Ukiumizwa usikubali kuua thamani yako

Ukiumizwa usikubali kuua thamani yako

royna

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2010
Posts
479
Reaction score
336
Ukweli kwenye maisha kuna watu wanaumiza nafsi za watu!Kuna mtu anakuuuuuumiza, mwingine anaishia tu kusema sorry, mwingine anakuona ndio kwanza unacomplicate maisha, mwingine anakupotezea tu na kuendelea na hamsini zake, ili mradi tu, wewe ndiyo unakuwa umebaki na majeraha ya ndani.Siku zote nasisitiza shida siyo jambo linalokupata, shida ni vile unavyolichukulia au kupambana nalo.(The problem is not a problem, but rather the way you react to problems.)

Kila mwanadamu ni wa thamani sana, kwake mwenyewe, kwa jamii inayomzunguka na kwa Mungu. Watu wanapokuumiza wengine ni makusudi na wengine ni ubinadamu wao umepungua sana ndani hadi wanakosa utu kabisa na kitu twaita empathy.

Hivyo kukubali kulia sana, kuumia sana, kununa, kususa, kuzira ni kuendelea kujiumiza wewe, MAANA UKWELI NI KUWA UKIKASIRIKA HUMUUMIZI ULIYEMKASIRIKIA BALI NAFSI YAKO YA NDANI.

Na kwa kuruhusu uchungu na hasira unajiumiza mwili wako kwa kuzeeka kabla ya siku, kukomaza uso, kupata magonjwa tabia na kujipunguzia wema kwenye mahusiano mengine.
 
Umesema kitu kilichonigusa sana.

Sipendi kuumiza lakini nilikuwa na makando kando yaliyo sababishwa na kuumizwa kwangu before napambana kuyafutilia mbali ingawa yamekuwa chanzo cha maumivu kwa wengine.
 
Well said mkuu royna. Mwenye macho na atazame na mwenye masikio na asikie.
 
Last edited by a moderator:
Yeah Ni kweli hakuna kitu kizur kamaa kukubali halii ukishakubali halii unakua umetibu sehem kubea ya jeraha
 
Umesema kitu kilichonigusa sana.



Sipendi kuumiza lakini nilikuwa na makando kando yaliyo sababishwa na kuumizwa kwangu before napambana kuyafutilia mbali ingawa yamekuwa chanzo cha maumivu kwa wengine.


Polee ndo maisha let it go alokutendea hayo Ata face his/her own karma
 
Yeah Ni kweli hakuna kitu kizur kamaa kukubali halii ukishakubali halii unakua umetibu sehem kubea ya jeraha


Muda mwingine inakera sana unajiuliza maswali ambayo unakosa maji lakini ndio hivyo life goes on
 
Muda mwingine inakera sana unajiuliza maswali ambayo unakosa maji lakini ndio hivyo life goes on


Of course 😊 unakubali hali halisi na unakua kimya Tu mtenda akifanyiwa hivi lazima aweweseke mtu akikutenda msamehe bure ndo ubinadam na usiyaweke rohoni
 
kwenye maisha tegemea mengi, cha muhimu ni kujipa moyo na kusonga mbele kwa kuwa huwez kubadili yaliyotokea
 
hisia ni kitu kibaya pale akili inaposhindwa kufanya kazi yake ipasavyo.
 
Na hawa wanaoumiza wenzao halafu hawaji kuapologize maana yake ni waovu wanaofurahia kujeruhi nafsi za wenzao, maana ibilisi hapendi kuona watu wana afya ya mwili, nafsi na roho!
 
Ni true isipokuwa ni ngumu sana,kuna jirani yangu mama mwenye watoto 4 mumewe alikuwa anatoka na binti jirani,huyo mume kamwambia kimada mke wangu ana bwawa na k yake nilikuta wameiharibu wanaume wengine,kuna siku pakatokea fumanizi yule kimada anamtukana yule mama yale maneno machafu alioambiwa na yule mume mbele za watu na watoto na mume akawa anapigilia misumari,kweli wewe una bwawa,baadae mume kamwomba msamaha wanaishi ila mke alikonda ghafla nadhani mawazo,aisee ningekuwa mimi nisingeweza kuendelea kuishi na huyo jamaa,.ebu angalia hilo jambo mke lazima atakawa na huzuni kila siku
 
Of course 😊 unakubali hali halisi na unakua kimya Tu mtenda akifanyiwa hivi lazima aweweseke mtu akikutenda msamehe bure ndo ubinadam na usiyaweke rohoni


All tha best mdada....nimejifunza kitu nitajaribu kujicontrol sababu nina temper flani ambayo inaweza nifanya kujibu mtu ninavyojickia.hakuna kitu ?mbacho sipendi kama mtu kudisturb akili yangu sababu naamini ina mambo ya kufanya mtu anapoisumbua nakereka sana
 
Mhhhhhh!!! ingekuwa kuna kidonge cha kusahau watu wangenunua.
 
Back
Top Bottom