Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,967
- 218,825
Cnn oyeeeeeeee !
Weka hiyo picha tuione
Natamani ningeona kwenye kuran iwe inataja msamaha kwa watenda dhambi, hapo ningeupenda sana uislamu
viongozi wetu wa dini wamekuwa sawa na wana siasa tu sioni tofauti yao,maana ukitazama msingi wa siasa ni mzuri sana lakini wanaosimamia huo msingi mambo wanayofanya ni kinyume kabisa,
ni sawa na viongozi wetu wa dini tena hapa ni wa dini zote wamekuwa wao ndio vyanzo vya kila upuuzi,wamekosa maadili wamekosa hekma wamekuwa wapo wapo tu,wengi wao mafundisho ya dini zao wameyasahau zaidi wanafata matamanio yao tu,
ntawapa mfano wa kiongozi muadilifu ambae aliwahi kutokea baada ya mtume muhammad huyu bwana alikuwa anaitwa omar bin khatab,huyu bwana historia inasema alikuwa katika ujinga na hakuwa muislam na alikuwa adui mkubwa wa uislam na aliuwa sana waislam,lakini baada ya miaka mingi huyu bwana akaamini yaani akasilimu akamfuata mtume,
basi huyu bwana alimsoma mtume sana akasoma sana dini mpaka ikamwingia akawa ni mtu wa karibu sana na mtume,na huyu bwana alikuwa ni mtu tajiri sana pale makkah na alikuwa ni maaruf pia,
historia inasema huyu ndio katika viongozi waadilifu duniani ambao walipata kutokea basi omar alikuwemo,
omar ni khalifa wa mtume wa 3 yaani baada ya kufariki mtume aliefuata kuwa mtawala wa makkah alikuwa ni abubakar siddiq, wa pili othman bin affan,na wa 3 alikuwa ni omar bin khattab,
kuna siku jamaa mmoja alitembelea ofisini kwake omar ilikuwa muda wa usiku alikuwa ana maongezi nae wakati huo akiwa omar ndio kiongozi mkuu wa saudi arabia,basi huyu bwana alikuwa akimuuliza omar maswali mengi tu ya dini na family yake anachanganya maswali, basi omar alikuwa na mishumaa miwili pale ofisini kwake basi alikuwa anawasha mshumaa mmoja mara anazima mwingine,yule mgeni wake ikabidi amuulize mbona mara anazima huu anawasha huu?
Omar akamjibu wewe unaniuliza maswali mchanganyiko kuna maswali unaniuliza yanahusu family yangu ndio maana nazima mshumaa huu nawasha mwingine'kwa sababu mshumaa mmoja nimenunua kwa pesa ya kwangu na mwingine kwa pesa ya waislam ndio maana hapa naogopa kupata dhambi kila ukiniuliza swali la family yangu nazima mshumaa wa waislam nawasha wangu nakujibu,na ukiniuliza swali la waislam nazima wangu nawasha wa waislam pia sitaki kuwafanyia dhulma family yangu,
hebu jaribu kufikiria uadilifu gani huyu jamaa aliokuwa nao?
Na historia inatuambia huyu omar alikufa kwa maradhi ya tumbo kwa sababu alikuwa hataki kula vizuri licha ya yeye kuwa tajiri alikuwa akisema hawezi kula chochote kizuri wakati mitaani kuna watoto yatima wamejaa na wajane wasio na misaada ndio akaona badala ya kula yeye vizuri bora wengine wale,
je viongozi wetu wa leo hata robo ya uadilifu wanayo?
naomba uelewe kwanza qur-an haina uhusiano na albadir, wala katika qur-an hakuna kitu kinaitwa albadir,na wala katika mafundisho ya uislam hakuna al badir sehem yeyote inapofundishwa,
kwanza hakuna ukweli kama al-badir ina madhara yeyote ila tunachoamini huwa kweli,kwa sababu huyo anaekusomea albadir anasoma kitabu cha majina ya watu ambao walipigana katika vita ya badri ndio maana kinaitwa al badir.ndani yake hakuna dua yeyote zaidi ya majina ya watu,ila kwa sababu tulishaamini toka enzi tunaumia kwa imani kuliko ukweli wenyewe
Asante sana mkuu kwa darasa zuri, watu wamekariri dini halafu wanataka kupotosha.
Uislam hauendi kwa mazoea bali dalili kutoka katika Quran na Sunnah.
Ukiwa unakaribia Tandika relini, ukiuliza kila mtu anaijua hii story.
Mimi Tomaso siamini hadi "maso" yangu yaone walau hata picha.Weka hiyo picha tuione