanya soon, they will have your ribs out
 
Watanzania nao wamekuwa wahuni.. pengine ni real tapeli.
Sikatai kuwa yawezekana kweli ni Tapeli ila kama alikamatwa Muhimbili National Hospital na ikatangazwa kama hivi leo kuwa alikuwa ni Tapeli ilikuwaje akaachiwa na kuendelea tena kuwa Tapeli na safari hii katika Hospitali ya Amana Ilala? Kwahiyo Sheria za Tanzania siku hizi nazo zimeenda Kaburini?

Je, ilikuwaje Kosa la Utapeli wake Muhimbili National Hospital likamfanya awe Huru na alipata wapi tena Kiburi na Jeuri ya kuendelea kuwa Tapeli na safari hii akifanya Utapeli wake Amana Hospital Amana? Nasubiria majibu yako yenye Akili Kubwa hapa ila endeleeni tu kudhania kuwa Watanzania wote ni Wapumbavu.
 
Hivi ni kwanini Wapuuzi wachache wanapenda sana Kucheza na Akili za Watanzania hasa tu kukiwa na Jambo muhimu?
"Sisi kama taifa tuliamua siasa au kupiga domo ndio iwe kazi yenye malipo makubwa sana kuliko taaluma,ndio maana sekta nyingine hazitiliwi mkazo coz hazina malipo makubwa na sio kipaumbele Kwa serikali ndio maana Bora liende TU mradi serikali inapata data za kusoma majukwaani"

Alisikika mwenye hekima Fulani akilia!!
 
Back
Top Bottom