Ukitaka kumchunguza mwanaume

Kumbuka hapo ukija kupatwa na lolote wazazi wako lazima watakulaumu..

Naona hawapo upande wako maana wao wanaamini kanisa lao..

Yeah naelewa but sitaki kuendelea na zinaa naona mtu yupo tayari na Mimi najisikia wito wa ndoa ni bora niende tu
 
Chomoka nenda kwa Nabii unayeona kuwa ni Nabii wa kweli...

Nenda utajua Kila jambo...

Ndoa sio sherehe ni mkataba...

Sikutishi Mamy

[emoji23][emoji23][emoji23] aiseee mama katika watu siwaamini ni manabii

Acha tu niombe mwenyewa

Labda kuna mchungaji fulani mtoto wake ni rafiki yangu huyo kidogo yuko peace nitajaribu kumshirikisha
 
Muombe Mungu tu atakuonyesha haya ya kuchunguzana litakukuta jambo
 
Chomoka nenda kwa Nabii unayeona kuwa ni Nabii wa kweli...

Nenda utajua Kila jambo...

Ndoa sio sherehe ni mkataba...

Sikutishi Mamy
Hata yeye mwenyewe kama ana imani / macho ya rohoni kuna vitu ataviona au kuoneshwa/ oteshwa!
 
Ukimchunguza sana bata, hutaweza kumla. Achana kabisa na hizo mambo. Wewe angalia kama mtaweza kuishi maisha marefu, mkubalie tu.
 
Umchunguze ili iweje?

Au unatafuta red flag umpige chini?

Uko tayari na wewe akuchunguze akikukuta na red flag yoyote akupige chini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…