Ukishangaa ya Mussa

Kuna jamaa alisema ukitaka kujua walimu ni waoga we tafuta landcruiser hardtop tafuta na marafiki zako wanne mvae suti alafu vamia shule yoyote unaweza kumpiga mkwara mkuu wa shule lisaa lizima bila kukuuliza we ni nani
Sio mkuu wa shule tu hata afisa elimu kata wao na wa wilaya wote watasanda sijui wanalishwaga nini huko vyuoni ni waoga vibaya
 
Nafikiri shida kubwa inaanzia kwenye wizi wa kura...nawaza kwa sauti
 
Hapana hamdharauliwi, ila mmekuwa walaini sana, CCM inawategemea nyie, ila ikipata mnasahaulika, umesahau mwenda zake hakuwaongeza hata mshahara,madaraja mkabaki pale pale lakini pamoja na yote hayo ni nyie wenyewe mkawa mnaimba nyimbo za kumsifu kwenye uchaguzi ni nyie wenyewe huwa mnaguhusika kuiba kura, tunajiuliza imekuaje? Walimu mnaofundisha ujasiri, iweje nyie hamna ujasiri? mnafundisha Haki na kupigania haki iweje haki zenu hamzipiganii? yaani mwalimu pamoja na kusoma kwake na umahiri wake anaweza kuchapwa fimbo na mkuu wa wilaya ambaye ana kadigrii kamoja What went wrong? Mwalimu aliyekuwa anaheshimika mtaani leo haeshimiki tena nini kimewakuta walimu?????? kuna mwalimu alijitahidi kumvimbia mpaka Raisi lakini angalieni walimu mlivyomsema
 
Nina rafiki yangu nI mwalimu serikalini jana alikuwa anaenda shule Saa tatu ,nikamwambia mbona umechelewa job hivyo ,akanijibu "kwa kazi ipi haswa ,kazi yenyewe stress tupu Mishahara yenyewe zero" Nawahi nini
🤣🤣🤣🤣 Hii kazi yahitaji moyo Ila tunashukuru tunalea watoto mamy
 
Inasikitisha Sana😓
 
Wao wenyewe ndo wa kwanza pia kuvaa kofia na vitenge vya ccm toleo la kwanza🤣
 
Hatushindani we si umetaka kujua kwanini mnadharaulika, kuna watumishi wana maisha magumu kama askari magereza? Lakini kwanini hawadharauliki km nyie? Kunifundisha aeiou haizuii kuuona ukilaza mlionao, mikopo kausha damu nyie, kutapeliwa nyie, kujiliza nyie, kama mmeweza kutufundisha mnashindwa nini kujisimamia mkaheshimika kama walimu wa enzi ya nyerere?
 
🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾Utatuulia mwalimu wetu bwan
 
Sio mkuu wa shule tu hata afisa elimu kata wao na wa wilaya wote watasanda sijui wanalishwaga nini huko vyuoni ni waoga vibaya
Alafu wakati mnapiga mkwara yule mwenye kitambi ndo aongee alafu mwenye mwili mdogo ajidai anaandika andika, wawili wanaobaki mmoja anakua anamsikiliza mkuu wa shule kwa makini alafu yule wa nne anachomekea swali moja moja
 
Kama mnataka heshima kama walivyo heshimiwa walimu wa zamani inabidi Elimu mliyo nayo iwakomboe akili sio wanasiasa na ccm wanawatumia kama karatasi za chooni kila mara na nyie mnakubali tuu alafu eti mnataka heshima ya kutoka wapi 🤔🤔 mtaendelea kudharaulika na kuchukuliwa watu wa hovyo hadi mtakapo jitambua
 
Kuna jamaa alisema ukitaka kujua walimu ni waoga we tafuta landcruiser hardtop tafuta na marafiki zako wanne mvae suti alafu vamia shule yoyote unaweza kumpiga mkwara mkuu wa shule lisaa lizima bila kukuuliza we ni nani
We jamaa comments zako zinachekeshaga sana ,nimecheka Hadi mbavu zinauma
 
Yani tukitaja matukio ya walimu wenzie ni aibu bora atulie tu, tatizo kubwa linaanzia kwenye uoga CCM sijui inawatishaga nini hawa watu, asichojua nimekua nikizungukwa na walimu, nawajua kuliko anavyodhani
Sawa imetosha na kakuelewa mweeee😂
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…